WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, June 30, 2014

EVANS AVEVA RAIS SIMBA

10
Matokeo yametangaza na Evance Aveva amechaguliwa kuwa rais mpya wa klabu ya Simba ya jijini Dar es salaam huku Makamu wa rais akichaguliwa Bw. Godfrey Nyange Kaburu matokeo ya uchaguzi huo yametangazwa leo alfajiri naidadi kamili ya kura walizopata tutawapatia baada ya muda, Kwa upande wa kamati ya utendaji waliochaguliwa ni Idd Kajuna, Coliins Friesh,Ally Suru na Saild Tully kwa upande wa mwanamke ni Jasmin.(A.I).

source: mjengwa blog

Sunday, June 29, 2014

RISALA YA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI

IMG_3462

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein akitoa salamu za Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kwa   Wananchi  wa Zanzibar na Tanzania kwa Ujumla,pia aliwatakia mfungo mwema  wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kwa kufanya ibada mbali mbali.[Picha na Ramadhan Othman Ikulu.].(A.I)

UKADIRIFU, MUNGUPAMOJANASI NA KAMAERA YA MAISHA NA VITUKO VYAKE BLOGS KWA PAMOJA ZINAWATAKIA WAUMINI WA KIISALAM MFUNGU MWEMA ULIOJAA AMANI UPENDO WAKATI WA KUTEKELEZA NGUZO HII MUHIMU.

RAMADHANI NJEMA;

Karibu tena Maximo kama unaijua Yanga

Maoni ya katuni

Kocha wa zamani wa timu ya taifa, Taifa Stars, Marcio Maximo ambaye aliigawa nchi katika siku zake za mwishoni madarakani baadhi wakimuona kikwazo cha maendeleo na wengine wakidhani ndiye muarubaini wa kudumaa kwa soka letu, aliwasili nchini juzi kuwafundisha mabingwa mara 23 wa Bara timu ya Yanga.

Baada ya kuiwezesha Taifa Stars kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za nyumbani, CHAN, 2009 lakini timu ikakosa chupuchupu kwenda fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, CHAN, za Ghana ilikuwa ni lazima pawe na kambi mbili zenye mawazo tofauti kuhusu Maximo.

Lakini ambalo halikuwa na ubishi, kimsingi, Maximo ni kocha mzuri miongoni mwa wana taaluma hiyo ikiwa nia ya mafanikio ya haraka itawekwa pembeni.

Kwa sababu Maximo ni kocha mzuri miongoni mwa wana taaluma hiyo ndiyo maana, basi, haikushangaza kuona Yanga ikikamilisha jitihada za muda mrefu za kumrudisha nchini Mbrazili huyo ambaye aliondoka baada ya mkataba wake na shirikisho la soka, TFF, kutoongezwa.

Ni kuondoka kwa Maximo huko, baada ya mkataba wake kutoongezwa, ndiko ambako kumetusukuma leo, Nipashe, kuwa na wasiwasi na hatma ya taswira ya heshima aliyoacha mwalimu huyo nchini sasa anapokwenda kuwa muajiriwa wa Yanga.

Ni siri iliyo wazi kwamba Yanga haijapata kuachana na mwalimu bila migogoro ya kifedha, hata pale ambapo makocha hao waliiwezesha kupata mafanikio barani Afrika achilia mbali kwenye ligi kuu ya Bara.

Lakini ni siri iliyo wazi pia kwamba Yanga haijapata kuheshimu taaluma ya ukocha, na hasa walimu wenye wepesi wa kutetea falsafa zao ndani ya klabu hiyo.

Tumesema, Nipashe, kwamba ambalo halina ubishi, kimsingi, Maximo ni kocha mzuri miongoni mwa wana taaluma hiyo ikiwa nia ya mafanikio ya haraka itawekwa pembeni. Kwa nini?

Kwa wanaokumbuka utawala wake Taifa Stars, wanajua kuwa ni mwalimu ambaye anaamini mno katika ukuzaji wa vipaji vya chipukizi ambao wapo ndani ya mipaka ya mfumo wa eneo la soka analoliongoza.

Wengi wa wachezaji walioko Botswana ambao nchi inajivuania sasa wakati Stars ikijaribu kwenda kule ambako Maximo alishindwa kutupeleka kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1980, ama waliibuliwa na kocha huyo ama walikuwa kwenye mipango yake 2009 kabla ya TFF kumgeukia Jan Poulsen na kisha Kim mwenye ubini kama huo pia.

Na wanaokumbuka utawala wake Taifa Stars, pia, wanajua kuwa ni mwalimu ambaye anaamini mno katika nidhamu ndani na nje ya uwanja kiasi kwamba yupo radhi kutofautiana hata na nusu ya taifa kama ilivyokuwa katika migogoro na Juma Kaseja, Haruna Moshi na Athumani Iddi kuliko kupindisha maadili.

