WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, October 19, 2011

VYAMA VYA UPINZANI NA WAJIBU WAKE


MAJUKUMU YA VYAMA VYA SIASA NI NINI BAADA YA UCHAGUZI?

 Je uchochezi na kuleta vurugu dhidi ya chama kilichoshinda kuongoza nchi?

Je  malumbano baina ya vyama vya upinzania vyenjewe?

Je vinabaki vyama vya msimu kwa kusubiri uchaguzi ujao na ruzuku?

Jukumu kubwa la chama chochote cha upinzani ni kuangalia kwa makini sera za chama tawala, na kuzipinga pale ipasapo, na kutoa mikakati na sera mbadala na kuwafahamisha wananchi kuhusu masuala yote ambayo yanahusu uendeshwaji wa serikali.

Kila kimoja kinapokuwa kwenye upinzani kinakuwa na kazi ya kukikosoa chama kilicho madarakani ili kukipa changamoto katika kufanya kazi vizuri. Uwajibikaji wao utawapa fursa wapiga kura kuafanya uamuzi wao kutokana na mafanikio ama kushindwa kwa chama kilichokuwa madarakani kutimiza yale iliyokusudia kuyafanya.

Je kama vyama vya upinzani vinalumbana vyenyewe kwa vyenjewe  matokeo yake nini?

·        Vinapoteza muda na malengo ya vyama vyao kwa kuanza kulumbana na wapinzani wenzao. Kwa kufanya hivyo, vinajidhoofisha vyenyewe.

·        Vinapopambana vyenyewe kwa vyenyewe vinakipa chama tawala kupata upenyo wa kuendelea kutawala na kupata hoja ya kuvisema na hata chama tawala kisipotekeleza sera zake kunakuwa hakuna chama mbadala cha kuwaambia wananchi mapungufu ya chama tawala

Umuhimu wa  Elimu ya uraia na  mikakati ya vyama kushika dola ya kuongoza nchi

Ukosefu wa elimu ya uraia imetufanya wengi wetu kuingia katika malumbano ambayo yanafanya safari ya kuelekea demokrasia bora kuwa sio nyepesi.

Kuna haja ya kuanziasha makakati wa kitaifa wa kutoa elimu ya uraia kwa wananchi. Jambo hili litafanyika kama serikali itakuwa na nia ya kuleta demokrasia ya kweli nchini.

Ulazima wa elimu ya uraia upo sana kwa mwananchi wa kawaida kuelewa dhana ya mfumo wa vyama vingi na umuhimu wake katika uendeshaji wa masuala ya kila siku ya serikali na sio ile maana ambayo ipo kwamba chama cha upinzani ni fujo, kupoteza amani na utulivu wa nchi, hawana sera au ni wapinzani wa kila kitu kumbe maana haswa sio hiyo bali ni waangaliaji wa kile kinachofanywa na serikali na penye mapungufu kukosoa

Ndo maana nasema elimu ya uraia ni muhimu sana katika kuhakikisha kuwa dhana nzima ya chama tawala na chama cha upinzani inaeleweka na nini umuhimu wa kuwepo kw achama cha upinzani katika kuhakikisha kuwa chama tawala kinawajibika kutekeleza sera zake

Kwa nini  vituko kati ya chama Tawala na vyama vya upinzani ni sehemu yapropaganda ya siasa?

Vyama vya upinzani vinatakiwa viendelee kuwajibika, katika mazingira yeyote yale dhidi ya chama tawala lakini kwa busara ili kukubalika miongoni mwa wananchi; chama tawala daima kitakuwa kinajitahidi kuhoofisha upinzani, kufanya uwe dhaifu,  na daima ili kuvipunguza kasi vyama vya upinzani  na kuvifanya kuwa haviwezi kuwa na majadiliano ya kuijenga nchi;

Demokrasia ni demokrasia na daima inataka Pande zote mbili kati ya chama tawala na upinzani kwa  pamoja kuzingatia sheria za mchezo. Demokrasia kama msimamiza wa kandanda ya siasa inapinga vikali wachezaji kucheza “ Rafu” na daima inawategemea wananchi katika kusaidia katika maamuzi ya sahihi na kufanya  kandanda ya siasa kuwa safi; kwa hiyo ni jukumu la wananchi  kuelewa sheria na elimu ya mchezo huu. Tusipofanya jitihada za dhati kabisa katika kulielewa hili  Demokrasia inakuwa fujo.

Ni dhahiri kwamba kama watu wako makini na wanachuikua taadhari , nguvu zote bila kupita katika mikono ya wanasiasa wajanja kitaalamu na waaribifu ambao mara chache hujitashidi kuwarubuni raia ambao hawana elimu ya kutosha na wale ambao wako katika mazingira magumu katika  kutekeleza sera ambazo kuwasaidia kuendeleza utawala wao.

Vyama vya upinzani wakati wote vinatakiwa kuwa na  uwezo wa hoja ili kuweza  kukuza  majadiliano  na mijadala,  na kujitahidi  kuachana na mayowe, hoja za nguvu ili kuviwezesha vyama hivyo  kubaki    katika mijadala ambayo itakuwa na tija kwa wananchi kama mijadala ya afya , ustawi wa jamii na uwajibishaji wa serikali iliyoko madarakani; na bila kusahau kuendeleza aina fulani ya "mazungumzo ya kitaifa" na kushinikiza mjadala wa kidemokrasia kwa kiwango cha juu ya ili kuleta zaidi ukomavu wa demokrasia nchini;

Ili kujiimarisha zaidi miongoni mwa wananchama wao na wananchi kwa ujumla nyama vya upinzani vinatakiwa daima viweze kujisafisha na kuwa na rekodi nzuri ya matumizi ya fedha. Kukumbuke kuwa uwajibikaji uanza ndani ya chama chenyewe; upinzani ili kudumisha uwazi, vinatakiwa wakati wa mikutano yao ya ndani itawaliwe na uwazi; kiwe ni chama cha wote na sio chama cha mtu Fulani au kikundi Fulani cha watu. kuhakikisha matumizi ya fedha za chama kuwajibika ni zaidi ya uwezekano wa kubeba sifa hizi ndani ya utawala wake

Vyama vingi vya upinzani daima vinakabiliwa sana migogoro ya ndani na ukosefu wa Utawala  bora ili kujihakikishia ushindi katika kinyanganyiro cha ushindi wa kuongoza nchi vyama vya upinzani lazima vijenge jitihada  za kichama katika kuimarisha  demokrasia mahiri wa ndani ili iweze kusamabaa baina ya wananchi ambao ndio washika dau wakuu tukumbuke kuwa “ Love starts at home”  kwa kufanya hivyo  vyama vya upinzani vitakuwa vimefanikiwa kutimiza Lengo  la kuimarisha demokrasia ndani ya chama kabla ya kuwa mabingwa wa demokrasia na utawala bora kitaifa. Demokrasia ya kweli  haiwezi kustawi bila upinzani mahiri.




Namaliza kwa kujiuliza je vyama vyetu vya upinzani hapa Tanzania vinafanyaje kazi zake?


vinapingana kwa hoja dhidi ya serikali iliyopo madarakani?


vimeweza kujiimarisha na kutoa elimu ya uraia kwa wananchi waishio vijijini, au vinajikiti katika miji mikuu tu ya wilaya au mikoa?


na wanapotofautia na serikali vinatumia mbinu gani katika kuhakikisha kuwa hoja imefika bila kuvunja amani yetu?


Lakini tusisahau kuwa  "Politics is a dirty game. A good person shouldn't be involved in it."

No comments:

Post a Comment