WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, May 16, 2011

TATIZO LA MHESHIMIWA DR. MAGUFULI NI NINI HASA?


                         Dr. John Pombe Magufuli

Kumekuwa na kilio kutoka kwa watendaji ndani ya Wizara ya Ujenzi ambayo Mheshimiwa Dr.Maguful anaongoza na kwa watendaji wengine nje ya wizara yake kama vile, viongozi wa manispaa zinazounda jiji la dare s salaam na hata pengine kutoka kwa wananchi kuhusu  utendaji wa Waziri Magufuli wakilinganisha utendaji kazi wake na Ubabe;

Swali amabalo mimi najiuliza je kama Waziri Dr. Magufuli utendaji wake unaonekana ni wa ubabe ni kwa nini?  Au watendaji wetu wamejenga mazingira ya kufanya kazi zao bora liende bila umakini wa kuzingatia sheria? Je kama Waziri anatekeleza Majukumu yake kisheria na sheria hiyo ili ifanikiwe inahitaji nguvu za ziada je huu ni ubabe?

Nafikiri umefika wakati ambao kama haturidhiki na utendaji kwa mantiki hii wa Mheshimiwa Dr. Magufuli na tunajua kabisa anakwenda kinyume na maadili ya uongozi, kinyume na sheria inayompa mamlaka ndani ya uwezo wake kama waziri hebu tuwe wakweli na tuyaainishe mapungufu ya ubabe huu ili hoja zetu ziwe za msingi; uropokaji na kusema sema tu bila kuwa na vielelzo nafikiri kama Waziri anatekeleza Majukumu yake kisheria na kuzielewa sheria hautapunguza kasi ya utekelezaji wake hata kama utakuwa wa ubabe; na tukumbuke kuwa binadamu bila kumshikia bango hasa kwetu sisi na nchi zetu hatutafuata sheria katika maisha yetu ya kila siku;

Hata mheshimiwa Rais Jk ameona hili ndio hata sasa ameanza kuwa mkali dhidi yenu ninyi watendaji wa serikali na kuwaeleza wasioweza kufanya kazi kwa kufuata sheria na maadili ya utumishi wa Umma wajiondoe; kauli amabazo zilikuwa hazipo; wakati wa kubebana umepita; tukitaka kuendelea lazima mambo ya kesho tuyaone leo na tusiyafumbie na kuyaonea aibu, hata kama utekelzaji wake sasa utaonekana mbaya lakini kesho kila mtu atafurahia; ebu jikumbushe ujenzi wa sehemu ya barabara ya ubungo –kimara mpaka kibaha; leo tunasema nini bado tunasikitika au tunafurahia hatua hiyo kubwa ya maendeleo?

Tuwe wakweli tuwajibike inavyotakiwa, tusimamie sheria ili kesho sheria isimfanye kiongozi mwingine kuonekana mbabe wakati akitekeleza mapungufu ya jana.

No comments:

Post a Comment