WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Thursday, October 6, 2011

NYERERE ON DEMOCRACY -


MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE 1922 - 1999

I AM QUITTING FROM ACTIVE POLITICS


“I am not resigning but, I am quitting, and I have decided to do so because, I feel time is in hand for another member to lead the Nation ….”


“The almighty God has granted people with many talents, and they can think about so many things. But the important thing is my faith that, what I am doing is good for the Nation I have no power to hide people to give out different interpretation, but interpretation is the second thing.” 


“Tanzania should not believe that a one-party state is a God’s which …. As for the debate they should just debate in today’s Tanzania it is stupid to make secret the debate of on more parties. It is treason to discuss why we have single party; we have been benefited from having a one-part. Tanzania should discuss the prons and cons of having one-party or many parties …. One party has its own limitations and tends to go sleep”.


“There is a time when countries limit their people’s liberties, this can be done during war time, war limits people freedoms.”


“Now when you suppress people who are educated and who want more freedom it becomes really a problem.”


“Tanzania should not believe that a one-party state is a God’s which … In to-day’s Tanzania it is stupid to make secret the debate of, or more parties ….. Tanzania should discuss the prons and cons of having one-party of many parties”


“I don’t propagate long live one-party system, but I do propagate long live CCM”


“We cannot remain an island, we must manage our own changes, don’t wait to be pushed, “

“The people of the majority view have to accept the rights of minority to express their opinions without intimidating social pressure and indeed must accommodate those views as far as possible”.

“Developing nations need democracy, but the need and necessity of democracy should come from within according to geographical necessity, maturity etc … And the internal situation of Tanzania is ready for Transformation”.

“We make mistake to imagine that we can import democracy like coca-cola or readymade garment … But ideas about democracy and democratic institutions are not divine truth, they mere to be accumulated and absorbed into the blood stream of the people and institutions through which ideas … grow out of people’s own practice”


“Leaders of the opposing parties should be serious and patriotic and they should not be money make … And if they fail during election they should know that they have failed and not to take stones and throw to their fellow members in demand to why they have failed”.


“We need at least two committed parties; we don’t want 30 small parties that will be chaos.”


“the west was struggling to post a new set of puppet leaders in the developing world. There is no other explanation rather than us efforts to influence removal rulers who were installed by Washington …. They want to install a new crop of surrogate’s leaders. I must caution them however that it is easier to do this by military coup than through democratic elections”.


“… People say that we should learn from outside from USSR ad other Eastern European countries … what should we learn from them … we should not agree to be pushed like tools …. The Soviet Union is finished … gone.



“You will never hear that any President of America had appointed a communist or socialist as the head of American army. If God himself advised that he should do so he would refuse.”


“… The majority of Tanzania would like to continue with a single party-system under CCM. But we cannot wait until the majority of the people have lost their faith in this party before the party itself seized and uses its responsibility to us her in such a major changes as this”.


“Democracy is more than a matter of majority rule, true democracy requires that minority views be respected and that everyone be given an opportunity to express their views freely and openly … every new thing starts with the support of minority…. True democracy demands that the minority have such freedom. Therefore CCM can and should welcome the opportunity to give a lead in yet another major peaceful political transition in our country”.

“No political party be permitted to exist if it is based on Religious … Religious is the right of all Tanzanians. But our party as a party has no religion… This is an absolute essential stand for the unity and peace in the country”.

“To lead is to show the way. But it is difficult to show the way in the dark, without either a light or compass. And its philosophy and its ideology are the light and the compass of political party.

“Take care of the Arusha Declaration otherwise there will come some people who will cheat you saying it is useless. The Arusha Declaration has strong foundation and will last forever and bring development in Tanzania.”

Thursday, September 29, 2011

IGUNGA, IGUNGA USIHARIBU USTARABU WETU WA AMANI NA UTULIVU

JE NI MAZINGIRA GANI YANAANDALIWA NA VYAMA KUELEKEA UCHAGUZI MDOGO IGUNGA- TABORA?

