WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Sunday, November 6, 2011

JE UWAJIBIKAJI WA PAMOJA WA KICHAMA HOZOROTESHA UADILIFU?


UWAJIBIKAJI WA PAMOJA WA WANASIASA NA VYAMA VYAO JE UNAPUNGUZA  UWAJIBIKAJI WA MWANASIASA MMOJA MMOJA KATIKA KUTETEA  MASILAHI YA WANANCHI?

Ni kweli kuwa Wanasiasa wengi huwa na uadilifu wa kutosha kupinga matendo maovu ambayo mengine hufanywa na viongozi ndani ya chama chao kama ufisadi na rushwa; lakini wakati mwingine nguvu hizo huishia ukingoni kutokana na shinikizo kubwa la chama chake, pale anapolazimishwa kufuata msimamo wa pamoja wa chama katika kufanya maamuzi; na pale itakapo tokea tu muhusika huyo amefanya maamuzi kinyume na uwajibikaji wa pamoja wa chama ni rahisi sana kutengwa na kuonekana msaliti: 




Kutokana na shinikizo hilo baadhi ya wanansiasa wazuri na waadilifu watetezi wa wanyonge hubaki  wamevaa ngozi ya unafiki. kwa msimamo huu ni kweli ambao haufichiki kuwa  sio kila mwanasiasa ni mla rushwa au fisadi bali baadhi ya wanasiasa huwa na sifa mbaya kwa sababu nguvu ya uwajibikaji wa pamoja wa kichama.


Nafikiri inafurahisha sasa kuona kuwa Wanasiasa wengi wameanza kuhodhi sifa mbalimbali za utaalam “professionalism” tumeanza kuona namana wabunge wenye sifa hizo wanavyoweza kujenga hoja na kuvuta hisia za watu wengi, na hata kuleta changamoto katika shughuli zao za siasa. Jingine ambalo tumejifunza tumeona kuwa “professionalism” husaidia kuzingatia maadili ya utendaji kazi na hulka ya kujiamini na kuwa tayari kukosoa ,kukosolewa  na kufanya maamuzi mazito hata wakiwa katika msimamo wa  pamoja ya kichama hawaburuzwi kihoja.


Pamoja na dhana ya kuwa lengo la kuwa chama cha siasa chochote, lengo la kwanza kabisa ni kushinda uchaguzi. Na kuna tofauti kati ya mwanansiasa mtaalam njisi ambavyo ana fanya kampeni walio wengi maadili ya husadia kupunguza kampeni chafu. Maadili ni muhimu zaidi na katika siasa na kwa maendeleo ya wananchi. Maadili ya kweli yatapunguza wanasiasa kujishughulisha na rushwa.

Katika demokrasia wananchi ndio wenye dhamana na uwezo wa mwisho wa kumrejesha mwanasiasa kuendelea kuhozi madaraka; pamoja na umaarufu wake, uadilifu na utaalam katika kushughulikia maswala ya siasa bila ridhaa ya mwananchi sio rahisi kurejea madarakani;

historia ya vyama vingi na chaguzi za Zambia zinaainisha kuwa ukomavu wa demokrasia ndani ya Zambia wananchi ndio wenye sauti ya mwisho wananchi wa Zambia wanapima na kuamua kulingana na utendaji wa viongozi wao na sio ushabiki wa vyama;
Tatizo la kushabikia sana vyama ndilo linaloponza sana maendeleo ya nchi nyingi za kiafrika; wananchi wanakumbatia zaidi chama na sio utendaji wa viongozi wa vyama vyao;

Kama wananchi tunatakiwa kuanza kuangalia upya maamuzi yetu dhidi ya viongozi wetu; tunahitaji viongozi waadilifu na viongozi wa namna hii  wataweza kuchukua hatua kwa maslahi ya jamii kwa manufaa ya wote, na wanaweza kubaki madarakani kwa muda mrefu iwezekanavyo kulingana na utaratibu wa nchi husika na kukendelea kukubalika kwako kwa masilahi ya wengi; Katika mfumo wa kidemokrasia wa serikali, ambapo nguvu ya utawala ina inapatika upya kila baada ya miaka mitano na wananchi ndio wenye dhamana ya kuwarejesha madarakani.

