WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Thursday, June 9, 2011

NINI KIFANYIKE KUEPUSHA AJALI ZA BARABARANI TANZANIA?


TATIZO LA AJALI ZINAZOENDELEA NA KUPOTEZA MAISHA YA WATANZANIA WENGI;


NI UBUTU WA SHERIA?


UBOVU NA UFINYU WA BARABARA ZETU


KIBURI CHA MADEREVA?

UBOVU WA MAGARI NA UBABE WA WAMILIKI?

Taifa la Tanzania limeendelea kushuhudia  mwendelezo wa ajali nyingi za barabarani ambazo zimeendelea kupoteza nguvu kazi ya taifa hili.  Kwa ujumla ajali hizi zimekuwa zikitokea kila kona wakati mamlaka za kisheria  zikiendelea kuhimiza kuwa zitahakikisha kuwa zitakomesha vifo vinavyoyokana na ajali hizo.husika kutekeleza yafuatayo;.
·         Kuimarisha doria katika njia kuu,
·         Askari wa Usalama Barabarani kuimarisha shughuli za ukaguzi wa magari mabovu,
·         Kuimarisha elimu kwa wananchi na wadau wengine juu ya umuhimu wa kuisaidia Serikali kwa kutoa taarifa kwa vyombo vya dola kuhusu madereva walezi, wanaoendesha mabasi yao kwa kasi, madereva wanaotiliwa mashaka kuhusu ujuzi wao wa kuendesha, na pia kukataa kupanda magari mabovu au yaliyojaa kupita kiwango kinachohitajika,
·         Kuendelea kuboresha sheria za Usalama Barabarani ili zichangie katika kudhibiti shughuli za usafiri na usafirishaji,. Kutoa elimu kwa madereva ili wazingatie sheria za kanuni za kazi zao,
·         Kukagua leseni za madereva ili kuhakikisha kuwa ni za halali,
·         Kuwashirikisha wenye magari ili washiriki kikamilifu katika kuhakikisha kuwa wanaajiri wadereva waaminifu na wenye kuwajibika. 

Pengine swali ambalo daima ninajiuliza pamoja na malengo mazuri yaliyoainishwa hapo juu, kwa nini serikali imeshindwa kabisa kisimamia utekelezaji wa sheria na sera zake za usalama barabarani kwa raia wake kwa muda mrefu?

Je serikali haina askari wa usalama barabarni wa kutosha kukabiliana na tatizo hili?

Je ni tatizo ni la wamiliki wa biashara hii wamefanikiwa kuiteka idara nzima ya usalama barabarani?

Je madereva wanaoendesha magari hayo wanafahamu fika maadili ambayo wanapaswa kuyafuata kulingana na sheria za usalama  barabarani wakati wa kuendesha magari hayo?

Tathimini ya muda mrefu kutoka  vyanzo mbalimbali inabaini kuwa licha askari hawa kuwapo na tunaambiwa kwa  kiasi kikubwa ajali zinazotokea zinasababishwa na madereva wazembe ambao wamekuwa wakikaidi kufuata sheria za usalama barabarani.

Tunajua, kwamba madereva wengi wa mabasi ya abiria  wanaendesha wamelewa. Je hakuna sheria inayowabana kama katika nchi nyingine kuhusu kilevi? Je, dereva huyu aliyekunywa pombe kabla ya kuanza kuendesha nap engine wakati wa safari  ataweza kuendelea kuwa na maarifa yake ya kawaida na uwezo wake wa kawaida kumudu gari na mazingira ya barabara yanayomkabili?

Inafahamika wazi mara nyingi  askari wa usalama barabarani wanabariki mwendo kasi wa madereva  kwa kupokea rushwa; je taifa linakubaliana na tabia hii izidi kuendelea? Tunawaacha wakimbize magari wanavyotaka mpaka lini?. Je tumeshindwa kabisa kusimamia “Speed Limit” ni ukweli ambao huupingiki kuwa Madereva wa mabasi wengi wanakimbia kupita speed waliyopangiwa. Je ni kweli kuwa serikali kupitia wizara yake kweli imeshindwa kuwadhibiti hawa madereva ambao ambao tunaweza kuwaita  wahuni  na wenye viburi kwani wamekuwa wakiendesha vyombo hivi vya moto kwa mwendo kasi, usiofuata taratibu za usalama barabarani na matokeo yake kusababisha ajali mbaya ambazo matokeo yake ni vifo vingi vya watu. Lo imefila wakati sasa serikali iamke na kusema basi inatosha kwa sasa hasa kwa kuanzaia na askari wake wa usalama barabarani wanaelezwa kuchangia uwepo wa ajali kwani wamekuwa wakiruhusu makosa kutendeka kwa sababu tu ya kuchukua rushwa ndogondogo.



