WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, July 8, 2015

SAA 48 ZA ANAKATWA, HAKATWI

MAKONGORO OGING NA OJUKU ABRAHAM
WAKATI jina la waziri mkuu wa zamani, Edward Ngoyai Lowassa likitajwa kila kona katika kinyang’anyiro cha kusaka nafasi ya kuwania urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), saa 48 zimesalia kufahamu kuwa jina la mgombea huyo litakatwa au halitakatwa katika mchujo wa kwanza, Uwazi linashuka nayo.
Waziri mkuu wa zamani, Edward Ngoyai Lowassa.
Duru za kisiasa nchini zinauangazia mkutano unaowahusisha wajumbe 32  wa Kamati Kuu (CC) ya chama hicho utakaofanyika keshokutwa (Alhamisi) kuwa ndiyo utakaotegua kitendawili cha wagombea gani watapenya kwenye hatua ya Tano Bora na majina yao kupelekwa Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) kwa ajili ya kupigiwa kura ya awamu ya pili.
ITAKAVYOKUWA
Muongozo wa kumpata mwakilishi wa nafasi ya urais kupitia CCM unaonesha kuwa, majina ya wagombea watano yatakayopitishwa na CC yatachekechwa tena na Nec na kuwapata wagombea watatu ambao watakwenda kupigiwa kura na wajumbe wa Mkutano Mkuu  ambapo mshindi mmoja atapatikana na kukiwakilisha chama kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba, mwaka huu.
ANAKATWA, HAKATWI YA LOWASSA INATOKA WAPI?
Pamoja na kuwa ndiye mgombea anayeonekana ana nguvu kwa kuungwa mkono ndani na nje ya chama chake, Lowassa amekuwa katika msukosuko mkubwa wa kisiasa kutoka kwa mahasimu wake ambao wamekuwa wakifanya kila linalowezekana kuhakikisha kwamba mwanasiasa huyo hapewi nafasi ya urais.
Mwenyekiti wa CCM,  D.r Kikwete makamu mwenyekiti Philip Mangula (katikati) na waziri mkuu Mizengo Punda wakifuatilia jambo.
Tuhuma ambazo wamekuwa wakimhusisha nazo ni pamoja na ufisadi, matumizi ya fedha katika kutafuta uungwaji mkono na uanzaji kampeni mapema, mambo ambayo yamewekewa zuio na CCM na hivyo kuwafanya wanaomjengea hoja za kukataliwa kushikilia silaha hiyo kwa lengo la kumdhoofisha matumaini ya kupitishwa na vikao vya chama.
Hata hivyo, wanaomuunga mkono pamoja na Lowassa mwenyewe wamekuwa akipuuza madai hayo huku wakiwataka wanaoshabikia mambo hayo kuweka ushahidi wa kutosha juu ya madai yao, la sivyo waache kufanya siasa za maji taka.
“Nimekuwa mwana CCM tangu mwaka 1977 nilipomaliza chuo kikuu, sijawahi kufanya kazi nje ya CCM. Hivyo nakijua chama na hakuna mgombea atakayeweza kuvunja rekodi ya utendaji wangu katika chama. Sasa leo anayetaka kukata jina langu anatoka wapi? Anakata kwa sababu gani?
Kinana.
“Sioni kosa la kukatwa jina na Watanzania hawaoni. Kwa hiyo msiwe na wasiwasi jina litarudi tu,” Lowassa aliwaambia maelfu ya watu waliojitokeza kumdhamini alipowasili mkoani Ruvuma hivi karibuni.
AKIKATWA ITAKUWAJE?
Mmoja kati ya wafuasi wa Lowassa, ambaye amekuwa akijipambanua pia kuwa ni msemaji wake, Hussein Bashe  amewahi kunukuliwa akisema: “Kama CCM watamkata Lowassa kwa hila watarajie kukutana na nguvu za umma.”
Ingawa Bashe hakufafanua zaidi nguvu ya umma itafanya nini na kwamba mgombea wao atafanyaje jina lake likiondolewa lakini duru za kisiasa zinaonesha kuwa huenda chama hicho kikapata mtikisiko mkubwa kutokana na kile kinachotajwa kuwa  ni Lowassa kuwa na mtaji mkubwa wa watu wanaomuunga mkono.
Katika safari yake ya kusaka wadhamini, mgombea huyo amekuwa akitikisa kwa kupata mapokezi makubwa karibu katika kila mkoa aliyokwenda ambapo ameweza kujikusanyia zaidi ya wadhamini laki nane, ingawa wanaohitajika na chama ni 450 tu kutoka katika mikoa 15.
Dr. Shein
CHAMA KIKOJE?
Kama ilivyo kwa jina lake kuondolewa, Lowassa bado anakiweka njia panda chama chake kutokana na kuwepo kwa makundi ndani ya chama hicho ambayo yanaonesha kuwa hayako tayari kumuunga mkono katika safari yake ya kuingia ikulu.
Yeye waziri mkuu wa zamani, Fredrick Sumaye ameshatangaza mgogoro na chama chake endapo jina lake litaondolewa na kwamba yuko tayari kukihama chama hicho kama dalili za kuwapendelea anaowaita mafisadi zinavyoonekana.
CHANZO: MJENGWA BLOG

No comments:

Post a Comment