WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Saturday, February 14, 2015

MATOKEO YA FORM FOUR 2014

Ili kuona matokeo ya CSEE, bofya hapa na kwa matokeo ya QT, bofya hapa
Katibu Mtedaji wa Baraza la Mitihani la Taifa Dk Charles Msonde ametangaza matokeo ya mitihani ya Shule za Sekondari ya Kidato cha Nne ya mwaka jana na kusema, kiwango cha ufaulu kimeongezeka kwa asilimia 10 ikilinganishwa na matokeo ya mwaka 2013.
Dk Msonde amesema kuongezeka kwa kiwango cha ufaulu kutoka asilimia 58.25 hadi asilimia 68.33 kumetokana na mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now - BRN).
Dk Msonde ameishukuru Serikali kwa BRN na Walimu kwa jitihada zilizofanikisha kupatikana kwa matokeo hayo.
Matokeo haya yametolewa kwa kutumia mfumo mpya wa wastani wa pointi badala ya madaraja kama ilivyozoeleka kwa miaka iliyotangulia.
Baraza hilo limewafutia metokeo watahiniwa 128 wa kujigetemea kutoka vituo vya Kisesa mkoani Mwanza na Lubabo huko Zanzibar kutokana na udanganyifu uliokithiri.

No comments:

Post a Comment