Kwa nini serikali imeshindwa kusimamia sheria ya kutowaruhusu madereva matumizi ya simu za mikononi wanapokuwa wakiwaendesha raia;  ni vigumu sana kufanya mambo mawili kwa wakati mmoja uwe makini barabarani na hapo hapo utumie simu kuongea na mtu mwingine;  Ni busara ya kawaida tu dhamana ambayo umebeba kama dereva ni zaidi ya Kuongea kwenye simu za mikononi kwa hiyo tabia hii  haifai kabisa kwa dereva wa gari la abiria aendeshapo gari. Hii ni hatari kwa abiria na watu wengine watembeao kwa miguu. Matokeo yake baada ya kujenga   madereva wanaleta kilio na hasara kubwa kwa taifa taifa letu na familia zetu kwa mambo tunayonaweza kuyazuia bila gharama yoyote


Je serikali kupitia wizara inakubali kuwaona askari wake wakikwepa maadili na kiapo chao cha kazi kwa kujihusisha na rushwa na kuhatarisha usalama wa watu wake; Tumke sasa kwa usalama wa watu wetu na kupinga kwa kauli moja mwendo kasi unaoendana na kutojali sheria na alama za barabarani

Ni ukweli ambao haufichiki kuwa hata sheria zetu zinatoa mwanya mkubwa kwa mahakama kuwatoza faini ndogo badala ya kifungo au adhabu kubwa ambayo itakuwa pigo kwa dereva mna mmiliki wa biashara hiyo. Wote ni mashahidi wa jinsi ambayo watu ambao wamesababisha ajali kwa uzembe wa kujitakia, tena ajali ambayo imesababisha vifo vingi , lakini wamekuwa wakipigwa faini ya Sh50,000 na kuachiwa huru.  Je nchi nyingine wamefanikiwa namna gani kudhibiti ajali hizo za uzembe? Kwa nini tusijifunze kutoka huko?  



Pamoja na kwamba ajali haziwezi kuzuilika jumla,lakini tuzipunguze.Ajali ya gari inapotokea sio dereva tu ndiye wakulaumiwa,ang alia hali za barabara zetu zilivyo,hali ya hewa,abiria nao je wanaelewa sheria za barabarani ili kumkemea dereva anapovunja sheria hizo.Jambo la msingi ni kuelimisha watanzania wote wajue sheria za barabarani.

Tuangalie sheria Namba 30 ya Mwaka1973 na marekebisho yake ya mwaka 1996 inayohusu ni jinsi gani magari yanatakiwa yawe yakiwa barabarani.  Pamoja na tatizo la madereva  tuzinagatie vile vile tatizo la ubovu wa magari amabayo vile viel huwa ni chanzo cha ajali nyingi;


je wamiliki wanatoa kipaumbele gani katika kuhakikisha kuwa magari yao yako katika hali nzuri ya kusafirisha abiria kwa usalama?



Kwani nini gari bovu ambalo halina break nzuri linaruhusiwa kusafiri? Kama dereva ambaye anajali akatae kuendesha mpaka litengenezwe; uungwana wa wamiliki utaweza kuepusha ajali nyingi ambazo zinaweza kuzuilika kwa kutumia muda wa ziada kutengeneza gari na kuhakikisha kuwa liko salama kwa matumizi ya wananchi;  kama wamamiliki watalazimisha matumizi ya gari bovu  hatulidanganyi jeshi la polisi bali tunajidanganya sisi wenyewe na hatimaye kupoteza nguvu kazi ya taifa.

Pamoja na tatizo kubwa la uchakavu wa miundombinu, ikizingatiwa kuwa   barabara nyingi haziko katika hali nzuri sana au nyingine pamoja na kutengenezwa hivi karibuni bado hazijeweza kusaidia kupunguza vifo kutokana na pengine kuwa chini ya kiwango  na kusababisha ajali haraka.  