Oscar Ameringer aliwahi sema kuwa "Politics is the gentle art of getting votes from the poor and campaign funds from the rich, by promising to protect each from the other" -
Hiki ndicho kinachotokea Igunga kwa sasa vyama kupitia wanasiasa wao wanajitahidi kuvuna kura kutoka kwa wananchi wa kawaida “ wenye kipato cha chini au kwa ufupi masikini; kwa msingi huu wanasiasa huwapumbaza masikini walala hoi kwa kuwanunua ili wawapigie kura bila wao wenyewe kujua kwa kutumia sera na mapenzi yao kwa chama husika na wakati mwingine kuwapatia pesa ambazo wanazipata kwa matajiri wenye malengo binafsi mara ushindi ukipatikana.

Pesa au rushwa ambayo inatolewa na wanasiasa ni mfumo wa utendaji wa kufikisha ujumbe kwa wanachama wao ili wahakikishe kwa naman yeyote ile ushindi unapatikana, kwa kauli mbio tofauti tofauti zinazoashiria maendeleo; kwa msingi huu  wa kampeni ni wakati wa neema au mavuno kwa wafuasi wao na wananchi wanyanja.
Siasa ni ushindani na ni utaalau wa juu kabisa wa kupangilia mikakati hata kama ni ya uwongo, ili mradi lengo la kushika dola litimie. Kutokana na falfasa hii Ifahamike kuwa sio kila mtu au kila chama kinanafasi sawa katika aina hii ya kushiriki katika kuufikisha ujembe; uzoefu hutumika vitisho nya kuwatisha wanyonge hutmika pia; pesa ndo usiseme; Nguvu hii ya pesa huviondoa vyama vidogo ambavyo haviwezi kushindana na kuviacha vyama vyenye nguvu kama inavyotokea Igunga wakati huu wa kampeni ya nafasi ya Ubunge.

Wanasiasa akisimama ulingoni kauli zao ni namana ya kutatua kero za wananchi katika kuondoa kero zao; sikiliza kiini chote cha kampeni huko Igunga kwa sasa ni kutatua kero za wananchi wa Igunga kwa kunadi sera mbalimbali za maendeleo tutafanya hili na lile;
Tatizo kubwa la wanansiasa sio wakweli na hawajali hasa wakisha pata au wakishachaguliwa; wanakuwa na sababu nyingi tu za kujitetea, lakini ukweli hawajali tena kwani walichotaka si wamepata kushika dola.

Kama semi hizi tatu za kiingereza zinavyosema:.
l  When the ruler himself is 'right,' then the people naturally follow him in his right course."
l  “Whatever the best man does, others do that also. The world follows the standard he sets for himself”.
l  "If a ruler himself is upright, all will go well even though he does not give orders. But if he himself is not upright, even though he gives orders, they will not be obeyed."

Semi hizi zinajumuisha tabia za wanasiasa wetu namna wanavyotakiwa wawe ili kujenga imani kwa wananchi na maendeleo ya taifa letu.
 Turudi Igunga; Kilio kikubwa kwa hivi sasa huko Igunga ni matumizi mabaya ya pesa, pengine rushwa na tukumbuke kuwa rushwa ni jiko ambao zambi  zote hupikwa huko; kwani watu hawa  hutaka kuwa viongozi ili wajitengenezee faida binafsi, ni sawa na mwanaume ambaye sio mkweli anavyoweza kumdanganya mwanamke ili aweze kuutumia mwili wa mwanamke huyo katika kutimiza kujifurahisha yeye mwenyewe; baada ya kufanikisha haja yake humdharau na kumwona sio kitu tena hata kama walikubaliana katika kusaidiana ahadi hizo zote huyeyuka na kumwacha mwnamke huyo akisononeka kwa uaminifu wake na kujitoa kwake.

