WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Saturday, April 30, 2011

REFLECTING BACK- POLITICAL CORNER;



Why opposition parties failed in the 2010 General Election in Tanzania?


1.  The ruling party CCM has very strong bases in various villages around the country where there is large number of voters while


2.  Opposition parties have strong holds in urban centers were the number of voters is low but the euphoria is huge


3.  The president has too much power to appoint and disappoint, this leads to a large number of senior government officials to be presidential appointees hence obedient to the president; 



4.  Power mongering, the big opposition parties of CUF, CHADEMA, NCCR were competing against each other instead of joining hands to present one candidate for the opposition, this lead to spread of votes and creation of weakness against opposition




Friday, April 22, 2011

MSHIKE MSHIKE BUNGENI



Kauli ya Spika wa Bunge Anne Makinda:  Wabunge wanafanya mambo ya KIJINGA ina maana gani kwa jamii
·        Tufunge mlango tupigane”
·        "Mmezowea kutuburuza"
·        "Naomba mjiheshimu hapa si sokoni, Watanzania wengi wanawaangalia mnavyofanya mambo ya kijinga na kupiga kelele,"

Tusiwalaumu tuu wabunge, tujiulize wameingiaje bungeni? Tatizo la ujinga kama uko ambao unatokea Bungeni kama alivyosema mheshimiwa Spika linatoka na sisi tunaowachagua; je tunatumia vigezo gani kujua kweli kama WABUNGE TUNAOWACHAGUA wanaweza kujenga hoja za kweli na sio itikadi tu ya chama atokacho mbunge? Kama bunge halifanyi kazi yake vizuri lawama ni kwetu wananchi tuliowachagua.

Kwa watanzania wengi ambao walibahatika kufuatilia nini kilikuwa kinajili bungeni Dodoma wiki chache zilizopita watakubaliana nami kuwa tuliweza kupata kioja cha kuhitimisha mijadala ya bunge katika kikao chake cha 10.

Ilimlazimu Mheshimiwa Spika kutamka maneno ambayo nafikiri yalikuwa hayastahili kutamkwa bungeni kwa heshima na majukumu makubwa ya kazi ya bunge kama chombo muhimu sana katika kusaidia kuendesha shughuli za serikali; katika majukumu ya Kiuwakilishi (representational),utungaji wa sheria (legislative), upitishaji wa bajeti, mapato na matumizi ya nchi (budgetary and resource approval) pamoja na uwajibishaji wa serikali iliyoko madarakani (accountability). Bunge pia ni chombo cha kutathmini mwenendo wa jumla wa kisera unaopendekezwa na serikali ili kubaini kama mwelekeo wake unasawiri matakwa ya wananchi walio wengi nchini. Aidha ni kazi ya Bunge katika mfumo wa kidemokrasia kuhakikisha kuwa matendo ya serikali iliyopo yanakidhi matakwa ya jamii wanayoiwakilisha, ikiwa ni pamoja na kuunga mkono hoja nzuri na kupinga zile zinazoonekana kukinzana na maslahi ya jumla ya kitaifa.

 Je Bunge letu linatekeleza kwa umakini majukumu haya au bunge kwa sasa limekuwa ni chombo kikuu cha ushauri tu kwa serikali bila kuwa na meno ya kuiwajibisha serikali pale ambapo inakosea?
Kwa maneno mengine wabunge wamechaguliwa na wananchi ili wawakilishe katika kuisimamia serikali. Hivyo wabunge hawatakiwi kabisa kupeleka mawazo na mitazamo yao wenyewe. Wanatakiwa wanapozungumza Bungeni au kupiga kura ni lazima wafikirie wapiga kura wao wamewatuma kufanya nini. 
Je tuliwatuma waende kupigana bungeni? Au kugeuza bunge kuwa ni soko kama mheshimmiwa makinda alivyowakemea wabunge wenzake;

Je wabunge wetu ambao tumewachagua  wanao uwezo wa kutawala katika kuchangia hoja bila kupigana na kutishana? Au ni wale ambao wanapenda sana kutawala hata kama hawana uwezo wa kutawala.”

