WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Tuesday, August 5, 2014

Ukawa wawatia kiwewe Wassira, Mwigulu, Lukuvi




Moshi/Dar. Mawaziri Stephen Wassira na Mwigulu Nchemba wamesema kuwa japo Bunge Maalumu la Katiba litaendelea na vikao vyake kuanzia kesho mjini Dodoma, halitakuwa na uhalali wa kisiasa.

“Tunakwenda bungeni kuendelea na vikao kwa sababu hatuvunji sheria. Kumbukeni hata walipotoka (Ukawa) wakati ule tuliendelea na vikao kwa sababu akidi inaruhusu, japo hatutakuwa na uhalali wa kisiasa lakini kisheria tuna uhalali,” alisema Wasira ambaye ni Waziri wa Nchi (Ofisi ya Rais, Uratibu na Uhusiano).
Hoja hiyo ilisisitizwa na Nchemba ambaye ni Naibu Waziri wa Fedha kuwa vikao hivyo havitakuwa na uhalali wa kisiasa japo kisheria vina uhalali.
“Unajua kilichosababisha mkwamo huu ni kila kundi kushikilia upande wake, kama kila kundi lingeweka masilahi ya Taifa tusingefika huko. Tunakwenda bungeni, ingawa hakutakuwa na uhalali wa kisiasa lakini tutaendelea kujadili mambo ya kitaifa,” alisema Mwigulu.
Viongozi hao walisema hayo baada ya mdahalo wa Katiba uliofanyika Dar es Salam jana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi akisema wanakwenda bungeni kuendelea na mijadala japo katiba haitakuwa na afya... “Nawaomba Ukawa warejee bungeni, ikishindikana sisi tutakwenda, tutajadiliana, tutawaletea Katiba bora ila haitakuwa na afya bila Ukawa.”
Wengi waendelea kupinga Bunge
Mbali na mawaziri hao, idadi ya wajumbe wa Bunge hilo wanaopinga vikao hivyo kuendelea bila kushirikisha wenzao wa Umoja wa Bunge la Wananchi (Ukawa) inazidi kuongezeka.
Maoni ya wajumbe hao, baadhi yao wakiwa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano kutoka CCM, yanatokana na Bunge la Katiba kugubikwa na giza nene baada ya Ukawa, kusisitiza kuwa hawatashiriki vikao hivyo.
Maoni ya wajumbe hao, baadhi yao wakiwa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano kutoka CCM, yanatokana na Bunge la Katiba kugubikwa na giza nene baada ya Ukawa, kusisitiza kuwa hawatashiriki vikao hivyo.
Mbunge wa Ludewa (CCM), Deo Filikunjombe alisema jana kuwa haungi mkono mpango wa wabunge wenzake wa CCM kuendelea na Bunge la Katiba bila maridhiano.
“Pengine niwakumbushe wabunge wenzangu wa CCM kuwa kinachoandaliwa kwenye Bunge la Katiba ni Katiba ya Watanzania wote na si Katiba ya CCM. Hatua tuliyofikia siiungi mkono, kitendo cha wabunge wenzangu wa CCM kuendelea na mchakato wa Katiba Mpya kwa sababu suala la Katiba halina mshindi ni jambo la maridhiano.
“Kitendo cha sisi wabunge wa CCM kuendelea na mchakato wa Katiba Mpya ni matumizi mabaya ya wingi wetu mle bungeni. Ni kweli CCM ina wabunge wengi na ni kweli kwenye demokrasia wengi wape, lakini pia demokrasia pevu na yenye tija ni ile inayoheshimu na kuyafanyia kazi maoni ya wachache.”
Hata hivyo, mbunge huyo alisema wajumbe wa Ukawa walipaswa kubaki ndani ya chombo hicho na kujenga hoja zao.
“Ni lazima (Ukawa) watambue sisi wajumbe siyo waamuzi wa mwisho. Tutafanya yote lakini waamuzi wa mwisho ni wananchi kwani ndiyo wanaoweza kupiga kura ya kuikataa au kuikubali,” alisema.
Mjumbe mwingine wa Bunge hilo, Maria Sarungi alisema Katiba inapaswa kuwa mkataba wa pamoja lakini bila maridhiano inakuwa ni waraka unayokosa uhalali wa kukubalika kwa jamii.
Mbunge wa Kahama (CCM), James Lembeli alimsihi Rais Jakaya Kikwete kuangalia njia bora ya kunusuru fedha za walipa kodi maskini zinazotumika katika mchakato wa Katiba Mpya.
“Kama Katiba ni ya wananchi tulipaswa kuwa kitu kimoja, kwamba tunaingia mle ndani kwa masilahi ya Watanzania lakini kama hakuna mwafaka hadi sasa huko mbele ni giza nene.
“Kwa maoni yangu hekima itumike. Ni busara tu imebaki kwa wakubwa kuona fedha za Watanzania zinatumika vizuri. Rais Kikwete awatazame Watanzania kwa macho ya huruma,” alisema.
Mbunge wa Mchinga (CCM), Said Mtanda alisema wajumbe kutoka CCM wanaweza kuendelea na vikao vya Bunge la Katiba, lakini lingekuwa jambo muhimu iwapo yangefanyika maridhiano ya pande mbili zinazovutana.
“Kama akidi itatimia vikao vitaendelea kama kawaida. Lakini hata kama itatimia nadhani si busara vikao vya Bunge kuendelea kwa mtindo huo, binafsi naona turidhiane ili kunusuru hali hii,” alisema.
Hata hivyo, Mtanda aliwataka Ukawa kutambua kuwa si lazima kila jambo wanalolitaka litakubaliwa na kuwa iwapo watashikilia msimamo huo ipo siku wananchi watawahukumu.
Mbunge wa Longido (CCM), Lekule Laizer alisema lingekuwa jambo la busara kama vikao vya Bunge hilo vingeitishwa baada ya pande mbili zinazovutana kukubaliana.
Mbunge wa Nzega (CCM), Dk Hamisi Kigwangalla alisema, “Yangefanyika maridhiano kwanza na kama hilo litashindikana ni vyema viongozi wa vyama vya siasa wangeondolewa kuwa sehemu ya Bunge hili, ili kuondoa hali ya kila upande kuvutia kwake.”

Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Anne Kilango alisema hata bila Ukawa vikao vya Bunge hilo vitaendelea kwa sababu wajumbe wa kundi hilo walisusia kikao cha maridhiano kilichoitishwa na Mwenyekiti wa Bunge la Katiba, Samuel Sitta.
“Bunge la Katiba lina wajumbe 629 na kama Ukawa wasipokuja sidhani kama watazuia vikao kuendelea kwa sababu hata watu 100 hawafiki. Kikao cha Sitta ndicho kilikuwa kizuri kwa maridhiano,” alisema Kilango
Mbunge wa Nkasi Kaskazini (CCM), Ali Keissy alisema, “Katiba ni ya wananchi wote ni vyema tungekubaliana kwanza.”
Tangu wajumbe wa Ukawa kususia Bunge, baadhi ya wajumbe, wakiwamo wabunge wa CCM wamekuwa wakitoa maoni yanayoonyesha kuwa bila wenzao hao, katiba itakayopatikana haitakuwa ya kidemokrasia.
Miongoni mwa wabunge hao ni Ridhiwani Kikwete wa Chalinze alisema katika mahojiano maalumu na gazeti hili kuwa iwapo wajumbe wa Bunge la Katiba kutoka CCM watalazimisha mambo bila ushiriki wa wenzao wa Ukawa, kuna hatari ya kupata Katiba isiyokuwa na misingi ya kidemokrasia.
“Kwa mazingira tuliyonayo wabunge wa CCM wanaweza kuamua kwamba walazimishe vitu, lakini ile misingi ya demokrasia haitakuwapo,” alisema Ridhiwani na ambaye pia ni mtoto wa Rais Kikwete na kuongeza: “Kwa sababu kupata Katiba ya kidemokrasia ni lazima taratibu zifuatwe na Ukawa washiriki, lakini bila wao kushiriki huwezi kusema Katiba tuliyopata ni ya kidemokrasia, tutakuwa tunajiongopea.
“Wao (Ukawa) wasipokuja na kama busara ya viongozi wetu wa chama, busara za Bunge letu na busara ya Rais itatuonyesha kwamba tukutane tu na tujadili, sisi tutakuja, tutajadili na tutaipitisha lakini mwisho wa siku, ule uhalali wa document (kilichopitishwa) hautakuwepo.”
Wiki iliyopita gazeti hili liliwanukuu wabunge wengine wa CCM wakipendekeza kusitishwa kwa Bunge hilo ili kutafuta maridhiano kwanza.
Miongoni mwao ni Charles Mwijage (Muleba Kaskazini) ambaye alisema, “Kukosekana kwa Ukawa bungeni kutaathiri upatikanaji wa Katiba Mpya...Ningekuwa na uwezo, ningeamua mchakato huu usitishwe na tuendelee kutumia Katiba iliyopo kwa sababu suala hili linahitaji zaidi maridhiano,” alisema.
Mjumbe mwingine, Ezekiah Oluoch (Kundi la 201) alisema: “Katiba haipatikani kwa ubabe au wengi wape, bali inapatikana kwa maridhiano na mwafaka bila kujali wingi wa wajumbe.”
Mbunge wa Mbeya Vijijini, Lackson Mwanjali alisema kitendo cha Ukawa kukataa kurejea bungeni ni pigo katika mchakato wa Katiba Mpya kwa sababu Katiba inatengenezwa kwa majadiliano na kufikia mwafaka.
Imeandikwa na Elias Msuya, Daniel Mjema na Fidelis Butahe
SOURCE: MWANANCHI

Funga kazi: Warioba, Kabudi, Butiku wawasha upya moto wa Katiba




Dar es Salaam. Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba na wajumbe wa tume hiyo, jana walitoa ufafanuzi wa hoja mbalimbali kuhusu mchakato wa Katiba katika mjadala uliofanyika hapa kiasi cha kuwafanya waliohudhuria siyo tu kumshangilia, bali walimsindikiza hadi alipoingia kwenye gari lake na wakilifuata na kulisukuma.