Tunaomba serikali ikishauriana na wataalamu wake kuangalia  namna ya  kuepusha janga hili kwa kuwa na usimamizi ulio bora na kurekebisha mapungufu yatokanayo na:

Barabara mbovu; Magari mabovu; Mwendo wa kasi; Udereva mbaya; Usimamizi dhaifu wa sheria; na Watembea kwa miguu wasiojali. Rushwa katika utoaji leseni za udereva umetajwa katika orodha ya sababu za ajali chini ya kifungu cha Usimamizi dhaifu wa sheria. Kuruhusiwa kwa magari mabovu.

Safari bila ajali zinawezekana kabisa

Monday, May 16, 2011

TATIZO LA MHESHIMIWA DR. MAGUFULI NI NINI HASA?


                         Dr. John Pombe Magufuli

Kumekuwa na kilio kutoka kwa watendaji ndani ya Wizara ya Ujenzi ambayo Mheshimiwa Dr.Maguful anaongoza na kwa watendaji wengine nje ya wizara yake kama vile, viongozi wa manispaa zinazounda jiji la dare s salaam na hata pengine kutoka kwa wananchi kuhusu  utendaji wa Waziri Magufuli wakilinganisha utendaji kazi wake na Ubabe;

Swali amabalo mimi najiuliza je kama Waziri Dr. Magufuli utendaji wake unaonekana ni wa ubabe ni kwa nini?  Au watendaji wetu wamejenga mazingira ya kufanya kazi zao bora liende bila umakini wa kuzingatia sheria? Je kama Waziri anatekeleza Majukumu yake kisheria na sheria hiyo ili ifanikiwe inahitaji nguvu za ziada je huu ni ubabe?

Nafikiri umefika wakati ambao kama haturidhiki na utendaji kwa mantiki hii wa Mheshimiwa Dr. Magufuli na tunajua kabisa anakwenda kinyume na maadili ya uongozi, kinyume na sheria inayompa mamlaka ndani ya uwezo wake kama waziri hebu tuwe wakweli na tuyaainishe mapungufu ya ubabe huu ili hoja zetu ziwe za msingi; uropokaji na kusema sema tu bila kuwa na vielelzo nafikiri kama Waziri anatekeleza Majukumu yake kisheria na kuzielewa sheria hautapunguza kasi ya utekelezaji wake hata kama utakuwa wa ubabe; na tukumbuke kuwa binadamu bila kumshikia bango hasa kwetu sisi na nchi zetu hatutafuata sheria katika maisha yetu ya kila siku;

Hata mheshimiwa Rais Jk ameona hili ndio hata sasa ameanza kuwa mkali dhidi yenu ninyi watendaji wa serikali na kuwaeleza wasioweza kufanya kazi kwa kufuata sheria na maadili ya utumishi wa Umma wajiondoe; kauli amabazo zilikuwa hazipo; wakati wa kubebana umepita; tukitaka kuendelea lazima mambo ya kesho tuyaone leo na tusiyafumbie na kuyaonea aibu, hata kama utekelzaji wake sasa utaonekana mbaya lakini kesho kila mtu atafurahia; ebu jikumbushe ujenzi wa sehemu ya barabara ya ubungo –kimara mpaka kibaha; leo tunasema nini bado tunasikitika au tunafurahia hatua hiyo kubwa ya maendeleo?

Tuwe wakweli tuwajibike inavyotakiwa, tusimamie sheria ili kesho sheria isimfanye kiongozi mwingine kuonekana mbabe wakati akitekeleza mapungufu ya jana.

Sunday, May 15, 2011

JE TUWAFANYE NINI WANASIASA?

                            Utajiri wetu ni mkubwa lakini?

Siasa ni sayansi ya utengenezaji wa maneno matamu matamu ambayo yanatumika katika kuibadili akili ya wananchi ili waweze kukubaliana na kikundi Fulani ambacho kimejipanga kisera ili kiweze kupata nafasi ya k utawala, ambacho mara nyingi huwa na mipango  mitamu ya kinadharia zaidi ya maendeleo kwa wananchi.
Kutokana na sera zao wakati mwingine upangaji wa hoja na utamu wa maneno yao hupelekea kuaamini kuwa wanasiasa ni watu wanaojua kila kitu. Na kila mtu anadhani hakuna mtu anayeweza kufanya kitu kwa maslahi ya nchi bila kuhusisha siasa.  Kinachoendele hapa ni dhana tunayoijenga kuwa mwanasiasa umekuwa bingwa wa kujenga hoja, wanataka kuona umekuwa bingwa wa kutatua matatizo na kuwaletea wananchi asali na maziwa.