Je wabunge wanafahamu kuwa Bunge letu la sasa bado lina nguvu kubwa ambayo halijaweza kuitumia vyema. 
Nafikiri tatizo la wabunge wengi wanatumia muda wao mwingi kulalamika na kushangaa mapungufu.  Wanatakiwa wawe na uwezo wa kupangua na kupanga upya mambo wanavyoona wao inafaa bila kujali maneno na minong’ono ya wanafiki wachache na wasio jali maslai ya wengi au kuwa na muono wa mbali.
Je wabunge wetu wengi ni kundi gani?

Je tunao wabunge wenye uwezo wa uongozi na wito wa uongozi kwa kuweka maslahi ya taifa mbele kwa manufaa ya watu.

Wabunge wetu wameingia bungeni kama moja ya njia sahihi za kujipatia neema, ubinafsi na maslahi binafsi;  
 
Je abunge wetu ni wale wenye uwezo mkubwa wa kushawishi kutokana na uwezo wao wa  kiuchumi, haautegemei mshahara wala marupurupu ya ubunge; Hawana muda wa kuchangia mijadala ya bungeni, wala hawana maswali, ila kwa sababu wana nguvu kubwa kiuchumi na jeuri ya pesa, wanao uwezo wa kuwabuluza wabunge wengine na kuhakikisha kuwa wanalolitaka liwe, ndilo linakuwa. Kwa maneno mengine aina hii ya wabunge ndio viongozi wenye nchi.

Friday, April 15, 2011

RASIMU YA KATIBA MPYA ISIYO KIDHI HAJA YA WATANZANIA WENGI

MWENENDO HUU WA MCHAKATO WA KATIBA MPYA UTATUFIKISHA WAPI?

Ilikuwa ni shangwe kubwa pale Rais wa Jamuhuri ya Tanzania Mheshimiwa JK alipotoa  taarifa rasmi kuwa serikali yake iko tayari kushughukikia mapendekezo ya kuandaa katiba mpya

Watanzania wengi kwa ujumla walikuwa wamejawa na shauku na hamu ya mabadiliko ya katiba wakijua kuwa wakati sasa umefika kwa wananchi wa Tanzania kuwa na katiba mpya ambayo itajumuisha misingi ya taifa itakayokuwa imelinda maslahi ya wananchi  kwa ustawi na maendeleo yao. 

Kwa msingi huu toka kongamano la kwanza ambalo lilifanyika chuo kikuu cha dar es salaam chini ya wenyekiti wa Prof Issa Shivji na Jenarali Uliwengu wananchi wengi walijitokeza wasomi, wanasiasa wananchi wa kawaidi na vikundi mbalimbali vya jamii; ili kushauri katiba mpya iwe na sura gani, na zoezi nzima la upatikanaji wa maoni uwe vipi.

Kama Makamu wa Kwnza wa serikali ya umoja wa kitaifa  Maalim Seif alivyo wahi sema“hali inavyokwenda wananchi wengi wamehamasika kutaka kutoa maoni juu ya kuwa na katiba mpya hivyo ni vizuri wananchi wakapata nafasi ya kutoa maoni yao kwa kuwa katiba inayowashirikisha wananchi ndio katiba madhubuti nchini”.

Msisitizo hu unatokana na dhana kuwa iwapo Wananchi wataweza kushiriki kikamilifu katika mchakato huo wa kuandaa Katiba mpya  itasaidia katika kuepusha  dhana kuwa suala la kuandika Katiba sio la kikundi Fulani, chama fulani au ni la Wanasheria,  kwa vile wao wamebobea katika sheria hasa za masuala ya Katiba.  

Wengi walipendekeza kuwa ni muhimu  wananchi wote, washirikishwe ikiwa ni pamoja na wale wasiojua kusoma wala kuandika na wanajamii mbalimbali mijini na vijijini watakavyowezeshwa kuweza kushiriki katika kuweka misingi ya uandikaji Katiba, kutoa maoni katika mijadala ya awali na kwa Tume ya kuratibu maoni, pamoja na kuchagua wawakilishi kutoka miongoni mwao kushiriki katika vyombo muhimu vya kujadili mapendekezo na rasimu za Katiba ikiwemo wajumbe wa Mkutano wa Kitaifa wa Katiba na mara nyingi mjadala unaishia kwenye kikao cha  Bunge Maalum la Katiba.

Nchi inapoamua kuandika katiba mpya ukweli wake ni kuwa ni  upanuzi wa demokrasia na maendeleo ya nchi kwa kuwa na katiba ya nchi inayoonyesha utashi wa wananchi.

