WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Thursday, July 23, 2015

Chadema yafunika Mwanza.

  Mbowe asisitiza Ukawa bado wamoja, Lembeli, Bulaya wakaribishwa rasmi.

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akihutubia maelfu ya wakazi wa jiji la Mwanza kwenye viwanja vya Magomeni jijini humo jana. (Picha: Mpigapicha Wetu).
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) jana kililifunika jiji la Mwanza, baada ya kufanya mkutano mkubwa wa hadhara uliokusanya maelfu ya wakazi wa jiji hilo katika viwanja vya Magomeni.
 
Mkutano huo uliohudhuria na viongozi wote wa juu wa Chadema pamoja na waliokuwa wabunge wawili wa CCM, James Lembeli (Kahama) na Esther Bulaya (Viti Maalum) waliopokelewa rasmi baada ya kujitoa katika Chama Cha Mapinduzi (CCM).
 
Mkutano huo ulikusanya wafuasi kutoka Mwanza na mikoa ya jirani ikiwamo Shinyanga (Kahama) na Mara (Bunda).
 
Kabla ya mkutano huo kuanza, wafuasi wa chama hicho walisimamisha kwa muda shughuli mbalimbali za wakazi wa jiji hilo baada ya kufunga barabara ya Makongoro kutoka uwanja wa ndege walikowapokea viongozi wao hadi katikati ya jiji.
 
Misururu ya waenda kwa miguu, pikipiki maarufu ‘bodaboda’ na magari yalisimamisha shughuli hizo kutokana na kuwapo katika msafara wa kuwapokea viongozi hao wa Chadema.
 
Wabunge hao waliohama CCM na kujiunga na Chadema waliokuwapo katika msafara huo hivyo kuongeza mbwembwe za wafuasi hao.
 
Hata hivyo, polisi wa usalama barabarani walijipanga vyema na kuhakikisha usalama unakuwapo kwa waenda kwa miguu na watumiaji wengine wa vyombo vya moto.
 
MBOWE
Akizungumza katika mkutano huo wa hadhara, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alisema wamefanya mkutano huo kwa lengo la kuwafahamisha wanachama na wapenzi wa chama hicho kuhusu siku atakayotangazwa mgombea atakayesimamishwa kupeperusha bendera ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) katika uchaguzi mkuu ujao.
 
“Tunawashukuru wakazi wa Mwanza kwani mmeonyesha jinsi mnavyotaka mabadiliko katika nchi hii, mmeteseka sana…tumenyimwa uwanja wa CCM Kirumba uliojengwa na Watanzania hadi tunatumia uwanja huu ambao umesababisha watu kuzimia kutokana na wingi wa watu,” alisema Mbowe.
 
Mbowe pia katika mkutano huo aliwatambulisha Lembeli na Bulaya pamoja na kuwakabidhi kadi za Chadema na wao kuzikabidhi zile za CCM walizokuwa nazo.
 
Mbowe pia aliwaeleza wananchi na wanachama wa Chadema kuwa Ukawa bado wamoja.
 
Hata hivyo, alisema baadhi ya viongozi wa vyama vinavyounda umoja huo wa CUF, NCCR-Mageuzi na NLD hawakuwapo kwenye mkutano huo kwa kuwa walikuwa wakiendelea na shughuli mbalimbali za vyama vyao.
 
Alisema CUF watakutana Julai 25 kuamua suala hilo na kuwa NCCR-Mageuzi na NLD nao watakutana wakati wowote na baada ya hapo vyama vyote vitakutana kutoa maamuzi juu ya mgombea watakaye msimamisha kugombea urais.
 
LEMBELI
Akizungumza kwenye mkutano huo baada ya kutambulishwa, Lembeli alisema: 
 
“Lazima sasa safari tuliyoitegemea itafanikiwa kwa wapinzani kuingia Ikulu katika uchaguzi mkuu Oktoba mwaka huu, nimewachukia kwa muda mrefu mafisadi na wezi ndani ya CCM, leo hii nimeamua kutangaza rasmi kuachana nao,” alisema Lembeli na kuongeza:
 
“Kabla sijajiunga Chadema Jumapili iliyopita nilisali sana na familia yangu ili njiachane na chama cha umasikini katika nchi na kwenda chama chenye neema, siku iliyoifuata nikaamua kutangaza kujiunga nanyi,” alisema Lembeli.
 