Siasa ili inafinikwe lazima ijengwe chini ya msingi wa sera, na sera hizo lazima ziwalenge  kwa watu Sera zote zinapotungwa ni kwa ajili ya watu, lakini tatizo ni kubwa wanasiasa wanawarubuni watu, hivyo  kuvurugu mipango ya maendeleo; Ni wazi kwamba mhemko wa kisiasa, umeikumba nchi yetu; Kila kitu tumekifanya ndani ya siasa, hili ni tatizo kubwa. Siasa uchwara tunazipa nafasi na kujikosesha maendeleo.  Kutokana na kushindwa   kuwaelimisha watu kuhusu tabianchi, ufahamu wa maisha, mbinu za kukabiliana na majanga na mengineyo, moja kwa moja vinasaliti jamii 

Tanzania ni nchi maskini ni lazima tuwe na viongozi ambao kweli wanasaidia wananchi. Muda wa kukubali kuendelea kudanganywa umekwisha, ni lazima sasa sisi kama wananchi tuwahukumu wanansiasa kutokana na namna wanavyotufanyia mambo, wanavyotufanya sisi masikini kana kuwa hatujui nini kinaendelea.  Kauli mbiu yetu iwe kama hawatujali kwa maendeleo  na kutuzidishia umasikini, inatunapasa kuachana nao tumechoka kuendelea kudanganywa..

Leo hii kigezo chetu cha maendeleo ni nini?  Tunayaangaliaje maendeleo ya wananchi? Kwa nini kuna tofauti kubwa kati ya mtu na mtu? Je tukisema wananchi hawajitumi kwa maendeleo yao je tumewawezesha?

Kipimo chetu cha maendeleo ni kuangalia maisha ya jumla au  ya mwananchi mmoja mmoja? Je tunayalinganisha maendeleo ya wananchi wetu kwa kuangalia uwezo wao wa kuzalisha mali  na wanatumia vifaa gani, na vinahusiana vipi na kuimarisha afya zao? je thamani ya fedha yetu, kiwango cha elimu na uimara wa sekta za viwanda  tunaviangaliaje katika kumletea maisha bora huyu mwananchi? Au tunaridhika na Msongamano wa magari na watu katika miji yetu mikuu ikianzia darn a miji mingine na tunaridhika kuwa  hii ishara tosha ya maendeleo  na maisha bora?

Je kuna uwiano kati ya uimarishaji wa bidhaa za ndani na zile zinazokuja toka nje ya nchi? Au tunaridhika na kilimo cha duni cha wananchi serikali kupitia wanasiasa hatuoni sababu ya  kuwasaidia wananchi  kuwajengea uwezo wa kupata masoko; Uwezo wetu wa kuwatafuti masoko yenye tija umefia wapi? Bila dhana bora na elimu nzuri ya kilimo tunaelewa kuwa tumepania kuwamaliza kabisa  wananchi kwa kuwaletea ushindani  wa kupambana na biashara kutoka nje  na hivyo kuwanjima uwezo wa ushindani katika midhani sawa.

Je Tanzania ya leo ni chama tawala pekee ndicho kinachoongoza kutoa ahadi ambazo baada ya uchaguzi zinakuwa mzigo ndani ya chama? Je vipi vyama vya upinzani vimefanikiwa kukibana chama tawala katika kuhakikisha kuwa wanatekeleza ahadi zake kwa wananchi? Ni ukweli ambao haufichiki kuwa wanaotawala ndio wenye meno ya kutafuna, basi la msingi wabanwe watekeleze ahadi zao; kwa msingi huu watawala kupitia vyama vyao wasipobanwa kitakachoendelea na tunakiona kikiendelea kutokea ni kuwa taifa letu litaendelea kuzalisha wafanyabiashara feki na bidhaa feki. Elimu na walimu feki, mitihani feki, wahitimu feki, na vyeti feki. Hospitali zitaendelea kutikiswa na dawa feki. Mwisho wa siku wimbo wetu utakuwa kila kitu ni feki  

Hivi sasa tunaona vyama ushindani vikipita sehemu mbali mbali kwa kauli ya kuhamasisha ubovu wa serikali inayotawala; swali la msingi hapa ni kweli wanachokisema ndicho wanachokiamini na kuwa tayari kuwaletea wananchi maendeleo punde wakipata nafasi ya kuongoza?