Je fujo zinazoendelea huko igunga je zinatokana na wananchi hasa vijana kuelewa haki zao na nia yao na kutaka kiongozi atayechaguliwa awe kweli mtatuzi wa shida zao? Au ni vurugu tu ambazo zinachochewa na wanasiasa kwa kutumia pesa ili iwe ni sababu ya kuvuruga amani ambayo ilitakiwa itawale uchaguzi huu mdogo? Au vyama vinaandaa sababu mapema ili hata vikishindwa katika uchaguzi viweza kuhalalisha matokea kuwa wameshindwa kwa sababu hii au ile;

Tatizo langu leo hii ni hili, aina hii ya kampeni inaharibu moja ya msingi wetu mkubwa san asana ambao ulijengwa na waasisi wa taifa hili utamaduni wa uvumilivu unavyobomoka hivi sasa. Tukumbuke kuwa taifa hili linafahamika ni miongoni mwa taifa ambalo lilikuwa limetulia na wananchi wake wamekuwa wakivumiliana sana. Je kwani nini leo hii wanasiasa wanatupeleka katika hali ya kuvunja umoja wetu? Wanatutakia nini hawa wanasiasa na vizazi vyetu? Wanatamani nchi hii isitawalike kwa faida yao? Kwa nini wanaingiza  roho ya ukatili kwa vijana wadogo?

Nafikiri bado kuna kila sababu ya wanansiasa kutambua kuwa ni dhambi sana kuchezea amani ya nchi kwa masilahi binafsi na ya muda mfupi na kuliacha taifa katika janga kubwa la uvunjaji wa amani.

Pamoja na ushindani wa siasa huko Igunga lakini uchaguzi huu mdogo usiwe sababu ya kuvunja amani; tunawaomba wasimamizi wa sheria zihusuzo uchaguzi wawe makini kuhakikisha kuwa taratibu zote zinafuatwa bila kumwogopa mtu, au kikundi chochote  au chama chochote kile.

Muhimu ni kwamba tuzike tofauti zetu kwa faida ya taifa letu na vizazi vyake.
MUNGU IBARIKI TANZANIA

Sunday, September 25, 2011

IGUNGA INATUPELEKA WAPI KAMA TAIFA


Igunga imegeuka fitina ugomvi na mbaya zaidi sio ugomvi wa hoja ni ugomvi wa misuri ambao hauna tija kwa Taifa letu.

Tunaendelea kujiuliza kwa nini wakati kampeni za hicho kiti kimoja tu zikiwa zinakaribia kufikia ukingoni  tunaendelea kushuhudia matukio yanayotishia uvunjaji wa amani, yanazidi kuongezeka.
Kama vile, Kudhalilishwa kwa watendaji serikali na vyama na serikali




Kujihami kwa baadhi ya viongozi hadharani, kama ndugu yetu Mbunge wa Tabora Mjini, Ismail Aden Rage (CCM), akiwa na bastola kiunoni akiwa akihutubia katika mkutano wa kampeni. Kama magazeti mengi  yalivyoonyesha kuwa” Bastola ya Rage ilionekana wakati mbunge huyo akijiandaa kupanda jukwaani kwa ajili ya kumnadi mgombea ubunge wa CCM kwenye moja ya mikutano ya kampeni jimboni humo”.





Kama Mwandishi  wa makala hiyo alipouliza”Kwa sababu hiyo, tunajiuliza, Rage alikuwa akikabiliwa na hatari gani hadi kulazimika kupanda jukwaani ni bastola? Hivi kila mwenye silaha ya moto Igunga akisema atembee na silaha yake hali itakuwaje?Na kwa wasio na silaha za moto, wakiamua kutoka na silaha za jadi kama mishale, visu, mapanga na zinginezo, Igunga patakalika? Sisi hatuungi mkono kitendo hicho na tunalitaka jeshi la Polisi kuchukua hatua ili kuhakikisha kampeni za uchaguzi Igunga na hatimaye uchaguzi wake, unafanyika katika mazingira ya utulivu na amani.”


Nakubaliana kabisa na mwandishi wa makala hii kuwa huu ni udhaifu mkubwa kabisa kwa wasimamizi wetu wa maswala ya amani na utulivu; Mheshimiwa Mbunge hakuwa na sababu yeyote ile ya kuja kwenye kampeni na silaha, kama alikuwa na uhakika kuwa usalama wake ulikuwa mashakani kulikuwa hakuna sababu yeyote kwa yeye kujumuika katika kampeni  kwa siku na wakati kama huo.



