WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Saturday, December 13, 2014

SIMBA SC YAICHAPA YANGA 2-0 MTANI JEMBE



Mshambuliaji wa Simba SC, Emmanuel Okwi akiwatoka mabeki wa Yanga SC, Kevin Yondan aliyelala chini na Juma Abdul 
Na BIN ZUBERY
SIMBA SC imeendeleza ubabe wake kwa mahasimu wao, Yanga SC katika mechi za Nani Mtani Jembe, baada ya jioni hii kuichapa mabao 2-0 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Desemba mwaka jana, Simba iliichapa Yanga SC mabao 3-1 katika mechi ya Mtani Jembe, inayoandaliwa na wadhamini wa timu hizo, Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia ya Kilimanjaro.
 
Katika mchezo wa leo, hadi mapumziko, Simba SC ilikuwa tayari inaongoza kwa mabao hayo mawili, yaliyotiwa kimiani na kiungo Awadh Juma na mshambuliaji Elias Maguri.
Awadh Juma alifunga bao la kwanza baada ya kuanzishiwa mpira wa adhabu uliopigwa na Emmanuel Okwi dakika ya 30, umbali wa mita 23.
Elias Maguri aliifungia Simba SC bao la pili dakika ya 42 akimalizia mpira uliorudi baada ya kugonga mwamba kufuatia shuti la Mganda, Simon Sserunkuma.
 
Kiungo wa Yanga SC, Mnyarwanda Mbuyu Twite aliumia dakika ya 39 na kutoka nje, nafasi yake ikichukuliwa na Hassan Dilunga. Mshambuliaji mpya Yanga SC, Mliberia Kpah Sherman alionyesha ni machachari, lakini hakupata ushirikiano mzuri pale mbele.
Refa Jonesia Rukyaa kutoka Bukoba mkoani Kagera, pamoja na kwamba ni mwanamke, lakini alijitahidi kuumudu mchezo huo kadiri ya uwezo wake. 
Mashabiki wa Yanga SC walianza kuondoka uwanjani mapema tu baada ya bao pili, huku wengine wakivamia chumba cha kubadilishia nguo wachezaji.
Kipindi cha pili, kocha wa Simba SC, Mzambia Patrick Phiri alianza na mabadiliko, akimuingiza Nahodha Joseph Owino kwenda kuchukua nafasi ya Juuko Murushid, wakati kocha Mbrazil wa Yanga SC, alimuingiza Salum Telela kwenda kuchukua nafasi ya Emerson na Danny Mrwanda kumrithi Andrey Coutinho.
Kikosi cha Simba SC kilikuwa; Ivo Mapunda, Nassor Masoud ‘Chollo’, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’/Issa Rashid ‘Baba Ubaya’ dk66, Hassan Isihaka, Juuko Murushid/Joseph Owino dk47, Jonas Mkude, Ramadhani Singano ‘Messi’/Said Ndemla dk74, Awadh Juma, Elias Maguri/Dan Sserunkuma dk84, Simon Sserunkuma/Shaaban Kisiga ‘Malone’ dk84 na Emmanuel Okwi.

Yanga SC; Deogratius Munishi ‘Dida’, Juma Abdul/Hussein Javu dk79, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Mbuyu Twite/Hassan Dilunga dk39, Emerson Roque/Salum Telela dk55, Haruna Niyonzima, Kpah Sherman/Mrisho Ngassa dk63, Simon Msuva na Andrey Coutinho/Danny Mrwanda dk46.
13 Dec 2014 

source: matukio na vijana