Jaji Warioba na wajumbe wenzake, Profesa Palamagamba Kabudi, Joseph Butiku, Hamphrey Polepole, Mwantumu Malale na Awadh Ali Said walitoa ufafanuzi huo katika mdahalo la Katiba lililoandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere jana.
Jaji Warioba ndiye alianza kuzungumza kwa kukanusha madai yaliyotolewa juzi katika mdahalo mwingine, kuwa amepeleka maoni mapya serikalini.
Alisema madai hayo hayana ukweli bali maoni aliyowasilisha serikalini yalitokana na maoni ya wananchi waliyokusanya wakati wakiandaa Rasimu ya Kwanza ya Katiba ambayo yataweza kusaidia katika kuandaa Katiba ya Tanganyika.
Juzi, katika mdahalo uliorushwa na Star TV, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi alidai kuwa Jaji Warioba amewasilisha serikalini maoni mapya, ukiacha yale ambayo yapo katika Rasimu ya Katiba.
Jaji Warioba alisema Tume iliandaa sura ya kwanza iliyohusu mali na maliasili na sura ya tano kuhusu Serikali ya Muungano na sura ya nne iliyoelezea serikali za mitaa.
“Sura ya nne na tano tulibaki nazo lakini Machi 27, mwaka huu niliandika barua kwa Waziri wa Katiba na Sheria, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Chikawe (Waziri wa Mambo ya Ndani, Mathias Chikawe) kwa kuwa alikuwa Waziri wa Katiba na Sheria kipindi hicho na nikawakabidhi ili isaidie katika mchakato wa Katiba hasa wakati wa kuandaa Katiba ya Tanganyika,” alisema Jaji Warioba.
Aliongeza; “Hayakuwa mawazo mapya wala sikupeleka mawazo mapya, bali ni mawazo tuliyoyakusanya kutoka kwa wananchi na nimeamua kufanya hivyo kwa kuwa tume kwa kipindi chote ilikuwa wazi na mimi nimeamua iwe ‘public’ (wazi) kwa kila mmoja kujua, ili iwasaidie kujua wakati wa uandaaji wa Katiba ya Tanganyika.”
Jaji Warioba pia alifafanua sababu za tume kupendekeza muundo wa serikali tatu, kwamba haikufanya hivyo kutokana na idadi ya watu waliotaka muundo huo, bali ilitizama uzito wa hoja zilizotolewa.
“Wapo wanaosema kuwa idadi ya watu waliotaka muundo wa serikali tatu ni wachache. Tulipendekeza muundo huo kwa sababu ya hoja zilizotolewa na siyo wingi au uchache wa waliotoa maoni,” alisema.
Alisema hoja ya kwanza ni Tanganyika kuvaa koti la Muungano pia akifafanua jinsi Tanzania Bara inavyoshughulikia masuala yake ya kiuchumi bila kugusa masuala hayo kwa upande wa Zanzibar.
“Leo hii mawaziri wangapi wa muungano wanaotembelea Zanzibar kukagua shughuli za maendeleo, pia kuna mgongano wa Katiba ya Tanzania Bara na Zanzibar. Pia suala la fedha nalo limekuwa na mvutano kwa muda mrefu hasa kuhusu pande hizi mbili kuwa na akaunti ya pamoja,” alisema na kuongeza:
“Wajumbe wa tume tulikuwa na itikadi tofauti lakini hata siku moja hatukuwahi kupiga kura kupitisha jambo lolote, kila tulichokipendekeza tulikubaliana. Nadhani waendelee na majadiliano ili wafikie mwafaka,” alisema.
Alisema hata kama mchakato wa Katiba utasitishwa kwa muda, jambo la msingi linalotakiwa kuheshimiwa ni kuachwa kwa maoni ya wananchi yaliyomo katika Rasimu ya Katiba.
Butiku: JK alitetea masilahi ya CCM
Katika mchango wake, Butiku ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi wa Mwalimu Nyerere, alisema hotuba ya Rais Jakaya Kikwete wakati akilifungua Bunge Maalumu la Katiba ililenga kutetea masilahi ya CCM.
Huku akishangiliwa na mamia ya watu waliohudhuria, Butiku alisema CCM imeficha maoni ya wananchi yaliyokusanywa na tume kwa muda wa miezi 18, vikiwamo vitabu mbalimbali vya mapendekezo ya Watanzania kuhusu nini wanataka kiwemo katika Katiba yao.
Hata hivyo, katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi aliyoitoa Alhamisi iliyoipita, Rais Kikwete alijivua lawama kuwa ndiye alikuwa chanzo cha kuvurugika kwa mchakato wa kupata Katiba Mpya.
Butiku alianza kwa kuuliza, “Nani anaficha maoni” watu wakaitikia “CCM”, akauliza tena, “Huyu anayeficha maoni anatuheshimu hatuheshimu,” wasikilizaji wakaitikia, “Hatuheshimu.”
Akijibu kauli ya Rais Kikwete wakati akilifungua Bunge la Katiba, Butiku alisema: “Unaposema ukweli hutakiwi kuuminya. Rais Kikwete alisema mashauriano kati yake na wajumbe wa tume hayakuwa ya kina, lakini ukweli ni kwamba mashauriano yetu yalikuwa ya kina.”
Aliongeza: “Tunaheshimu maoni yake aliyoyatoa ila kuna maoni aliyotoa yalioonekana kuelekea kuitetea CCM na kama mnakumbuka katika hotuba yake alikuwa akisisitiza kwamba ‘Tumieni akili zenu mjadiliane na kupata uamuzi.”
Huku akinukuu baadhi ya vifungu vya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba vinavyoeleza jukumu la Bunge Maalumu la Katiba, Butiku alisema kilichoandikwa katika Rasimu ya Katiba ni maoni ya wananchi na ndiyo yanayotakiwa kuheshimiwa kama inavyoeleza sheria hiyo.