Tunafahamu kuwa vikosi vyetu vya ulinzi na usalama jamani viko na vinaendelea kuwa makini katika kulinda amani ya wakaazi wa Igunga na taifa kwa ujumla katika wakati huu wote wa kampeni;



Tukio nyingine ambalo nalo limepigiwa sana kelele ni kitendo alichofanyiwa DC; kwa wahusika wote wale katika sakata hili la kumdhalilisha Mama huyu; kumekuwa na matumizi ya nguvu zaidi kuliko busara;hata kama wahusika wanakana na kuona waliyofanya ni sawa, ukweli ni kuwa kosa lilifanyika watake wasitake; Busara busara jamani tunahitaji sasa kuliko wakati mwingine wowote huko nyuma.


Bado ni ukweli ambao haufichiki kuwa Heshima kwa viongozi wetu  na hata kwa mtanzania yeyote na  mtu yeyote ni muhimu. Nafikiri tulitakiwa kuangalia sheria na hatua zake na sio kumdhalisha kama alivyofanyiwa huko igunga katika eneo lake la kazi. Ni busara kujaribu kuepuka kujichukulia sheria mkononi;

Tukikumbuka sana wosia wa  Baba wa Taifa kuwa watanzania wote ni ndugu. Ni vema basi sote kama taifa tukafuata sheria tulizojiwekea bila kujali itikadi za vyama; na wabunge wetu wakawa mstari wa mbele katika kuishi kwa matendo yale wanayoyapitisha bungeni na sio kuwa vinara wa kuongoza fujo na uvunjaji wa sheria hizo. Sisi kama taifa tujitahidi kwa pamoja kudumisha amani! “Inawezekana timiza wajibu wako”

Hakuna umaskini mbaya kama umaskini wa mawazo, ni umaskini mbaya  sana'  Mwalimu J. K. Nyerere,

Mtu mwenye akili akikuambia neno la kipumbavu -ukalikubali, anakudharau!'  Mwalimu Nyerere


Kama  Taifa tusimame imara katika kupigania "umoja, amani na upendo miongoni mwetu" hii ni kati ya zawadi kubwa sana ambayo  waasisi wa taifa letu Mwalimu Nyeyere na Mzee Abeid Karume walituachia

Tuache kuburuzwa na upepo wa siasa na wanasiasa; ambao wanapigania zaidi masilahi binafsi  na sio masilahi ya taifa, tufunguke sasa.

Nawatakieni Kampeni za mwisho mwisho zenye amani  na nguvu ya Hoja na sio matumizi ya Misuri

Friday, September 23, 2011

KAULI YA WAZIRI MKUU MHESHIMIWA MIZENGO PINDA KUHUSU UTENDAJI WA POLISI NA SAKATA LA SUKARI


POLISI WANAPOSHINDWA  KUSIMAMIA SHERIA NA WAJIBU WAO; FIKRA YAKO NI IPI?

Polisi ni chombo cha serikali chenye nguvu ya kisheria ya kuhakikisha kuwa sheria zinafuatwa, na usalama wa raia na mali zao unakuwepo.

Maswali ambayo sisi raia tunajiuliza leo kama polisi wanalindwa na sheria ya kuhakikisha kuwa nchi inaendelea kubaki salama;
Je Polisi wanaposhindwa kuwajibika kinyume na kiapo cha utii wa sheria zilizowaweka kazini kwa kushindwa kuitumikia nchi na wananchi wake kwa uadilifu nini kifanyike? Kuyahamisha majukumu yao kwa chombo kingine cha ulinzi au kuwawajibisha?
Je tuwafanye nini baadhi ya polisi wanaotumia lugha za ubabe, vitisho na kutumia nguvu hata wakati hakuna sababu ya kutumia nguvu kutatua katika utendaji wake.

