WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Thursday, March 1, 2012

TANZANIA BILA UCHAFU INAWEZEKANA


JE TATIZO LA UCHAFU WA MAZINGIRA UNAOKABILI MIJI YETU NI SEHEMU YA UTAMADUNI WETU?

Tatizo la uchafu wa miji yetu ukiongwozwa na jiji la dare s salaam  limeendelea kuwa ni kero kubwa sana katika jamii yetu; kama wananchi wengi na wanaharakati wameendelea kusema kupiga kelele na kuandika kuwa  “ Kama kuna suala ambalo linakera pia ni uchafuzi wa mazingira. Sio kwamba huwa ni kero tu, lakini uchafu huleta magonjwa mbali mbali na hatimae vifo ambavyo mara nyingi ni vya kujitakia.”



Najiuliza leo tatizo letu kama watanzania ambao tumesherekea miaka 50 ya uhuru wetu kwa amani na utulivu lakini kwa upande mwingine sherehe zilizozungukwa na uvundo wa taka kila mahali sisi kama watanzania tumekosa nini au ni nini tunashindwa kufanya ili hata kupunguza tatizo hili?

Je serikali yetu na viongozi wake hawalione hili, na hali wakeri? Au wao wanaishio katika nchi nyingine tofauti nah ii tunayoilalamikia? Au wako kwenye ya kufikirika ambako wao uchafu hauwakeri na wanashindwa kuusimamia?

Je ni tatizo la pesa za kusiamamia usafi au zile kidogo zinazopatika zinatumika bila kuangalia kipaumbele? Je  miji yetu lina itaweza kuandaa utaratibu mzuri wa kuwa na Vifaa Vya Kuwekwa Takataka hii itakuwa na mwanzo mzuri wa kuanza kuwaelimisha wananchi utaratibu na kuwezesha  Kila  mtu kuweza kutupa  taka taka Popote Alipo.  Wananchi wasipoweza kutafutiwa utaratibu wa kuweza kuwa na ukahika wa wapi watupe takataka tutawapa sababu ya kutoana  kama kuna sababu ya Kujali Usafi Wa Miji miji husika. Je Usafi Wa Miji Yetu Tanzania Inahitaji Pesa Za Kigeni?  Tufanye Nini Ili Tutunze Usafi Wa Miji Yetu

JE TATIZO LA  KUKITHIRI KWA UCHAFU JE VIONGOZI WETU WANAHUSIKA?

viongozi hawawezi kukwepa jukumu lao katika hili Tusijaribu kuwavua wajibu viongozi wetu. Uchafu unaanzia kwao. Je uongozi wa miji yetu kwa nini usiwajibishwe? Kwa nini tunawalaaumu viongozi wetu ? kwa falfasa ya kirahisi tu tunawaona viongozi wetu wanaonyesha kabisa haw anjali kwani wao wanaangalia sasa na sio chanzo. Watasimamia usafi  kwa ajili ya kiongozi mwingine  anayekuja  wa nchi tofauti  kusafisha mazingira na kupamba mji, lakini, baada ya hapo uchafu unabaki pale pale. Hii ni aibu kwetu. Je hata kuweka vifaa vya kutupa taka ndani yake inashindikana? je hata kutunga sheria ndogo za kuwajibisha wachafuzi wa mazingira inashindikana?

Elimu ya usafi wa mazingira yafaa iwashirikishe watendaji wote kuanzia ngazi za chini katika serikali za mitaa, kata hata tarafa. Kama taifa tunahitaji wananchi waelemishwe vya  kutosha kwa wananchi kuhusu usafi wa mazingira. Kwa mfano uchafu katika jiji la Dar es Salaam na vitongoji vyake ni moja ya matatizo makubwa na ambayo ni dhahiri uongozi wa jiji hili unaelekea kuwa umeshindwa kulipatia ufumbuzi. 

JE NINI KIFANYIKE KATIKA KUTATUA TATIZO HILI KWA JUMLA;

Je tunazo sheria za kusimamia usafi wa mazingira?  
Je sheria zetu zinawabanaje  wafanyabiashara ndogondogo ambao wamekuwa wakijiendeshea shughuli zao mahali popote wanapojisikia na sehemu ambazo si rasmi na kufanya kuacha taka ngumu katika maeneo ya  biashara zao?