Au tuendelee kuamini kuwa hii ni siasa kila mtu anatafuta ulaji kwa staili ya kuonyesha mabaya ya mwenzake? Je hakuna jema ambalo serikali inayopingwa sasa hivi imewafanyia wananchi? Nikifikiri haya yote ninaishia kwa kusema kuwa TUWAFANYE NINI WANASIASA KWANI HAWAAMINIKI HATA KIDOGO; wanaendelea kuwafanya wananchi kama watoto wa kuku watanyonya kesho wakati hakuna uwezekano wa kuwatoa katika umasikini uliopindukia;

Utajiri huu wote tulio nao kwa nini tunaendelea kuwa masikini inauma sana wanasiasa mnatutesa jamani;

Saturday, April 30, 2011

REFLECTING BACK- POLITICAL CORNER;



Why opposition parties failed in the 2010 General Election in Tanzania?


1.  The ruling party CCM has very strong bases in various villages around the country where there is large number of voters while


2.  Opposition parties have strong holds in urban centers were the number of voters is low but the euphoria is huge


3.  The president has too much power to appoint and disappoint, this leads to a large number of senior government officials to be presidential appointees hence obedient to the president; 



4.  Power mongering, the big opposition parties of CUF, CHADEMA, NCCR were competing against each other instead of joining hands to present one candidate for the opposition, this lead to spread of votes and creation of weakness against opposition




Friday, April 22, 2011

MSHIKE MSHIKE BUNGENI



Kauli ya Spika wa Bunge Anne Makinda:  Wabunge wanafanya mambo ya KIJINGA ina maana gani kwa jamii
·        Tufunge mlango tupigane”
·        "Mmezowea kutuburuza"
·        "Naomba mjiheshimu hapa si sokoni, Watanzania wengi wanawaangalia mnavyofanya mambo ya kijinga na kupiga kelele,"

Tusiwalaumu tuu wabunge, tujiulize wameingiaje bungeni? Tatizo la ujinga kama uko ambao unatokea Bungeni kama alivyosema mheshimiwa Spika linatoka na sisi tunaowachagua; je tunatumia vigezo gani kujua kweli kama WABUNGE TUNAOWACHAGUA wanaweza kujenga hoja za kweli na sio itikadi tu ya chama atokacho mbunge? Kama bunge halifanyi kazi yake vizuri lawama ni kwetu wananchi tuliowachagua.

Kwa watanzania wengi ambao walibahatika kufuatilia nini kilikuwa kinajili bungeni Dodoma wiki chache zilizopita watakubaliana nami kuwa tuliweza kupata kioja cha kuhitimisha mijadala ya bunge katika kikao chake cha 10.

Ilimlazimu Mheshimiwa Spika kutamka maneno ambayo nafikiri yalikuwa hayastahili kutamkwa bungeni kwa heshima na majukumu makubwa ya kazi ya bunge kama chombo muhimu sana katika kusaidia kuendesha shughuli za serikali; katika majukumu ya Kiuwakilishi (representational),utungaji wa sheria (legislative), upitishaji wa bajeti, mapato na matumizi ya nchi (budgetary and resource approval) pamoja na uwajibishaji wa serikali iliyoko madarakani (accountability). Bunge pia ni chombo cha kutathmini mwenendo wa jumla wa kisera unaopendekezwa na serikali ili kubaini kama mwelekeo wake unasawiri matakwa ya wananchi walio wengi nchini. Aidha ni kazi ya Bunge katika mfumo wa kidemokrasia kuhakikisha kuwa matendo ya serikali iliyopo yanakidhi matakwa ya jamii wanayoiwakilisha, ikiwa ni pamoja na kuunga mkono hoja nzuri na kupinga zile zinazoonekana kukinzana na maslahi ya jumla ya kitaifa.

