WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, April 30, 2014

Ukawa: Tutaidai Tanganyika nje ya Bunge


Mbowe, Profesa Lipumba, Mchungaji Mtikila wahutubia.

Zanzibar. Viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), wameapa kuendelea kudai mfumo wa Muungano wa serikali tatu nje ya Bunge la Katiba kwa nguvu zote, ikiwamo kufanya maandamano ya amani nchi nzima.
Msimamo huo ulielezwa na viongozi hao kwa nyakati tofauti katika mkutano wa hadhara uliofurika mashabiki kwenye Viwanja vya Kibandamaiti, Unguja jana.
Mwenyekiti Ukawa, Freeman Mbowe alisema wameamua kuliacha Bunge la Katiba kutokana na harufu za rushwa, vitisho na matusi huku baadhi ya wabunge wakiahidiwa vyeo. Mbowe ambaye hata hivyo hakufafanua zaidi, alisema Ukawa wameamua kwenda kwa wananchi kuwaeleza dhamira chafu walionayo wabunge wa CCM katika mpango wao wa kukataa Rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyowasilishwa na Jaji Joseph Warioba.
“Ni jambo la hatari katika mchakato wa Katiba wananchi kuwa waoga au hofu... Lazima tuwe tayari kuwaonyesha watawala kuwa tuna umoja imara, tunayapigania mataifa huru ya Tanganyika na Zanzibar, Rais Kikwete (Jakaya) asiwatishe wananchi kwa kivuli cha jeshi kuchukua madaraka,” alisema Mbowe.
Lipumba anena
Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa, Profesa Ibrahim Lipumba alisema wajumbe wa Ukawa wameamua kujitoa bungeni kutokana na kauli ya Rais Jakaya Kikwete ambayo alidai kuwa iliibeza na kuidhalilisha Tume ya Warioba.
Alisema hawatarudi bungeni na kwamba hawawezi kujadili Katiba ambayo siyo maoni ya wananchi.
Alidai kwamba kwa makusudi Rais Kikwete aliamua kutetea sera za chama chake na kupingana na maoni yaliyotolewa na wananchi kupitia Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
“Rais Kikwete ameharibu nia ya kupatikana Katiba Mpya, amekuwa akijulishwa kila hatua na jinsi maoni ya wananchi walivyokuwa wakipendekeza serikali tatu katika Rasimu ya Kwanza na ya Pili naye akawa anaafiki, inashangaza amegeuka na kukataa maoni ya wengi,” alisema Profesa Lipumba.
Mtikila akumbushia jela
Mwenyekiti wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila alisema aliwahi kufungwa jela mara tatu, kuwekwa mahabusu mara 43 kwa kudai lipatikane Taifa la Tanganyika huku watawala wakikataa matakwa ya wengi kwa sababu na hoja dhaifu.
Mchungaji Mtikila aliongeza kusema kwamba wanachokitaka CCM na Serikali zake ni kuendelea kuwabana wananchi wa Tanganyika na Zanzibar wasiweze kuwa huru na kujivunia mataifa yao.
Seif: Mimi Ukawa damu
Akihutubia mkutano huo, Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad alieleza msimamo wake kuwa anaunga mkono harakati hizo na yeye ni Ukawa damudamu.
“Walikuwa hawajui msimamo wangu, waelewe kwamba mimi ni Ukawa damu,” alisema.
Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, alisema wanaotetea mfumo wa serikali mbili ni sawa na watu wanaopigania kuendelea kuwapo kwa dhuluma Tanzania.
“Hatuwezi kuendelea na mfumo huu, tumekuwa tukipiga kelele kwamba Muungano huu wa serikali mbili umeteka mamlaka yetu,” alisema Maalim Seif. Alimtaka Rais Kikwete asiwatishe wananchi kwa sababu wamependekeza mfumo mpya wa serikali... “Unaposema kwamba jeshi litapindua nchi kama tukiwa na Muungano wa serikali tatu, unamaanisha nini kama Amiri Jeshi Mkuu?” alihoji Maalim.
Katika mkutano huo, ulinzi uliimarishwa vya kutosha huku magari ya FFU na vikosi vya SMZ yakiwa yameegeshwa pembeni na askari waliokuwa wamebeba silaha na mabomu viunoni wakilinda

source: mwananchi

BASI LA AM COACH LAPATA AJALI ENEO LA IPULI NA KUSABASHA KIFO CHA MWANAFUNZI MMOJA KUFARIKI HAPO HAPO.



Askari Polisi Kitengo cha usalama barabarani wakiuchukua mwili wa mtoto aliyegongwa na basi la kampuni ya A.M maeneo ya Ipuli Mnadani ambalo lilikuwa likitokea jijini Mwanza,katika ajali hiyo watu kadhaa wamejeruhiwa.