Kazi ambayo iko mbele yetu ni kubwa sana sisi kama  Watanzania ni lazima tuhakikishe kuwa mchakato wa kufikia katiba mpya unakuwa huru, yenye uwigo mpana sio wa kulindana bali ni wa uwazi na ambao una uhalali wa kutosha kuweza kufikia kusema kuwa Katiba itakayopatikana kweli imetokana na watu na mazingira yetu.

Mchakato wa kufikia Katiba Mpya usipoweka misingi ambayo utahakikisha wananchi wote wana nafasi sawa ya kuchangia mawazo yao ya dhati  bila kuogopa au kununuliwa tutakuwa tumefanikiwa kuifikisha katiba mahali pazuri kwa usalama wan chi bali  kama kutakuwa na mchakato mbovu tutakuwa tumeiharibu kabisa nchi yetu na maendeleo yake kidogo ambayo tunayo hivi sasa.
Lengo la kila mtanzania tunatamani kuandika Katiba Mpya ili kuweza kukiachia kizazi kijacho mfumo mzuri wa utawala ambao utawapa nafasi ya kufanikiwa katika maisha na mipango yao na ambao utawahakikishia mtiririko mzuri wa mahusiano na kuwajibishana kati yao na watawala wao.

Nini kinatokea sasa?

1.  Wengi wamepinga rasimu hiyo ya katiba kwa sababu tofauti mojawapo ikiwa inafanyika katika kipindi kifupi na pengine wananchi wengi hawatapata nafasi ya kutoa maoni yao.

2.  Mikutano iliyofanyika Dodoma na Dar es salaam imeonyesha mapungufu makubwa katika siku za awali tu; je kamati au wizara inayoshughulikia rasimu ya kuratibu maoni ya utayarishaji wa katiba mpya kweli wamejiandaa kwa katiba mpya au ni ubabaishaji tu?

3.  Je Kamati waliangalia mahitaji halisi ya wananchi na kiu ya wananchi kutoa mawazo yao?

4.  Hebu angalia mambo yalivyokuwa Dar es salaam, ilikuwa ni tatizo kubwa pale ukumbi ulipojaa wananchi wengi ambao kwa sababu moja au nyingine waliishia kulala tu , nini kilikuwa kunaendelea, je wapi tutapata hiyo rasimu bora ambayo inakizi haja wakati hatuna ushindani katika uchangiaji hoja wakati wananchi waliopokelewa au kuletwa katika ukumbi huu kwa sababu moja au nyingine waliishia kulala tu?

5.  Kule Zanzibar kwa kulitokea tukio la kuchana Rasimu hiyo wananchi na wachangiaji wakiwa wamejawa na hasira ya utaratibu mzima wa uandaji na mwonekano wa rasimu hiyo; Je ni kweli kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar hakuhusishwa kikamilifu? Je Rasimu unaelezaje swala la Muungano? Je linakizi haja kwa pande zote? Je wale wanaona wanamezwa wamepewa kinga gani ili wasipatwe na janga hilo?

6.  Je kama zoezi hili halitakwenda vizuri kwa kigezo cha muda nani atawajibishwa kulipa gharama halisi ambayo imetumika  katika maandalizi hayo? Ikumbukwe kuwa bado pesa hiyo ni ya mlala hoi.

HITIMISHO

Lazima tukubali kuwa Mheshimiwa Rais amebariki utaratibu mzima wa uandikaji wa katiba upya, hili ni jambo la kihistoria na ambalo halitakiwi kufanyiwa mzaha na watendaji wachache kwa masilahi yao binafsi au chama chochote,  hebu tulifanye jambo hili kwa masilahi ya wananchi wa Tanzania na sio kwa manufaa ya wana siasa na vyama vyao;
Mungu ibariki Tanzania na watu wake

Tuesday, April 12, 2011

KIKWETE NA MCHAKATO NDANI YA CCM

MZEE MAKAMBA INATOSHA  NA INAFAA UPUMZIKE
                          SEHEMU YA KWANZA


Mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi Mheshimiwa Rais JK alivunja kamati Kuu ya CCM  huko   Dodoma tarehe 9/4/2011 tukio ambalo lilihusisha kustaafishwa kwa  Katibu wake Mkuu mzee wetu  Bwana Yusufu Makamba;

