WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, January 25, 2012

KATIBA HII NI YETU SOTE;

MARIDHIANO KATI YA VYAMA vYA UPINZANI NA ASASI ZINAZOTAKA KUSHIRIKI MCHAKATO HUU KWA MANUFAA YA WATANZANIA NI JAMBO LA BUSARA SANA;



"Kazi ya kutengeneza katiba ni ya wananchi, katiba ni ya wananchi, kwa manufaa ya wananchi," anasema Bw. Kiwanga

Kauli za makamu wa pili wa Rais Zanzibar Mheshimiwa Maalim Seif “Wananchi wanapaswa kujiandaa kutoa maoni bila ya uoga, na jambo muhimu ni kuhakikisha katika maoni yao hawamtukani mtu: Nyinyi Wazanzibari na ndugu zetu wa Tanzania Bara ndio tuliovaa kiyatu (Muungano) na aliyevaa kiyatu ndiye anayejua msumari unachomea wapi, au anayelala kwenye kitanda ndiye anayejua kunguni wake”,


Mheshimiwa Maalim Seif aliendelea kueleza kuwa “katika kuzingatia mambo yenye maslahi kwa Zanzibar wasitokee watu wakaweka maslahi binafsi mbele, alisema haitakuwa jambo la manufaa kwa Zanzibar iwapo watajitokeza baadhi ya viongozi wakaanza kujadili nafasi zao za Ubunge na uongozi, iwapo muundo Fulani wa Muungano utapita”

Kauli za Mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi James Mbatia   “Tunakupongeza kwa kusimammia suala la Katiba vizuri, ni suala zito ambalo litatupa uhai vizazi na vizazi vijavyo. Upinzani sio uadui, tunahitaji kufanya marekebisho ya Katiba kwa amani na hoja bila kuvuruga amani yetu suala la Katiba linahitaji ushirikiano wa pamoja kwa nia njema, kwani taifa hili ni letu sote;  Ni jambo kubwa sana, wewe ndiyo Rais wa kwanza kutengeneza sheria ya kupata katiba mpya na kuanzisha Mchakato wa kupata Katiba Mpya.”

WAZIRI wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, “Katiba mpya izingatie matakwa ya wananchi ili kuliweka taifa katika hali ya utulivu. Hili la Katiba mpya ni jambo mhimu na nyeti…tunataka Katiba ijayo ikidhi matakwa ya Watanzania. Tume itakayoundwa na rais kukusanya maoni ifanye hivyo bila konakona fulani fulani,”

Mheshimiwa John Mnyika “Izingatiwe kuwa kwa sasa Tanzania haifanyi marekebisho ya Katiba bali tunakwenda kufanya mapitio (review) na hatimaye kuwa na katiba mpya; hivyo suala la ushirikishwaji wa umma sio katika kutoa maoni tu bali kuamua misingi muhimu ya katiba ni suala lenye umuhimu wa pekee ili tuwe na katiba inayokubalika na umma mpana isije yakajirudia tena yaliyojitokeza kwenye kuandikwa kwa katiba ya mwaka 1977”.


Mheshimiwa Mbowe amekuwa akisisitiza kuwa "Suala la katiba mpya limetekwa na baadhi ya wanasiasa ambao hawajui ni fursa ya kila mtanzania, wapo wengine wanaona chadema inapinga kuwepo kwa katiba mpya, sisi tunahitaji sana na tunachokitaka wananchi washirikishwe na waamue wenyewe,”



Hivi karibuni tumeendelea kuona nia njema ya Rais wetu Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akiendelea na majadiliano na wawakilishi wa vyama mbalimbali vya siasa ambavyo vinajenga kambi ya upinzani; kama waandishi wengi walivyoandika na kuendelea kuandika kuwa “ Tunachotaka kusema hapa ni kwamba viongozi hao wa pande hizo mbili wametupa matumaini mapya kwamba sasa upo uwezekano mkubwa wa kupata Katiba Mpya ya kuipeleka nchi yetu kwenye maendeleo katika misingi ya demokrasia na utawala bora. Tunasema hivyo kutokana na dhamira ya kweli iliyoonyeshwa na pande hizo mbili katika mazungumzo hayo ambayo vyanzo vyetu ndani ya Serikali vimethibitisha kuwa, mazungumzo hayo yalikuwa magumu na yasingefanikiwa iwapo pande hizo zingetanguliza ubinafsi na  itikadi za vyama vyao.”