 BULAYA
Alisema atashirikiana na viongozi wa Chadema mkoa wa Mara kuhakikisha anachukua Jimbo la Bunda Mjini na kumtoa Stephen Wasira ambaye amekaa madarakani kwa vipindi vyote vya  marais wa nchi hii,” alisema Bulaya.
          
PROF. SAFARI
Naye Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Prof. Abdallah Safari, alisema chama hicho kimejipanga kukabiliana na nguvu ya mgombea wa CCM, Dk. John Magufuli, muda wa kampeni utakapowadia.
 
Alisema Chadema wana ‘silaha’ za kumwangamiza mgombea huyo wa CCM, kutokana na kufahamu mambo mengi aliyonayo ya kifisadi ndani ya chama chake.
 
 DK. SLAA
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbroad Slaa, alisema chama hicho kimejipanga kuwashitaki wagombea wake watakaotangaza kujitoa katika kinyang’anyiro cha uchaguzi kwa kuhongwa na wapinzani wao.
 
“Mtu akichukua fomu, atasainishwa fomu maalum mbele ya mwanasheria kisha akijitoa tu kwa kuhongwa, ataipata kwani sheria itasema naye,” alisema Dk. Slaa.
 
 JOHN MNYIKA
John Mnyika Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Bara, alisema chama hicho kinawakaribisha wabunge hao wapya pamoja na wengine wenye nia nzuri na maendeleo ya nchi yao.
 
“Tumekubaliana kwa pamoja kuchukua utawala wa nchi hii ili kuwakomboa Watanzania wanaoteseka na maisha magumu yaliyosababishwa na utawala wa CCM,” alisema Mnyika.
 
 SALUM MWALIMU
Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar, Salum Mwalimu, alisema:
“Chadema tumebalisha staili ili kukabiliana na ‘goli la mkono’ la CCM…kwani Wazanzibar wanaunga mkono umoja wetu wa Ukawa kutokana na wao kuhitaji muundo wa serikali tatu.”  
 
HALIMA MDEE
Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha), Halima Mdee, alisema ‘goli la mkono’ lililosemwa na CCM litafungwa na Chadema badala ya wao.
 
“Hilo goli tutalifunga sisi, kwani hawa wabunge wawili tuliowakaribisha tayari wameingia katika ufalme wa Watanzania waliochoka maisha ya chama tawala,” alisema Mdee.
 
 ARCODO NTAGAZWA
Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya chama hicho, Arcardo Ntagazwa, alisema Chadema siku zote inaanza na Mungu na kumaliza na Mungu, hivyo wana uhakika wa kuchukua Ikulu mwaka huu.
 
LISSU
Mwanasheria wa Chadema na aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, alisema hawana shaka na mgombea urais wa CCM, Dk. Magufuli, kwani tayari wamemuandalia ‘silaha’ ambazo zinaweza kummaliza katika kampeni muda ukifika. 
CHANZO: NIPASHE

