WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Friday, June 5, 2015

Maalim Seif ‘kidedea’, kuwania urais Zanzibar

  Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF,Maalim Seif  Sharif Hamad. 
Na Mwinyi Sadallah

Zanzibar. Chama cha Wananchi CUF kimempitisha katibu mkuu wake, Maalim Seif Sharif Hamad kuwa mgombea urais wa Zanzibar kwa mara ya tano.
Pia, CUF imewarudisha baadhi ya wagombea wa nafasi za ubunge na uwakilishi walioanguka katika kura za maoni za majimboni.
Maalim Seif amepitishwa na CUF kuwania nafasi hiyo kwa mara tano tangu kurejeshwa kwa mfumo wa siasa za ushindani na mara moja akiwa CCM mwaka 1984 wakati alipochuana na Marehemu Idirisa Abdulwakili.
Akizungumza na wanahabari ofisini kwake Vuga mjini hapa, mkurugenzi wa mipango na uchaguzi wa CUF, Omar Ali Shehe alisema kwamba, Maalim Seif amechaguliwa baada ya kupata ushindi wa asilimia 100 kwa kuzoa kura zote 56 za wajumbe wa Baraza Kuu.
Alisema wajumbe wa Baraza Kuu la Taifa walilazimika kupiga kura ya “Ndiyo” na “Hapana” kutokana na kuwa na mgombea mmoja na kura zote zilimuunga mkono mwanasiasa huyo mkongwe na hakuna kura iliyoharibika.
Shehe aliwataja wagombea waliorudishwa kuwa ni mbunge wa Mtambile, Masoud Abdalla Salim na mwakilishi wa Jimbo la Kojani, Hassan Hamad Omar huku kukiwa hakujapatikana kwa wagombea kwenye majimbo ya Raha Leo, Makunduchi na Mtambwe kutokana na sababu mbalimbali ikiwamo ya kukatiwa rufaa pamoja na Baraza kuu kutoridhika.
Wagombea waliopitishwa kugombea ubunge na uwakilishi ni Ismail Jussa Ladhu (uwakilishi) na Ali Saleh Abdalla (ubunge) wa Jimbo la Jangombe, Ali Haki Mwadini (uwakilishi) na Mohamed Yussuf Maalim (uwakilishi).
Katika Jimbo la Kikwajuni, Moh’d Khalfan Sultani (uwakilishi) na nafasi ya ubunge imeachiwa Chadema.
Jimbo la Chumbuni ni Maulid Suleiman Juma (uwakilishi) na Omar Ali Khamis (ubunge), Jimbo la Kwamtipura Amina Rashid Salum (uwakilisihi) na Abdi Seif Hamad (ubunge), Jimbo la Magomeni Yussuf Idrisa Mudu (uwakilishi ) na Ahmed Khamis Hamad (ubunge).
Jimbo la Mpendae ni Ali Hamad Ali (uwakilishi) na Omar Moh’d Omar (ubunge), Jimbo la Amani ni Khamis Rashid Abeid (uwakilishi) na Khamis Silima Ame (ubunge) . Jimbo la Kwahani Hassan Juma Hassan (uwakilishi) na Khamis Mussa Haji (ubunge) Magomeni, Abdilahi Jihad Hassan (uwakilishi) na Saleh Mohamed Saleh (ubunge).
Jimbo la Bububu, Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano, Juma Duni Haji (uwakilishi) na Juma Khamis Juma (ubunge). Jimbo la Mfenesini ni Saleh Khamis Omar (uwakilishi) na Hassan Othman Makame (ubunge) huku Jimbo la Mtoni ni Waziri wa Biashara na Masoko, Nassor Ahmed Mazrui (uwakilishi) na Ali Ame Ali (ubunge).
Katika jimbo la Dole amepitishwa Yussuf Omar Muhine (uwakilishi) na Khamis Msabah Mzee (ubunge) Jimbo la Dimani ni Mohamed Hashim Ismail (uwakilishi) na Khalid Said Suleiman (ubunge) na Jimbo Kiembesamaki ni Waziri wa zamani SMZ Mansour Yussuf Himid (uwakilishi) na Mohamed Nassor Mohammed (ubunge), Mwanakwerekwe ni Ussi Juma Hassan (uwakilishi) na Ali Salum Khamis (ubunge). wakati Jimbo la Fuoni Suleiman Simai Pandu (Uwakilishi) na Mohamed Juma Aminia (Ubunge) na jimbo la Nungwi Hassan Jani Masoud (Uwakilishi) na Yussuf Haji Khamis (Ubunge).