“Huu haukuwa mchakato wa kienyeji, nasema wazi mimi ni mwanachama wa CCM lakini sitarajii Rais awe na kikundi cha kwenda kuuliza kuhusu utekelezaji wa masuala ya kitaifa. Katika hili CCM tumekosea,” alisema Butiku.
Aliongeza: “Tume ilitoa vitabu na takwimu mbalimbali ambazo ziliwekwa katika tovuti ambayo imefungwa. Kuna nyaraka mbalimbali ambazo Tume ilizikusanya baada ya kukusanya maoni lakini zimefichwa.”
Akizungumza kwa njia ya kuuliza zaidi maswali, Butiku alisema kama muundo wa serikali tatu umekuwa na mgogoro je, ni sawa kuwa na muundo wa serikali mbili wenye nchi mbili?
Alisema hakuna aliyekataa muundo wa serikali mbili, ila muundo huo unatakiwa kufanyiwa maboresho makubwa ambayo utekelezaji wake ndiyo tatizo... “Inakuwaje leo watu wazima tunabishana jambo lililo wazi kabisa wakati suluhisho tunalijua?”
Polepole na gharama za serikali tatu
Polepole ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi za Kiraia alisema kauli ambazo zinatolewa kuhusu gharama za kuendesha serikali tatu hazina ukweli wowote kwani katika rasimu hiyo wamebainisha vyanzo vya mapato.
Polepole alisema waliiandikia barua Hazina kuomba taarifa zitakazotumika kuendesha Serikali ya Muungano na kwa mwaka 2011/12 bajeti ilikuwa Sh1.4 trilioni, mwaka 2012/13 (Sh1.8 trilioni) na mwaka 2013/14 ni Sh1.9 trilioni.
“Kwa kiwango hiki, Serikali ya Muungano haitakuwa na gharama zozote zile za ziada na kinachojitokeza sasa ni tatizo la masilahi binafsi,” alisema Polepole na kuongeza: “Watu wanataka serikali mbili kwa sababu ina mambo yote ya Muungano na Tanganyika kwa sababu ndiyo inayoteua wakurugenzi, makatibu wakuu na wengineo, hivyo wakipata urais wanalipana fadhila.”
Alisema wakati wakikusanya maoni, makatibu wakuu wa Serikali ya Zanzibar walipendekeza serikali tatu, kamati ya makatibu wakuu Serikali ya Muungano walipendekeza serikali mbili lakini zilizoongezwa mambo ya Muungano.
Alisema Ofisi ya Waziri Mkuu inayoshughulikia mambo yote ya Tanzania bara ilipendekeza serikali tatu na Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano iliyopewa dhamana ya kuimarisha Muungano ilipendekeza serikali tatu.
“Kwa hali yoyote ile huwezi kuepuka mapendekezo yaliyomo katika Rasimu kwani yataondoa kero zilizopo kwa pande zote,” alisema Polepole.
Kabudi atoa somo
Akitoa mchango wake, Profesa Kabudi alisema: “Nchi hii ni kubwa kuliko sisi sote, hakuna mkubwa zaidi ya nchi hii, sisi sote tutakufa, tutazikwa na tutaoza lakini nchi hii itaendelea kuwapo.”
Alisema kuhusu Muungano, Wazanzibari wanazungumza kuliko Watanganyika, lakini ukifika wakati Watanganyika wakazungumza, itakuwa hatari hivyo akasema ufike wakati Watanganyika wapewe serikali yao wakati wakiogopa, wasisubiri waanze kuidai Tanganyika yao.
Alisema baada ya kuvurugwa kwa Kongo, Tanzania ndiyo imekuwa kama nyonga ya Afrika na kuwa na umuhimu wa kipekee kwa ulinzi wa nchi nane zilizoizunguka na Bahari ya Hindi.
Alishangazwa na hatua ya kuwekwa kando kwa tume baada tu ya kuwasilisha Rasimu ya Katiba na kwamba hatua hiyo ndiyo chanzo cha mkwamo uliopo kwa sasa kwa kuwa ndiyo iliyokuwa ikijua chanzo na kila ibara na sababu za kuwapo kwake, hivyo ingeweza kutoa ufafanuzi pale ambako litatokea tatizo.
Wakati akitoa kauli hiyo, watu waliofurika katika ukumbi huo walilipuka kwa shangwe, “Sema usiogope sema,” huku Profesa huyo akihitimisha kwa kuwataka Watanzania kujadili mambo hayo kwa ajili ya mustakabali wa Taifa.
Awadh azungumzia misukosuko
Awadh ambaye ni Rais wa Chama cha Wanasheria Zanzibar (ZLS) alisema Muungano umefika hapa baada ya kupitia misukosuko mingi.
“Hakuna sehemu Tume iliambiwa itumie takwimu, bali ni hoja zinazofanana na kutofautiana na kufanya uamuzi, ndicho ambacho tulikuwa tukikifanya wakati wote,” alisema na kuongeza: “Watu wengi suala la muungano hawalielewi na wanaupotosha umma. Muungano unatakiwa kuweka haki sawa, fursa sawa na hadhi sawa, lakini usipokuwa na haya hatuwezi kuwa na muungano imara.”
Alitoa angalizo kwa wanasiasa kuzungumza kama wachumi hasa katika gharama, jambo ambalo hawana uzoefu na uelewa nalo akisema wanaongeza vitu visivyo na ukweli ndani yake.
Malale: Hatuwezi kutumia maoni kama kichaka
Malale alisema kuwa Tume ilikusanya maoni ya wananchi nchi nzima na kamwe haiwezi kuyatumia kama kichaka, kama wanavyofanya watu wengine.
“Watu waache kutumia maoni ya wananchi kama kichaka cha hoja zao. Tume imechukua maoni ya wananchi na kuyaweka kwa pamoja. Maoni yao yanatakiwa kuheshimiwa na yasitumike kama kichaka kwa wengine,” alisema Malale.
Jaji Warioba alihitimisha mdahalo huo kwa kuwajibu wanasiasa wanaodai kuwa takwimu za idadi ya wananchi waliotoa maoni si sahihi kutokana na idadi kupishana kati ya Mkoa wa Kigoma na Tabora.

