WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Friday, October 14, 2011

SIKU MAALUM YA KUMKUMBUKA HAYATI MWALIMU NYERERE



Kwa nini tunaikumbuka Mwalimu  Nyerere  siku hii ya leo miaka 12 baada ya kifo chake?

 Nyerere alikuwa anawaambia viongozi waliokuwa chini yake kuwa:

·        kama unahitaji heshimna yangu nionyeshe kuwa unastahili kwa kutimiza wajibu wako

·        Wewe sio mtu mbaya kama umefanya kosa lakini utakuwa mtu mbaya kwa taifa la Tanzania kama utashindwakujifunza kutokana na kosa lako.

·        Kimya changu wakati mwingine si kwamba nimesahau au nimedharau hapana kwani hata mlima unaweza kuwa kimya lakini  una volcano ndani  yake na siku ikilipuka matokeo yake tunayajua

·        Sio kila jambo mtakalo lifanya litamfurahisha kila mtu hapana,  lakini kuna kitu kimoja tu kizuri kuhusu kila mtu katika taifa hili ni ustawi wa jamii yetu na amani yetu

·        Kama kuna viongozi wanasababisha utendaji ulio mbovu,  lazima tuwawajibishe na  tusiwaonee huruma hata kidogo

·        Kwa nini tusiwatendee wananchi wetu vile tunavyotaka  sisi kutendewa au vile sisi tunavyojitendea?

·        Nyerere daima macho yake yalikuwa yakiuma kwa kulilia haki za wanyonge, moyo wake ulikuwa ukiuma kwa kujaribu kuwaletea maendeleo wanyonge lakini mafanikio yalikuwa madogo kutokana na umasikini wa taifa letu na Roho yake ulikuwa ikiuma kwa kuwaombea wananchi wake amani na ustawi kitu ambacho alifurahi mpaka kufa kwake kulikuwa na amani na utulivu; kwa kuendelea kukosoana kwa hoja na sio matumizi ya nguvu.


·        Kwa kweli  wakati mwingine maisha yanakuwa magumu lakini mara nyingi sisi viongozi tunayafanya maisha kuwa magumu kwa wananchi wetu kwa maslahi yetu binafsi; Ugumu wa upatikanaji wa huduma za jamii nani anasababisha ugumu wa mafanikio yake? tatizo la mgao wa umeme linaloendelea hivi sasa nchini nini chanzo chake kikubwa? uzembe uko wapi? nani wa kulaumiwa?

·        Katika maisha yetu ya kila siku ni kweli kuwa matatizo yanayoikumba taifa letu yataendeleea kuwapo na kamwe hayataisha mara moja, basi inatupasa kama viongozi kuendelea kuyataua, na kuyakabili  bila kuchoka. Je taifa letu limejipanga vipi kuhusu kuhusu ongezeko la watu ukilingananisha na huduma zinazotolewa? je uwiano wa huduma na ukuaji  miji yetu  na ongezeko la watu ni sawa? nini kifanyike sasa?




No comments:

Post a Comment