WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, April 6, 2015

UJUMBE WA PASAKA 2015: AMANI YETU ITALINDWAJE TUNAVYOELEKEA KATIKA UCHAGUZI WA TAIFA LETU 2015?




"Sauti ya mtu imesikika jangwani: `Mtayarishieni Bwana njia yake; nyosheni mapito yake.  Kila bonde litafukiwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa; palipopindika patanyooshwa, njia mbaya zitatengenezwa.  Na, watu wote watauona wokovu utokao kwa Mungu."`

 "Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea kwamba mngeweza kuiepuka ghadhabu inayokuja?  Basi, onyesheni kwa matendo kwamba mmetubu”.

Umati wa watu ukamwuliza, “Tufanye nini basi? Akawajibu, Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo. Nao watoza ushuru wakaja pia ili wabatizwe, wakamwuliza, Mwalimu, tufanye nini?  Naye akawaambia, Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa.  Nao askari wakamwuliza, "Na sisi tufanye nini?  Naye akawajibu, Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo. Toshekeni na mishahara yenu."

Leo tunavyosherekea siku hii ya Pasaka ujumbe mzito kwa viongozi wa serikali, vyama vya siasa na viongozi wa dini tudumishieni amani yetu; na hii itawezekana kwa kutekeleza kauli ya Yohana Mbatizaji  Toshekeni na masilahi” na kwa viongozi wa dini “Hubirini ukweli na muwe wa kweli; hivi vikitekelezwa vitalijengeeni Taifa letu Amani ya kweli”:

Neno  hili ni zito japo lilizungumzwa kipindi kirefu nyuma lakini tunaendelea kulishuhudia leo tunapowaangalia watendaji wetu katika serikali zetu, ndani ya vyama vya siasa na sasa hata miongoni mwa viongozi wa dini ambao nao wameanza kupenyeza masilahi yao binafsi, na kuanza kuzoofisha amani ya Taifa letu.

Neno hili linatufundisha uadilifu, uwajibikaji kulingana na maadali  na kanuni za kazi ambazo zinatulazimu sisi kama watendaji wa Taifa kuweka mbele matakwa ya Taifa na sio masihahi binafsi;

Najiuliza tena  leo hii hata viongozi wa dini mbona wamekuwa mbele katika kutanguliza masilahi binafsi mbele kuliko mwongozo wa Vitabu vikatifu kwa katika kujenga amani; Je wanafanya hivyo kwa kivuli cha nani? Na  hili linamaana gani kwa taifa letu? 

wananchi wa Taifa hili wanahitajii uhuru wa kiuchumi ambao unatokana na viongozi wetu watangulize mbele masilahi ya Taifa, warizike kidogo wananchokipata; kinyume chake kama hawatarizika na hicho kidogo hawataweza  kuweka mbele masilahi ya taifa na bali watatanguliza mbele vitendo vya  rushwa na ufisadi ambao unarudisha maendeleo ya Taifa nyuma sana na kudhoofisha amani yetu.

Ujumbe wa  Pasaka ya mwaka 2015  itukumbushe sisi  Kama Taifa na kama Raia na watendaji ambao tumekula kiapo cha utii na maadili bora ya uwajibikaji kwa Taifa letu kuwapa wananchi wanyonge zawadi kubwa ya  uhuru  wa kiuchumi,  ili kila mmoja wetu aweze kuyafurahia  zawadi pekee ya rasilimali  ambayo Mungu amelijalia Taifa letu. Hakuna atayepingana nami kuwa  nchi yetu imefurika kwa  asali na maziwa tatizo ni wachache tu ambao wanafaidi kwa kutoridhika na mishahara yao. 

kwa kipindi kirefu tumeona kuwa nchi yetu  Tanzania iliyokuwa ikifurika neema  ya rasilimali sasa imegeuka; kuwa nchi inayofurika machungu; matendo yaleyale ya kifisadi, ya ukandamizaji, ya unyanyasaji ambao  Farao aliwatendea wana wa Israeli huko misri miaka hiyo; lakini kwa kuangalia falsafa hiyo ya matendo ya Farao ndio tunaishuhudia sasa namna watendaji wetu walikokabidhiwa dhamana ndani ya Taifa letu  ambao sio waadilifu wananyo haribu nchi, na kuacha machingu kwa wananchi ambao bado wako kwenye dimbwi la umasikini.

je viongozi wetu wa dini leo hii wanahubiri amani ambayo Yohane Mbatizaji aliifafafanua kulingana na makundi yaliyokusanyika?
Je viongozi wa dini wanahubiri amani au wanaendeleza chuki moingoni mwa wananchi wa Taifa letu?