Utendaji wa kusua sua wa Mzee makamba umekuwa kilio cha siku nyingi cha wanachama wa CCM; wengi walikuwa hawaridhishwi na utendaji wake wa kazi hasa katika maswalal yote ambayo yanahusu kumshauri Mheshimiwa Rais kama kiongozi wa serikali na kama Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi;

Pamoja na mapungufu Mengi ya Mzee wetu Makamba lakini Mheshimiwa Rais ataendelea kubeba lawama kwa kuchelewa kuliona tatizo hili pamoja na kilio kirefu cha wana CCM kuwa Makamba alikuwa mzigo kwa Chama katika ufanisi;


Pamoja na uamuzi huu Mzuri na mzito swali la msingi hapa ni hili Kwa nini imemchukua Mwenyekiti wa Chama nuda mrefu kusafisha utendaji ndani ya chama?


kama Kweli  kamati yake kuu ya chama chake ilikuwa haifanyi kazi vizuri, na imemwangusha kwa kiasi kikubwa, kwa nini alikubali  kuendelea kuibeba?, "ni sawa kama kuendesha gari ambalo halina balance nzuri ya upepo unaotakiwa  kwenye matairi yake, kwani kabla ya ajali utalazimika kutumia  nguvu zaidi katika kuhakikisha kuwa gari hilo inakwenda vizuri na haliachi barabara", kitu ambacho kimekuwa sicho, kwani katika hali tofauti tofauti Mwenyekiti amejikuta akishindwa kuhimili mikiki mikiki ya barabarani ambayo imekuwa ikisababishwa na ubovu wa matairi( watendaji) kwa au kujali masilai yao binafsi, na kupoteza mwelekeo wa sera na dira za Chama;

Sijui nini kimemtokea Dereva Wetu(mheshimiwa Rais Na Mwenyekiti wa CCM) mpaka ameamua kulitosa gari hilo amabalo  fundi wake Mkuu alikuwa Mzee Makamba; na kuamua kuchukua gari nyingine; 


Kwa tafakari yangu na kama nilivyowahi kuandika katika blog hii huko nyuma kuwa  kuwa Mzee Makamba alishindwa kutekeleza yafuatayo;

  • ·        Kutoa ushauri sahii kwa wakati sahihi



  • ·        Kutumia sana sera za ubabe wakati hakuna haja ya sera hizo
  • ·        Kutumia lugha ambazo zilikuwa hazivuti ushawishi kwa wanachama wake na wananchi kwa ujumla
  • ·        Kushindwa kutoa ushauri mzuri kwa Mwenyekiti wake wakati yeye ndio mtendaji mkuu wa chama;

Tukumbuke siasa yenye msingi wa utawala Bora sio ubabe na ukitumika sana huondoa busara na hekima; uongozi bora unatawaliwa na uongozi hekima, ambayo itazaa uadilifu, uwajibikaji na umoja.

Wakati umefika kama saa izungukavyo, saa yako imefika kwa wewe mzee wetu Makamba  uweze pumzika,  inatosha hapo ulipomfikisha Mwenyekiti panatosha, tuwaachie na wengine nao tuone watamsaidiaje Mwenyekiti katika kuitengeneza Tanzania yetu na kuleta neema kwa watanzania wote.




Mungu Ibariki Tanzania na Afrika


Thursday, March 31, 2011

UWAJIBIKAJI WA PAMOJA WA SERIKALI

KAULI ZINAZOTOFAUTIANA MIONGONI MWA WATENDAJI WAKUU WA SERIKALI NI WAJIBIKAJI WA PAMOJA?


Uwajibika wa pamoja kati ya watendaji wakuu wa serikali ni dhana muhimu katika utekelezaji wa majukumu na sera za serikali;
Kila kiongozi anamchango ambao unaweza kusaidia kuleta  mabadiliko katika jamii, la msingi katika kufanikisha hilo kunahitajika kuwepo kwa njia makini, kufuata taratibu na kuwa na mawasiliano ya hali ya juu (effective Communication) miongoni mwao. Ni muhimu kuhakikisha kuwa hoja zao na utekelezaji wao unachambuliwa katka vikao muhimu vya pamoja (in Camera) na kama unafaa  utumike  katika kutekeleza majukumu yao ( ministry Responsibility) katika wizara na idara zao husika katika kuwaleta maendeleo wananchi wake.