Umati mkubwa wa watu ambao ulifiika kushuhudia ajali hiyo mbaya

Maafisa wa Chama cha Msalaba Mwekundu mkoa wa Tabora walifika eneo la tukio na kusaidia majeruhi wa ajali hiyo.

Wananchi wakishuhudia mwili wa mtoto aliyegongwa na basi hilo ambapo walishauri Serikali iliifungie kampuni hiyo ya A.M Coach kuleta mabasi mkoani Tabora ambayo walidai kuwa ni mabovu na yanausalama mdogo kwa wasafiri.
 

Huu ndio uskani wa basi hilo ni mbovu kupindukia na si salama kwa kutumika  kwenye magari ya usafirishaji wa binadamu

Kufuatia kutokea kwa ajali za mara kwa mara zinazosababishwa na mabasi ya kampuni ya A.M,wananchi mkoani Tabora wameiomba Serikali kuyapiga marufuku mabasi ya kampuni hiyo kwakuwa yamebainika kuwa ni mabovu na si salama kwa wasafiri na wapita njia.

Wananchi hao ambao walifika katika moja ya tukio la ajali iliyotokea eneo la Ipuli mnadani kushuhudia ambapo wanafunzi wawili waliokuwa wakienda shuleni kwa ajili ya masomo kwa muda wa ziada,mwanafunzi mmoja alifariki papo hapo na mwingine kujeruhiwa vibaya baada ya kugongwa na basi la A.M Coach lenye nambari za usajili T 861 ATZ lililokuwa likifanya safari zake kutoka Mwanza kwenda Tabora.

Aidha wananchi hao ambao hawakutaka kutajwa majina yao wamedai kuwa mabasi ya kampuni hiyo yamekuwa yakiingia mjini kwa kasi kubwa huku yakionekana kuyumba barabarani na kuzidi kutia shaka hata watumiaji wa barabara kuu za mkoa wa Tabora.



Wameitahadharisha Serikali kuwa endapo watayaachia mabasi hayo huenda yatasababisha ajali mbaya zaidi na hata vifo visivyo vya lazima.

source: blog ya mwananchi

RAIS KIKWETE AHUDHURIA MKUTANO WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI ARUSHA

Rais  Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Arusha(AICC) kwenye mkutano
wa 12 wa Wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika mjini
Arusha.Rais Kenyatta ndiye mwenyekiti wa jumuiya hiyo ya wnanachama watano.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya na Rais
Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda wakijadiliana jambo kabla ya ufunguzi wa
Mkutano wa siku moja wa  wakuu wa nchi za  Jumuiya ya Afrika Masharariki
uliofanyika mjini Arusha leo(picha na Freddy Maro).
 
source: blog ya mwananchi

ANGALIA PICHA MAPOKEZI YA RAIS WA KENYA ARUSHA JANA















Sunday, April 27, 2014

Mkumbo: Vyama vyakosa mwelekeo kwa kutaka kuuvunja Muungano

Dk. Kitila Mkumbo
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Kitila Mkumbo, amesema baadhi ya vyama vya upinzani vimekosa mwelekeo kutokana na kubeba ajenda inayoelekea kuvunja Muungano.
Akizungumza katika kongamano la Muungano lilofanyika chuoni hapo jana, Dk. Mkumbo alisema katika mwelekeo uliopo sasa haionyeshi utashi wa vyama hivyo kutaka kuulinda na kujenga Muungano imara, badala yake kuna vita vya kugombea madaraka nje ya Muungano.

Alisema kihistoria hakuna chama kinachoweza kujiweka kando ya Chama cha mapinduzi (CCM) ambapo katika muundo huo wamebeba ajenda ya siri ya kuona Mungano huo unavunjika ili wapate nafasi ya kushika uongozi katika nchi za Zanzibar na Tanganyika zitakazoundwa.

Alisema endapo watafanikiwa jambo hilo, Zanzibar kama nchi haitakuwa kwenye usalama na itasababisha Tanganyika kuwa shakani.

Alisema kosa lilofanyika ni kuweka suala la Muungano kuwa la kisera ndani ya vyama vya siasa, kitu kinaleta mvutano kati ya CCM wanaotaka serikali mbili na wapinzani wanaotaka serikali tatu.

"Tukiamua kama Muungano kuwa sera ya kisiasa tutakosea sana, mambo yote yanayogusa uhai wa nchi lazima yasiingiliwe na chama chochote," alisema Mkumbo.

Alishauri Rasimu ya Katiba mpya itamke wazi kujenga Muungano imara na sio kujenga nchi legelege.

Kongamano hilo liliandaliwa na Umoja wa Wasomi wa Chuo Kikuu hicho (UDASA) ambapo wasomi mbalimbali walijadili mustakabali wa Muungano na nini kifanyike kunusuru usivunjike.
 