“Kwani wananchi wa Kigoma siyo Watanzania? Jumla ya wananchi 8,600 walitoa maoni mkoani Kigoma na wananchi 3,011 mkoani Tabora,” alisema na kuongeza: “Mkoa wa Kigoma na Kagera ndiyo iliyoko pembezoni, hivyo ina matatizo lukuki ndiyo maana walijitokeza kutoa maoni kwa wingi ili yaingizwe katika Katiba.”
Alisisitiza kuwa hata kama yatazungumzwa maneno gani, Tume ya Mabadiliko ya Katiba ndiyo iliyohoji wananchi, hivyo inajua kila jambo walilopendekeza na kipi ambacho wananchi wanakitaka.
Alipoulizwa nini hatma ya Bunge Maalumu la Katiba kutokana na baadhi ya wajumbe wake kususia vikao vyake alisema: “Nawashauri waache masilahi binafsi ya makundi yao na wafanye kazi. Wajifiche chumbani na wapate mwafaka wa kuijadili rasimu.
 Fidelis Butahe na Ibrahim Yamola, Mwananchi
Dar es Salaam. Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba na wajumbe wa tume hiyo, jana walitoa ufafanuzi wa hoja mbalimbali kuhusu mchakato wa Katiba katika mjadala uliofanyika hapa kiasi cha kuwafanya waliohudhuria siyo tu kumshangilia, bali walimsindikiza hadi alipoingia kwenye gari lake na wakilifuata na kulisukuma.
Jaji Warioba na wajumbe wenzake, Profesa Palamagamba Kabudi, Joseph Butiku, Hamphrey Polepole, Mwantumu Malale na Awadh Ali Said walitoa ufafanuzi huo katika mdahalo la Katiba lililoandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere jana.
Jaji Warioba ndiye alianza kuzungumza kwa kukanusha madai yaliyotolewa juzi katika mdahalo mwingine, kuwa amepeleka maoni mapya serikalini.
Alisema madai hayo hayana ukweli bali maoni aliyowasilisha serikalini yalitokana na maoni ya wananchi waliyokusanya wakati wakiandaa Rasimu ya Kwanza ya Katiba ambayo yataweza kusaidia katika kuandaa Katiba ya Tanganyika.
Juzi, katika mdahalo uliorushwa na Star TV, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi alidai kuwa Jaji Warioba amewasilisha serikalini maoni mapya, ukiacha yale ambayo yapo katika Rasimu ya Katiba.
Jaji Warioba alisema Tume iliandaa sura ya kwanza iliyohusu mali na maliasili na sura ya tano kuhusu Serikali ya Muungano na sura ya nne iliyoelezea serikali za mitaa.
“Sura ya nne na tano tulibaki nazo lakini Machi 27, mwaka huu niliandika barua kwa Waziri wa Katiba na Sheria, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Chikawe (Waziri wa Mambo ya Ndani, Mathias Chikawe) kwa kuwa alikuwa Waziri wa Katiba na Sheria kipindi hicho na nikawakabidhi ili isaidie katika mchakato wa Katiba hasa wakati wa kuandaa Katiba ya Tanganyika,” alisema Jaji Warioba.
Aliongeza; “Hayakuwa mawazo mapya wala sikupeleka mawazo mapya, bali ni mawazo tuliyoyakusanya kutoka kwa wananchi na nimeamua kufanya hivyo kwa kuwa tume kwa kipindi chote ilikuwa wazi na mimi nimeamua iwe ‘public’ (wazi) kwa kila mmoja kujua, ili iwasaidie kujua wakati wa uandaaji wa Katiba ya Tanganyika.”
Jaji Warioba pia alifafanua sababu za tume kupendekeza muundo wa serikali tatu, kwamba haikufanya hivyo kutokana na idadi ya watu waliotaka muundo huo, bali ilitizama uzito wa hoja zilizotolewa.
“Wapo wanaosema kuwa idadi ya watu waliotaka muundo wa serikali tatu ni wachache. Tulipendekeza muundo huo kwa sababu ya hoja zilizotolewa na siyo wingi au uchache wa waliotoa maoni,” alisema.
Alisema hoja ya kwanza ni Tanganyika kuvaa koti la Muungano pia akifafanua jinsi Tanzania Bara inavyoshughulikia masuala yake ya kiuchumi bila kugusa masuala hayo kwa upande wa Zanzibar.
“Leo hii mawaziri wangapi wa muungano wanaotembelea Zanzibar kukagua shughuli za maendeleo, pia kuna mgongano wa Katiba ya Tanzania Bara na Zanzibar. Pia suala la fedha nalo limekuwa na mvutano kwa muda mrefu hasa kuhusu pande hizi mbili kuwa na akaunti ya pamoja,” alisema na kuongeza:
“Wajumbe wa tume tulikuwa na itikadi tofauti lakini hata siku moja hatukuwahi kupiga kura kupitisha jambo lolote, kila tulichokipendekeza tulikubaliana. Nadhani waendelee na majadiliano ili wafikie mwafaka,” alisema.
Alisema hata kama mchakato wa Katiba utasitishwa kwa muda, jambo la msingi linalotakiwa kuheshimiwa ni kuachwa kwa maoni ya wananchi yaliyomo katika Rasimu ya Katiba.
Butiku: JK alitetea masilahi ya CCM
Katika mchango wake, Butiku ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi wa Mwalimu Nyerere, alisema hotuba ya Rais Jakaya Kikwete wakati akilifungua Bunge Maalumu la Katiba ililenga kutetea masilahi ya CCM.
Huku akishangiliwa na mamia ya watu waliohudhuria, Butiku alisema CCM imeficha maoni ya wananchi yaliyokusanywa na tume kwa muda wa miezi 18, vikiwamo vitabu mbalimbali vya mapendekezo ya Watanzania kuhusu nini wanataka kiwemo katika Katiba yao.
Hata hivyo, katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi aliyoitoa Alhamisi iliyoipita, Rais Kikwete alijivua lawama kuwa ndiye alikuwa chanzo cha kuvurugika kwa mchakato wa kupata Katiba Mpya.
Butiku alianza kwa kuuliza, “Nani anaficha maoni” watu wakaitikia “CCM”, akauliza tena, “Huyu anayeficha maoni anatuheshimu hatuheshimu,” wasikilizaji wakaitikia, “Hatuheshimu.”
Akijibu kauli ya Rais Kikwete wakati akilifungua Bunge la Katiba, Butiku alisema: “Unaposema ukweli hutakiwi kuuminya. Rais Kikwete alisema mashauriano kati yake na wajumbe wa tume hayakuwa ya kina, lakini ukweli ni kwamba mashauriano yetu yalikuwa ya kina.”
Aliongeza: “Tunaheshimu maoni yake aliyoyatoa ila kuna maoni aliyotoa yalioonekana kuelekea kuitetea CCM na kama mnakumbuka katika hotuba yake alikuwa akisisitiza kwamba ‘Tumieni akili zenu mjadiliane 
Huku akinukuu baadhi ya vifungu vya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba vinavyoeleza jukumu la Bunge Maalumu la Katiba, Butiku alisema kilichoandikwa katika Rasimu ya Katiba ni maoni ya wananchi na ndiyo yanayotakiwa kuheshimiwa kama inavyoeleza sheria hiyo.