 Je Bunge letu linatekeleza kwa umakini majukumu haya au bunge kwa sasa limekuwa ni chombo kikuu cha ushauri tu kwa serikali bila kuwa na meno ya kuiwajibisha serikali pale ambapo inakosea?
Kwa maneno mengine wabunge wamechaguliwa na wananchi ili wawakilishe katika kuisimamia serikali. Hivyo wabunge hawatakiwi kabisa kupeleka mawazo na mitazamo yao wenyewe. Wanatakiwa wanapozungumza Bungeni au kupiga kura ni lazima wafikirie wapiga kura wao wamewatuma kufanya nini. 
Je tuliwatuma waende kupigana bungeni? Au kugeuza bunge kuwa ni soko kama mheshimmiwa makinda alivyowakemea wabunge wenzake;

Je wabunge wetu ambao tumewachagua  wanao uwezo wa kutawala katika kuchangia hoja bila kupigana na kutishana? Au ni wale ambao wanapenda sana kutawala hata kama hawana uwezo wa kutawala.”

Je wabunge wanafahamu kuwa Bunge letu la sasa bado lina nguvu kubwa ambayo halijaweza kuitumia vyema. 
Nafikiri tatizo la wabunge wengi wanatumia muda wao mwingi kulalamika na kushangaa mapungufu.  Wanatakiwa wawe na uwezo wa kupangua na kupanga upya mambo wanavyoona wao inafaa bila kujali maneno na minong’ono ya wanafiki wachache na wasio jali maslai ya wengi au kuwa na muono wa mbali.
Je wabunge wetu wengi ni kundi gani?

Je tunao wabunge wenye uwezo wa uongozi na wito wa uongozi kwa kuweka maslahi ya taifa mbele kwa manufaa ya watu.

Wabunge wetu wameingia bungeni kama moja ya njia sahihi za kujipatia neema, ubinafsi na maslahi binafsi;  
 
Je abunge wetu ni wale wenye uwezo mkubwa wa kushawishi kutokana na uwezo wao wa  kiuchumi, haautegemei mshahara wala marupurupu ya ubunge; Hawana muda wa kuchangia mijadala ya bungeni, wala hawana maswali, ila kwa sababu wana nguvu kubwa kiuchumi na jeuri ya pesa, wanao uwezo wa kuwabuluza wabunge wengine na kuhakikisha kuwa wanalolitaka liwe, ndilo linakuwa. Kwa maneno mengine aina hii ya wabunge ndio viongozi wenye nchi.

Friday, April 15, 2011

RASIMU YA KATIBA MPYA ISIYO KIDHI HAJA YA WATANZANIA WENGI

MWENENDO HUU WA MCHAKATO WA KATIBA MPYA UTATUFIKISHA WAPI?

Ilikuwa ni shangwe kubwa pale Rais wa Jamuhuri ya Tanzania Mheshimiwa JK alipotoa  taarifa rasmi kuwa serikali yake iko tayari kushughukikia mapendekezo ya kuandaa katiba mpya

Watanzania wengi kwa ujumla walikuwa wamejawa na shauku na hamu ya mabadiliko ya katiba wakijua kuwa wakati sasa umefika kwa wananchi wa Tanzania kuwa na katiba mpya ambayo itajumuisha misingi ya taifa itakayokuwa imelinda maslahi ya wananchi  kwa ustawi na maendeleo yao. 

Kwa msingi huu toka kongamano la kwanza ambalo lilifanyika chuo kikuu cha dar es salaam chini ya wenyekiti wa Prof Issa Shivji na Jenarali Uliwengu wananchi wengi walijitokeza wasomi, wanasiasa wananchi wa kawaidi na vikundi mbalimbali vya jamii; ili kushauri katiba mpya iwe na sura gani, na zoezi nzima la upatikanaji wa maoni uwe vipi.

Kama Makamu wa Kwnza wa serikali ya umoja wa kitaifa  Maalim Seif alivyo wahi sema“hali inavyokwenda wananchi wengi wamehamasika kutaka kutoa maoni juu ya kuwa na katiba mpya hivyo ni vizuri wananchi wakapata nafasi ya kutoa maoni yao kwa kuwa katiba inayowashirikisha wananchi ndio katiba madhubuti nchini”.

Msisitizo hu unatokana na dhana kuwa iwapo Wananchi wataweza kushiriki kikamilifu katika mchakato huo wa kuandaa Katiba mpya  itasaidia katika kuepusha  dhana kuwa suala la kuandika Katiba sio la kikundi Fulani, chama fulani au ni la Wanasheria,  kwa vile wao wamebobea katika sheria hasa za masuala ya Katiba.  

