WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, September 12, 2011

SALAMU ZA RAMBI RAMBI KUFUATIA AJALI YA MELI ZANZIBAR


Kwa niaba ya Blogu ya Ukadirifu na Mungupamojanasi,  tumopokea kwa mshituko mkubwa sana na kwa majonzi makubwa sana taarifa kufuatia ajali ya kuzama kwa Meli “ MV  Spice Islander” ambayo ilitokea huko Nungwi tarehe 10/09/2011;  ambayo imesababisha vifo vingi vya watanzania wenzetu ambao walikuwa wanasafiri kati ya Dar es salaam, Unguja na Pemba.



Tunatoa salamu zetu za rambirambi kwa wahanga wote wa ajali hii, ambao wamepoteza wapendwa wao, ndugu  na marafiki.

Tunatoa salamu zetu kwa viongozi wetu wakuu wan chi Rais wa Serikali ya Mapinduzi Dr Ali M. Shein, Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dr. Jakaya Mrisho Kikwete;
Tunatoa shukrani na pongezi za dhati kwa wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine katika harakati za  kuokoa maisha ya waanga wa ajali hii na vile viele katika shughuli za kuopoa maiti;

Mwenyezi Mungu aendelee kuwapa, nguvu na faraja ndugu zetu ambao wameguswa na msiba huu mkubwa  na katika kipindi hiki chote kigumu ambacho kipo mbele yetu;


No comments:

Post a Comment