Tunahitaji kuendelea kuelewa kuwa tutapata katiba mpya lakini tunahitaji katiba ya aina gani? Katiba ambayo itaelemea upande mmoja wa mlengo Fulani wa kikundi cha watu na chama chao; jibu ni hapana tunahitaji katiba ambayo italenga mpya kuwakwamua wananchi wa Tanzania wa pande zote bila ubaguzi; tunachohitaji sana wanasiasa wetu katika kipindi hiki wawe kweli wanaupeo  na  wawe na ukomavu wa kisiasa  ambao ni pamoja viongozi kuwa na uvumilivu na kujua jinsi ya kutatua matatizo bila kusababisha malumbano , na kujenga chuki miongoni mwa wananchi.

Majadiliano  ya hivi karibuni ya vyama vya CHADEMA, NCCR-MAGEUZI, CUF  pamoja na serikali ambayo ndio msimamizi mkuu wa mchakato huu wa katiba ambayo sasa tunaanza kuona kuwa inamwelekeo wa  unaoleta matumaini zaidi kwa masilahi ya Taifa na sio chama au kikundi Fulani cha watu; au kuingiza siasa  za vyama ndani ya mchakato kwa vile katiba itabeba  sheria mama ya nchi ni vizuri kutatoa ushirikiano wa dhati katika mchakato huu kwa maslahi ya nchi


Itakuwa ni kitu cha busara na cha kupongezwa sana kama vyama vya siasa kwa uwezo wao wa uenezi kuanza kuwaelimisha na  kuwashirikisha wananchi katika utoaji wa maoni  katika mchakato wa kutengeneza Katiba amabayo itaweza kutuvusha  sio tu katika  kuendeleza amani bali hata katika kuleta maendeleo ambayo tunayahitaji sasa kuliko wakati mwingine wowote; kama tutaweza kuhamasiha wananchi wetu waweze kuchangia tutakuwa  kumeipa (legitimacy ) yaani kweli ni katiba inayokubalika kwa kila mtu na hakutakuwa na malalamiko kuwa wananchi wameporwa mamlaka  ya utengenezaji katiba.
kama wataalamu wengi walivyowahi kuseaka kuwa Demokrasia kwa ufupi ni dhana inayolenga ushiriki wa wananchi, katika kuweka misingi sahihi ya uendeshaji wa nchi na wao wakiwa ndio msingi wa mamlaka yote ya nchi nawalio na uwezo wa mwisho wa kuipa serikali madaraka na mamlaka hayo ya kuongoza nchi. Kwa mantiki hii moja ya msingi mkuu unaokuza demokrasia ya namna hii ni Katiba ya Nchi. Katiba ni msingi mkuu wa uendeshji wa nchi,ukuaji wa demokrasia na utawala wa sheria. Yenyewe ndiyo sheria na ni kioo cha maisha bora  ya wananchi wake:



Tunahitaji Katiba iliyomadhubuti huwa  ambayo ni msingi mkubwawa utawala bora; kwani katiba bora  inazingatia uwazi, uwajibikaji na utawala wa sheria dhana ambayo kwa ujumla ni msingi wa kwanza wa  demokrasia na maendeleo ya nchi. Lazima tuendelee kusisitiza kuwa ukweli ni kuwa katiba inayopendekezwa  inatakiwa iwe ni  mradi wawananchi wa Tanzania Bara na Visiwani. Katiba mpya itakuwa ya watanzania wote na tusikubali ifanywe kuwa ya serikali iliyopo leo na itakayokuja kesho.

