WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, June 6, 2012

UFISADI NA WATENDAJI WA SERIKALI


KWA NINI TUMEUINGIZA UFISADI  KATIKA UTAMADUNI WETU WA UTENDAJI KAZI ZA SERIKALI?

Ufisadi kwa uchambuzi wa haraka haraka ni vitendo vya utapeli, udanganyifu mkubwa unaoleta hasara kubwa kwa nchi.
Chimbuko la ufisadi ndani ya nchi yetu ni matumizi mabaya ya madaraka hususa katika matumizi ya pesa za uma na viashiria vyovyote vinavyhohusishwa na matumizi mabaya yanayolenga manufaa binafsi hususa kwa wale ambao wamekabidhiwa madaraka na wana access katika rasilimali ya ya Taifa kulingana na nafasi zao.

Kama mwana zuoni mmoja alivyowahi sema “Ufisadi na rushwa ni adui namba moja wa haki ya wananchi katika kudai uwajibikaji wa viongozi kwa sababu vitendo hivyo viovu vinaharibu kabisa dhana nzima ya uadilifu katika uongozi na hivyo kuhatarisha maendeleo ya uchumi, amani, mshikamano na umoja wa kitaifa”.

NINI HASA KINACHOCHEA UFISADI?

Tanzania ni moja ya nchi za Kiafrika ambazo baada ya kupata uhuru wake ziliweka utaratibu wa kupata viongozi wake wa kuongoza taifa kwa kutumia mfumo wa chama kimoja cha siasa. Wakati huo chama kilikuwa kinaweka misingi thabiti ya uongozi ili kuhakikisha kuwa anayependekezwa na chama kugombea uongozi ni mtu mwadilifu anayeweka maslahi ya taifa mbele. kwa ufupi chanzo cha ufisadi ni:

  • maslahi  binafsi na ya vyama vyao


  • kutotosheka na kile wananchopata kama gawio lao stahiri linalotokana  mishahara na marupurupu mengine ambayo yameainishwa kisheria


  • vitendo vya rushwa, wizi, ukwapuaji au udanganyifu mkubwa wa kupindukia wa fedha na mali za umma unaofanywa na kikundi kidogo cha watu. 

  • kuwawezesha kubaki madarakani kwa gharama yoyote ile hata kama kwa kufanya hivyo kutaathiri kwa kiwango kikubwa uwezo, heshima,


JE UFISADI KWA SASA NI SEHEMU YA UTAMADUNI WETU KIUTENDAJI?

Kwa nini tunaweza kusema kuwa ufisadi umekuwa kama utamaduni wetu?

Kama nilivyoonyesha hapo juu Fisadi mtu au kikundi cha watu ambao anafuja/wanafuja mali za umma bila aibu wala huruma. Ni yuko tayari kuishi maisha  ya hali ya juu bila kusutwa na dhamiri yake.

Dr. Avazaeli Lwaitama yeye anaelezea ufisadi “Ufisadi, kwa maana yenye mashiko kisiasa, ni kushiriki kwenye vitendo vya kupata kipato cha siri kama malipo kwa kutumia cheo chako serikalini au katika chama tawala kufanikisha malengo yakujitajirisha kinyume cha sheria ya mtu au kakundi ka watu”.

Ufisadi unapokuwa ni sehemu kubwa ya utamaduni kwa taifa ni jambo la hatari kubwa sana. Hii ni kwa sababu rushwa, wizi na udanganyifu wa kutisha havitaishia kufanywa na watu wenye mamlaka serikalini peke yake, bali vitendo hivyo husambaa na kujengeka kama tabia ya wanajamii kwa sababu mienendo, vitendo na tabia za watawala huigwa kirahisi na watawaliwa.

Kimsingi ufisadi huwa unaikumba nchi endapo chama tawala kwa wakati husika, hasa kama viongozi, makada na wanachama wake wanajali zaidi maslahi yao binafsi na ya chama chao kuliko maslahi ya taifa lao. 

ATHARI ZA UFISADI NINI?

Kwa hiyo, kama sote hatutaki ufisadi uhatarishe demokrasia ya vyama vingi, amani, mshikamano na maendeleo ya taifa letu, ni vema makundi yote muhimu katika jamii yajitoe mhanga kushinikiza uwajibikaji dhidi ya tuhuma za ufisadi zinazoikabili nchi hivi sasa ili hatua madhubuti zichukuliwe kuhakikisha kuwa wanaotaka kupeleka taifa kubaya hawaogopwi na wanawajibishwa.

NANI ATAWEZA KUONDOA UTAMADUNI HUU NDANI YA SERIKALI YETU?

