WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, October 17, 2011

UTAWALA BORA NA ELIMU YA URAIA VIJIJINI


UONGOZI USIO NA TIJA HUZORETESHA ELIMU BORA YA URAIA MIONGONI MWA WAPIGA KURA WAISHIO VIJIJINI



Kipimo cha uongozi bora ambao hutokana na uongozi uliotukuka  ni  pale tu wapiga kura wanapoufurahia uwajibikaji wa viongozi walioko madarakani kwa  kuwatatulia kero ambazo zinahitaji nguvu ya serikali kama huduma bora za jamii kwa  maendeleo yao.

Lakini katika nchi zinazoendelea, bado zinabaki kuwa wahanga wa migogoro ya kiuchumi na kisiasa. sababu kubwa ya migogoro hii ni uongozi mbaya katika nchi husika.

Tanzania kama nchi nyingine za kiafrika bado tunakabiliwa na hali mbaya inayotokana na ubadhirifu wa fedha na utumiaji mbaya wa madaraka ambayo baada ya kumsaidia Mwananchi kumkwamua kiuchumi na kijamii bado mwananchi wanaendelee kukabiliwa na tatizo la umasikini.

Uchambuzi wa maswala ya kiuchumi unatukumbusha kuwa nchi ikifikia katika hali hii inatuonyesha kuwa kuna tatizo la utawala bora, kuna tatizo la uzalendo  kuna tatizo la balance of power;Je serikali inasimama upande upi? Kumsaidia wananchi wa kawaida au kuwatajirisha mtu mtu mmoja mmoja au kikundi cha watu wachache kwa masilahi binafsi?
Je ni nani waliowaweka viongozi madarakami ni wananchi wanyonge walio wengi au ni kikundi kidogo cha watu wenye pesa?
Kama ni wananchi ambao ndio waliowachagua viongozi kwa kura zao; kwa maoni yangu  kama wananchi kuendelea kuishi katika lindi la umasikini katika nchi yenye rasilimali  nyingi ambazo nchi inamiliki ni ukiukaji wa haki za binadamu.

Hivi sasa kama Taifa tunahitaji viongozi ambao wataweza kuwatetea na kuwaletea wananchi wao maendeleo;

Tunahitaji viongozi waaminifu na wasafi; hili ni jambo la muhimu sana kwa maendeleo ya taifa tukuangalia sana viongozi wetu wanakosa sana sifa hizi mbili kuu muhimu; viongozi wengi wa Afrika wamechagua kutekeleza sera maovu(ufisadi) badala ya upendo mkubwa kwa taifa( utawala Bora) husika.

Nafikiri itakuwa ni jambo la busara kama viongozi wetu watakubali kusimamia elimu ya uraia kwa wananchi wa vijijini ili kusaidia katika mageuzi ya kuboresha utawala na kwa maendeleo endelevu ya kiuchumi, na utulivu wa kisiasa ambao ni sehemu ya  utawala bora na utekelezaji wa kidemokrasia wanayohubiri. 
Tatizo la viongozi wetu wanashindwa kuja na vision nzuri ambayo kweli itasaidia maendeleo  na kuondoa kero ambazo wananchi wanakabiliwa nazo kila siku;
Hali hii tata kushindwa kutatua malalamiko ya wananchi kwa miaka mingi  ilimpelekea Robert Wheelen wa Taasisi ya Uchumi. Katika jarida la taasisi ya mwezi Septemba 1996 kuuliza’ kwa nini nchi ya afrika isibinafsishwe kwa nchi tajiri ili kuwasaidia kutatua kero zinazowakabili na kuwasaidia katika kusimamia katika kutoa huduma bora na kuleta ufanisi na nidhamu  wa ukusanyaji  kodi kwa maendeleo ya nchi zao’

Kauli hii wakati mwingine inaingia akilini pengine kuna kweli  kama viongozi wetu wanaelekea kushindwa kutatua kweli za wananchi wao pengine swala hili la ubinafsishaji linaweza kuwa ni suluhisho la maendeleo kwa wote;
Maswali ninayojiuliza kutoka na kauli hii;
·        Je Serikali yetu ya Tanzania imefanikiwa kwa kiasi gani katika ukusanyaji wa kodi hali ambayo imefikiwa sasa tunaweza kujisifu tumepiga hatua au bado juhudi zinahitajika katika kuendelea kufanikisha hili?
·        Je Serikali yetu inasimamiaje shughuli zake za kuendesha serikali kwa faida ya wote, je utawala bora unatekelezwa au bado tuna usugu wa usimamizi mbovu chini na ukosefu wa uwezo wa utawala bora?.
·        Je Serikali yetu imeandaaje miundo na mageuzi ambayo yataimarisha utawala wa sheria, kusaidia kukuza demokrasia na uwajibikaji na uwazi.
·        Je kwa nini wazee wetu kama Mandela, Nkrumah na Nyerere wameendelea kuwa  viongozi bora na wa kuheshimika ndani ya nchi na nje ya nchi zao?
·        Je viongozi bora wanatakiwa wawe na sifa gani?
 kwa matazamo wangu:
  • anayeweza kuwasiliana  na kuwasilisha hoja kwa ufasaha,
  • mwenye uwazi na mawazo mapya,
  • uwezo wa kusikiliza pande zote za mipango endelevu,
  • mwenye hekima na akili ya kawaida,
  • uwezo wa kusimama  na kuongoza wakati political or economic crises ,
  • kujua ukweli kabla ya kufanya maamuzi,
  • Kiongozi bora lazima awe mchapa kazi na mwajibikaji
Tunamkumbuka Mwalimu Nyerere alipoamua kwa hiari yake kuachia madaraka na kutengeneza platform kwa kiongozi wa kuchukua madaraka ya urais kwa kupitia vikao halali ndani ya chama chake na nje ya chama chake.


Kwa msingi huu  Viongozi bora kuandaa watu wao wa kuendeleza safari ya uongozi wa nchi bila woga wa kushitakiwa wakiwa nje ya madaraka; viongozi wetu lazima wajifunze kuwa  mabadiliko ya uongozi ni muhimu kwa ajili ya kuanzisha tawala mpya.  Hapa ndipo tunapoona umuhimu wa elimu bora ya Uraia.


Utawala bora ni utekelezaji wa uwezo na mamlaka na serikali kwa njia ya kuwa watumishi bora wanaoweza kuboresha ubora wa maisha ya wananchi wake. Hii itasaidia kujenga jamii bora na yenye uwezo wa kujikwamua na kupambana na changamoto zinapojitokeza

Na hitimisha kwa kusema kuwa Kuwa kiongozi bora si kazi rahisi wakati mwingine inahitaji mtu kuwa na maono ya mabadiliko, elimu ya utambuzi, mawasiliano ya wazi bila woga, na kuwa tayari kufanya maamuzi  magumu. Tunahitaji viongozi  ambao ni wawajibikaji wa maendeleo yetu; ambao watusaidia sisi kukimbia wakati wenzetu wanatembea katika kuyatafuta maisha bora. Tunawaombea viongozi wetu waweze kuwa charisma na maono ya kujenga upya taifa letu kisiasa na kiuchumi kwa maendeleo ya wananchi wao bila kusahau elimu bora ya uraia.

No comments:

Post a Comment