WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Sunday, October 23, 2011

HONGERA DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE KWA KUTUNUKIWA SHAHADA ZA HESHIMA


“HONORIS CAUSA”



Kama ilivyoelezwa na wataalum wa vyuo vikuu ambavyo ndio watoaji wa Shahada ya Heshima “ Honoris Causa” kuwa;

shahada ya heshima ni ile itolewayo kwa mtu mwenye vigezo stahiki na aliyetoa mchango mkubwa wa maarifa, elimu au ujuzi katika eneo fulani la kitaaluma.

Kwa kawaida shahada hizi hutolewa kama njia ya kuheshimu na kutambua michango ya watu hao katika maarifa, ujuzi au eneo la kitaaluma kwa mfano, afya, uchumi, mazingira, sayansi au fasihi,
mtunukiwa wa shahada hiyo hapasi kuwa na uhusiano wa awali na taasisi inayompa heshima hiyo.

Mtu anayependekezwa kupewa shahada katika chuo chetu ni yule aliyetoa mchango mkubwa kwa umma au kwa taifa na sio lazima mchango katika taaluma bali ni kazi ya ziada yenye manufaa kwa umma nje ya wajibu wake wa kazi.

Mheshimiwa Dr. Jakaya Mrisho Kikwete toka alipochagualiwa kuwa rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania amekuwa kiongozi ambaye amepata shahada zaidi ya moja nje ya nchi na ndani ya nchi;

Kwa maneno mengine ni kuwa Dr. Kikwete amekuwa na mchango mkubwa kwa maendeleo ya jamii katika mfumo wa moja kwa moja (direct) na kwa kupitia viongozi wengine ( in direct) katika kuonyesha njia na kutekeleza majukumu amabayo amekabidhiwa kwa kulingana na katiba yetu;

Shahada hizi zote ambazo amepata zinahusiana na utendaji wa kazi ambao unampa sifa yeye kufikia kilele hiki na utekelezaji wa majukumu.  Kwa wale wote ambao wanakaa darasani na kufanaya utafiti na hatimaye kufanikiwa kutunikiwa shahada mbalimbali lengo kubwa na la msingi wake ni kuwawezesha  kuelewa na mambo mbali mbali kupita uchambuzi wa vitabu na utafiti na kutumia elimu hiyo katika kutatua matatizo ya jamii inayowazunguka;

Lakini kwa upande mwingine viongozi mbali mbali ambao hawana shahada ya juu wanaweza kwa namna moja au nyingine wakawa ni wasomi wakubwa sana ambao wanaweza kutatua matatizo ya jamii kuliko hata kama wengekuwa wamesomea kozi husika. Tuchukue utambuzi ambao Kenya waliona na kuamua kumtunukia Mheshimiwa Kikwete shahada ya heshima kupitia  chuo kikuu cha kenyatta,” kwa ujasiri wake wa kusuluhisha ugonvi wa kibaki na oginga 2008; suluhu hii ya ugomvi ilikuwa na maana kubwa sana katika nchi ya Kenya baada ya vifo vya wenyewe kwa wenyewe;

Je unafikiri kuwa “baadhi ya maelezo” ya hapo chini  yana mpa sifa  
Dr. Kikwete kutunukiwa shahada hizo zote za heshima?

Dr. Kikwete kama kiongozi wa chama na serikali ametumia muda wake mwingi kukemea Ufisadi unaofanywa ndani ya chama twawala na , serikali yake

Dr. Kikwete amekuwa mbele katika  kuimarisha utawala bora miongoni mwa  jamii;

Dr.Kikwete ariruhusu kuundwa kwa  tume huru ya kuchunguza mikataba mibovu katka sekta mbalimbali  zenye kulalamikiwa na wananchi

Kuhusu demokrasia, Kikwete amepiga hatua kwa kuruhusu kwa wazi mijadala mbalimbali. Vyombo vya habari na wananchi wamekuwa huru kuibua hoja mbalimbali zikiwamo hata zile zinazodhalilisha serikali pamoja na  kuagizi kuandikwa upya kwa katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania iweze kuendana na miaka hamsini ya uhuru

Rais Kikwete ameendelea kuwa msikivu na kupokea hoja zilizotolewa na makundi mbalimbali ya Watanzania na kuzitafutia majibu kulingana na mipaka yake na bila kuingilia chombo kingine cha maamuzi.

Dr. Kikwete ameweza kuiagiza chombo kinachuhusika kutenda haki kwa watuhumiwa wa fedha za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA)  na wale wote waliotumia madaraka yao vibaya; uamuzi huu wa busara unatoa  matumaini kwamba rais kweli amedhamiria kupambana na ufisadi ambao unatishia uhai wa uchumi wa nchi yetu,

Kikwete kwa kiasi kikubwa kaonyesha kutoingilia Bunge wala Mahakama katika utendaji, ndiyo maana baadhi ya mambo yamefanikiwa.

Dr. Kikwete amesaidia kuleta suluhu Kenya na Zimbabwe na kuuweka uongozi wa umma Comoro, baada ya kutuma vikosi vyetu huko.

Amesimamia muafaka kati ya CCM na CUF  mpaka serikali ya umoja wa kitaifa imepatika na inafanya kazi kwa kushirikiana vizuri sana.

Lakini ikumbukwe kuwa hata wasomi ambao wanakaa darasani katiki kusomea shahada kama aliyopewa mheshimiwa Kikwete wanakabilia na “ challenges”; na kwa msingi huu Si rahisi kwa binadamu akawa na mazuri matupu; hakuna aliye mkamilifu kwani sisi si malaika na Mheshimiwa Kikwete kadhalika,kama binadamu anayomapungufu yake;

Rais Kikwete kwa mazuri aliyofanya anastahili heshima hiyo kwa  pamoja na mapungufu yake na kama kiongozi bado ana muda wa kurekebisha kasoro zilizojitokeza katika uongozi wake kwa kuendelea kuwabana watendaji wake walio chini yake; lakini tusisahau kuwa nasi tunamchango wa kufanikisha maendeleo yetu tukishirikiana na Mheshimiwa Rais wetu.

HONGERA SANA MHESHIMIWA DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE KWA KUTUNIKIWA SHAHADA ZA JUU ZA  HESHIMA  NJE NA NDANI YA NCHI

Karibu tujadili kwa maendeleo ya Taifa letu

1 comment:

  1. Nilihudhuria siku ambapo JK alipata digirii ya heshima ya udaktari katika Chuo Kikuu cha St. Thomas hapa Minneapolis. Habari za tukio hilo ni hizi hapa.

    ReplyDelete