Wengine ni Nahoda Khamis Haji (Uwakilishi) jimbo la Matemwe na Dunia Haji Pandu (Ubunge ) Jimbo la Mkwajuni Haji Kesi Haji (Uwakilishi) na Khamis Masoud Nasor (Ubunge).
Katika jimbo la Chaani Khamis Amour Vuai (Uwakilishi) na Khatib Ali Juma (Ubunge) wakati jimbo la Tumbatu Makame Haji Makame (Uwakilishi) na Rashid Khamis Rashid (Ubunge) pamoja na jimbo la Donge Suleiman Ahmed Sleiman (Uwakilishi) na Kombo Mohamed Kombo (Ubunge)
Wagombea wengine waliteuliwa ni Zahran Juma Mshamba (Uwakilishi) Jimbo la Bubwini na Mohamed Amour Mohamed (Ubunge) Jimbo la Kitope Hassan Khatib Kheir (Uwakilishi) na Mwinshaha Shehe Abdalla (Ubunge).
Jimbo la Uzini Asha Simai Issa (Uwakilishi) na Adam Ali Wazir (Ubunge) Khamis Malik Khamis (Uwakilishi) Jimbo Koani Shaaban Iddi Ame (Ubunge)na jimbo la Chwaka Arafa Shauri Mjaka (Uwakilishi ) pamoja na Ali Khamis Ame (Ubunge).
Wagombea wengine Asha Abdu Haji (Uwakilishi) Jimbo la Muyuni na Baswira Hassan Suleiman (Ubunge) wakati nJimbo la Tumbe Mohamed Hemed (Uwakilishi) na Rashid Ali Abdalla (Ubunge) pamoja na Jimbo la Micheweni Subeit Khamis Faki (Uwakilishi) na Haji Khatib Kai (Ubunge).
Wengine Issa Said Juma Jimbo la Konde (Uwakilishi) na Khatib Said Haji (Ubunge) pamoja na Waziri wa Katiba na Sheria Abubakar Khamis Bakar Jimbo la Mgogoni (Uwakilishi) na Juma Kombo Hamad (Ubunge) wakati Jimbo la Wete DK Suleiman Ali Yussuf (Uwakilishi) na Mbarouk Salum Ali (Ubunge).
Hamad Masoud Hamad Jimbo la Ole (Uwakilishi) na Rajab Mbarouk Mohamed (Ubunge) pamoja na Waziri wa Habari Utamaduni, Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk Jimbo la Gando (Uwakilishi) na Othman Omar Haji (Ubunge).
Katika jimbo la Mtambwe Mwakilishi hajapatikana kutokana na matokeo ya kura ya maoni kukatiwa rufaa lakini Khalifa Mohamed amepitishwa nafasi ya (Ubunge) na Jimbo la Kojani Hassan Hamad Omar (Uwakilishi) na Hamad Salum Maalim (Ubunge).
Jimbo la Chake Chake Omar Ali Shehe (Uwakilishi) na Yussuf Kaiza Makame (Ubunge) wakati Jimbo la Chonga Khamis Faki Marango (Uwakilishi) na Moh’d Juma Khatib (Ubunge) Jimbo la Ziwani Mohamed Ali Salum (Uwakilishi) na Ahmed Juma Ngwali (Ubunge)
Wengine Khalifa Abdalla Ali Jimbo la Wawi (Uwakilishi) na Waziri wa zamani wa Utalii katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano Juma Hamad Omar (Ubunge) na jimbo la Chamabani Mohamed Mbwana Hamad (Uwakilishi) Yussuf Salim Husein (Ubunge) wakati Jimbo la Kiwani Hija Hassan Hija (Uwakilishi) na Abdalla Haji Ali (Ubunge).
Katika Jimbo la mkanyageni Tahir Aweis Mohamed (Uwakilishi) na . Mohamed Habibu Juma Mnyaa (Ubunge) na Seif Khamis Mohamed Jimbo la Mkoani (Uwakilishi) na Ali Khamis Seif (Ubunge) wakati Jimbo la Mtambile Abdalla Bakar Hassan (Uwakilishi) na Masoud Abdalla Salim (Ubunge)
Wagombea hao kwa tiketi ya Chama cha wananchi CUF ndiyo wanatarajia kuchuana na vyama vingine vitakavyosimamisha wagombea katika uchaguzi wa mwaka huu.

chanzo: mwananchi

No comments:

Post a Comment