Kulingana na Yohane matajiri wanaotakiwa kuangalia haki ya maskini, "Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo."(Lk 3,11), kwa watoza ushuru waepuke rushwa na matendo ya kifisadi "Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa."(Lk 3,13) na kwa maaskari wazingatie haki "Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo. Toshekeni na mishahara yenu."(Lk 3,14).

Leo hii ndani ya Taifa vitendo hivi vimeshamiri tena kwa kiasi kikubwa; na pengine kila mmoja ameshiriki kwa namna moja au nyingine katika uovu huu. Hii inaweza kuwa moja kwa moja au kwa kutokuwajibika ipasavyo katika eneo lake la kazi na hivyo kusababisha mianya katika kukua kwa matendo haya maovu. Wito wakati tunasherekea Pasaka 2015 sisi kama Taifa inatupasa tubadilike na kuhakikisha haki na upendo vinashamiri katika jamii yetu.

Kama tutafanikiwa kuishi kwa ujumbe huu wa Yohani Mbatizaji kuwa tutosheke ni mishahara yetu mimi naamini kuwa tukiweka mbele maslahi ya nchi, nchi itasonga mbele. TUKUMBUKE KAULI YA YOHANA MBATIZAJI KWA WALE ASKARI kuhusu dhuluma:
TOSHEKENI NA MISHAHARA YENU, watu wana madaraka makubwa mishahara mikubwa na masurufu manono lakini bado wanaiibia nchi. Kwa nini lakini? Hii choyo ulafi kwa nini?

Nafikiri Tatizo la wanasiasa na Viongozi wa dini wakishafanikiwa kujikwamua kimasilahi wanasahau kuwa wananchi bado ni masikini na wanahitaji masaada ili nao waweze kufarahia zawadi ya maisha ambayo wamezawadiwa na Mwenyezi Mungu.

Amani kwao sio wimbo ulio bora tena kwao, maisha bora ya wananchi wao inabaki katika slogan tu.

Wanatumia muda mwingi kutukanana na kuonyeshana ufahari wao, ambao wamepata kwa kuendelea kuwakamua hawa wanachi masikini.

Je watendaji wetu wako tayari kutoa hesabu za utendaji wao siku watakapotakiwa na Mwenyezi Mungu tukiamini kuwa kazi zote hutoka kwa Mungu?

Nafiki Pasaka hii kujifunze kitu kingine kipya kuwa “Jihadharini na tabia ya kupenda fedha, na “toshekeni na mlivyonavyo” kwa sababu Mungu mwenyewe alisema,

“Kwa vyo vyote sitakupungukia kabisa, wala sitakutelekeza na kukuacha bila msaada. Kamwe, kamwe, sitakuacha hata kwa kiwango kidogo, kukuacha bila msaada, au kukuacha, au kukuangusha, au kulegeza mkono wangu kwako. Hakika sitafanya hivyo! Kwahiyo tunafarijika na kutiwa moyo, na kwa uhakika na ujasiri twathubutu kusema, ‘Bwana ndiye anisaidiaye” (Ebr 13:5, 6)

Kwa kutosheka na mishahara yetu na kwa kuamini kuwa sisi ni wachache ambao tumechaguliwa na Mwenyezi Mungu kuwa saidia wengine ili waweze kupata ridhiki zao; au kufurahia asali na maziwa kwa vipaji vyetu kwa kutimiza wajibu wetu tutakuwa tunatekeleza ujumbe huu wa “Utafuteni kwanza ufalme wa Mungu na haki yake na hivi vitu vingine vyote mtapewa kwa maelefu.

Tukitenda kila kitu kwa haki kamwe hatutakosa chochote unachohitaji kitakuwa ziada. Mwenyezi Mungu atakupa namna ya kupata kila uchokihitaji zaidi.

Imani yangu ni kama ile ya Paulo kama tutatosheka ni mishahara yetu,na kuwajali wanyonge katika Kupata Riziki
zao, “Na Mungu wangu atawajazeni na kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu wake …”. Lakini hili litawezekana kama viongozi wetu wa serikali, vyama vya siasa na wale wa dini watafanya kazi zao kulingana na na viapo vya kazi zao.

"Mungu hatakosa KUWAONGEZEA wale wote wanaoifanya kazi yake sawasawa na mapenzi yake" huu ndio ujumbe wa Pasaka 2015

No comments:

Post a Comment