Tuachane na yale yaliyo katika uwezekano wa kugongana na falsafa yake Yanga, kama kupangiwa wachezaji wa kucheza na baadhi ya viongozi ama kuingiliwa katika masuala ya udhibiti wa nidhamu dhidi ya wachezaji mastaa wenye kuchelewa kambi za mazoezi ama vipindi vya mazoezi hayo.

Je, Maximo anafahamu kwamba hakuna mwalimu, wakiwemo marehemu Tambwe Leya na marehemu Tito Mwaluvanda, ambaye hakuacha deni katika klabu hiyo ambayo haina subira linapouja suala la ubingwa wa Bara?

Kama Maximo anayajua yote hayo, ikiwemo ukweli kuwa Mbelgiji Tom Seintfeit alifukuzwa baada ya mechi tatu za kwanza za msimu na kwamba wazungu wengine si chini ya wawili wameishitaki FIFA, shirikisho la dunia, wakililia mafao yao, basi tunamkaribisha Yanga Nipashe.  

CHANZO: NIPASHE

Saturday, June 28, 2014

SIMBA SC YAWAALIKA WANACHAMA, WANAHABARI KUONA MAENDELEO YA UWANJA BUNJU

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

AZAM FC pekee ndio klabu ya Tanzania yenye uwanja wake wa kisasa kwa ajili ya mazoezi, mechi za ligi kuu na michuano yote inayosimamiwa na shirikisho la soka barani Afrika, CAF.
Katika historia ya soka la Tanzania, Azam fc haiwezi kunusa ukongwe wa klabu mbili za Simba na Yanga.
Hizi ni klabu zenye mafanikio ndani na nje ya uwanja. Ni klabu zenye mashabiki kila kona ya nchi hii.

Lakini licha ya kukaa miaka mingi katika soka la ushindani nchini Tanzania na michuano ya Kimataifa, Yanga na Simba hazijawahi kumiliki viwanja vyake vya mazoezi na mechi za ligi kuu.
Kwa miaka mingi sasa viongozi wanaopita katika klabu hizo wanakuja na ndoto za kujenga viwanja, lakini zinayeyuka kutokana sababu mbalimbali ikiwemo kuendekeza siasa kuliko vitendo.

Kwasasa mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji ana mkakati kabambe wa kujenga uwanja wa klabu hiyo maeneo ya Jangwani, wakati huo huo, naye mwenyekiti wa Simba, Alhaj Ismail Rage akipambana na mpango kama huo maeneo ya Bunju jijini Dar es salaam.

Kwa miezi miwili sasa, Uongozi wa Simba unaendelea na ujenzi wa uwanjao wake na sasa umefikia hatua nzuri ya kuanza kutumika kwenye mazoezi ya klabu hiyo ikiwa ni mara ya kwanza kumiliki uwanja katika historia yake.

Kutokana na maendeleo hayo,uongozi wa Simba umewakaribisha wapenzi na wanachama wake kesho  Jumamosi katika Uwanja wao Bunju kwa ajili ya kuangalia maendeleo ya ujenzi wa uwanja wa mazoezi wa klabu.

Katibu mkuu wa Simba sc, Ezekiel Kamwaga amesema ujenzi huo ulioanza miezi miwili iliyopita, unakaribia kukamilika na utakuwa uwanja wa kwanza rasmi wa mazoezi wa klabu katika historia yake.
Vyombo vya habari navyo vinaalikwa katika tukio hilo litakaloanza saa tano kamili asubuhi.

source: matukiotz.com

MAXIMO, MAXIMO, MAXIMO

MAXIMO AAHIDI MAKUBWA YANGA SC, ASEMA TIMU ITATISHA HADI AFRIKA KAMA MAZEMBE, KUANZISHA PIA NA ‘AKADEMI’ JANGWANI

KOCHA mpya wa Yanga SC, Mbrazi Marcio Maximo Barcellos, amesema timu hiyo itatisha katika Ligi Kuu ya Bara na michuano ya Afrika chini yake.

Kocha huyo wa zamani wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars aliyezaliwa Aprili 29, mwaka 1962, amesaini mkataba wa miaka miwili kwa ajili ya kuifundisha timu hiyo akirithi mikoba ya Mholanzi Hans van der Pluijm.