SERIKALI yoyote yenye mafanikio ya uwajibikaji wa pamoja ni ile ambayo inaheshimu misingi ya utawala bora, ambayo moja ya nguzo zake kubwa ni nidhamu ya utendaji wa kazi na mahusiano mazuri ya kazi kati ya watumishi, wakiwamo viongozi wa kada mbalimbali.

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania mheshimiwa JK katika moja ya mikutano yake pamoja na watendaji wake wakuu, amewakumbusha wateule wake kuhusu uwajibikaji wa pamoja (collective responsibility) katika kuongoza nchi, akisisitiza kuwa uwajibikaji huo unaelezwa kwa ufasaha katika Hati Maalum (Instrument) ya Majukumu ya kila Wizara. Katka msisitizo Rais Kikwete alisema kuwa
·        Uzoefu unaonyesha kuwa Mawaziri wengi ni wazito kufanya mawasiliano na wananchi hata pale ambako Wizara imefanya mambo mengi mazuri. Hivyo, Mawaziri muwe mstari wa mbele kuelezea mafanikio ya utendaji wa Serikali katika Wizara zetu,” ameelekeza Rais Kikwete na kuongeza: 
·        Lazima ujengwe utamaduni wa kudumu wa kuwasiliana na wananchi wote ambao ndio waajiri wetu kupitia kura zao. Mawaziri wote tumieni Vitengo vyenu vya Mawasiliano na vyombo vya habari kwa ustadi ipasavyo,
·        Ni rahisi kunyoosha vidole, na kuwabandikia  watu wengine lawama za matatizo haya.


JE KUWEPO KWA TOFAUTI ZA KAULI KATIKA SIKU ZA KARIBUNI MIONGONI MWA WATENDAJI WAKUU WA SERIKALI INAONDOA UWAJIBIKAJI WA PAMOJA AU INAIMARISHA UWAJIBIKAJI;

Katika siku hizi za karibuni kumekuwako sana na kutofautiana kwa kauli miongoni mwa watendaji wakuu wa serikala huhusa mawaziri kuhusu hoja moja ambazo zinaishia kuwa na mielekeo miwili tofauti  na misimamo tofauti;

kuhusu swala la loliondo waziri mwenye dhamana ya Afya na Ustawi wa Jamii Dk Haji Mponda ilimwagiza Mkuu wa Mkoa wa Arusha kusitisha kwa muda utoaji wa huduma hiyo hadi itakapojiridhisha kwamba dawa inakidhi ubora na inatolewa katika mazingira safi; agizo hilo likiwa mbioni kutekelezwa jana Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi alisema Serikali haina tena mpango wa kuzuia huduma hiyo kwa kuwa inahusisha imani za watu

kuhusu bomoa bomoa waziri mwenye dhaman  Dr John Pombe Magufuli  alijikuta akipigwa stop na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wakati akihutubia mkutano wa hadhara alipomuagiza, waziri  John Magufuli kuwa asitishe mara moja ubomoaji wa majengo yaliyo katika hifadhi ya barabara hadi Baraza la Mawaziri litakapoamua vinginevyo. Kama haitoshi Mheshimiwa Rais JK alipotembelea wizara ya Ujenzi alimuagiza Waziri Magufuli kuzingatia kile alichokiita “utu” na “ubinadamu”

kwa nini Rais Kikwete na Waziri Mkuu Pinda waliona vyema kumkaripia Waziri Magufuli hadharani, tena kwa kauli za kumdhalilisha mbele ya wafanyakazi na wapigakura wake ili aonekane kama mtu katili asiye na utu wala ubinadamu? Kwa nini hoja na kauli zao hazikupelekwa kwanza katika Baraza la Mawaziri kama kweli walikuwa na nia ya kufanya hivyo? Na kama wanaona kuwa sheria inayosimamia hifadhi za barabara haifai kwa nini wasizungumzie haja ya kupeleka muswada bungeni ili sheria hiyo iwekewe “utu” na “ubinadamu” badala ya kumsingizia waziri huyo kwamba anatumia ubabe”?


