WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Friday, November 18, 2011

AMANI YA KWELI HULETA MATUMAINI;




JE AMANI TUYAHUBIRI SASA KUELEKEA MIAKA HAMSINI YA UHURU WA TAIFA LETU INAMWELEKEO WA KULETA MATUMAINI NA MAENDELEO KWA TAIFA LETU?

JE AMANAI HUZAA UPENDO MIONGONI MWETU?
JE HIVI SASA TUNAHUBIRI AMANI AU UNAFIKI  WA KUBOMOA TAIFA kwa masilahi binafsi?

Mwandishi  Ezekiel Kamwaga, KATIKA MOJA YA MAKALA ZAKE  aliwahi andika kuwa  “Bila ya UPENDO miongoni mwa Watanzania, taifa hili halitakwenda popote. Tutabaki tu kuwa nchi ya manyang’au”.

Wakati tuapojianda kusherekea miaka hamsini  ya uhuru wa taifa letu kuna mambo mengi tumejifunza na tunaendelea kujifunza katika kuhakikisha kuwa amani ambayo waasisi wetu wametuachia  hatuko tayari kuipoteza; tatizo langu je mikakati yetu ya kudumisha amani yetu ni imara au inayumba kwa hivi sasa? Na kama inayumba inayumbishwa na nini?

Ni ukweli ambao hatuwezi kuuficha kuwa kwa hivi sasa wananchi wengi  wanajaribu kutathimini uzoefu wa sera za vyama vyao ambao ndio chimbuko  linalotumika kuidumisha amani nchini. wananchi na wananchama katika kipindi hiki cha sasa wanachukua kwa hamu fursa hii ya demokrasia  ili kushiriki katika shughuli za vyama vyao katika kuleta maendeleo, lakini pengine kwa wengine wanaishiwa na hamu mara moja baada ya kuona pengine ni kwa namna gani chama kinaweza husika katika kuhatarisha amani kwa kuleta vurugu, na hivyo kuhatararisha utawala wa sheria ndani ya  demokrasia huru  ambayo huwa kama ni  kikwazo kwenye fikra bunifu katika fursa  ya kujenga  amani ya kweli.

Kama nilivyowahi kusema huko nyuma katika makala zangu kuwa tusipo ongeze jihudi za  uwekezaji wa elimu ya uraia (civic education) kwa wananchi na wanachama wa vya vyama mbalimbali vya siasa amani tunayotamani kuitunza itabaki kuwa ni ndoto; ili kuhakikisha kuwa wananchi wanaelewa haki zao za msingi na matumizi ya sheria ndani ya demokrasia, hii ni fursa pekee katka kuhakikisha  kuwa tunakuwa na amani yenye vigezo vya juu vya ubora, lakini  tukishindwa kufanya hivyo tutaendelea kudhoofisha sana juhudi zetu za kudumisha amani na upendo katika taifa letu.

Katika kipindi hiki tukiwa tunajiandaa kusherekea miaka hamsini ya uhuru  wa taifa letu si vibaya kujiuliza  amani bora inapatikanaje? Au amani bora hujengwa na watu au inashushwa tu kama neema kwetu kama taifa kutoka Kwa Mwenyezi Mungu?

Je yale yanayofanyika hivi sasa sehemu mbali mbali ya nchi yetu na wanachama mbalimbali wa vyama vya siasa na kusababisha vurugu kwa kivuli cha demokrasia, ni sehemu ya kudumisha amani yetu? Je wananchi na wananachama wa vyama husika wanaelewa nini wananchofanya au ni kufuata tu mkumbo bila kuelewa kwa undani kwa nini kitu fulani kinatokea na kwa nini mimi nikipiganie? Je ni kwa sababu kiongozi wangu ndio amesema nifanye hivyo? Au kwa vile rafiki yangu amefanya hivyo?