Yanga itatisha: Kocha Mbrazil, Marcio Maximo akizungumza na Waandishi wa Habari mchana wa leo Dar es Salaam

WASIFU WA MAXIMO:

JINA: Márcio Máximo Barcellos
KUZALIWA: 29 April 1962 (age 52)
ALIKOZALIWA: Rio de Janeiro (RJ) Brazil
TIMU ALIZOFUNDISHA:
Klabu ya sasa: Yanga SC
Timu  Mwaka
1992-1993 Brazil U20
1992-1993 Brazil U17
1992 Mesquita
1994 Barra da Tijuca FC
1994 Qatar U20
1995 Al-Ahli
2002 Cayman Islands
2003 Livingston
2006-2010 Tanzania
2012 Democrata-GV
2013 Francana
Tangu Juni 27, 2014;  Yanga SC

Mbrazil akizungumza na Waandishi wa Habari mchana wa leo mjini Dar es Salaam, amesema pamoja na changamoto ambazo anatarajia kuzipata kutoka timu pinzani wa Yanga, kama  Azam FC, Simba na Mbeya City, lakini atahakikisha  anajenga msingi  bora ya soka  itakayowezesha kutimiza majukumu yake vizuri.
Amesema anataka kuona timu inashinda mechi zake za  ndani ya nchi na nje, kwani anaamini Yanga ni klabu kubwa barani Afrika.
“Nataka kuibadilisha soka ya Yanga ili liweze kufikia katika kiwango wa kimataifa na hili linawezekana, kwani nani alikuwa anaijua TP Mazembe ya DRC, lakini kwa kuwa iliandaliwa na kufanyika uwekezaji sasa ni klabu kubwa Afrika” amesema Maximo.
Maximo amesema, atahakikisha anajenga soka ya vijana kwa kuwa  ni msingi  wa soka inapoanzia ambapo atakuwa na timu zenye umri tofauti.
Amesema, kikubwa anatarajia kuona jitihadi za wachezaji wa timu hiyo ndani ya uwanja, kwani kitu muhimu kwake  ni ushindi.
Maximo, pia atakuwa ni Mkurugenzi wa ufundi wa timu hiyo, akisaidiwa na Mbrazil mwenzake Leornado Neiva ambaye atafundisha timu ya vijana waliochini ya umri wa  miaka 20, aliyesaini mkataba wa miaka miwili juzi.
Neiva pamoja na kuwa na kocha wa vijana atamsaidia Maximo katika majukumu yake katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo.
Maximo akiwa kocha mkuu  wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ aliyeifundisha kuanzia mwaka 2006-2010, aliwahi kumleta wasaidizi wake kutoka Brazili, ambao ni Markus  Tinoco, ambaye alikuwa kocha wa timu ya vijana waliochini ya miaka 20.
Maximo na Msaidizi wake, Leonardo Neiva Martins kulia
Lakini  Yanga wanatarajia  kumwajiri kocha mwingine mzawa na kuwa wanne akiwemo kocha wa makipa, Juma Pondamali kwa lengo la kuleta ufanisi zaidi.
Katika hatua nyingine, Maximo alisema anatarajia kuanza programu ya mazoezi Jumatatu ijayo kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu Bara.
Maximo aliyezaliwa mjini Rio de Janeiro, alikuwepo kwenye mabenchi ya Ufundi ya timu za taifa za vijana za Brazil chini ya umri wa miaka 17 na 20 kuanzia mwaka 1992 hadi 1993. 
Vikosi hivyo ndani yake vilikuwa vina wachezaji walioibuka nyota wakubwa Brazil baadaye kama Ronaldo Lima na Ronaldinho Gaucho, ambaye wote sasa wamestaafu baada ya kuwika hadi kuwa Wanasoka Bora wa Dunia. 
Kabla ya hapo, mwaka 1992 alifundisha Mesquita, 1994 Barra da Tijuca FC za kwao Brazil, 1994 akainoa U20 ya Qatar na mwaka 1995 akafundisha  Al-Ahliya huko.
Alifanya kazi pia kama Mkurugenzi wa Ufundi wa viswia vya Grand Cayman kwa miaka mitatu ambako alikataa ofa ya kuongeza mkataba kwa miaka 10 ili akajiunge na Livingston FC ya Scotland Juni 5 mwaka 2003, alikosaini Mkataba wa mwaka mmoja na kuwa kocha wa kwanza Mbrazil kufundisha timu ya Uingereza. 
Pamoja na hayo, mambo hayakumuendea vizuri huko, baada ya mechi tisa akiambulia ushindi wa mechi tatu, sare tatu na vipigo vitatu, akajiuzulu Oktoba 14.
Juni 29 mwaka 2006, Maximo akasaini Mkataba wa kuifundisha Taifa Stars ambayo mwaka 2009, aliiwezesha kufuzu kucheza fainali za kwanza za CHAN nchini Ivory Coast.
Maximo alijiuzulu kuifundisha Taifa Stars mwaka 2010, akiwaacha Watanzania bado wanampenda- akaenda Democrata ya nyumbani kwao, Brazil. 
Alifukuzwa katika timu hiyo Februari 13 mwaka 2012 na Juni mwaka huo huo alikaribia kujiunga na Yanga SC kurithi mikoba ya Mserbia, Kosta Papic, lakini wakashindwana dau na klabu hiyo ikamchukua Mbelgiji, Tom Saintfiet.
Novemba 2012, akajiunga na Francana ya kwao Brazil ambako ndipo anatokea sasa kuja Yanga SC baada ya kumaliza Mkataba wake.

source: matukiotz.com

Friday, June 20, 2014

MTEI ALEZEA KIZUNGUMKUTI CHA HISA ZA WANZANZIBARI KATIKA EAC-BANK ILIYOVUNJIKA.