“Huu haukuwa mchakato wa kienyeji, nasema wazi mimi ni mwanachama wa CCM lakini sitarajii Rais awe na kikundi cha kwenda kuuliza kuhusu utekelezaji wa masuala ya kitaifa. Katika hili CCM tumekosea,” alisema Butiku.
Aliongeza: “Tume ilitoa vitabu na takwimu mbalimbali ambazo ziliwekwa katika tovuti ambayo imefungwa. Kuna nyaraka mbalimbali ambazo Tume ilizikusanya baada ya kukusanya maoni lakini zimefichwa.”
Akizungumza kwa njia ya kuuliza zaidi maswali, Butiku alisema kama muundo wa serikali tatu umekuwa na mgogoro je, ni sawa kuwa na muundo wa serikali mbili wenye nchi mbili?
Alisema hakuna aliyekataa muundo wa serikali mbili, ila muundo huo unatakiwa kufanyiwa maboresho makubwa ambayo utekelezaji wake ndiyo tatizo... “Inakuwaje leo watu wazima tunabishana jambo lililo wazi kabisa wakati suluhisho tunalijua?”
Polepole na gharama za serikali tatu
Polepole ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi za Kiraia alisema kauli ambazo zinatolewa kuhusu gharama za kuendesha serikali tatu hazina ukweli wowote kwani katika rasimu hiyo wamebainisha vyanzo vya mapato.
Polepole alisema waliiandikia barua Hazina kuomba taarifa zitakazotumika kuendesha Serikali ya Muungano na kwa mwaka 2011/12 bajeti ilikuwa Sh1.4 trilioni, mwaka 2012/13 (Sh1.8 trilioni) na mwaka 2013/14 ni Sh1.9 trilioni.
“Kwa kiwango hiki, Serikali ya Muungano haitakuwa na gharama zozote zile za ziada na kinachojitokeza sasa ni tatizo la masilahi binafsi,” alisema Polepole na kuongeza: “Watu wanataka serikali mbili kwa sababu ina mambo yote ya Muungano na Tanganyika kwa sababu ndiyo inayoteua wakurugenzi, makatibu wakuu na wengineo, hivyo wakipata urais wanalipana fadhila.”
Alisema wakati wakikusanya maoni, makatibu wakuu wa Serikali ya Zanzibar walipendekeza serikali tatu, kamati ya makatibu wakuu Serikali ya Muungano walipendekeza serikali mbili lakini zilizoongezwa mambo ya Muungano.
Alisema Ofisi ya Waziri Mkuu inayoshughulikia mambo yote ya Tanzania bara ilipendekeza serikali tatu na Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano iliyopewa dhamana ya kuimarisha Muungano ilipendekeza serikali tatu.
“Kwa hali yoyote ile huwezi kuepuka mapendekezo yaliyomo katika Rasimu kwani yataondoa kero zilizopo kwa pande zote,” alisema Polepole.
Kabudi atoa somo
Akitoa mchango wake, Profesa Kabudi alisema: “Nchi hii ni kubwa kuliko sisi sote, hakuna mkubwa zaidi ya nchi hii, sisi sote tutakufa, tutazikwa na tutaoza lakini nchi hii itaendelea kuwapo.”
Alisema kuhusu Muungano, Wazanzibari wanazungumza kuliko Watanganyika, lakini ukifika wakati Watanganyika wakazungumza, itakuwa hatari hivyo akasema ufike wakati Watanganyika wapewe serikali yao wakati wakiogopa, wasisubiri waanze kuidai Tanganyika yao.
Alisema baada ya kuvurugwa kwa Kongo, Tanzania ndiyo imekuwa kama nyonga ya Afrika na kuwa na umuhimu wa kipekee kwa ulinzi wa nchi nane zilizoizunguka na Bahari ya Hindi.
Alishangazwa na hatua ya kuwekwa kando kwa tume baada tu ya kuwasilisha Rasimu ya Katiba na kwamba hatua hiyo ndiyo chanzo cha mkwamo uliopo kwa sasa kwa kuwa ndiyo iliyokuwa ikijua chanzo na kila ibara na sababu za kuwapo kwake, hivyo ingeweza kutoa ufafanuzi pale ambako litatokea tatizo.
Wakati akitoa kauli hiyo, watu waliofurika katika ukumbi huo walilipuka kwa shangwe, “Sema usiogope sema,” huku Profesa huyo akihitimisha kwa kuwataka Watanzania kujadili mambo hayo kwa ajili ya mustakabali wa Taifa.
Awadh azungumzia misukosuko
Awadh ambaye ni Rais wa Chama cha Wanasheria Zanzibar (ZLS) alisema Muungano umefika hapa baada ya kupitia misukosuko mingi.
“Hakuna sehemu Tume iliambiwa itumie takwimu, bali ni hoja zinazofanana na kutofautiana na kufanya uamuzi, ndicho ambacho tulikuwa tukikifanya wakati wote,” alisema na kuongeza: “Watu wengi suala la muungano hawalielewi na wanaupotosha umma. Muungano unatakiwa kuweka haki sawa, fursa sawa na hadhi sawa, lakini usipokuwa na haya hatuwezi kuwa na muungano imara.”
Alitoa angalizo kwa wanasiasa kuzungumza kama wachumi hasa katika gharama, jambo ambalo hawana uzoefu na uelewa nalo akisema wanaongeza vitu visivyo na ukweli ndani yake.
Malale: Hatuwezi kutumia maoni kama kichaka
Malale alisema kuwa Tume ilikusanya maoni ya wananchi nchi nzima na kamwe haiwezi kuyatumia kama kichaka, kama wanavyofanya watu wengine.
“Watu waache kutumia maoni ya wananchi kama kichaka cha hoja zao. Tume imechukua maoni ya wananchi na kuyaweka kwa pamoja. Maoni yao yanatakiwa kuheshimiwa na yasitumike kama kichaka kwa wengine,” alisema Malale.
Jaji Warioba alihitimisha mdahalo huo kwa kuwajibu wanasiasa wanaodai kuwa takwimu za idadi ya wananchi waliotoa maoni si sahihi kutokana na idadi kupishana kati ya Mkoa wa Kigoma na Tabora.
“Kwani wananchi wa Kigoma siyo Watanzania? Jumla ya wananchi 8,600 walitoa maoni mkoani Kigoma na wananchi 3,011 mkoani Tabora,” alisema na kuongeza: “Mkoa wa Kigoma na Kagera ndiyo iliyoko pembezoni, hivyo ina matatizo lukuki ndiyo maana walijitokeza kutoa maoni kwa wingi ili yaingizwe katika Katiba.”
Alisisitiza kuwa hata kama yatazungumzwa maneno gani, Tume ya Mabadiliko ya Katiba ndiyo iliyohoji wananchi, hivyo inajua kila jambo walilopendekeza na kipi ambacho wananchi wanakitaka.
Alipoulizwa nini hatma ya Bunge Maalumu la Katiba kutokana na baadhi ya wajumbe wake kususia vikao vyake alisema: “Nawashauri waache masilahi binafsi ya makundi yao na wafanye kazi. Wajifiche chumbani na wapate mwafaka wa kuijadili rasimu.
SOURCE: MWANANCHI