Wengi walipendekeza kuwa ni muhimu  wananchi wote, washirikishwe ikiwa ni pamoja na wale wasiojua kusoma wala kuandika na wanajamii mbalimbali mijini na vijijini watakavyowezeshwa kuweza kushiriki katika kuweka misingi ya uandikaji Katiba, kutoa maoni katika mijadala ya awali na kwa Tume ya kuratibu maoni, pamoja na kuchagua wawakilishi kutoka miongoni mwao kushiriki katika vyombo muhimu vya kujadili mapendekezo na rasimu za Katiba ikiwemo wajumbe wa Mkutano wa Kitaifa wa Katiba na mara nyingi mjadala unaishia kwenye kikao cha  Bunge Maalum la Katiba.

Nchi inapoamua kuandika katiba mpya ukweli wake ni kuwa ni  upanuzi wa demokrasia na maendeleo ya nchi kwa kuwa na katiba ya nchi inayoonyesha utashi wa wananchi.

Kazi ambayo iko mbele yetu ni kubwa sana sisi kama  Watanzania ni lazima tuhakikishe kuwa mchakato wa kufikia katiba mpya unakuwa huru, yenye uwigo mpana sio wa kulindana bali ni wa uwazi na ambao una uhalali wa kutosha kuweza kufikia kusema kuwa Katiba itakayopatikana kweli imetokana na watu na mazingira yetu.

Mchakato wa kufikia Katiba Mpya usipoweka misingi ambayo utahakikisha wananchi wote wana nafasi sawa ya kuchangia mawazo yao ya dhati  bila kuogopa au kununuliwa tutakuwa tumefanikiwa kuifikisha katiba mahali pazuri kwa usalama wan chi bali  kama kutakuwa na mchakato mbovu tutakuwa tumeiharibu kabisa nchi yetu na maendeleo yake kidogo ambayo tunayo hivi sasa.
Lengo la kila mtanzania tunatamani kuandika Katiba Mpya ili kuweza kukiachia kizazi kijacho mfumo mzuri wa utawala ambao utawapa nafasi ya kufanikiwa katika maisha na mipango yao na ambao utawahakikishia mtiririko mzuri wa mahusiano na kuwajibishana kati yao na watawala wao.

Nini kinatokea sasa?

1.  Wengi wamepinga rasimu hiyo ya katiba kwa sababu tofauti mojawapo ikiwa inafanyika katika kipindi kifupi na pengine wananchi wengi hawatapata nafasi ya kutoa maoni yao.

2.  Mikutano iliyofanyika Dodoma na Dar es salaam imeonyesha mapungufu makubwa katika siku za awali tu; je kamati au wizara inayoshughulikia rasimu ya kuratibu maoni ya utayarishaji wa katiba mpya kweli wamejiandaa kwa katiba mpya au ni ubabaishaji tu?

3.  Je Kamati waliangalia mahitaji halisi ya wananchi na kiu ya wananchi kutoa mawazo yao?

4.  Hebu angalia mambo yalivyokuwa Dar es salaam, ilikuwa ni tatizo kubwa pale ukumbi ulipojaa wananchi wengi ambao kwa sababu moja au nyingine waliishia kulala tu , nini kilikuwa kunaendelea, je wapi tutapata hiyo rasimu bora ambayo inakizi haja wakati hatuna ushindani katika uchangiaji hoja wakati wananchi waliopokelewa au kuletwa katika ukumbi huu kwa sababu moja au nyingine waliishia kulala tu?

5.  Kule Zanzibar kwa kulitokea tukio la kuchana Rasimu hiyo wananchi na wachangiaji wakiwa wamejawa na hasira ya utaratibu mzima wa uandaji na mwonekano wa rasimu hiyo; Je ni kweli kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar hakuhusishwa kikamilifu? Je Rasimu unaelezaje swala la Muungano? Je linakizi haja kwa pande zote? Je wale wanaona wanamezwa wamepewa kinga gani ili wasipatwe na janga hilo?

6.  Je kama zoezi hili halitakwenda vizuri kwa kigezo cha muda nani atawajibishwa kulipa gharama halisi ambayo imetumika  katika maandalizi hayo? Ikumbukwe kuwa bado pesa hiyo ni ya mlala hoi.