Katiba mpya ikikamilika tunatamani itufanyie haya yafuatayo:
·        Ituletea kiongozi Mzuri pamoja na serikali yake;
·        Ituletea chama chenye sera bora, kwa masilahi ya wanachi
·        Ituletea watumishi wa serikali na umma ambao ni waadilifu
·        Iendelee kutudumishia amani ambayo tumeifurahia kwa muda mrefu sasa


Nahitimisha kwa kusema hivi jamani watanzania wenzangu, wanasiasa, wananchi na wananchi wote kwa ujumla kuwa;

"Tanzania ni yetu, hatma ya taifa hili iko mikononi mwetu, tuwajibike, tuache woga, tujadili, tufikie mwafaka wa kitaifa. Katiba mpya ni jibu. Jibu la kurudisha maadili ya taifa na kulinda rasilimali za taifa. Tuchukue hatua, Hivyo Katiba inapaswa kuwa ni matokeo ya mwafaka wa kitaifa kwenye masuala yote ya msingi ya nchi husika”

HIZI ZIMEKAAJE













Je umejiuliza maswali mangapi hapa? na umepata majibu mangapi? je majibu yako ni HASI au CHANYA?

Wednesday, January 18, 2012

BYE BYE REGIA MTEMA

"A simple smile takes a moment, but the memory of it sometimes lasts forever"

Sunday, January 15, 2012

TANZIA


Mjengwa
 
  
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepatwa na majonzi makubwa na kinasikitika sana kwa kifo cha Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Taifa, Mheshimiwa Regia Mtema ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum na Waziri Kivuli wa Kazi na Ajira. Mheshimiwa Regia Mtema amefariki leo tarehe 14 Januari 2011 kwa ajali ya gari katika eneo la Ruvu darajani.

Katika uhai wake marehemu Regia Mtema amefanya kazi mbalimbali za kisiasa na kijamii katika taifa. Marehemu Regia Mtema amezaliwa tarehe 21 mwezi Aprili mwaka 1980 na kusoma shule za sekondari kidato cha kwanza mpaka cha sita katika shule ya sekondari ya Forodhani na Shule ya Wasichana ya Sekondari ya Machame. Marehemu Regia Mtema alipata shahada yake ya kwanza (Bsc Home Economics and Human Nutrition) katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine.

Mara baada ya kuhitimu masomo yake marehemu Regia Mtema alifanya kazi katika taasisi mbalimbali kabla ya kujiunga na CHADEMA na kuteuliwa kuwa Afisa Mwandamizi katika Kurugenzi ya Vijana ya CHADEMA na baadaye kuteuliwa kuwa Afisa Mwandamizi katika Kurugenzi ya Mafunzo ya CHADEMA nafasi ambayo aliishikilia hadi mwaka 2010 alipoteuliwa kuwa mbunge wa viti maalum.

Viongozi wakuu wa CHADEMA wakiongozwa na Mwenyekiti Freeman Mbowe ambaye pia ni kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni, Katibu Mkuu Dr. Wilbroad Slaa, wajumbe wa kamati kuu, wakurugenzi wa chama makao makuu na wabunge wamejumuika hivi sasa na familia ya marehemu katika kipindi hiki kigumu.

CHADEMA inatoa pole kwa familia ya marehemu Regia Mtema, wanachama wote na wananchi wa Mkoa wa Morogoro hususani wa Jimbo la Kilombero kutokana na msiba huu wa ghafla katika wakati ambapo mchango wake ukihitajika kwa chama na kwa taifa.

Taarifa zaidi kuhusu taratibu za maziko, itatolewa mara baada ya kukamilisha majadiliano baina ya familia ya marehemu, chama na Ofisi ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mipango ya mazishi ya marehemu inapangwa nyumbani kwa Baba wa Marehemu Regia Mtema, Ndugu Estelatus Mtema, Tabata Chang'ombe. Ratiba ya maziko itatolewa baada ya kukamilika kwa taratibu zinazopangwa na familia ya marehemu, Ofisi ya Bunge na chama.

Mungu ailaze roho ya Marehemu Regia Mtema, mahali pema peponi. Amina.