HIVI SERIKALI HAINA MGAWANYO WA MAJUKUMU KWA MAWAZIRI WAKE
 Wakati huo huo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utawala Bora, Mathias Chikawe, alisema ni kosa kwa mawaziri kupingana hadharani na kuongeza kuwa kama kuna mwenye dukuduku kuna namna ya kuwasilisha maoni yao. Kwa mujibu wa Chikawe, taratibu hizo ni kwa mawaziri husika kuwasiliana na kushauriana na inapotokea anayeshauriwa haelewi, upo utaratibu wa kupeleka maoni hayo kwa Waziri Mkuu.

maswali ya kujiuliza sasa  je na pale ambapo Waziri Mkuu na hatimaye Mheshimiwa Rais hawaoni umuhimu wa kutumia vikao vya Baraza la mawaziri katika kurekebisha jambo lolote na kumkosoa waziri mwenye dhaman mbele ya watu bila waziri kujua nini kinaendelea;
Je kuna umuhimu gani wa wale ambao wako chini yao kutekeleza huo uwajibikaji wa pamoja?  Kama waandishi wengi walivyo hoji, Je Kwa nini hoja na kauli zao  hazikupelekwa kwanza katika Baraza la Mawaziri kama kweli walikuwa na nia ya kufanya hivyo? Na kama wanaona kuwa sheria inayosimamia hifadhi za barabara haifai kwa nini wasizungumzie haja ya kupeleka muswada bungeni ili sheria hiyo iwekewe “utu” na “ubinadamu” badala ya kumsingizia waziri huyo kwamba anatumia ubabe”?  je  kumkaripia Waziri Magufuli hadharani, tena kwa kauli za kumdhalilisha mbele ya wafanyakazi na wapigakura wake ili aonekane kama mtu katili asiye na utu wala ubinadamu inaimarisha uwajibikaji wa pamoja au inabomoa?
Nafikiri viongozi wetu wengi wanatakiwa watumie muda wa kutosha kujifunza faida za” effective communications” na wapi wanastahili kusema hoja gani kwa faida ya nani?

Kama taifa tutuweza sana kusonga mbele pale tutakapo weza kuondoa kabisa hulka za kisiasa katika kutekeleza maendeleo ya wananchi, busara na hekima ni silaha ya uwajibikaji wa pamoja 

Tuesday, March 22, 2011

JE SERIKALI YETU TANZANIA INAYO WASHAURI WAZURI?

JE MATATIZO YANAYOENDELEA KUTOKEA TANZANIA LEO: JE RAIS WETU AMEKOSA WASHAURI WAZURI?


Sehemu ya Pili



katika hizi siku za karibuni kumeanza kujitokeza maandamano yenye “sura ya amani” yakiwa na kibwagizo cha kudai maisha bora kwa watanzania, ambayo yanaendeshwa na CDM yakishinikiza serikali ya CCM kutatua kero za wananchi kwa haraka iwezekanavyo. Ikumbukwe kuwa Tangu 1989, mapambano ya raia yasiyotumia nguvu yamesababisha kuvunjika kwa utawala wa kikomunisti wa chama kimoja cha Urusi, vyama Ulaya ya mashariki, Jamuhuri ya Baltes na Mongolie na muungano kwa amani wa Ujeremani na kukomesha utawala wa ubaguzi wa rangi wa Afrika kusini. Ijapokuwa mapambano hayo, pengine yalikuwa na vifo (Birmanie 1988, Chine 1989), kuna tofauti kabisa na mapinduzi ya kale kama yale ya Amerika ,Ufaransa, Urusi, Uchina yaliyogupikwa na mauaji mengi zaidi. Pembeni ya maandamano makubwa yanayoonekana wazi ya kutafuta mabadiliko ya utawala, kuna vyama vya kisiasa ambavyo vinatumia mwanya wa kuuza sera zao kwa wananchi dhidi ya chama kilicho madarakani kwa msingi wa kuwa kimeshindwa kuatatua kero za wananchi. Je chama ambacho kipo madarakani kinatakiwa kujipanga vipi? Ni ukweli ambao haufichiki kuwa Rais kama kiongozi wa juu kabisa katika nchi anatawala kwa msaada mkubwa wa washauri wake; Je kama washauri wameiona hali hii wanamshauri nini?