Monday, July 20, 2015

MAGUFULI AWAAGA WAKAZI WA MGANZA



























   Mgombea Urais kwa chama cha Mapinduzi CCM,Dkt John Pombe Magufuli akipokea kadi za Wanachama wa vyama mbalimbali vya upinzani na kujiunga na CCM,jioni hii katika viwanja vya mji mdogo wa Muganza,wilayni Chato Mkoani Geita,Mh Magufuli amezoa wanachama wapya waliorudisha kadi zao wapatao zaidi ya 150.
  Mgombea Urais kwa chama cha Mapinduzi CCM,Dkt John Pombe Magufuli akipokea kadi za Wanachama wa vyama mbalimbali vya upinzani na kujiunga na CCM,jioni hii katika viwanja vya mji mdogo wa Muganza,wilayni Chato Mkoani Geita,Mh Magufuli amezoa wanachama wapya waliorudisha kadi zao wapatao zaidi ya 150.Mh Magufuli yuko jimboni kwake Wilayani Chato kuwaaga na kuwashukuru Wananchi wake kwa kumpa ridhaa ya kuwaongoza kwa miaka 20 akiwa Mbunge.
   MKe wa Mgombea Urais wa CCM,Mama Janeth Magufuli akiwasalimia na kuwashukuru Wananchi wa mji huo kwa mapokezi mazuri na makubwa waliyoyapata wilayani humo.
  Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara),Ndugu Rajab Luhwavi akiwasalimia wanachama wa CCM pamoja na Wananchi waliofika kumlaki Dkt Magufuli jioni ya leo katika viwanja vya mji mdogo wa Muganza wilayani Chato mkoa wa Geita.
   Mgombea Urais kwa chama cha Mapinduzi CCM,Dkt John Pombe Magufuli akiwapungia mkono pia na kuwashukuru Wananchi wake kwa kumpa ridhaa ya kuwaongoza kwa miaka 20 akiwa Mbunge wao. 
  Baadhi ya Wananchi wa mji mdogo wa Muganza,Wilayani Chato na vitongoji vyake waliokuwa wamekusanyika kwenye viwanja vya mji mdogo wa Muganza jioni ya leo wakishangilia kwa  furaha kubwa mara baada ya Mbunge wao na Mgombea Urais kwa chama cha Mapinduzi CCM,Dkt John Pombe Magufuli kujitambulisha kwao na pia kuwashukuru kwa kumpa ridhaa ya kuwaongoza kwa miaka 20 ya Ubunge ndani ya jimbo hilo.
  Baadhi ya Wananchi wa mji mdogo wa Muganza,Wilayani Chato na vitongoji vyake wakimsikiliza Dkt Magufuli alipokuwa akiwasalimia na kuwashukuru katika viwanja vya mji mdogo wa Muganza jioni ya leo.


  Baadhi ya Wananchi wa mji mdogo wa Muganza,Wilayani Chato na vitongoji vyake waliokuwa wamekusanyika kwenye viwanja vya mji mdogo wa Muganza jioni ya leo wakishangilia kwa  furaha kubwa mara baada ya Mbunge wao na Mgombea Urais kwa chama cha Mapinduzi CCM,Dkt John Pombe Magufuli kujitambulisha kwao na pia kuwashukuru kwa kumpa ridhaa ya kuwaongoza kwa miaka 20 ya Ubunge ndani ya jimbo hilo.
    Baadhi ya Wananchi wa mji mdogo wa Muganza,Wilayani Chato na vitongoji vyake waliokuwa wamekusanyika kwenye viwanja vya mji mdogo wa Muganza jioni ya leo wakishangilia kwa  furaha kubwa mara baada ya Mbunge wao na Mgombea Urais kwa chama cha Mapinduzi CCM,Dkt John Pombe Magufuli kujitambulisha kwao.
   Baadhi ya Wananchi wa mji mdogo wa Muganza,Wilayani Chato na vitongoji vyake waliokuwa wamekusanyika kwenye viwanja vya mji mdogo wa Muganza jioni ya leo wakishangilia kwa  furaha kubwa mara baada ya Mbunge wao na Mgombea Urais kwa chama cha Mapinduzi CCM,Dkt John Pombe Magufuli kujitambulisha kwao.
   Mgombea Urais kwa chama cha Mapinduzi CCM,Dkt John Pombe Magufuli akiwaaga na kuwashukuru Wananchi wake kwa kumpa ridhaa ya kuwaongoza kwa miaka 20 akiwa Mbunge wao.
  Mgombea Urais kwa chama cha Mapinduzi CCM,Dkt John Pombe Magufuli akiwaaga na kuwashukuru Wananchi wake kwa kumpa ridhaa ya kuwaongoza kwa miaka 20 akiwa Mbunge wao.