Je miundo mbinu yetu inafanya kazi vizuri au hatuna mfumo taka  unaoeleweka? Je gharama za kusafisha vyoo vilivyojaa mwananchi wa kawaida amaweza kumudu? Kama hawezi kumudu sheria zetu zinawaruhusu kusafisha vyoo vyao/au kuzibua wakati wa mvua?
Je ushuru amabao wananchi na wafanya biashara unatumika katika kufanya usafi au matumizi makubwa ya ushuru huo unatumika kwa matumizi ya kiofisi?

Kama mwanaharakati mmojai alivyowahi andika kuwa “ Swala la uchafu kukidhiri Dar ni watu kutowajibika Ufisadi tu watu wanalipa ushuru lakini Halimashauri ya jiji wanatupia tumboni.Kama jiji Chafu basi hata watu wenyewe usafi wao binafsi ninawasiwasi mno.Hata hivyo usafi si kila mtu anaweza. Uchafu na harufu mbaya katika jiji hilo umekuwa ni jambo la kawaida, hali hiyo inalitofautisha jiji hilo lenye hadhi Tanzania na majiji mengine makubwa duniani.” 

Waziri wetu Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda (Mtoto Wa Mkulima) baada ya moja ya ziara zake za kutembelea Jiji la Dar es Salaam  aliwahi sema kuwa “hali hairidhishi, Hali hii isipochukuliwa hatua haraka na kupewa kipaumbele kamwe magonjwa ya milipuko kama vile kichocho na kipindupindu hayatodhibitiwa na watu wataendelea kupoteza maisha kwa vitu ambavyo kama kuna mkakati mzuri vinaweza kudhibitiwa”.

MTAZAMO KWA UJUMLA

Tunaweza kufanya miji yetu kung’ara kama kila mtu atajitahidi kuwajibika na kujijengea utamamduni mpya wa kutunza mazingira, na kukataa tabia ya kutupa taka ovyo na kila mtu kuwa mlinzi wa mwenzake na kumkemea yeyoye ambaye atakuwa na tabia ya kutupa taka ovyo;

Wananchi wawajibike kwa upande wao na viongozi wetu nao wawajibike kwa upande wao kwani wao  ndio msingi wa kufanikisha zoezi nzima kwa kuweza kufacilitate utaratibu,

·        Kuandaa sheria ambazo zinatekelezeka;

·        Kuandaa vifaa vya kuwekea taka katika sehemu mbalimbali za jiji ili kuwarahisishia wananchi kutupa taka  na kuwapunguzia wananchi ushawishi wa kutupa taka ovyo;

·        Viongozi waandae magari yanayotakiwa kwa ajili ya kubeba taka na sio magari ambayo baada ya kuondoa tatizo la taka, yanaongeza uchafu kwa kutupa uchafu kila yakiwa yakipita na taka.

·        iko haja ya kuwekwa kwa sheria kali za kudhibiti kwanza utupaji taka hovyo kama ilivyo katika miji mingine ya kitaifa na sheria hizo zisiwe mapambo, bali zitumike kwa vitendo kwa wahusika kuchukuliwa hatua ikibidi kutangazwa ili iwe ifundisho. 

·        Viongozi waweze kuona aibu ya miji yetu kuwa michafu na inanuka

Kama tatizo la uchafu litaendelea kuwa ni tatizo sugu kwa taifa letu swala hili litakuwa ni aibu kwa taifa zima na si kwa wakazi miji husika; kama taifa tuweze kuwatumia wataalamu waliopo  kuwaomba kuaandaa  mikakati bora ya utupaji taka ikiwa ni pamoja na kutenga maeneo maalumu kwa ajili ya kutupia taka ambayo hayapo katika maeneo ya makazi ya watu.

Nafikiri sio jambo la busara kuendelea kutupiana lawama, ni vyema kwa pamoja serikali na wananchi wakakutana kama wadau na kujadiliana namna ya kuondokana na aibu hii. Kwa kufanya hivyo tutaweza kuliepusha Taifa na magonjwa ya mlipuko na kulijengee taifa usalama wa afya  za wananchi.



Naamini kuwa usafi hauhitaji kwenda shule au  ufadhili kutoka nje; bali yatupasa kubadilisha tabia na utamaduni wetu; tunaweza kubadilisha tabia zetu na kubadilisha maisha yetu ya kutoka kuzungukwa na uchafu na kuwa taifa safi na litakalo heshimika kwa utunzaji wa mazingira.

TANZANIA BILA UCHAFU INAWEZEKANA

No comments:

Post a Comment