Kiongozi ambaye anaweza kuwa katika msitari wa mbele wa kupambana dhidi ya ufisadi ni yule aliye msafi kabisa mbele ya ufisadi. Ni mtu yule ambaye haogopi vita hivi maana hajawahi kushiriki katika ufisadi kwa njia yoyote ile. Tena awe ni mzalendo, mkweli na mtu mwenye utu ambaye amejikomboa kutoka kwa vishawishi vya tamaa za ulimbikizaji wa pesa na mali za binafsi ambazo anazitumia kuwatawala, kuwadanganya, kuwanyonyanya na kuwanyanyasa wengine.

Swali katika taifa letu je tuna mtu kama huyu?

Mtu ambaye anaweka masilahi ya kitaifa mbele na anaeishi ili kuishi ili kuboresha maisha ya kila Mkenya kwa kutumia mamlaka aliyo nayo kupigania uhuru, usawa, haki na ukombozi wa taifa lake, huyo anaweza kutegemewa kuongoza mapambano dhidi ya adui ufisadi. Aidha, shujaa wa vita dhidi ya ufisadi anahitajika kuwa jasiri, mtu ngangari, ambaye wakati wowote ako tayari na mbioni kuutafuta na kuupiga vita popote ufisadi popote pale unapojitokeza, hata kama u miongoni mwa watu anaohusiana nao kiukoo, kikabila, kidini, kisiasa au kirafiki. Je, nani katika serikali inayotawala anaweza kuwa shujaa wa kupambana dhidi ya ufisadi kwa kutumia vigezo hivi?

Wadau wa amani ni wale wanaojitoa bila ya kujibakiza kwa ajili ya kutafuta mafao ya wengi, kulinda na kudumisha: haki msingi za binadamu, utu na heshima yake. Lakini, maadui wa amani ni watu wanaoelemewa na ubinafsi, uchu wa mali na madaraka, kiasi kwamba, hata dhamiri zao nyofu zimekufa.

Nyerere alikuwa mkali na alipitisha sheria ya mtu yoyote aliyepatikana na hatia ya kula au kulisha rushwa afungwe na halafu atandikwe viboko 24. “Viboko 12 apigwe akiingia gerezani na 12 akitoka, akamuonyeshe mkewe,” alisema Nyerere.

Pengine hiyo ilikuwa hukumu ya kimabavu lakini hukumu kama hiyo inaashiria ujasiri wa kiongozi na Serikali yake kupambana na rushwa. Daima ujasiri katika uongozi wa nchi huwa unaanzia juu. Pindi kiongozi akishindwa kuwa na ujasiri mapambano kama hayo hayawezi kufanikiwa. Tabasamu za jukwaani wakati wa kuzungumzia masuala mazito ya ufisadi huchukuliwa na wanamtandao wa rushwa kuwa ni mzaha au kwa lugha ya kileo usanii tu.

Kama wanaharakati wengi walivyowahi kusema kuwa, “mpaka atapopatikana Sokoine wa pili, kiongozi atayefanana na Marehemu Edward Moringe Sokoine kwa nia, ujasiri, vitendo na uadilifu”. Kiongozi wa aina hiyo ni yule ambaye ukimuangalia utajua kweli huyu ana uchungu na taifa lake na watu wake. Kiongozi wa aina hiyo atasaidiwa na sheria na uhuru wa Mahakama katika mfumo wa utawala bora utaohakikisha kwamba wananchi wote ni sawa mbele ya sheria. Hivi sasa vyombo vya sheria haviaminiki kwa vile vinaonekana kwamba navyo vimeambukizwa ugonjwa wa rushwa.

Tatizo sugu la rushwa ni kubwa mno na haliwezi kumalizwa kwa siasa hizi za ahadi hewa na kuwakumbatia viongozi wabovu na wasiojali kabisa wananchi wa Tanzania. Je Muswada wa kutenganisha biashara na siasa umefanikiwa kwa kiasi gani?

Katika hali hii ya uzalendo ya kuipenda nchi yake na kujitoa muhanga kwa ajili ya wanyonge wa taifa lake Mwalimu Nyerere alikuwa mfano katika mapambano haya kwa dhati kabisa na bila kujali masilahi binafsi mpaka anaachia madaraka kwa msingi huu name naungana na wanazuoni walio wahi sema kuwa 

  • “ Acheni Mwalimu Nyerere aitwe Mwalimu hakuna kama yeye enzi hizi na kama yupo ajitokeza hadharani na kufanya mabadiliko makubwa ya kiuongozi na kiuchumi”.

No comments:

Post a Comment