WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, June 25, 2012

JE BUNGE LETU LINA VIONGOZI WENYE SURA MBILI?



Kuna mwanasiasa mmoja mkongwe aliwahi sema katika moja ya mikutano yake kuwa; “Msishangae, tuna viongozi wenye sura mbili, wapo wanaofikiri kwa kutumia matumbo yao jinsi ambavyo wataneemeka na kujinufaisha wenyewe, hawa ni wale wabinafsi lakini wapo viongozi ambao wanatumia ubongo katika kufikiri jinsi ambavyo watatumia uwezo wao wote katika kuwatumikia wananchi, mimi ni miongoni mwa hawa,” 

Mwannasiasa mwingine naye aliwahi sema kuwa “Mawaziri ni lazima wajenge umoja na wakubali uwajibikaji wa pamoja. Katika uwajibikaji wa pamoja, hakuna wa kuwaruka wenzake.”

Na aliendelea kusisitiza kuwa “uadilifu si usomi, bali ni tabia akisema hivi sasa bungeni kuna vijana wengi tu waliosoma kuliko enzi zao, lakini linazidi kupoteza hadhi yake. Alisema viongozi wanaochaguliwa wanapaswa waache baadhi ya mambo ili kulinda hadhi yao...Huwezi kuwa mbunge au jaji halafu unakwenda baa unalewa hadi unaning’iniza miguu juu.”

Naungana na mheshimiwa mmoja mabaye aliwapa rai wabuge au wanasiasa wenzake kuwa “Lazima wanasiasa wa Tanzania tubadilike, kulaumiana na kunung’unika tu hakutusaidii. Leo wananchi wananung’unika na viongozi wananung’unika, kinachotakiwa ni kutafuta majibu.”

Lakini tukiangalia mbali kwa faida ya Taifa letu a tukiangalia utendaji wa wanasiasa wetu hasa wakiwa bungeni, kuzomeana, kulaumiana, kunyosheana vidole, hakutatuvusha katika maisha bora tunayoyafikiria kwa faida ya Taifa letu, nafikiri itastusaidia sana kama tafakari ya maisha bora itaanzia kwa waheshimiwa wabunge ambao wanabeba dhamana kubwa ya maisha ya watanzania;

Katika maisha ya kawaida ya binadamu na wabunge wetu wakiwa ni sehemu ya binadamu hawa ni ukweli ambao haufichiki kuwa hata waheshimiwa wabunge wana vibanzi au mapungufu ambayo wanayaona kwa wenzao na sio kwao, tukifanya tathimini ya kichama; na kujihesabu wao kama chama wako safi na wana hoja ambazo zinakidhi haja na wenzao wananamapungufu kihoja au katika kuleta utatuzi wa tatizo; matokeo yake mchango wa mbunge mwingine hugeuka kichekesho kebei na hatimaye kuhatarisha mwenendo wa mjadala.

Bunge imara linajengwa katika msingi wa uwazi kwa kukosoana na kuheshimiana kihoja; ushindani na uchambuzi wa hoja ni sehemu muhimu sana katika kusaidia Taifa kusonga mbele; wabunge wote hawawezi kamwe kuwa na mtazamo wa pamoja; Mwenyezi Mungu ametujalia vipaji tofauti katika kufikiri na katika kutatua matatizo; Waheshimiwa wabunge wetu  ni lazima wajifunze kujenga bunge lenye ushindani wa hoja kama sehemu ya  kutatua matatizo mbalimbali. Tutaweza kushinda tu kama tutafanikiwa kujenge jamii inayotafakari na si jamii ya kulalamika kila wakati na kuishia kutukanana bila aibu.

Tunafahamu kuwa Bunge ndicho chombo cha kutunga sheria na muhimili mkuu sana wa uchumi kutokana na michango yao bungeni hasa wakati huu wa bunge la Bajeti. Bunge linatakiwa liwe na uwezo wa kuchangia na kuandaa mazingira yanayofaa kwa maendeleo yetu. Lakini Kama Bunge halina   uwezo wa kuyaangalia matatizo ya nchi hii na kuyatafutia ufumbuzi, basi, kuna tatizo kubwa katika jamii yetu, kuna tatizo kubwa ambalo kama tukibweteka, litatutafuna sisi na vizazi vijavyo.