BUNGE LA KATIBA LAANZA DODOMA

HOTUBA YA MWENYEKITI WA BUNGE MAALUM LA KATIBA MHE. SAMUEL SITTA KATIKA UFUNGUZI WA AWAMU YA PILI YA BUNGE HILO, DODOMA TAREHE 5 AGOSTI 2014

Karibuni tena Dodoma Waheshimiwa Wajumbe wa Bunge Maalum la kutunga Katiba ya nchi yetu. Sote tuna kila sababu ya kumshukuru Mwenyezi Mungu wetu kwa kuendelea kutupa uhai na afya hadi leo kutuwezesha kuwepo ndani ya ukumbi huu. Tupo humu ili tuitekeleze kazi waliyotukabidhi Watanzania wenzetu milioni arobaini na sita (46) ya kuwapatia Katiba mpya. Dhamana hii ni nzito na haistahili kufanyiwa ajizi.

Tunaendelea na shughuli zetu za Bunge Maalum kwa kuzingatia Kanuni ya 30 (1) inayosema
Akidi kwa kila kikao cha Bunge Maalum isipokuwa wakati wa kupitisha uamuzi wa Bunge Maalum itakuwa ni nusu ya Wajumbe wote wa Bunge Maalum“.
Nimetaarifiwa na Katibu kwamba wajumbe waliokuja Dodoma kuhudhuria ni zaidi ya robo tatu ya Wajumbe wote wa Bunge Maalum. Nawashukuruni nyote kwa kuja hapa Dodoma ili kutimiza wajibu wenu.
Kwa niaba yenu, nawashukuru Watanzania wenzetu wote ambao kwa mamilioni wamedhihirisha utashi mwema wa kisiasa kwa kuunga mkono hatua ya Bunge Maalum kuendelea na kazi zake hadi tuipate Katiba inayopendekezwa ambayo wataipigia kura ya maoni. Kipekee na kwa niaba yenu, nawashukuru kwa dhati viongozi wetu wa dini wa madhehebu yote wanaloliombea Taifa hili mafanikio Bunge Maalum, wakitanguliza utaifa pamoja na amani ya nchi na umoja ndani ya nchi na siyo ubinafsi na maslahi ya makundi.
 Kwa leo sikupenda sana kuzungumzia hoja mbali mbali zinazotawala magumzo ya mchakato wa Katiba mpya hapa nchini, magumzo yanayoendeshwa na makundi maalum kwa jazba na hata matusi. Hata hivyo nalazimika kutoa maelezo ya ufafanuzi kuhusu upotoshaji mkubwa unaoendeshwa na baadhi ya watu kuhusu Bunge Maalum. Nikiwa Mwenyekiti wenu ninao wajibu wa kuwafafanulia wananchi kuhusu uhalali wa shughuli za Bunge Maalum linaloendelea na utaratibu wa shughuli zetu.
Ni Rasimu ya Tume au la
Wapo wanaodai kuwa eti hapa Bungeni hatujadili Rasimu ya Tume. Tuhuma hii haina ukweli hata kidogo. Msingi wa majadiliano yote tangu tumeanza ni Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa na Tume ya Katiba. Utaratibu ni kwamba pale ambapo wajumbe wanaona panafaa kurekebishwa wanafanya hivyo. Maana ya rasimu ni andiko ambalo halijajitosheleza bila kupata ithibati ya taasisi ya juu zaidi. Anayekabidhiwa rasimu anayo haki na mamlaka ya kuirekebisha. Vinginevyo kujadili rasimu hakuna sababu. Itakuwa ni jambo la ajabu na lisilo na mantiki yoyote kuwa taasisi iliyopewa mamlaka ya kujadili Rasimu ikishaijadili iiache ibaki kama ilivyokuwa wakati ilipowasilishwa!
 Je suala ni muundo wa Muungano tu?
Maudhui ya Rasimu yanajumuisha baadhi ya masuala muhimu yafuatayo:
-      Kuimarisha Muungano wetu kwa kuleta uwiano     bora zaidi wa mamlaka ya Zanzibar na Tanzania      Bara ndani ya Muungano
-      Kuimarisha haki za binadamu ili kuwawezesha      raia wa kawaida kufaidi uhuru wa demokrasia     bila ubabe na dhuluma
-      Kuzuia wachache kufuja rasilimali za taifa bila       kujali maslahi ya wengi na ya vizazi vijavyo.
-      Kujenga uwiano sahihi na wenye haki baina ya      wanawake na wanaume katika nafasi za uongozi.
-      Kubainisha hatua zenye kuleta matumaini mapya ya maendeleo kwa makundi maalum ya vijana     wakulima wadogo, wafugaji, wafanyakazi wa ngazi   za kawaida, walemavu, wafanya biashara wadogo   na wajasiriamali wengine.
-      Kuweka msingi imara wa kutungwa kwa sheria      kakamavu za kuzuia ukandamizaji wa raia,        unyonyaji, wizi wa mali ya umma, rushwa,    hujuma dhidi ya uchumi na kuzuia mapato        haramu na fedha chafu.
-      Kutambua haki za ardhi kwa wakulima, wafugaji    na wajasiriamali wengine ili kupunguza migongano na migogoro.
-      Kuweka Misingi ya utawala bora inayozingatia        uadilifu, sifa stahiki na ufanisi.
-      Kuwezesha kutungwa kwa sheria bora zaidi     zitakazosimamia chaguzi zilizo za haki na huru    zaidi pamoja na kuwepo Tume za Uchaguzi       zilizoboreshwa.