Imetolewa na:

John Mnyika(Mb)
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi

HABARI KWA HISANI YA MJENGWA BLOG

Sunday, January 8, 2012

BAADHI YA WANASIASA TUKIWAENDEKEZA SANA WANARUDISHA NYUMA MAENDELEO;


·        FUATILIA MALUMBANO YA WANASIASA WETU

Hakuna kitu kibaya katika maendeleo ya jamii yetu kama siasa ikitumika vibaya katika maumuzi mbalimbali; Siasa ni safi sana usipoijua haitakusumbua, lakini ukiijua na ukiendekeza kwa misingi tu ya siasa inaweza kukupa ugonjwa wa moyo na itakupa  shida; kwa mtazamo mwingine siasa kwa nchi zetu ambazo tunaziita dunia ya tatu mara nyingi zinarudisha maendeleo nyuma katika kivuli cha unafiki wakati wanasiasa wakivaa ngozi ya kondoo wakati kwa ujumla wao ni chui wa ubinafsi;  
Mtihani mkubwa ambao unawakabili sana wananchi wanatakiwa kweli wajue wanasiasa ni nani pamoja na mapenzi ya vyama vyao; kwa maneno mengine wananchi wanatakiwa kuelewa kuwa Siasa ni matokeo ya wanasiasa, wakiwa wenye hekima na waliojaa busara siasa ni nzuri sana, lakini wakiwa wale ambao  wanatafuta umaarufu siasa  inakuwa haina tija kwa maendeleo ya wananchi na Taifa kwa jumla. Kwa hiyo siasa hubaki kuwa ni porojo za kujinufaisha kwa kikundi Fulani cha watu, na maamuzi yao daima yanalenga sana katika unafiki na sio ukweli wa maendeleo; Maamuzi yao yanaendelea kuwa “sisi na wao” au “hiki ni chetu wao hawana haki
Unajua mwanasiasa wa kweli ni Yule ambaye atamwambia mwananchi ukweli hata kama anajua kwa kufanya hivyo utapoteza umarufu wake, lakini mwisho wa siku mwananchi atafaidika na maamuzi hayo kwa vizazi vijavyo;
Nionavyo mimi wanasiasa wetu wengi  wamebaki na mtazamo unaolenga sana katika kuwafanya wao waweze kuchaguliwa katika chaguzi mbalimbali:
Hebu angalia wabunge wengi na kampeni zao je utetezi wao ni wa maendeleo endelevu au inaishia kumfurahisha mwananchi kwa kipindi Fulani? Na ukiangalia sana utetezi wao mwisho una kuwa na majuto makubwa “ Maafa ya Jagwani mfano, furaha ya wananchi kuishi kwenye bonde hilo ambalo sio salama imeleta matokea gani kwa taifa na wananchi kwa ujumla?furaha yao imedumu kwa kipindi kifupi sana tumejionea wenyewe;
Sasa lipi bora umwambie mwananchi ukweli ajue na akasirike na akija kugundua kuwa ushauri wako ulikuwa mwiba kwake lakini umemletea amani na maendeleo endelevu, kwani haitaji tena kutafuta pesa kujenga nyumba nyingine, na kwa kweli kwa msimamo wako wa ukweli na unaofikiria miaka 100 mbele wananchi na vizazi vyao watakushukuru kwa maisha yao yote?
Tunaendelea kushuhudia kuwa wanasiasa wetu  hasa wabunge ambao wanajifanya watetezi wakati huhu ni  wanawakaanga wapiga kura wao kwa mafuta yao wenyewe bila kujua; ni bora Yule anayekuambia ukweli  kwani utamchukia lakini utakuwa na maswali utaendelevu kujiuliza na utapata majibu mazuri hatimaye.
 Nawauliza wanasiasa wetu, kweli wanakuwa na washuri wakuwashauri nini wanatakiwa kuzungumza ili wanachokiongee kiwe na tija kwa muda mrefu? Au wamezoea tu kuropoka kupata cheap popularity? Hebu liangalie sakata la kupanda kwa bei ya ferry kigamboni nini kinaendelea ni siasa au malumbano? Ni ufanisi au uwakilishi? Ni tija au kutafuta umaaurufu? Ongezeko la nauli linahitajika kwa sasa kulingana na kupanda kwa gharama za uendeshaji na kushuka kwa shilingi au hakuna haja ya kupandisha?