Edwin Mtei Kuzaliwa:  Mwaka 1932, Marangu Mkoani Kilimanjaro Kazi: Gavana wa Kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) •Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki •Waziri wa Fedha chini ya uongozi wa Mwalimu Nyerere  Elimu: Shahada ya Sanaa (Sayansi ya Siasa na Historia na Jiografia) Siasa: Mwanzilishi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) 

Arusha. Kero za Muungano zimetokea kuwa msamiati maarufu katika siku za karibuni nchini, hasa pale ulipoanza mchakato wa kupatikana kwa Katiba mpya.
Wengi wamekuwa wakieleza kuwa kero zipo lukuki katika Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambao umetimiza miaka 50 sasa.
Kero hizo zimetumika kama kete ya kutetea muundo unaofaa wa Muungano ingawa mjadala sasa umehamia kwenye  serikali mbili au tatu.
Hata hivyo, katika kero hizo, zipo ambazo zimeanza kupatiwa ufumbuzi na zipo ambazo zimeibuka upya tena kwa kasi.
Miongoni mwa kero ambazo ni ngeni kwa wengi, ni kutokujulikana zilipopelekwa fedha za Zanzibar zilizokuwa katika Bodi ya Sarafu ya Afrika  Mashariki  (EACB) iliyonjika mwaka 1965.
Kero hiyo, ilikuwa ikizungumzwa chini chini na baadhi ya viongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) na hata wanasiasa wa pande zote mbili za Muungano.
Kutokana na watu wengi kuhoji, fedha hizo, wakati wa uzinduzi wa Bunge Maalumu la Katiba  mjini Dodoma, Rais Jakaya Kikwete naye alizungumzia kero hiyo na kuahidi kuwa itafanyiwa kazi.
Hata hivyo, ili kupata maelezo ya kina juu ya kero hii, gazeti hili linazungumza na Gavana wa kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Edwin Mtei, ambaye pia aliyekuwa Waziri wa Fedha kati ya mwaka 1978 hadi 1981.
Mtei, ambaye pia aliwahi kuwa katibu mkuu wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC) na ameshika nafasi mbalimbali katika jumuiya hiyo kabla ya kuvunjika, anaeleza historia ya akiba hiyo ya Zanzibar na wapi ilipo.
Anasema ni kweli kuwa baada ya kuvunjika kwa EACB mwaka 1965, Zanzibar ilikuwa na akiba ya fedha zake katika bodi hiyo.
Anasema Zanzibar ilikuwa na kiasi cha fedha kama asilimia 4, huku Kenya, Uganda na Tanzania (Bara) zikiwa na kiasi kikubwa cha fedha.
Je, zipo wapi fedha za Zanzibar?
Mwanasiasa huyo anasema fedha hizo  baada ya kuvunjika kwa bodi hiyo, fedha hazipo tena na anashangazwa na watu wanaoibuka leo na kudai sasa kana kwamba bado zipo BoT.
Anasema anakumbuka wakati huo, mara baada ya kuvunjika kwa bodi hiyo, ulifanyika mgawanyo wa fedha katika hazina za nchi hizo kuanzisha benki kuu.
Anasema fedha za Tanzania Bara zilifanya kazi mbalimbali  na zile za   Zanzibar  ziliingizwa katika kazi ya kuanzishwa kwa tawi la BoT Zanzibar kwani wakati huo kulikuwa na tawi moja  lililokuwa Dar es Salaam.
“Nakumbuka fedha za Zanzibar tulitumia katika ujenzi wa BoT, tawi la Zanzibar, ujenzi ambao ulikuwa na gharama kubwa ukihusisha kujengwa kwa eneo maalumu la  kuhifadhi fedha hizo,” anasema Mtei.
Anaongeza kuwa kabla ya hapo, Zanzibar ilikuwa haina tawi la Benki Kuu hivyo, fedha hizo ndizo zilitumika kuanzishwa tawi la kwanza.
