WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Friday, June 29, 2012

HEBU TUJIKUMBUSHE HII NA MGOMO WA MADAKTARI NA MATUKIO YANAYOENDELEA SASA;


MIGOMO NA KUKOSEKANA KWA EFFECTIVE COMMUNICATIONS


KWA NINI SWALA LA MIGOMO LINACHUKUA MUDA MREFU KUPATA UFUMBUZI?

Kama wataalamu wengi walivyowahi kusema huku nyuma kuwa chanzo cha migomo mingi kutokea na kuchukua sura mpya inatokana na  kupungua kwa mawasiliano miongoni mwa  pande mbili ambazo zinatofautiana au kama kuna mawasiliano mawasiliano hayo yanakuwa hayakubaliki kwa upande mmoja au kutohusishwa moja kwa moja katika majadiliano husika katika  kututua tatizo husika. 

Tatizo wakati mwingine wakati wa majadiliano mhusika mkuu mara nyingi Serikali  anachokizungumza pengine kinatia mashaka ya ukweli wa suluhu;  Baba Wa Taifa akikuwa akisuluhisha Mgomo  wengi walikuwa wakijenga imani  kwani  alichokuwa akikiongea unaona kabisa anachosema ndio anachomaanisha. Tofauti na viongozi wetu wa sasa mara nyingi wanachoongea na hali halisi ni tofauti kwani wanachukua mno hali ya kujilinda zaidi  na mbaya zaidi wanakimbilia kutupa taarifa ambazo zinaongeza wasiwasi baada ya kutatua tatizo.

Nafikiri katika hali yeyote ile serikali kama msimamizi wa sera na  taratibu za maisha ya watanzania katika hali ya migomo  ambayo imeendelea kujitokeza katika taifa letu, tunahitaji uthubutu katika kutatua tatizo hili;

Katika sakata la mgomo wa serikali na  madaktari ambao umedumu kwa takribani wiki tatu sasa;

  • Swali ambalo tunahitaji kujuuliza leo ni hili  Hivi serikali imeonyesha nia ya kumaliza mgogoro huo katika meza ya majadiliano mapema?

  • Je madaktari  wanajisikia vipi wakiona ndugu zao marafiki au watanzania wakipoteza maisha kwa kukosa hudumu muhimu ya afya ikiwa ni  sehemu haki ya wananchi kikatiba?

  • Nafikiri Majadiliano na maelewano ni sehemu muhimu katika kufikia muafaka wa migogoro

Hii ni vita ya mafahari wawili na wanaoumia kwa kiasi kukubwa ni wananchi ambao hawana kosa pamoja na mchango mkubwa mkubwa wa kodi zao wameishaia kupoteza maisha na kwa mvutano unaoendelea;

 Ni kweli kuwa Ikumbukwe kuwa, serikali ikitenda wajibu wake na  na kutoa haki kwa wahusiaka bila upendeleo  kwa wakati  sahihi kwa kila jamii ambayo inahusika kulingana na tatizo linalosababisha mgomo. Migomo mingi ambayo inajitokeza katika taifa letu inahusiana na tatizo la uwiano wa masilahi (mishahara) katika jamii pale panapotokea  tofauti ya mishahara iliyowekwa kwa makusudi ya kuwapa nafuu wafanyakazi wa kundi moja ndiyo inayotumiwa katika kudai nafuu ya wajibu na haki kwa kundi lingine.

Pengine hata swala la mgomo huu wa madaktari katika kipindi hiki unaweza kusababisha na mvutano wa posha za viongozi wetu watunga sheria (wabunge) ambao walitaka walipwe posho ya shilling 200,000 kutoka elfu sabini;(70,000) hii ni assumption moja ambayo imekuwa kichocheo cha mgomo;

Kama ni kweli kwa nini  wanasiasa  wanajifikira sana wao wenyewe na kujijengea hoja na kubeza hoja za wananchi  au makundi mengine ndani ya jamii hasa wanapozungumzia masilahi;  ni ukweli ambao haufichi kuwa wanasiasa ambao ni watawala amabo tumewapa dhamana ya kutuongoza  mara nyingi wanajitengenezea masilahi bora, posho  nono na marupurupu mengine yanayowafanya waishi maisha bora na pale wanapoumwa na familia zao wanatibiwa nje ya nchi. 

 Mwalimu Nyererealiwahi sema kuwa , “leo ukigoma unamgomea nani; tafakari matokeo!”  Jibu ni rahisi kada zinagoma kwa kukosa majibu sahihi ya maswali yao, na kukosekana kwa effective communication ya madaia husika.

Mwalimu Nyerere kwenye alitukumbusha kuwa , “Wafanyakazi wa Tanzania wanayo haki ya kuheshimiwa na wafanyakazi wengine na wananchi wote. Lakini kwa heshima yao wanayoipata, lazima wafanyakazi wote wakubali kufanya kazi kwa bidii. Ndiyo kusema kwamba kila mfanyakazi lazima afuate masharti ya kazi anayopewa. Kama kwa sababu fulani hayapendi masharti hayo, anaweza kupeleka shauri hilo katika kikao kwa utaratibu uliokubaliwa. Lakini kwa sasa lazima atafuata masharti yaliyopo.”

Tatizo la wakati wetu tabaka la masilahi bora linaongezeka na kusababisha  migomo  miongoni mwa jamii; kwa viongozi wetu na wanansiasa wetu nafikiri ni wakati mwafaka wa kuitafakari hali hii na kuijengea mikakati ya kuhakikisha kuwa migomo inatokomea kabisa ndani ya jamii zetu; Hakuna lisikowezekana; Pamoja tukisima tutaendelea kwa faida ya wote

No comments:

Post a Comment