HITIMISHO

Lazima tukubali kuwa Mheshimiwa Rais amebariki utaratibu mzima wa uandikaji wa katiba upya, hili ni jambo la kihistoria na ambalo halitakiwi kufanyiwa mzaha na watendaji wachache kwa masilahi yao binafsi au chama chochote,  hebu tulifanye jambo hili kwa masilahi ya wananchi wa Tanzania na sio kwa manufaa ya wana siasa na vyama vyao;
Mungu ibariki Tanzania na watu wake

Tuesday, April 12, 2011

KIKWETE NA MCHAKATO NDANI YA CCM

MZEE MAKAMBA INATOSHA  NA INAFAA UPUMZIKE
                          SEHEMU YA KWANZA


Mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi Mheshimiwa Rais JK alivunja kamati Kuu ya CCM  huko   Dodoma tarehe 9/4/2011 tukio ambalo lilihusisha kustaafishwa kwa  Katibu wake Mkuu mzee wetu  Bwana Yusufu Makamba;

Utendaji wa kusua sua wa Mzee makamba umekuwa kilio cha siku nyingi cha wanachama wa CCM; wengi walikuwa hawaridhishwi na utendaji wake wa kazi hasa katika maswalal yote ambayo yanahusu kumshauri Mheshimiwa Rais kama kiongozi wa serikali na kama Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi;

Pamoja na mapungufu Mengi ya Mzee wetu Makamba lakini Mheshimiwa Rais ataendelea kubeba lawama kwa kuchelewa kuliona tatizo hili pamoja na kilio kirefu cha wana CCM kuwa Makamba alikuwa mzigo kwa Chama katika ufanisi;


Pamoja na uamuzi huu Mzuri na mzito swali la msingi hapa ni hili Kwa nini imemchukua Mwenyekiti wa Chama nuda mrefu kusafisha utendaji ndani ya chama?


kama Kweli  kamati yake kuu ya chama chake ilikuwa haifanyi kazi vizuri, na imemwangusha kwa kiasi kikubwa, kwa nini alikubali  kuendelea kuibeba?, "ni sawa kama kuendesha gari ambalo halina balance nzuri ya upepo unaotakiwa  kwenye matairi yake, kwani kabla ya ajali utalazimika kutumia  nguvu zaidi katika kuhakikisha kuwa gari hilo inakwenda vizuri na haliachi barabara", kitu ambacho kimekuwa sicho, kwani katika hali tofauti tofauti Mwenyekiti amejikuta akishindwa kuhimili mikiki mikiki ya barabarani ambayo imekuwa ikisababishwa na ubovu wa matairi( watendaji) kwa au kujali masilai yao binafsi, na kupoteza mwelekeo wa sera na dira za Chama;

Sijui nini kimemtokea Dereva Wetu(mheshimiwa Rais Na Mwenyekiti wa CCM) mpaka ameamua kulitosa gari hilo amabalo  fundi wake Mkuu alikuwa Mzee Makamba; na kuamua kuchukua gari nyingine; 


Kwa tafakari yangu na kama nilivyowahi kuandika katika blog hii huko nyuma kuwa  kuwa Mzee Makamba alishindwa kutekeleza yafuatayo;

  • ·        Kutoa ushauri sahii kwa wakati sahihi



  • ·        Kutumia sana sera za ubabe wakati hakuna haja ya sera hizo
  • ·        Kutumia lugha ambazo zilikuwa hazivuti ushawishi kwa wanachama wake na wananchi kwa ujumla
  • ·        Kushindwa kutoa ushauri mzuri kwa Mwenyekiti wake wakati yeye ndio mtendaji mkuu wa chama;

Tukumbuke siasa yenye msingi wa utawala Bora sio ubabe na ukitumika sana huondoa busara na hekima; uongozi bora unatawaliwa na uongozi hekima, ambayo itazaa uadilifu, uwajibikaji na umoja.

Wakati umefika kama saa izungukavyo, saa yako imefika kwa wewe mzee wetu Makamba  uweze pumzika,  inatosha hapo ulipomfikisha Mwenyekiti panatosha, tuwaachie na wengine nao tuone watamsaidiaje Mwenyekiti katika kuitengeneza Tanzania yetu na kuleta neema kwa watanzania wote.




Mungu Ibariki Tanzania na Afrika