  • Je ni kweli kuwa wabunge wa chama tawala wanatanguliza maslahi ya chama chao kabla ya kuangalia na kuwakilisha matatizo na hoja za wananchi waliowapigia kura?


  • Je ni kweli kuwa wabunge wa upinzani ndio wabunge wanafanya jitihada kubwa za kuleta hoja za maendeleo bungeni?


  • Au wote kwa pamoja na wabunge wetu  wanaamini kuwa wao wanaostahili kula kwanza kisha wananchi wale baadaye?


  • Je  kama hivi ndivyo  baadaye hiyo ikifika kunakuwa hakuna zaidi ya makombo na ukoko uliobakia?


Nafikiri linalowezekana leo lifanyike leo kwani hakuna kesho katika maendeleo ya binadamu kwani sisi tunaishi leo na sio kesho; kesho inabaki katika hazina ya Muumba wetu tu;

Baba wa Taifa aliwahi kusema kuwa “Kupanga ni kuchagua”. Je wabunge wetu wanapanga nini kwa maasilahi ya jamii? inatupasa kuwakumbusha waheshimiwa wabunge  watambue kwamba chochote wanachokipanga na kukitekeleza ambacho hakiongezi uhuru na umoja wetu wala hakina manufaa kwa walio wengi sio kitendo cha maendeleo.

Kwa nini kila kikao cha bunge Bunge kinachofanyika tunaendelea kuona kuwa Bunge letu Tukufu  linakuwa ni jepesi mno katika kuwapigania wananchi? Hoja nyingi zinazotolewa hazilengi sana katika kumnufahisha mwananchi kumwondoa katika tope alilonaswa la umasikini? 

Je tunafaidika nini kama waheshimiwa wabunge baada ya kujadili hoja kwa kumletea maendeleo mwananchi wa kawaida wanajadili hoja namana ya kukomoana wao wenyewe;  kama bunge letu litaendelea hivyo basi itatupasa kuamini kuwa baadhi ya mambo yanayofanywa na Bunge hili hayana tija kwa maendeleo ya Taifa letu. Wabunge Wasisahau kuwa Wabunge wanapokuwa bungeni wanatumia fedha za walipa kodi. Je hilo linawauma na wanaojiona wanafiki na waongo pale wanaposhindwa akutimiza wajibu wao? Kama inawauma na kuwakereketa ni vyema basi kila wakiwa bungeni lazima watumie kwa tija pesa ya mlipa kodi mnyonge ambaye hakwepi kodi ili kumnufaisha huyu anayewakilishwa na kumfanya aweze kuishi vizuri huko bungeni wakati wote wa kikao cha Bunge.

Nafikiri kama wabunge Kuna haja ya kuweka mbele mjadala wa  maslahi ya taifa letu. Tumeshaona na kusikia tabia mbaya wa baadhi ya mabunge ya wenzetu kupigana bungeni, kutukanan lakini hapa kwetu kwa waheshimiwa wabunge kuiga tabia hii nafikiri sio jambo njem; majadiliano ya amani kuhusu hoja mbalimbali za kumkomboa Mtanzania sitasaidia zaidi katika kuleta umoja wa kitaifa na itatusaidia kama taifa kuweka  maslahi ya taifa letu.

Inafurahisha pale tunapowaona waheshimiwa wabunge bila kujali chama wakikubaliana hoja za msingi ambazo zinasaidia kujenga uzalendo wa kutetea maslahi ya  ya watanzania  ambayo hayafungamani na chama chochote cha siasa wala dini. Bunge letu likiweza kufanya kazi yake katika msingi huu kuondoa taswira ya BUNGE LENYE SURA MBILI NA MBAYA ZAIDI LINALOANGALIA MASALAHI BINAFSI YAKUWANUFAISHA WAO NA KUTOKUMJALI MTANZANIA WA KAWAIDA AMBAYE NDIYE AMEWACHAGUA NA UNASALITIWA.


MUNGU IBARIKI TANZANIA

No comments:

Post a Comment