“Ni kweli kulikuwa na malalamiko ya Zanzibar baada ya bodi  kuvunjika, lakini hatukuzitumia fedha hizi kwa mambo mengine, ila tulifungua tawi la Benki Kuu Zanzibar,” anasema.
Anaeleza kuwa anachokumbuka ni kuwa fedha za Zanzibar zilikuwa asilimia nne katika jumuiya hiyo na kwa jumla Tanzania ilikuwa na asilimia 35 katika bodi hiyo.
“Kuanzisha  BoT Zanzibar  haikuwa kazi ndogo kwani ilibidi tutafute majumba strong (imara). Tujenge mahali pa kuhifadhi fedha na ujenzi ni gharama hasa  strong room (chumba maalumu cha kuhifadhi fedha), ” anasema Mtei.
Anaongeza kuwa kwa kumbukumbu zangu, wakati huo, kwenye vikao vya uamuzi huo, Zanzibar ilikuwa inaongozwa na Katibu wa Wizara ya  Fedha aliyemtaja kwa jina moja la Sheha.
“Sheha ndiye aliyekuwa anahudhuria vikao, alikuwa akija na kukutana nami tunajadili,” anasema.
 Serikali moja  EAC
Akizungumzia mvutano wa kisiasa kwa sasa, kutokana na mapendekezo ya rasimu ya Katiba mpya, anasema ni vyema maoni ya wengi yafuatwe na kuheshimiwa.
Hata hivyo, anasema  baada ya  Muungano kudumu kwa miaka 50, angetaka ndoto iwe ni kuwa na nchi moja katika ukanda wa Afrika ya Mashariki.
“Mimi  kama mchumi nataka nchi kubwa moja. Tuache kuzungumzia mambo ya kutugawanya, inawezekana kuna nchi ndogondogo lakini lazima ziunganishwe na kuwa moja kubwa kupitia Shirikisho la Afrika ya Mashariki,” anasema.
“Nchi hii ni moja ambayo nadhani tuanze kuifikiria sasa iwe na Tanganyika, Zanzibar, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na hata  Zambia na  Malawi
“Mimi nimejifunza katika political science (sayansi ya siasa) kuwa nchi inapokuwa moja kubwa, basi uchumi wake unastawi na watu wanapata maendeleo ya kiuchumi kuliko kuwa nchi ndogo,” anasema.
Anaongeza, hata hivyo, kuwa ni vyema kujiuliza ni kwa nini miaka 50 ya Muungano sasa, bado Watanzania wengi ni maskini?
“Lazima, tufikirie mbele zaidi, kwenye vikao vya umoja wa mataifa, zinapozungumza nchi kubwa, utaona kabisa kila mjumbe anakuwa makini na hata kama yupo nje anarudi kusikiliza, lakini kama ni nchi ndogo wajumbe wanatoka kuvuta sigara nje ya ukumbi.”
 Anaongeza kuwa Watanzania na wakazi wa ukanda wa Afrika ya Mashariki wanapaswa kufikiria kuwa na nchi moja kubwa kama Marekani, Ujerumani  au Brazil kama kweli wanataka kukuza uchumi wao.
Muungano ni maridhiano.
Akizungumza muundo wa Muungano, Mtei  anasema ni muhimu kuwapo kwa Muungano ambao unaridhiwa na nchi zote wanachama.
Anasema Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni lazima uendelezwe na kulindwa, lakini, kwa kuzingatia masilahi na maridhiano ya kila upande.
“Tuwapinge wote ambao wanataka kuvunja Muungano, pia tuondoe kero zote zilizopo kwani Muungano ni makubaliano ya watu wote kwa masilahi yao,” anasema.
Mtei ambaye ni muumini wa Kilutheri ana historia ndefu ya maisha ambayo yanafurahisha. Ni mtu ambaye alilelewa na mama yake mzazi na kukulia katika maisha ya umaskini, akichunga mbuzi baada ya kutoka shule ya Ngaruma iliyokuwa ikimilikiwa na Kanisa la Kiinjili la  Kilutheri Tanzania. Baadaye alikwenda  Old Moshi, Tabora, kisha Chuo Kikuu Makerere, Uganda.
source: mwananchi

MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI DEBORAH JOHN SAID AMEFARIKI DUNIA


Taarifa zilizotufikia katika Chumba cha Habari muda huu zinasema kwamba , Muimbaji wa Nyimbo za Injili Deborah John Said Amefariki Dunia katika Hospitali ya Muhimbili. Endelea kufuatilia hapa kwa taarifa zaidi. Tunatoa pole kwa wote waliopatwa na Msiba huu Mkubwa.

Amen

source: matukiotz.com

Halima Mdee (CHADEMA), Amemtaka Mbunge Mwenzake, Leticia Nyerere, Aache Ubunge na Akajiunge na CCM.

MBUNGE wa Kawe, Halima Mdee (CHADEMA), amemtaka mbunge mwenzake, Leticia Nyerere, aache ubunge na akajiunge na Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuliko kuendelea kukipigia debe chama hicho akiwa upinzani.
Kauli hiyo ameitoa jana alipokuwa akichangia bajeti ya serikali kwa mwaka 2014/2015 ambapo alisema matendo anayofanya Leticia ya kujipendekeza kwa CCM yatamgharimu kama ilivyotokea kwa wenzake.
Juzi wakati akichangia bajeti hiyo, Leticia alisema serikali ikifanya vizuri, lazima ipongezwe kwakuwa imepeleka maendeleo katika jimbo analotoka.
“Serikali yangu imefanya mambo mengi, imeniletea maji, walimu katika jimbo langu la Kwimba, ni lazima tuipongeze si kila wakati tunailaumu humu ndani,” alisema.
Katika mchango wake jana, Mdee, alisema jukumu kubwa la upinzani ni kuikosoa serikali na kuonyesha mbadala katika masuala mbalimbali na si kuisifia kwa kutekeleza wajibu wake wa kuwahudumia wananchi.
“Serikali inapata fedha kutokana na kodi za wananchi, inalazimika kupeleka maji, barabara na huduma mbalimbali kwa lazima si hiyari, tunapoikosoa tunatimiza wajibu wetu kama yenyewe inavyotekeleza inapowahudumia wananchi.
“Leticia Nyerere anaweza kwenda CCM, kwakuwa Rais Kikwete ana nafasi mbili za uteuzi wa wabunge, lakini lazima ajue waliojipendekeza CCM wamepigika sana hivi sasa, aachie ubunge aende huko kwakuwa ana mapenzi nao,” alisema.
Mdee alisema kuwa Leticia anaiaibisha kambi ya upinzani inayofanya kazi usiku na mchana kuhakikisha serikali inaboresha huduma inazozitoa kwa wananchi.
“Upinzani si lelemama, kama anafikiria CCM ni kuzuri zaidi ni vema akaenda huko kuliko kubakia hapa pasipomfaa,” alisema.

source: matukiotz.com

Tuesday, June 17, 2014

PICHA ZAIDI ZA MASHAMBULIZI MAPYA KENYA....WATU 48 WAUWAWA..AL-SHABAAB WAHUSISWA


WATU 48 wameripotiwa kuuawa, hoteli mbili, kituo cha polisi na kituo cha mafuta kuchomwa moto baada ya shambulio lililotokea eneo la Mpeketoni, Lamu nchini Kenya jana usiku.Kituo cha Polisi cha Mpeketoni, hoteli ya Breeze View na Taweel ndivyo vilivyochomwa moto na moshi ulikuwa bado unafuka leo  asubuhi .Imeelezwa kuwa washambuliaji walitokomea na silaha na magari ya polisi kutoka kutuo hicho cha polisi baada ya kushambulia.

  
Awali washambuliaji hao waliteka daladala mbili 'matatu' eneo la Witu kabla ya kufanya shambulio hilo.
 
Wananchi walikimbilia katika nyumba zao wakati polisi wakijibizana risasi na magaidi hao ambapo mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo anadai kusikia washambuliaji hao wakisema "ambieni baba yenu atoe jeshi Somalia”wakimaanisha wamwambie Rais Kenyatta aondoe jeshi nchini Somalia.
  
Makundi ya Al Shabaab na MRC militia yanadaiwa kuhusika na shambulio hilo



   

Monday, June 16, 2014

AWAMU YA PILI YA MAJADILIANO YA KATIBA MPYA TANZANIA- WAJUMBE WEKENI UBINAFSI WENU PEMBENI





  • ILETEENI TAIFA KATIBA MPYA


  • MSIPOFANYA HIVYO DHAMBI HII ITAWATAFUNA MPAKA MNAINGIA KABURINI;

 

LAKINI: BADO TUNAHITAJI BUSARA ZAIDI KUTOKA KWA WAJUMBE HASA WALE WANAOTOKANA NA VYAMA;

  • Tukumbuke kuwa “Siasa si mchezo mchafu, ila wachezaji wake ndiyo wachafu.”


  • Je wajumbe wa bunge la katiba wanapofanya maaumuzi kuhusu katiba mpya wanaangalia, dhana  ya “wao” na “sisi”



  • Ni kweli kuwa  Siasa hutafasiriwa kuwa ni fikra, busara na mipango ya kuendesha nchi au ya kujinufaisha wao wenyewe?


  • Litakuwa ni jambo la kuheshimiwa ka viongozi wetu kama Waheshimiwa wajumbe wa bunge la katiba  watakuwa wakweli na wenye Uzalendo wa kweli ndani ya mioyo kwa faida ya wananchi wao.


  • Confucius aliwahi sema kuwa  ‘Utajiri na vyeo ndivyo vitu ambavyo kila bianadamu anavitamani; lakini ikiwa njia ya kuvipata ni kwa kwenda kinyume na misingi yake, anapaswa ajiepushe navyo.



  • Rudolph Giuliani aliwahi sema kuwa ‘Kiongozi huchaguliwa kwa kuwa yeyote anayemuweka pale huwa anaamini maamuzi, tabia na uwezo wa maarifa yake – siyo ujuzi wa kufuata maoni. Ni wajibu wa kiongozi kuchukua hatua kufuatana na sifa hizo.’