Swali nyingine ninalojiuliza ni kitu gani kitapelekea uwepo wa maandamano haya yenye kibwagizo cha amani (sauti ya umma)? je yanakuja kwa sura ya kudai nini? ni uhuru wa watu, usawa , maendeleo mazuri ya kwa wananchi wote?, au ni sehemu tu ya kuanzisha uvunjaji wa amani miongoni mwa watanzania? ama kuna alama gani za ki-historia au za nyakati hizi za siasa, uchumi, jamii, utamanduni, zinazo onyesha kuwa jamii ya kitanzania imefikia mwenendo wa maisha ya kutojali na kutotii serikali yake iliyochaguliwa kihalali? Hapa namnukuu mwanafalsafa Jean Jacques ROUSSEAU (1712 – 1778) alivyoandika kwamba “wanainchi ni lazima waheshimu viongozi wao walio na majukumu ya kutoa amri kwa ajili ya wote. Serikali inayo haki ya kupiga vita watu wote wasiotii amri zake na kuwahukumu kifo. Pia, serikali inayo mamlaka ya kuamru watu wajitoe muhanga kwa ajili yake.”

Pengine tuwaulize washauri wa Mheshimiwa Rais kuwa je mabadiliko gani yametokea ndani ya jamii iliyokuwa imetulia bila msisimko wa kisiasa, na leo hii imekuwa tayari kuungana na vyama vya siasa katika maandamano yanayoendelea sehemu mbalimbali hata wengine wakiwa tayari kuyapoteza maisha yao, kwanini?
·        Kujitokeza kwa wingi katika maandamano haya ya amani ni kielelezo hali halisi kuwa wananchi wamechoshwa na:
·        Ugumu wa maisha na wakati huo huo kundi la watu wachache wanafaidi rasilimali za nchi na watoto wao wakifaidi elimu bora nje ya nchi
·        Wananchi wanasikitika kuona kuwa taifa lenye rasilimali nyingi na za pekee dunia linaendelea kuwa masikini na watoto wa taifa hili wakiendelea kuwa wapumbavu kwa kukosa haki ya msingi ya elimu

 Ni ukweli siopingika kuwa wananchi wanachoshwa na hali hii ndio maana kiongozi mwinigine yeyyote anayejitokeza  na kuwagusa katika kuboresha maisha yao, wanakuwa tayari kumkimbilia na kuamaini kuwa ataleta khali nzuri ya maisha hata kama hali haitabadilika; Inasikitisha miaka 49 ya uhuru Tanzania bado  haina umeme wa uhakika; maji safi na barabara, na kadhalika; wananchi wamechoshwa na umasikini katika nchi yao tajiri; Matatizo yote ambayo yanajitokeza leo wananchi wanona  in kazi ya mikono Serikali na chama kilicho madarakani;

Rai yangu washauri wa Mheshimiwa Rais wetu wawajibike ipasavyo kwa faida ya taifa na sio kwa masilahi ya kikundi kidogo cha watu; na mheshimiwa rais akiona ushauri wao hauna tija kwa wananchi basi awawajibishe kwani taifa hili lina rasilimali kubwa sana ya wataalamu ambao wako tayari kuifikisha nchi mahali pazuri sana kwa manufaa ya wote.


Mungu Ibariki Tanzania na utuepushe na fikra zozote za kuvunyika kwa amani 

Saturday, March 19, 2011

JE SERIKALI YETU TANZANIA INAYO WASHAURI WAZURI?

JE MATATIZO YANAYOENDELEA KUTOKEA TANZANIA LEO: JE RAIS WETU AMEKOSA WASHAURI WAZURI?
                           Sehemu ya Kwanza

Tanzania tumebarikiwa kuwa na uchaguzi mkuu ambao ulifanyika kwa amani bila vurugu zozote za umwagaji wa damu, pamoja na kasoro hapa na pale, ambazo zilijitokeza kabla na baada ya upigaji kura;ambazo zilipelekea Chama cha Maendeleo na Demokrasia kutokuwa na imani na tume ya uchaguzi na hatimaye kususia matokea kwa msingi kuwa uchaguzi hakuwa huru na matokeo ya urais YALICHAKACHULIWA ili kumsaidia mgombea wa CCM kushinda uchaguzi huu  mwezi October 2010;

Maswali ya Msingi hapa Je washauri wa rais wa siasa , uchumi na huduma za jamii, na kadhalika  wanamshauri Rais wetu nini katika kushughulikia kero za wananchi na katika kutimiza ahadi alizozitoa wakati wa kampeni? Au wanakuwa kama bendera wakiogopa kusema ukweli kwa msingi wa kuogopa kupoteza ajira zao na wakijua kuwa kazi zao ni za msimu mfupi?

