WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, July 23, 2014

LOGA AULA MKATABA I YA MWAKA MMOJA SIMBA SC, ATAMBA KUTWAA UBINGWA MSIMU UJAO!

KAMA ilivyotegemewa na kushauriwa na watu wengi, uongozi wa klabu ya Simba chini ya rais Evans Aveva umemsainisha mkataba wa mwaka mmoja kocha mkuu wa klabu hiyo, Mcroatia, Zdravko Logarusic.
Loga amesaini mkataba huo leo makau makuu ya klabu ya Simba, mtaa wa Msimbazi, Kariokoo jijini Dar es salaam na kueleza kuwa kikosi chake kitakuwa bora  msimu ujao, huku lengo kubwa likiwa ni kutwaa ubingwa.
Kitendo cha kupewa kandarasi ya mwaka mmoja kimemfurahisa Logarusic  na kuahidi mambo mazuri kwa mashabiki na wanachama wa Simba katika mikikimikiki ya ligi kuu msimuawa 2014/2015 unaotarajia kuanza septemba 20 mwaka huu.
Makamu wa Rais wa Simba, Geofrey Nyange `Kaburu` ndiye aliongoza zoezi la kumsainisha Loga kandarasi hiyo.
Kaburu alieleza kuwa uongozi umeamua kumpa majukumu kocha huyo na msalaba uliopo mbele yake ni kuhakikisha Simba inarudisha heshima kwa kutwaa ubingwa wa ligi kuu bara.
Kwa upande wa kocha msaidizi, Suleiman Abdallah Matola `Veron`, Kaburu alisema kocha huyo tayari alishasaini mkataba wa miaka miwili tangu mwezi desema mwaka jana, hivyo hakuna mabadiliko.
Awali kulikuwa na taarifa za uongozi wa Simba kumtimua Loga, lakini uongozi umeamua kumbakisha kwa kueleza kuwa wameridhishwa na utendaji wa kazi yake.
Kocha huyo wa zamani wa Gor Mahia ya Kenya alijiunga na Simba desemba mwaka jana na mechi ya kwanza kuiongozo Simba ilikuwa ile ya Nani Mtani Jembe ambapo alishinda mabao 3-2.
Hata hivyo alipoanza kushiriki ligi kuu mzunguka wa pili baada ya kurithi mikoba ya Abdallah Kibadeni, Loga alimaliza msimu kwa kushika nafasi ya nne.
Mcroatia huyo anasifika kwa kuwa na msimamo mkali hasa suala la nidhamu kwa wachezaji.
Mara kadhaa wachezaji walidai kocha huyo ni mkali mno na kuna wakati anashindwa kuwatetea badala yake anawakalipia.

Lakini kwa tamadauni za wachezaji wa Tanzania, nidhamu ya mpira ni ndogo na kocha anayewasimamia sana anaonekana kuwa mbaya.

chanzo: matukiotz.com

No comments:

Post a Comment