Nchi ya Zambia imetufundisha kuwa  hakuna kiongozi anayemiliki watu, hakuna chama chenye hatimiliki ya kuwa na kundi la wananchi kama itakuwa hivyo basi kuna tatizo na wananchi katika nchi hiyo; wananchi mara zote wanategemea na wanataka  mabadiliko makubwa ya kiuchumi hawahitaji propaganda za chuki, wanahitaji kufaidi raslimali zao  wazambia walikuwa wanashangaa utajiri wote unaotokana na shaba unakwenda wapi? Pale ambapo hawakuridhika hawakuwa na papara walisubiri tu wakati ulipofika walimweka pembeni kiongozi na kumpa dhamana kiongozi mwingine. Lazima tukubali kuwa katika nchi zilizopo kusini mwa Afrika  Zambia ni moja ya changamoto za mabadiliko ya kisiasa:

Maamuzi ya wananchi katika awamu tofauti Zambia umeendelea kuwashangaza viongozi walioko madarakani kuanzaia enzi  Kaunda, pamoja na ukongwe wake wa kutawala kwa miaka 27 hadi awamu ya Banda; Kiini cha msukumo huu nini? Wananchi wanatamani kupata maisha bora; na kuwa viongozi wenye kiwango cha juu kabisa cha uadilifu kuweza kuwatumikia wananchi na kuleta maendeleo sio kwa nadharia bali vitendo;


Viongozi wetu wa vyama vya siasa wamesahau kuwa, Kimsingi, raia huzaliwa wakiwa huru dhidi ya mikingamo ya kijamii, kwa lugha ya kitaalamu tabula rasa. Lakini mikingamo hii ya kijamii huingizwa katika fikra za wananchi kupitia itikadi na elimu ya siasa katika vyama ambavyo wanafuata; na wakati mwingine hata kupitia shule na sehemu za ibada.

Cha ajabu haitoshi kuivuruga jamii peke yake tumeona na tunaendelea kuon kuwa viongozi wetu wa kisiasa hapa nchini wamekuwa wakigombana kila mara katika mambo ya msingi na yasiyo na msingi. Kugombana si kubaya kama kunaleta tija, lakini kule kugombana kunakofanywa kwa misingi ya kujitafutia umaarufu kunasabaisha viongozi kushindwa kutekeleza majukumu yao ambayo yanatokana na ahadi wakati wakiomba ridhaa ya kuchaguliwa na wananchi, ni dhambi ambayo haiwezi kuvumilika hata kidogo. 

Wakati tunaelekea kusherekea miaka hii 50 ya uhuru wetu  itakuwa busara kama serikali kwa upande mmoja , vyama vya siasa kwa upande mwingine kupunguza matumizi nguvu ya kiuchumi katika maswala yanayohusu zaidi umaarufu wa kisiasa na kupeleka nguvu hizo katika maswala ya kijamii; bado wananchi wetu hali zao bado ziko duni sana (masikini), tunahitaji barabara bora; huduma za afya nzuri, elimu bora kwa vijana wetu; ajira za kutosha kwa wenye sifa za kuajiriwa;


Kama Rais Kenedy wa Marekani alivyowahi kusema ‘Wewe UMELIFANYIA NINI TAIFA LA TANZANIA’ ni wajibu wa msingi kabisa kwa wale wote ambao wamepata ajira ya serikali kutimiza wajibu wao; ni aibu kubwa pale inapogundulika kuwa wafanyakazi wengi wa serikali wanafanya kazi chini ya masaa nane; tusitarajie maisha bora kama sisi kama watumishi wa umma hatutawajibika ipasavyo; tutimize wajibu wetu kwa maisha bora kwa kila mtu,

MUNGU IBARIKI TANZANIA TUNAVYOELEKEA KUSHEREKEA MIAKA 50 YA UHURU

No comments:

Post a Comment