  • “kiongozi ajiulize ni vipi atalitumikia Taifa na si Taifa kumtumikia yeye Kiongozi Umashuhuri na uzuri wa Kiongozi unatokana na hekima, busara, uchapakazi, ufanisi, ufuatiliaji, uimara, uungwana, uwajibikaji na unyenyekevu wake. Ama fikra endelevu na upeo wa kuongoza ni muhimu na si kauli tamu za kuwafurahisha viongozi wengine”


 
  • Tamaa ya kujilimbikizia mali huo ni udhaifu wa mwanadamu ambao hapaswi kuupa nafasi iwapo unazingatia uadilifu wa uongozi kama wajumbe wetu hizo ndizo fikra zao hawatufai hao.



Demokrasia kama falsafa ya Plato ambayo inahusiana na uendeshaji wa shughuli za kisiasa inalenga zaidi katika  utumishi kwa umma na uendeshaji wa jamii na taifa. Wananchi wote hawawezi ongoza nchi kwa mara moja; Katika msingi huu wananchi kutokana na wingi wao waliridhika itakuwa sio rahisi kwa wao wote kukutana, kufanya maamuzi na kuyasimamia moja kwa moja maamuzi hayo yanayowahusu wao kama jamii; dhana ya kuwachagua viongozi wachache huzaliwa kwa chimbuko hili na kuruhusiwa kuunda serikali. Ambayo huendesha kulingana na katiba ya nchi ambayo imetokana na wananchi.


Tatizo kubwa tulilonalo kama Taifa ni ufinyu wa viongozi bora na utashi binafsi wa wachache walio katika nyanja za uongozi kwa kukosa sifa muhimu kwa viongozi. Kwani inatupasa kutambua kuwa uongozi si lelemama, ni kipaji na ni kazi ngumu. Lakini ridhaa hiyo haitolewi hivi hivi tu, inaambatana na amana, kwamba waongozi watatekeleza dhamana  na wajibu  wao kwa makubaliano na maelewano ya kufuata barabara na kuheshimu ipasavyo kanuni na maadili fulani yanayoitambulisha na kuiongoza jamii husika. 


Kwa kauli zinazotofautiana na misimamo inayotofautiana kuhusu ukamilishaji wa uandikaji wa katiba mpya kufuatia mgomgano wa mawazo na itikadi; zoezi la uandikaji wa katiba mpya unaishia kwenye  fursa na ushawishi kwa malengo ya chama au itikadi Fulani ndio iwe kinara wa katiba mpya. ikumbukwe kuwa kiongozi muadilifu hakubali kufuata  au kutoa maamuzi bila kufanya ukadirifu wa hoja na hali husika.


Uongozi ni kujitolea na kuweka matwakwa na maslahi ya wengine kuwa mstari wa mbele na si matakwa binafsi na kujinufaisha. Marehemu John Kennedy rais wa Marekani alitoa kauli moja maarufu iliyosema kuwa. Tuchague viongozi si kwa kuangalia vyama au sura, bali tuangalie uwezo wao wa kuongoza, kuhamasisha na kufanya kazi. Tupime kauli zao na matokeo ya kazi zao kama wanavyojinadi.


Serikali ni watu, inaundwa na watu tuliowachagua na tunawapa watu hawa na Serikali mamlaka makubwa ya kutuongoza, kupanga na kulinda Taifa na Katiba yetu. Dhamana hii imefanywa kwa kuaminiana kuwa Serikali itafanya kazi kwa manufaa ya Wananchi wake na kwa matakwa na utashi wa Wananchi wake.


  • Kuna amani gani na utulivu gani katika nchi yetu wakati mioyo yetu sisi kama wananchi imevimba kwa kujaa hasira za ubinafsi wa hoja na matusi ya wajumbe waliopewa dhamana ya kutuwakilisha?


Uadilifu wa wajumbe wa bunge la katiba umeporwa na wachache kwa manufaa binafsi nap engine kujiwekea matumaini makubwa ya utajiri kwa baadae. Je mijadala ya hivi sasa kuhusu katiba mpya nje ya bunge yataimarisha hoja za ufanisi wa katiba mpya au kuleta zaidi mgawanyo? Je kuhusu amani yetu?