Zaidi ya hivyo, yapo mapungufu katika Rasimu iliyopo kwa kuachwa masuala ya kuwezesha Serikali za mitaa; kutoa maelekezo kuhusu masuala ya matumizi ya ardhi na rasilimali nyingine za Taifa. Nini kinatuzuia kuiboresha Rasimu kwa kuyaongeza mambo haya ndani ya Katiba kwa faida ya Taifa?
 Yote haya ni masuala muhimu ambayo yamo ndani ya rasimu na wakati wake wa kuyaweka sawa ndiyo huu. Pamoja na umuhimu wake suala la muundo wa Muungano si suala la kutulazimisha tuyaahirishe mazuri yote yaliyomo katika Rasimu tuliyopewa.
 Uhalali wa Shughuli za Bunge Maalum
Pamoja na uhalali wa kisheria wa Bunge hili Maalum kuendelea kufanya kazi zake, linao pia uhalali wa kisiasa kutokana na sifa za uwakilishi wetu na pia maudhui yaliyomo ndani ya Rasimu. Kutofautiana maoni hakuwapi hadhi tofauti baadhi ya wajumbe kujiona wao wana uhalali zaidi mbele ya wananchi kuliko wenzao. Ndiyo maana utaratibu umewekwa wa kupiga kura na wa maridhiano. Utamaduni mpya unaoanza kujengwa na baadhi ya viongozi wa jamii wa kususia mijadala halali na kwenda nje kuelezea hoja za upande mmoja hauna nafasi katika Tanzania jamii isiyotaka fujo na utengano.
 Wajumbe wa Bunge Maalum wanaoendelea na kazi mjini Dodoma ni wateule wa Rais kwa niaba ya wananchi kwa kazi ya kutunga Katiba. Kazi hii haiwezi kusitishwa kwa sababu tu wajumbe wachache wameisusia. Tutazingatia matakwa ya sheria katika kufikia hatma ya mchakato wa Katiba.
 Mabadiliko ya Kanuni
Kama nilivyoeleza hapo mwanzo, Rasimu ina jumla ya sura kumi na saba (17) zenye mambo mengi yenye maslahi kwa Watanzania wote. Kwa muda tuliopewa wa siku sitini (60) isingewezekana kuikamilisha kazi tuliyopewa ndani ya muda. Ikumbukwe kwamba kwa Kanuni zilivyo, kila sura mbili zinahitaji siku tisa kuzifanyia kazi. Kwa njia hiyo, ingetuchukua siku takriban mia moja thelathini (130) ili kuikamilisha kazi hii! Pendekezo la msingi hapa ni kwamba Kamati zetu kumi na mbili (12) zizingatie na kuzijadili sura kumi na tano (15) za Rasimu na pia zikamilishe uandishi wa sura mbili zilizojadiliwa awali na ikibidi ziongeze sura ambazo zitadhihirika kuwa ni muhimu. Naamini mtiririko huu utatuwezesha kuwa na mpangilio bora zaidi wa sura na ibara katika Katiba mpya. Tusingependa na wala isingefaa kuomba tena muda wa ziada wa kazi ya Katiba ndio maana tunafanya mabadiliko ya Kanuni. Kamati ya Uongozi iliyoketi Dar es Salaam tarehe 28 Julai 2014 imependekeza yafanywe mabadiliko ya Kanuni za Bunge Maalum kuwezesha kazi ikamilike ndani ya muda tuliopewa. Kwa hiyo nitawaomba tuyatafakari mapendekezo ya mabadiliko ya Kanuni na hatimaye kuyapitisha ili ratiba ya kazi zetu iende sawa. Nitawaomba muikubali ratiba iliyogawanywa leo na pia mkubali kuzibadilisha Kanuni kwa lengo nililolieleza hapa.
 HITIMISHO
Pamoja na maoni ya kila namna yanayoendelezwa kujadili mchakato wa Katiba nje ya Bunge hili, ni muhimu wahusika wapunguze jazba, chuki na upotoshaji. Bunge Maalum lisaidiwe kwa mawazo chanya ili limalize kazi yake.
Sisi tuliomo humu katika Bunge Maalum tuna wajibu wa kuifanya kazi yetu kwa umakini na kwa uadilifu ili kazi yetu iwe bora. Tujadiliane kwa uungwana. Tofauti za mawazo zisitufanye tuingize chuki na maneno yasiyofaa. Katika mabadiliko ya Kanuni nashukuru sasa Kiti kimepewa mamlaka ya kushughulikia utovu wa nidhamu ndani ya wakati. Lakini ninaamini haitakuwa lazima kwangu mimi au Makamu Mwenyekiti kutumia nguvu za mamlaka yetu ila tu pale itakapobidi.
 Nawatakia nyote Mkutano wenye mafanikio kwa maslahi mapana ya nchi yetu.
 MUNGU IBARIKI TANZANIA!
 Samuel Sitta – MB
MWENYEKITI BUNGE MAALUM LA KATIBA
SOURCE: MATUKIOTZ.COM

Sunday, August 3, 2014

EMMANUEL P. MYAMBA A.K.A "PASTOR MYAMBA" ABADILISHA MWELEKEO WA MAISHA

Pastor Myamba Leo Tarehe 02- Agosti 2014 ameamua kwa hiari yake mwenyewe kubadilisha mwelekeo wa maisha pale alipokubalia na mwenzi wake kuanza kuishi maisha ya mume na mke, harusi ya kufana sana iliyofanyika huko visiwani Zanzibar;

Hebu angalia baadhi ya picha habari zaidi itawajia punde.