Wanasiasa wanasahau kuwa siasa inatakiwa kuwa ni sehemu ya uongozi ambao unatakiwa utawaliwe na maadili ya kusimamia ukweli; siasa zetu na wanasiasa wetu wanatabia ya kufanya maamuzi ya pamoja, lakini tukumbuke falsafa ya maamuzi ya wengi ni kuwa  “kila mtu miongoni mwao anapoiteza uwezo wake wa kufikiri sahihi na anaanza kufikiri kulingana na fikra  za mwenzake na tatizo ni hili kama Yule mwenye ushawishi mkubwa atakuwa na mawazoa mgando basi itakuwa tatizo kwa wote”

Wanasiasa wanatakiwa wakumbuke yafuatayo;
·        Kufanya vitu muhimu na vikubwa ni ngumu sana kwa wanansiasa na hata kutoa maelekezo  ya mambo muhimu ni ngumu pia kwa ajili ya ufanisi, kwani mawazo mazuri na mazito mara nyingi yanaanza  na mengi yataishia kugusa maisha ya watu kwa wakati uliopo na sio kwa faida ya baadae.
·        Kadiri ambavyo wanafanya na kutekeleza wajibu wao bila kuogopa ndani ya jamii  ni ukweli kuwa hata jamii itaendelea kuwahitaji na kamwe haitatamani wanasiasa hao waondoke madarakani;
wanasiasa  tunaomba yafuatayo toka kwenu Chonde:
·        Mtufungulie  njia za maendeleo kwa kuwa wakweli;
·        Tunawaomba mfanye kazi kwa umakinifu fikra zenu ziwe daima katika kuboresha maisha ya wananchi kwa utaratibu ambao utazingatia sheria zilizopo, uwezo wa kujiendesha sisi wenyewe kiuchumi ili kuboresha huduma kwa kuwatumia washauri wa ndani.
·        Kuondoa woga wa kuthubutu kimaamuzi na kujua maendeleo maana yake ni nini? Tumefikaje hapa na sasa tufanye nini? Hebu angalia matatizo mengi ambayo Taifa limepitia ambayo imesababishwa na misimamo ya wanasiasa wake?
·        je wanasiasa wameshajaribu kujiuliza kuwa kwanini tupo katika hali hii na tufanye nini kuibadilisha. Mmeshawahi kutoa changamoto kwa wananchi katika sehemu husika  je tutayafikiaje maisha bora? Tupende au tusipende kamwe maisha bora hatyatapatikana kwa njia za mkato.
Katika mambo mengi ambayo wananchi wanayafurahia ni yale ambayo wananchi wanaambia kuwa tutaendelea bila kazi ngumu, mtatembea bure bila kulipa nauli hapo itakuwa shangwe; kwa kweli tatizo letu tunafurahia mambo ambayo yameshatengenezwa hata Marekani imeendelea kwa kujituma na kazi ngumu na wananchi wake kuambiwa ukweli;
Tutake tusitake msingi bora wa maendeleo lazima tuhakikishe kuwa wananchi wanashiriki kikamilifu katika kila hatua ya kujenga nchi na kuleta mabadiliko ambayo yanatokana na mikono yao wenyewe.
Kama taifa ili tuweze kusonga mbele Kimaendeleo kauli ya Baba Wa Taifa bado ina nguvu kwamba maendeleo yetu yatategemea sana “ Siasa safi iliyojaa uadilifu na sio unafiki; Watu ambao nasi lazima tujitume sisi wenyewe na kuondoa dhana ya kusubiri tufanyiwe kila kitu eti na wanasiasa;  na uongozi ambao hauogopi kuondolewa madarakani kwa kumwambia mwananchi ukweli kwa ajili ya maendeleo yake na kizazi chake hapo baadae;
Huu ni muda wa kushirikiana wote tulete maendeleo ya nchi kwa haraka hebu tusimame na tufanye maamuzi ya kutufanya tuendelee kwa haraka kwa nyenzo zetu 
 Kamwe wanasiasa tusiwape nafasi ya kuendelea kutugawa sisi wananchi katika matabaka mawili;
  • Tabaka la uadui miongoni mwetu sisi wenyewe
  • kuendelea kututumia sisi kama nyenzo/ngazi ya kujinufaisha na  kufanikisha maisha yao binafsi?