Nionavyo mimi Kama wananchi na wananchama wa vyama mbalimbali watendelea kufuata kila jambo kwa mkumbo kwa kweli Watabaki wamefungiwa katika hali ya hasara, bila uwezo wa kushindana; watakuwa wakitumika katika uchumi na utamaduni wa utandawazi kwa masilahi ya wachache na kuwajengea umaarufu watu wachache na pengine kwa undani na hawatakuwa na masilahi na wengi.  Na wataendelea tu  kudumaza vichwa vyao na kuwatia ganzi ya usikivu na utiifu, badala ya kuwapatia ujuzi na kuwapa nyenzo wanazohitaji kuwafanya wabunifu na watu wa fikra, watabaki kama tulivyo leo: wenye mapungufu, tusiotimilika, usiowashindani, na, kama kundi, maskini kiuchumi.

Lakini siyo lazima iwe hivyo. Maamuzi tunayofanya leo yanaweza kuwasaidia wananchama  kuwa watetezi wa mawazo yao wenyewe, pamoja na mitazamo na misimamo yao. Wananchama wanahitaji kuwa na ufahamu na ujuzi unaoweza kutumika katika mazingira yanayobadilika. Wanahitaji uhodari na imani ya kuamini silika zao. Wanahitaji nidhamu ya kufikia kilele cha uwezo wao.

Pengine vyama vyetu vimejikita katika mawazo yaliyokuwa sahihi kwa wakati uliopita. Wengi wetu tumezoea kufikiri kuwa siasa na vyama vya siasa ni sehemu tu ya propaganda ambayo  wanasiasa wanajifunza kutoa propaganda pengine kwa  kukariri kilichoandikwa ndani ya ilani ya chama husika hata kama hawaelewi na hawawezi kupambanua vizuri. Kwa kufanya hivyo nafikiri tunalenga kuwajengea hofu ya kuvunja sheria na madhara yake. Ikiwa hivyo basi vyama vyetu vinajiendesha kwa kuwatisha na kuwajengea wachama nidhamu ya woga ili wafanye yanayotarajiwa kutoka kwao nafikiri ina madhara makubwa kwa kuzingatia kuwa;

1    Kila mmoja anakubali kuwa watu wazima wana nafasi muhimu katika kuelekeza makuzi yamawazo yao ndani ya chama.

2    Tatizo ni wengi wa wananchama hawa  wanatoka katika  katika mazingira ambayo hawafahamu sana elimu kuhusu haki zao za msingi ndani ya vyama vyao na nje ya vyama vyao wamebakia kuwa na kiwango kidogo sana cha uwezo wanaohitaji ili kufanikiwa katika kueelewa na kumbambanua maswala mbali mbali ya  kisiasa.

3    mara nyingi inawezekana kuwa viongozi wa vyama wanaweza  kulazimisha utiifu kwa muda mfupi na kujenga chuki na uasi kwa muda mrefu miongoni mwa wananchi wa jamii moja. Wananchama  wengi wa vyama kutokana na kukosa elimu ya uraia  wanabaki kuwa wananchama watiifu na waoga wanajifunza kuendana na njia zilizozoeleka za kuwa na za kufikiri na, kwa hiyo, hawaendelezi stadi za lazima kuleta majibu muafaka kwa matatizo mapya.

Je, huku siyo kuwa tunashindwa, licha ya kudhani tumefanikiwa kuwaelimisha wananchama wetu? Kutokana na mahitaji yetu ya haraka ya watu wabunifu na wenye fikra?  Je tunajifunza nini kutokana na migomo, machafuko ambayo yanasababisha watu kujeruhiwa katika kipindi hiki tunavyoelekea kusherekea miaka hamsini ya uhuru wetu?

Nafikiri kama tutafanikiwa kuwafanya wananchama wetu wawe na elimu  ya uraia na itasaidia Kukuza utambuzi:  kujifunza wajibu wao katika kuhusiana na wengine. Ukuaji kimaadili: Kupitia miundo ya kidemokrasia na uwajibikaji, kuwa mfano mzuri wa kuigwa, na sera endelevu, elimu bora ya uraia  huendeleza uwezo wa wananchi  kushiriki kutekeleza sera hizo na kuonyesha hali ya kujali kama raia. Elimu bora  hupalilia viwango dhahiri vya maadili ambavyo huwasaidia wananchi kujijengea ndani mwao mfumo wa maadili kwa maisha yao yote.