  Mmoja wa Wafuasi wa chama cha Chadema Jumanne Majani akionekana kuwa na furaha ya kupitiliza mara baada kumuona Dkt Magufuli,katika kijiji cha Kibehe alipokuwa akielekea Mji Mdogo wa Muganza kuwasalimia na kuwashukuru wananchi wa mji huo
  Mmoja wa Wafuasi wa chama cha Chadema Jumanne Majani akionekana kuwa na furaha ya kupitiliza mara baada kupewa ruhusa ya kusalimiana na Dkt Magufuli,katika kijiji cha Kibehe alipokuwa akielekea Mji Mdogo wa Muganza kuwasalimia na kuwashukuru wananchi wa mji huo
 Mmoja wa Wafuasi wa chama cha Chadema Jumanne Majani akionekana kuwa na furaha ya kupitiliza mara baada kupewa ruhusa ya kusalimiana na Dkt Magufuli,katika kijiji cha Kibehe alipokuwa akielekea Mji Mdogo wa Muganza kuwasalimia na kuwashukuru wananchi wa mji huo
 Baadhi ya Wananchi wakiwa wameziba barabara wakitaka kumuona na kumsalimia Dkt Magufuli ikiwemo pia kumpongeza kwa kuteuliwa kuipeperusha bendera ya CCM katika kuwania Uraisi kupitia chama hicho
  Wafuasi wa CCM wakishangilia mara baada ya kumuona Dkt Magufuli alipokuwa akipita kuwasalimia wananchi akielekea Mji mdogo wa Muganza,wilayani Chato jioni ya leo
 Mmoja wa Wafuasi wa CCM akishangilia mara baada ya kumuona Dkt Magufuli alipokuwa akipita kuwasalimia wananchi akielekea Mji mdogo wa Muganza,wilayani Chato jioni ya leo

source : ccm blog/  ADAM MZEE

Wabunge marafiki wa Lowassa wajitosa tena kuwania ubunge.

Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.
Wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliokuwa wakimuunga mkono Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, katika harakati za kusaka urais, wamechukua fomu za kuomba kuteuliwa kuwania ubunge kupitia chama hicho.
 
Kabla ya hapo, kulikuwa na uvumi kuwa wabunge hao hawatachukua fomu kutokana na kukatwa kwa Lowassa katika kinyang’anyiro cha urais.
 
Baadhi ya wabunge hao ambao wamechukua fomu hizo na kuzirejesha jana ni pamoja na Kangi Lugola (Mwibara), Andrew Chenge (Bariadi Mashariki), Philipo Mulugo (Songwe).
 
TANGA
Mkoani Tanga, wabunge watatu waliokuwa wakimuunga mkono Lowassa nao wamechukua na kurudisha fomu za kuomba kutetea majimbo yao.
 
Wabunge hao ni Stephen Ngonyani maarufu kama Majimarefu ambaye ni Mbunge wa Korogwe Vijijini, Beatrice Shelukindo (Kilindi) na Henry Shekifu wa Lushoto.
 
NIPASHE imefuatilia mchakato wa uchukuaji na urudishaji fomu ndani ya CCM ambao ulihitimishwa jana saa 10:00 jioni na kubaini kuwa wabunge hao wameshachukua na kurudisha fomu za kutetea nafasi zao licha ya kuwapo kwenye ushindani mkali kutokana na idadi ya wagombea kuongezeka kwenye majimbo yao.
 
Katika majimbo yote 11 ya Mkoa wa Tanga, wabunge wote waliokuwapo katika awamu inayomalizika, wamejitosa tena na kuchukua fomu za kuwania nafasi hiyo.
 
Kwa sasa Mkoa wa Tanga una jumla ya majimbo 12 baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) kuongeza jimbo moja la Handeni Vijijini.
 
KILIMANJARO
Vigogo watano wa CCM mkoani Kilimanjaro wakiwamo Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Anne Kilango-Malecela na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Aggrey Mwanri, ni miongoni mwa mawaziri `waliokabwa koo' kwa kupata upinzani mkali ndani ya majimbo yao.
 