Je polisi wetu  wanatumiaje mafunzo yao  katika kuwaelimisha raia kuhusu makosa mbalimbali yanayofanyika, kwa sababu sio makosa yote yanapelekwa mahakamani?

Je askari wetu wanauhusiano wa namna gani  na jamii inayowazunguka? Je polisi wetu wanatumia sheria zaidi au ubabe katika kushughulikia kero za raia wake?

"Je polisi anapomiliki biashara  kama daladala anaweza kusimamia sheria vizuri ambayo inahusiana na biashara yake hiyo ya daladala pale uvunjaji wa sheria ukitokea?"


Je polisi wetu ni msaada kwa raia wenye shida kama inavyofanyika katika nchi nyingine au ndo wanakuwa chanzo cha kero?
je ni jakumu la askari yeyote ambaye anayefanya doria dhidi ya majambazi  ni lipi au anaruhusiwa pia kufukazana na wakosaji wangine kama “daladala” kwa wakati mmoja?

Je ni sahihi kwa polisi kusindikiza magari ambayo yanabeba magendo kama swala la sukari hivi sasa? “ escot ya Mzigo”? Kilio cha waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda katika ziara yake huko Mara jinsi polisi wanavyoshiriki kuhujumu uchumi wa nchi.

Nafikiri itakuwa vyema kama  polisi wetu wataendelea kuwa rafiki wa raia wema ili kuwawezesha kupata ushirikiano katika kubaini wahalifu. Tunazidi kuwaomba  waendelea kufanya kazi zao kwa kufuata sheria na kiapo chao.UWEZO kuchapa kazi vizuri wanao, SABABU wanayo kuendelea kulinda amani; tatizo tu NIA inachechemea pengine kwa sabau ya uduni wa masilahi basi tunaiomba na serikali yetu iliangalie hili la masilahi bora kwa polisi wetu.

Thursday, September 22, 2011

Friday, September 16, 2011

SHERIA ZETU TUNAPOZIPA MUHALI NI UWAJIBIKAJI AU UZEMBE?


KUFUATIA AJALI YA MELI YA “MV SPICE ISALANDER “SISI KAMA TAIFA TUFANYE NINI KUEPUSHA HALI HII ISITOKEE TENA?

Mwishoni mwa wiki kulitokea ajali mbaya ya kupinduka kwa Meli na kuzama, ajali ambayo imesababisha vifo vya watanzania wenzetu zaidi ya 200 wengi wao wakiwa wananwake na watoto, ajali ambayo ilitokea katika bahari ya Hindi katika eneo lenye mkondo mkali wa Nungwi ikiwa inaelekea Pemba;

Msiba huo ni mkubwa kitaifa kwani umekatisha maisha ya watanzania wenzetu ambao ni nguvu kazi yetu kwa maendeleo yetu; wengi wa aliofariki ni wazazi wa familia zetu na watoto ambao walikuwa wanaandaliwa kwa ajili ya maendeleo yetu ya kesho.

Kwa mara nyingine nachukua nafasi hii kutoa pole kwa  kwa ndugu, jamaa na marafiki kwa wazazi kwa msiba huu mkubwa. Na kwa viongozi wetu wakuu wa taifa letu Raisi wa Serikali ya Mapinduzi Ya Zanzibar pamoja na timu yake yote ya uongozi; Raisi wa Jamuhuri wa Muungano wa Tanzania na timu yake vile vile;

Swali ambalo limenigusa sana siku hii ya leo ni hili kwa nini ajali hii ilitokea?

Ni kweli imekuwa ajali kama ajali ambayo imekuja bila hodi na haikuwezekana kabisa kuepukwa?

Je ni ajali ambayo imechangiwa na uzembe wa usimamizi wa wajibu wetu kama watendaji?

Je ni tatizo la uwajibikaji na kuweka rehani ya maisha ya watanzania  kwa kuendekeza “ muhali” na kushindwa kusimamia na kukemea sheria katika atendaji pale panapohitaji kufanya hivyo?

Je ni tatizo la tamaa ya wamiliki wa vyombo na wasimamizi wa miradi hivyo kushindwa kufuata taratibu zinazoongoza biashaya zao?

