WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Friday, September 23, 2011

KAULI YA WAZIRI MKUU MHESHIMIWA MIZENGO PINDA KUHUSU UTENDAJI WA POLISI NA SAKATA LA SUKARI


POLISI WANAPOSHINDWA  KUSIMAMIA SHERIA NA WAJIBU WAO; FIKRA YAKO NI IPI?

Polisi ni chombo cha serikali chenye nguvu ya kisheria ya kuhakikisha kuwa sheria zinafuatwa, na usalama wa raia na mali zao unakuwepo.

Maswali ambayo sisi raia tunajiuliza leo kama polisi wanalindwa na sheria ya kuhakikisha kuwa nchi inaendelea kubaki salama;
Je Polisi wanaposhindwa kuwajibika kinyume na kiapo cha utii wa sheria zilizowaweka kazini kwa kushindwa kuitumikia nchi na wananchi wake kwa uadilifu nini kifanyike? Kuyahamisha majukumu yao kwa chombo kingine cha ulinzi au kuwawajibisha?
Je tuwafanye nini baadhi ya polisi wanaotumia lugha za ubabe, vitisho na kutumia nguvu hata wakati hakuna sababu ya kutumia nguvu kutatua katika utendaji wake.

Je polisi wetu  wanatumiaje mafunzo yao  katika kuwaelimisha raia kuhusu makosa mbalimbali yanayofanyika, kwa sababu sio makosa yote yanapelekwa mahakamani?

Je askari wetu wanauhusiano wa namna gani  na jamii inayowazunguka? Je polisi wetu wanatumia sheria zaidi au ubabe katika kushughulikia kero za raia wake?

"Je polisi anapomiliki biashara  kama daladala anaweza kusimamia sheria vizuri ambayo inahusiana na biashara yake hiyo ya daladala pale uvunjaji wa sheria ukitokea?"


Je polisi wetu ni msaada kwa raia wenye shida kama inavyofanyika katika nchi nyingine au ndo wanakuwa chanzo cha kero?
je ni jakumu la askari yeyote ambaye anayefanya doria dhidi ya majambazi  ni lipi au anaruhusiwa pia kufukazana na wakosaji wangine kama “daladala” kwa wakati mmoja?

Je ni sahihi kwa polisi kusindikiza magari ambayo yanabeba magendo kama swala la sukari hivi sasa? “ escot ya Mzigo”? Kilio cha waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda katika ziara yake huko Mara jinsi polisi wanavyoshiriki kuhujumu uchumi wa nchi.

Nafikiri itakuwa vyema kama  polisi wetu wataendelea kuwa rafiki wa raia wema ili kuwawezesha kupata ushirikiano katika kubaini wahalifu. Tunazidi kuwaomba  waendelea kufanya kazi zao kwa kufuata sheria na kiapo chao.UWEZO kuchapa kazi vizuri wanao, SABABU wanayo kuendelea kulinda amani; tatizo tu NIA inachechemea pengine kwa sabau ya uduni wa masilahi basi tunaiomba na serikali yetu iliangalie hili la masilahi bora kwa polisi wetu.

No comments:

Post a Comment