Wengine ni Waziri wa zamani wa Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi, Dk. Mathayo David Mathayo, ambaye anakabiliwa na upinzani mkali baada ya makada wenzake 13 kuchukua fomu za kuomba kuteuliwa kugombea kiti hicho katika Jimbo la Same Mashariki.
 
Waliojitosa kutaka kumng’oa Dk. Mathayo David ni John Chaggama, Daniel Mkemi, Alfred Ngelula, David Mawa, Amon Shahidi, Gerald William, Katery Daniel, Yusuph Singo, Michael Mrindoko, Ahadi Kakore, Jordan Mmbaga na Mwalimu John Singo.
 
Anne Kilango naye anakabiliwa na upinzani baada ya makada wanane akiwamo Dk. Michael Kadeghe, Dk. Eliji Kibacha, Semi Kiondo, Abraham Shakuri, Nyangasu Werema, Daudi Mambo na Ombeni Mfariji kujitosa kuwania kiti cha ubunge wa jimbo hilo.
 
Kigogo mwingine aliyepata upinzani, ni Naibu Waziri wa Tamisemi, Mwanri, ambaye jimboni kwake, wazee wa kimila wa jamii ya wafugaji wa Kimasai wamelazimika kumwangukia, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (Nec), Meijo Laizer, kujitoa katika orodha ya makada watatu waliotangaza kuchukua fomu za kuomba kuteuliwa kugombea kiti hicho.
 
Kwa upande wa Jimbo Moshi Mjini ambalo kwa muda mrefu limekuwa ngome ya Chadema, makada 12 wamejitokeza kuwania kiti hicho.
 
Makada hao ni Patrick Boisafi, David Mosha, Buni Ramole, Priscus Tarimo, Edmund Utaraka, Shaniel Ngindu, Innocent Siriwa, Amani Ngowi, Omari Mwariko, Michael Mwita, Daudi Mrindoko na Khalifa Kiwango.
 
Katika Jimbo la Moshi Vijijini, Waziri wa zamani wa Viwanda na Biashara, Dk. Cyril Chami, amekutana na kikwazo baada makada watano kujitokeza kutaka kuteuliwa kugombea kiti hicho, huku Jimbo la Vunjo likiwa na watia nia wanane ambao wanakabana koo kutaka kuteuliwa kugombea kiti hicho.
 
DODOMA
Waziri wa Nishati na Madini ambaye ni Mbunge anayemaliza muda wake Jimbo la Kibakwe, George Simbachawene, Livingstone Lusinde (Mtera), Gregory Teu (Mpwapwa), Omari Badwel (Bahi) na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Job Ndugai (Kongwa), ni miongoni mwa makada waliochukua fomu kutetea nafasi zao.
 
BAHI: 
Mbunge wa sasa Badwel atapambana na Pascal Mwaja, Levison Chilewa, Donald Mejitii, Hebron Kipiko, Anthony Lyamunda, Salum Kanyika na Kondo Chaurembo.
 
MPWAPWA:
Mbunge wa sasa Teu, amepata wapinzani ambao ni George Lubeleje, June Fusi, Nyange Mtoro, Charles Kuziganika, Rehema Halahala, Emmanuel Mbeho na Gabriel Hango.
 
KIBAKWE:
Simbachawene atapambana na Amani Bendera, Gabriel Mwikola, Sabas Chambas, Shahel Gayesh, Aclay Mnyang’ali na Solomoni Ngiliule.
 
KONGWA:
Ndugui amepata wapinzani wake ambao ni Samwel Chimanyni, Dk. Elieza Chilongani, Epafra Mtango, Pascal Mahinyila, Hussein Madeni, Simon Katunga na Joseph Palingo.
 
MTERA:
Lusinde atapambana na Richard Masimba, Samwel Malecela, Essan Mzuri, Lameck Lubote na Dk. Michael Msendekwa.
 