Kama ilivyo kwa umoja wa kitaifa, kiongozi muadilifu pia hufanya kila bidii kuhakikisha amani na utulivu wa kweli katika nchi vinapatikana. Amani na utulivu ni chachu ya wananchi kwa kushirikiana na Serikali yao kujiletea maendeleo. Maendeleo hayaji mahala penye magomvi na hasama. Lakini na amani na utulivu pia haviji mahala pasipo na haki na uadilifu. Uvunjifu wa amani na utulivu wa nchi hupelekea hasara ya maisha na mali ya watu na hayo hayawi malengo ya uongozi muadilifu katika nchi


Uadilifu wa uongozi unadai kuheshimu nguvu ya hoja na fikra bora na hayo yanaweza kupatikana tu iwapo nchi inaongozwa kwa misingi ya kidemokrasia. Hivyo, katika kutoa uongozi sahihi, kwa kuzingatia maslahi bora ya nchi na watu wake, haki, uadilifu, umoja, amani na utulivu, hapana budi kwa kiongozi kuiamini, kuiheshimu na kuifuata barabara misingi ya kidemokrasia.


Bado binadamu si mkamilifu na kwa vyovyote vile hufikia mahala akafanya maamuzi ambayo si sahihi hata kama yalifanywa kwa nia njema na kwa kuzingatia taarifa zilizopatikana wakati maamuzi hayo yanafanywa. Hayo yanaeleweka na kiongozi muadilifu anapaswa kuyakubali na kuliomba radhi Taifa. Hiki ndiyo kilele na kigezo kikuu cha uadilifu wa uongozi katika siasa. Kukubali kubeba dhamana kwa madhara yaliyotokana na maamuzi yako au yaliyofanywa kwa jina lako.

Maamuzi ya kiongozi wa kisiasa huathiri taifa zima, busara na hekima huzaa maamuzi yanayotokana na tafakuri ya kina, yanayozingatia hali halisi ya mambo na maslahi na manufaa ya muda mrefu. Kiongozi muadilifu anatakiwa ayaone haya na ayazigatie kwa kila hatua anayochukua.


Je kama baadhi ya wajumbe wa bunge la katiba watasusia kikao ambacho kinatarajia kuanza mwezi wa Nane je watakuwa wame  kurupuka katika kufanya maamuzi hayo bila kuyafanyia kazi vizuri na kukiuka msingi mkubwa sana wa demokrasia? Tukubali tu kuwa njia ya kusonga mbele ni kukubali kutofautiana katika fikra lakini tubaki kuwa wamoja katika hoja na maridhiano.


Wajumbe wa bunge la katika 2014 mnapaswa kujitafakari wenyewe na kuona mzigo mzito ambao uko mbele yenu leo hii kwa faida ya Taifa na sio kundeleza matusi, vijembe, ubabe shindaneni kwa hoja na hatimaye mkubaliane kwa maridhiano.


Wananchi tunasubiri kilicho bora bila kuathiri amani na umoja wetu wa kitaifa.



MUNGU IBARIKI TANZANIA

RAIS KIKWETE KUWALETA TREY SONGZ NA USHER RAYMOND MWEZI UJAO KUZUNGUMZA NA WASANII WA FILAMU NA MUZIKI.


Rais Kikwete na baadhi ya wasanii
Rais Kikwete anatarajia kuwaleta nchini wanamuziki maarufu wa Marekani Usher Raymond na Trey Songz mwezi ujao yaani July.Wasanii hao watatumbuiza na pia kuzungumza na wasanii wa muziki na filamu nchini kwa mujibu wake mwenyewe. Juzi wasanii na Rais Kikwete walikuwa Dodoma katika uzinduzi wa video ya campaign ya Muungano.

CREDIT : SWAHILI PLANET 
Trey Songz na Usher Raymond

source: matukiotz.com

RAIS KIKWETE ATETA NA WASANII DODOMA

D92A1853
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisistiza jambo wakati akizungumza na msanii wa kizazi kipya Nasib Abdul “Diamond” ikulu ndogo mjini Dodoma wakati chakula cha usiku alichowaandalia wasanii walioshiriki katika tamasha la Uzalendo na Uzinduzi wa Video ya wimbo maalum wa miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar lililofanyika katika uwanja wa michezo wa Jamhuri mjini Dodoma jumamosi.Kulia ni mbunge wa Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete.
D92A1860
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana  na msanii wa kizazi kipya Nasib Abdul “Diamond” ikulu ndogo mjini Dodoma wakati chakula cha usiku alichowaandalia wasanii walioshiriki katika tamasha la Uzalendo na Uzinduzi wa Video ya wimbo maalum wa miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar lililofanyika katika uwanja wa michezo wa Jamhuri mjini Dodoma jumamosi.Kulia ni mbunge wa Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete.
D92A1891
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimsikiliza kwa makini mwanamuziki wa kizazi kipya Ommy Dimpoz wakati chakula cha usiku alichowaandalia wasanii walioshiriki katika tamasha la Uzalendo na Uzinduzi wa Video ya wimbo maalum wa miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar lililofanyika katika uwanja wa michezo wa Jamhuri mjini Dodoma jumamosi iliyopita kulia ni Mh. Ridhiwani Kikwete Mbunge wa jimbo la Chalinze(picha na Freddy Maro).