Mwananchi wa kawaida atajiuliza lakini serikali zetu ziko wapi katika kuwajibika?

Au zinasubiri kuwajibika baada ya tatizo kutokea au hufanya kazi vipi ( management in crisis or management after crisis or crisis management)?

Leo naungana na kauli ya Waziri katika Afisi ya Makamo wa pili wa Rais, Mhe Mohamed Aboud Mohamed

 “amesema,kuwa kamati maalum itaundwa ili kuchunguza juu ya ajali hiyo na ikibainika kuwa uzembe umepatikana sheria itachukua mkondo wake”. ..
”kuwa tatizo kubwa la wazanzibari ni muhali, na amesema ili utendaji mzuri uwepo, lazima suala hili la muhali liwekwe upande ili nchi ipige hatua za maendeleo, na ikibainika kuna watu wanafanya uzembe wa kikazi lazima hatua za sheria zichukuliwe”

Tunaipongeza kauli hii ya awali ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuwa itawachukulia hatua za kisheria wale wote watakaobainiika kufanya uzembe uliosababisha kuzama kwa meli ya Spice Islanders huko katika mkondo wa Nungwi na kusababisha vifo vya watu watanzania wenzetu zaidi ya 200.

Wasiwasi wangu ni huu kuwa, pamoja na kusisitiza umuhimu wa kuangalia na kukagua kila mara vyombo vya usafiri ili kunusuru ajali ambazo zinaweza kuepukika. 


Je wakibainika kwa uzembe huu watachukuliwa hatua za kweli ambazo zitakuwa fundisho kwa wamiliki na watendaji wengine?

Tatizo letu kama taifa siku zote tume zinazoundwa zinaishia kuwa ni viini macho tu na hakuna msukumo wa kweli wa adhabu ambazo zinakidhi haja na haki kwa wafiwa;

Kwa nini meli hiyo ilipakia kupita uwezo wake? Kwa nini captain alikubali kuendelea na safari? Kama yuko hai inapasa awajibishwe kulingana na uzito wa madhara ambayo yametokea  tusimwonee muhari;

Je tunaweza kuthubutu kama serikali ya China inavyothubutu kwa raia wake ambao wanasababisha hasara kwa taifa? Wao hawana mchezo;

Kama tukiweza kuthubutu kwa wavunjaji sheria, uwajibishaji huu tutaweza kuzilinda na kuzitekeleza sheria  na kanuni ambazo zimewekwa kwa ajili ya vyombo vya usafiri ili kudhibiti na kuzuia ajali zisitokee, kwa bahati mbaya sana baadhi ya wamiliki wa vyombo hivyo huacha kufuata kanuni hizo ama kwa makusudi na masilahi binafsi.

Ni kweli kuwa ajali haziepukiki, lakini ajali nyingine husababishwa na uzembe wa wamiliki pamoja nawatendaji wake na hili ndilo lilitokea wiki iliyopita huko Nungwi. 

Natoa wito kwa wadau wote kushikamana katika kuhakikisha vifo vinavyosababishwa na ajali vinapungua kama si kumalizika kabisa kama tukisimama pamoja na kukataa kuburuzwa na wenye mali na kuweza kuwakatalia wengine kupanda kwenye ambacho kimejaa kulingana na uwezo wake tutakuwa tumeweza kuthubutu kwa masilahi ya taifa. 

udhaifu wa usimamiaji wa sheria na muhali umetupa wakati mgumu wa kujua meli hiyo ilikuwa na abiria wangapi? Kwa nini kunakuwa na taarifa ya idadi inayotofautiana? Huu ni uzembe ambao kwa kweli hautakiwi kuendelea kuvumiliwa;

Mwisho tunaiomba Serikali  yetu ambayo ndio muhimili wa maisha bora ya raia wake na usalama wao kuhakikisha inasimamia  utekelezaji wa sheria zake; serikali lazima ithubutu katika  kuwawajibisha wote waliohusika na kuwachukulia adhabu kali na kuacha MUHALI