CHILONWA:
Waliojitokeza kutaka kuwania jimbo hilo ni Peter Nasoni Mlugu (Mwalimu wa Shule ya Msingi Chilonwa), Kusakula Amosi (mfanyabiashara jijini Dar es Salaam), Chibutii Masagasi, Charles Ulang, (Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Chamwino) na Vincent Chomol.Wenslous Mazanda (Mwalimu wa Shule ya sekondari Mpunguzi), Joel Mwaka  (Mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi, Wilaya ya Chamwino), Daniel Robina Logoha, Palolet  K. Mgema (Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea), Deo Ndejembi, Godrick Ngoli, Anderson Kusenha Magolola na Kk. David Mapana.
 
KYELA
WANACHAMA 10 wamejitokeza kuchukua fomu ya kuwania ubunge Jimbo la Kyela mkoani Mbeya kupambana na Mbunge wa sasa, Dk. Harrison Mwakyembe.
 
Dk.Mwakyembe ambaye ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki alichukuliwa fomu na baadhi ya wananchi ambao walijichangisha fedha na kumkabidhi jana mjini Kyela ambaye alizirudisha Makao Makuu ya CCM Kyela.
 
Wengine waliochukua fomu na kurejesha katika jimbo hilo ni Gabriel Kipija, ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela, John Mwaipopo, Profesa Leonard Mwaikambo, Gwakisa Mwandembwa, Vincent Mwamakingula, George Mwakalinga, Benjamin Richard, Asajile Mwambambale na Ackim Jackison.
 
MBEYA VIJIJINI
Waliochukua fomu Jimbo la Mbeya Vijijini ni Mbunge wa sasa, Luckison Mwanjale, Oran Njera, Godon Kalulunga (Mwandishi wa Habari),Japhet Mwanasenga, Anderson Kabenga, Walimu Sikwembe, Kassim Chakachaka.
 
ILEJE 
Aliko Kibona (Mbunge wa sasa) na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Janneth Mbene.
 
MBEYA MJINI
Nwaka Mwakisu, Aman Kajuna, Charles Mwakipesile
 
VWAWA
Mchungaji Tito Nduka, Japhet Hasunga na Mtella Mwampamba.
 
MASWA MAGHARIBI
Waliochukua fomu ni Michael Bukwimba, Mashimba Ndaki, Benjamin Rungu, Aaron Mbojo (Mjumbe wa Nec) na Henry Mbichi.
 
MASWA MASHARIKI
Waliojitokeza kuwania ubunge Jimbo la Maswi Mashariki ni George Nangale (Mbunge wa Afrika Mashariki), Peter Bunyongole (Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Maswi), George Lugomela, Ali Ntegwa, Stanslaus Nyongo na Jonathan Mnyela.
 
Imeandikwa na Thobias Mwanakatwe, Emmanuel Lengwa, Lulu George, Godfrey Mushi, Editha Majura, Jacqueline Massano, Ibrahim Joseph na Peter Mkwavila, Dodoma.
CHANZO: NIPASHE

