WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Saturday, July 9, 2011

WAMACHINGA VS SERIKALI TANZANIA

Wamachinga na Harakati za Kujikomboa au ni harakati za kuwakomesha wengine?

Maswali haya wameulizwa na waandishi wengi sana wa habari kuhusu wamamchinga zidi ya Serikali

·        Je ni nini chimbuko la wamachinga?
·        kwanini 'wamachinga' wanakuwa ni tatizo ?
·        je huduma wanayoitoa inatakiwa na wananchi au haitakiwi ?
·        Ni njia gani zinazoweza kufanyika ili tatizo ligeuzwe ni fursa ya kiuchumi kwa manufaa ya wote? 
·        Je wa wafanyabiashara hao ni wa rika gani wanafikia wangapi hivi sasa?

Ni ukweli kuwa wamachinga ni wachuuzi waliozagaa katika maeneo tofauti wakifanya shughuli zao kiholela ambao waiibuka kwa wingi miaka ya 1980s wakati wa sera za Ruksa. Ni ajira ambayo inaweza kusemwa sio rasmi kama hawalipi kodi lakini kama wanalipa Kodi ni ajira Rasmi kwani taifa linafaidika na kodi yao na kwa msingi huo, na kwa upande mwingine na wao wnafanikiwa kupata riziki inayowasaidia kuendesha maisha yao

Idadi ya Wamachinga “nifikiri” ni  zadi ya wafanya biashara milioni moja: kwa upande mwingine kama ajira zaidi ya Milioni moja zimetengenezwa hapa, taifa limepunguziwa mzigo wa kuwatafutia ajira vijana hao.

Kwa nini wamamchinga wengi wanazagaa sana?
Nafikiri tuyaangalie maeneo ambayo pengine serikali wamewapangia hawa wamamchinga; je Maeneo  hayo yanajitosheleza?  Je yanavutia kibiashara, je kuna usafiri wa kuweza kuwaunganisha wafanya biashara hawa na wateja?

Je wakifukuzwa na wakakosa kuingiza ridhiki hata ya shilling mia moja nini kitatokea?
 Serikali inatakiw akuwa makini kwani, Nafikiri wamachiga wengi kama watafukuwza bila kupewa msaada woote, na kubaki kuwa hawana kazi,watagueka vibaka na kuliletea taifa  na raia wake.

Je serikali kuwafukuza wamamchinga ni suluhisho la tatizo?
Kuwaondoa wamachinga kabla ya kuwaandalia maeneo mbadala ya kufanyia biashashara zao ni mfumo mbaya wa namna serikali isivyojali maisha ya watu wake. Hakuna ustaarabu ulio bora zaidi duniani zaidi ya ule wa kujali uhai wa mtu kwanza kabal ya kumpokonya rizika yake. Wenzetu walioendelea wana progam kama kuwalipa raia wao ambao kwa namna moja au nyingine wameshindwa kufanya kazi “ unemployment Payments” au msaada wa chakula kwa familia za kipato kidogo “ food stamps” hata nyumba za watu wenye vipato vidogo “ low income Housing” sasa tunapowafukuza wamamchinga tunawapa msaada gani? Zaidi ya askari Mgambo kuwapora Mali zao

Tunaiomba serikali pamoja na kufanya maamuzi ya kuwaondoa wamachinga bila utaratibu makini, bado ina nafasi ya kuhakikisha inaboresha mazingira ya machinga hao kufanya biashara huko walikopelekwa, malalamiko ya machinga yanayoendelea hadi sasa kuwa huko walikopelekwa palikuwa tayari pamenunuliwa na baadhi ya watu ambao si wafanyabiashara ni mfano mbaya wa utekelezaji wa zoezi hili na serikali inapaswa kuwajibika katika hilo mapema iwezekanavyo.

Je mfumo wete wa elimu ya msingi inatusaidia katika kutatua tatizo la wamamchinga kuzagaa zagaa?
Nafikiri tunahitaji (innovative education system) mwanafunzi anayehitimu elimu ya msingi au sekondari asiwe tegemezi na badala yake awe mbunifu kwa maendeleo yake binafsi na kwa  Taifa. Zama hizi  zinahitaji hat kam ni mmachinga  inapaswa kuwa mbunifu. Tusitegemee wachinga bila ubunifu katika hizi zama za sayansi na teknolojia.

Kama taifa tutaweza kuuwezesha mfumo wetu wa elimu ukawafundisha vijana wetu Sayansi na teknolojia hii itakuwa ndiyo njia pekee ya kuokoa nguvu kazi inayoendelea kupotea kwa kujiunga na mfumo maisha wa machinga nchini Tanzania.

Je yanayotokea sasa sehemu mbali mbali za wamachinga kupigana na polisi na kuharibu mali za watu wengine hata kuiba ni sahii?
Katika jamii ambayo mambo yake mengi yako shaghalabadhala saa zingine inaonekana ni uonevu na dhuluma kuanza kukamata wavunja sheria wadogo wadogo wanaokidhi haja zao kila siku za. Tatizo hakuna  hakuna mipango madhubuti na mibadala ya kusaidia na kuwafanya wamachinga wajisikie kuwa wanatakiwa kubadilika na kufanya biashara zao kwa taratibu zinazoeleweka; kinachotokea kila tatizo likijitokeza na mapigano kuumizwa na mali kuharibiwa;


Serikali inatakiwa ifanye nini?
Ni ukweli ambao haukwepeki kuwa nchi imeshindwa kutoa ajira kwa vijana na vijana wameamua kujiajiri wenyewe kwa kuuza chochote kile wakipatacho mitaani.

Nakubali kabisa kwamba kitendo cha wafanyabiashara ndogondogo kuamua kufanya biashara zao sehemu yoyote wanayotaka na kujenga vibanda vyao vya biashara sehemu yoyote bila kuzingatia mipango miji ni ukiukaji wa sheria na taratibu za nchi kuhusiana mipango miji.

Kwa hali hiyo suala la biashara ndogondogo ni suala la maisha.
Kwa mtazamo huo tatizo la Wamachinga ni pana kuliko kuwavunjia vibanda vyao na kuwahamishia sehemu maalumu. Ni suala ambalo linatoa wito wa kurekebisha mfumo mzima wa kiuchumi na kijamii tulionao.

Ni suala ambalo linaitaka Serilaki kusimamia utekelezaji wa sheria na kutumia mbinu zote ili kuepusha hasara kwa raia wake. Ni bora kukinga kwa kutumia busara kuliko kuboboa kwa sababu za siasa;
Kwa nini tusiwe tekeleze sherai ya kuwazuia kujenga vibanda sehemu ambazo sio stahili?, tukiweza kuzuia ujenzi ni utu kuliko kuliko kumbomolea hata kama anastahili kubomolewa kwa kukiuka taratibu.

No comments:

Post a Comment