Baada ya uchaguzi tumeoona vyama vya upinzani vikiongozwa na CUF na CHADEMA wakiwahamasiha wafuasi wao katika madai ya kuandika Katiba upya , kilio hicho cha madai ya katiba mpya kilipata majibu kutoka kwa msheshimiwa Rais JK kuwa serikali yake iko tayari kuridhia mabadiliko hayo.

Tatizo nyingine ambalo bado limeendelea kuliweka taifa mahali pabaya ni pamoja na kukidhiri kwa vitendo vya rushwa (ufisadi uliobebea) ambao bado unaendelea kufanya na viongozi na washirika wao ndani ya serikali; tatizo hilo kwa hivi sasa  linahusishwa na tatizo sugu la kukosekana kwa umeme na wananchi kupinga kwa sauti moja malipo ya kampuni ya kufua umeme wa generator Dowans. Kama kweli huu ni mradi wa wazito ndani chama na serikali basi itafika mahali ambapo wananchi watalazimika kufuata msimamo wa Karl Marx (1818 – 1883) na Friedrich ENGELS (1820 – 1895) wanasema kwamba matajiri na wanaoshikilia vyombo vya utajiri mara nyingi hutumia nguvu kwa kukuza na kulinda mali zao. Ila, ungandamizaji wao unapofikia kilele, masikini wana haki ya kuleta uasi mkubwa kwa mageuzi ya kiuchumi na ya kisiasa. Ndio maana leo tunaona kuwa wananchi wengi wameanza kusimama kiume na kuanza kudai haki zao; wakiitumia kauli mbiu kuwa “hutulipi Dowans” hata kama serikali itaishia kulipa kwa siri lakini kilio cha wananchi kimeshasikika; washauri mpo na umeshauri nini katika utata huu wa zabuni za mitambo hii?

Mauaji wa raia kadhaa huko  Arusha ambayo yalitokea baada ya wafuasi wa CHADEMA kufanya maandamano yaliyokuwa yakipinga matokeo ya ushindi wa Meya wa arusha kwa tiketi ya CCM. Mauaji hayo katika msingi wowote ule yameendelea kuchafua historia nzuri ya nchi yetu na kutukumbusha kile kilichofanyika Zanzibar miaka kadhaa iliyopita; katika hili, je washauri wa rais waliishauri serikali kutumia nguvu kuzima maandamano hayo? Kama ndio je walifuata msimamo wa Mwanafalsafa Machiavel (1462 – 1527) katika maamdishi yake alishauri kwamba viongozi watumie nguvu ili wabaki madarakani na kulinda heshima za nchi zao. Pia anaomba viongozi wawe wenye busara na itakapohitajika, wawe wakali kama simba. Je huu ndio ni msimamo wa serikali yetu? Au ilikuwa bahati mbaya kwa kukosekana kwa mawasiliano mazuri miongoni mwa Taasisi husuka? Je taratibu za gani zifuatwe ili kuepusha hali hii siku za usoni? Hili ni jukumu la washauri wa Mweshimiwa Rais pamoja na busara na uvumilivu wa viongozi wetu;

Kumekuwako pia na uharibifu uliotokana na mabomu yaiyolipuka  Gongo la Mboto ambayo yamesababisha wananchi zaidi ya 20 kupoteza maisha na mali pia, swali la msingi hapa je taasisi zetu zinazoshughulikia usalama zinawajibika vipi katika ukaguzi wa vifaa vyao na wanatumia utaratibu gani wa uhifadhi wa vifaa ambavyo vinaweza kuleta madhara yatokanayo na mabadiliko ya hali ya hewa (Joto au baridi);je wanautaratibu wa kukagua vifaa hivyo kutokana na ukaji wa siku nyingi? Je washauri wetu wanamshauri Mheshimiwa Rais nini kuhusu uwajibikaji katika mazingira ya namna hii: Je katika kuhakisha kuwa hali hii haitokei tena je  washauri wa mheshimiwa Rais watamsaidiaje kwa faida ya watanzania wote?