Friday, July 17, 2015

Magufuli apata mapokezi ya kishindo Zanzibar


Mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dk John Mgufuli na mgombea mwenza, Samia Suluhu Hassan wakiwapungia mikono wananchi walipokuwa wakitoka Uwanja wa Ndege wa Zanzibar kwenda Ofisi Kuu ya CCM, Kisiwandui Mjini Zanzibar kwa ajili ya utambulisho jana. Picha na Bashir Nkoromo 
Zanzibar. Mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli jana alipata mapokezi ya kishindo alipokwenda Zanzibar kujitambulisha baada ya kuteuliwa na chama hicho wiki iliyopita.
Akizungumza na wafuasi wa chama hicho katika ofisi ya CCM, Kisiwandui, Dk Magufuli alirejea kauli yake kuwa hivi sasa CCM ipo imara na wagombea wote walioshiriki katika mchakato wa kutafuta mgombea wamevunja kambi zao na kutangaza kumuunga mkono.
Dk Magufuli ambaye alifuatana na mgombea wake mwenza, Samia Suluhu Hassan alisema lengo la CCM ni kushinda katika uchaguzi huku kaulimbiu yao ikiwa ni umoja ni ushindi.
“Sisi tulijitokeza wengi katika kinyang’anyiro hiki lakini kwenye wengi wanachaguliwa wachache, mwisho anateuliwa mmoja lakini mimi nimezungumza na wagombea wenzangu ambao wote wamenikubalia kwamba wataniunga mkono katika safari yetu hii na nina imani kubwa ya kushinda urais wa Muungano kwa kuwa umoja ni ushindi,” alisema.
Akitoa ahadi mbele ya wana CCM, Dk Magufuli alisema akichaguliwa kuwa rais atahakikisha kwamba anaulinda Muungano kwa kufanya kazi na mgombea urais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein ambaye alimsifu kwa umakini wake na ujasiri wake katika uongozi.
“Ndugu wanachama wa CCM, mimi nimefanya kazi kwa karibu sana na Dk Shein katika Baraza la Mawaziri, ni kiongozi hodari, shupavu asiye na maringo na tabia yake ya ucheshi kwa kila mtu inawafurahisha wengi,” alisema Dk Magufuli ambaye pia ni Waziri wa Ujenzi.
Alisema moja ya kazi kubwa atakazozifanya ni kuulinda Muungano kama kitambulisho na kielelezo ya wananchi wa Tanzania Bara na Zanzibar lakini pia atahakikisha Mapinduzi ya Zanzibar yanalindwa na kuheshimiwa.
Mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Zanzibar, Dk Magufuli pamoja na msafara wake walisafiri kwa gari la wazi huku wakishangiliwa na wafuasi wa CCM hadi Kisiwandui.
Katika mkutano huo, Dk Shein alisema utekelezaji wa Ilani ya CCM ndiyo pigo kwa wapinzani.
source: mwananchi

Wednesday, July 15, 2015

Haya ndio mapokezi ya Dk. John Magufuli ndani ya Dar es Salaam July 14 2015…

Screen Shot 2015-07-14 at 4.35.50 PM
Jina la Waziri Wa Ujenzi Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli lilipata Headlines zenye uzito zaidi baada ya Chama Cha Mapinduzi CCM kumtangaza kwamba ndiye Mgombea Urais aliyepitishwa na Chama hicho kwenye Uchaguzi unaofanyika October 2015.
Screen Shot 2015-07-14 at 4.35.26 PM
Yeye pamoja na Mgombea mwenza, Samia Suluhu Hassantayari wamefika Dar es Salaam na leo July 14 2015 ilikuwa siku rasmi ambayo ilitangazwa kwa ajili ya kuwatambulisha Wagombea hao.
Watu wa Dar es Salaam wamejitokeza katika Viwanja vya Zakhiem Mbagala kwa ajili ya kufanya mapokezi hayo.. Pichaz za tukio lote ninazo hapa.
Screen Shot 2015-07-14 at 4.35.17 PM
Screen Shot 2015-07-14 at 4.35.33 PM
Dk. John Magufuli akiongea katika Viwanja vya Zakhiem Mbagala, Dar es Salaam.
Screen Shot 2015-07-14 at 4.35.40 PM
Screen Shot 2015-07-14 at 4.35.57 PM
Screen Shot 2015-07-14 at 4.36.04 PM
Dk. John Magufuli.
Screen Shot 2015-07-14 at 4.36.11 PM
Screen Shot 2015-07-14 at 4.36.20 PM
Waziri Magufuli akionesha uwezo wake kwenye kupiga ngoma. Pembeni yake yuko Katibu Mwenezi wa Itikadi CCM, Nape Nnauye.
Screen Shot 2015-07-14 at 4.36.30 PM
Screen Shot 2015-07-14 at 4.37.11 PM
Katibu Mwenezi Nape Nnauye.
Screen Shot 2015-07-14 at 4.37.21 PM
Mkuu wa Mkoa Dar Es Salaam, Said Meck Sadick.
Screen Shot 2015-07-14 at 4.37.29 PM
Screen Shot 2015-07-14 at 4.37.37 PM
Screen Shot 2015-07-14 at 4.37.44 PM
 chanzo: Milladayo.com