Kama tutafanikiwa kuwa na Vyama bora vya siasa vitasaidia sana kuleta haya yafuatayo;

• kujenga nidhamu chanya ndani ya chama chake na vyama vingine,

• kudumisha  kuheshimu na utu wa kila mwananchi wa taifa letu.

• kuimarisha amani ambayo sisi kama taifa tunaipigania kuilinda kwa nguvu zote.

 Ni ukweli kuwa katika kipindi hiki cha miaka Hamsini ya uhuru, wananchi walio wengi wamebaki kwenye kifungo cha mzunguko wa hali ngumu na umaskini wa kujua haki zao za msingi kwa ukosefu wa elimu bora ya uraia. Wananchi wengi wamebaki kuwa wapokeaji na watekelezaji wa sera za viongozi wao hata kama sera hizo haziwanufaishi wao wananchi.

Kupitia elimu ya uraia tunajifunza kuwa  Kuongoza ni kuwasiliana.  Ili uongozi uwepo, tunahitaji walao watu wawili ambao kwa kiasi fulani wanashirikiana na kuhusiana.  Kwa maneno menginekatika duru za kisiasa tunahitaji chama zaidi ya kimoja ili kuleta ushindani wa kimaendeleo;Hakuna awezaye kuongoza akiwa katika upweke.  Kwa hiyo, uongozi ni mojawapo ya aina za mawasiliamo. Kuna uhusiano mkubwa kati ya jinsi mtu anavyoongoza na jinsi anavyowasiliana na wengine;

Je katika kipindi hiki cha miaka hamsini tumeongoza vipi? Au tumewasiliana vipi katika kuliletea taifa hili tija ya maendeleo kwa kigezo cha amani na utulivu?


Hayati Mwalimu Nyerere katika harakati zake zote za uongozi  alijua anahitaji sana hali ya amani, utulivu na ushirikiano katika kujenga nchi mpya, nchi huru. Mwalimu alitambua vile vile nchi ilikuwa na makabila mengi zaidi ya 120 yaliyokuwa na lugha, mila na desturi zinazotofautiana, na ingekuwa vigumu kuongoza watu wasioelewana kifikra, na tofauti nyingine nyingi.

Alijua tofauti hizi zingeweza kuchochea chuki na hivyo kuondoa matumaini ya kuwa na amani na maendeleo. Baba wa taifa Mwalimu Nyerere alifahamu kuwa watanzania kuelimishwa juu ya haki zao ili waweze kuzidai si kuvunja amani, amani ya kweli ni ili ambayo imejengwa katika misingi ya ukweli, haki na democrasia ya kweli. Amani ya kweli ni uwepo wa haki na uwajibikaji wa viongozi.

Kwa hiyo tunakila sababu ya kuhakikisha kuwa amani ambayo tunayo tunaendelea kuilinda kwa nguvu zote; tunawaomba wapinzani waendelee kutufunua kuikosoa serikali pale ambapo inakiuka na inashindwa kuwajibika; ni ukweli kuwa mengi tulikua hatuyajui tunafikiri kila kitu kinachofanywa na serikali ni sawa. Analisho kwa vyama vya upinzani tunaomba chonde chonde tupitisheni katika barabara sahihi ya kudai haki zetu au unapoiwajibisha serikali, tunatamani sana amani ambayo tunayo iendelee kuwako kwa miaka mingine hamsini inayokuja, vurugu na hasira zitahatarisha amani yetu;

MUNGU IBARIKI TANZANIA NA TUENDELEE KUKUMBUKA KUWA “Bila ya UPENDO miongoni mwa Watanzania, taifa hili halitakwenda popote. Tutabaki tu kuwa nchi ya manyang’au”. NA ISIYO NA AMANI YA KWELI.

No comments:

Post a Comment