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

Warioba atunukiwa nishani iliyotukuka.

unnamed19 1e6c5
Na Hudugu Ng'amilo
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba juzi usiku alikuwa miongoni mwa viongozi na watu mashuhuri waliotunukiwa nishani na Rais Jakaya Kikwete, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Katika maelezo ya kutoa nishani ya kumbukumbu ya miaka 50 ya Muungano daraja la kwanza, ilielezwa kuwa Jaji Warioba, aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliuenzi na bado anauenzi Muungano huo.
"Katika kipindi chako, pamoja na nyadhifa nyingine, ulikuwa Waziri Mkuu na Makamu wa kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani...katika kipindi hicho na hadi sasa umeendelea kuwa mwaminifu, umeutunza, umeulinda na umeuenzi Muungano," ilisema sehemu ya taarifa ya kutoa nishani.
Hivi karibuni, Jaji Warioba amekuwa akishambuliwa na baadhi ya Wajumbe wa Bunge la Maalumu la Katiba, pia baadhi ya wana CCM kutokana na Rasimu ya Pili ya Katiba Mpya iliyoandaliwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba aliyoiongoza, kupendekeza muundo wa Muungano wa Serikali tatu.
Hata hivyo, upande mwingine wajumbe wanaojitambulisha kama Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wamekuwa wakiunga mkono mapendekezo ya rasimu hiyo.
Mbali na Jaji Warioba, wengine waliopewa nishani katika daraja hilo ni Aboud Jumbe Mwinyi aliyekuwa Rais wa Pili wa Zanzibar, Aman Karume, John Malecela, Cleopa Msuya na Dk Salmin Amour Juma.
Wengine ni Omar Ali Juma na Idrissa Abdul Wakil, ambao sasa ni marehemu.
Walioanza kupata tuzo na nishani hizo ni waasisi wa Muungano wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere na Abeid Karume(wote ni marehemu) na walioendeleza ambao ni Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa.
Wengine waliopewa tuzo ni pamoja na viongozi wa majeshi ya ulinzi na usalama akiwemo Mkuu wa Jenshi la Wananchi (JWTZ), Jenerali Davis Mwamunyange na Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Ernest Mangu. Wakuu wa JWTZ wastaafu pia walikumbukwa akiwemo, Jenerali Mirisho Sarakikya, Jenerali David Musuguri.
Katika nishani ya kumbukumbu ya miaka 50 ya Muungano daraja la nne lilikuwa na Mama Maria Nyerere na Mama Fatma Karume, Bendi ya Msondo Ngoma pia ilipewa tuzo kwa kuuenzi Muungano.Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni za IPP, Reginald Mengi alipewa tuzo maalumu akiwa raia wa Tanzania aliyetoa mchango muhimu katika huduma za jamii.
Wasifu
Mwenyewe Joseph Warioba aliingia serikalini mwaka 1966, akiwa mwanasheria wa mji wa Dar er Salaam, nafasi aliyoitumikia kwa muda wa miaka miwili, kisha kuhamia kuwa mwanasheria wa Baraza la Jiji mpaka mwaka 1970.
Kuanzia mwaka 1976 mpaka 1983 Warioba alitumikia taifa kwa wadhifa wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Warioba pia aliwahi kuwa Waziri wa Sheria katika awamu ya kwanza iliyokuwa ikiongozwa na Mwalimu Julius Nyerere.
Mwaka 1984 aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais, nafasi aliyoitumikia hadi mwaka 1990.
Mwaka 1996 Rais Benjamin Mkapa alimteua kuongoza tume ya kupambana na rushwa.
Mwaka 2007 alioongoza jopo la waangalizi kutoka nchi za Jumuiya ya Madola katika uangalizi wa uchaguzi mkuu wa Nigeria.
Mwaka 2012 Rais wa awamu ya nne alimteua Warioba kuongoza Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

CHANZO MWANANCHI

Neno La Leo: CCM Na Upinzani Hawana Cha Kujifunza Kutoka Kenya!

Photo: Neno La Leo: CCM Na Upinzani Hawana Cha Kujifunza Kutoka Kenya!
Ndugu zangu,
Uchaguzi Mkuu wa Kenya umefuatiliwa kwa karibu sana na sisi Watanzania, ni pamoja na wanasiasa wa vyama vya siasa; Chama tawala, CCM na wapinzani.
Lakini, nahofia, kuwa hakuna ambacho vyama hivi vyetu vya siasa vitajifunza kutoka Kenya.
Ndio, pamoja na mapungufu ya hapa na pale, lakini Wakenya, kupitia Uchaguzi wao wametuachia somo kubwa sana; kuwa hata Afrika tunaweza kuendesha siasa za kistaarabu ikiwemo chaguzi Huru.
Ni kawaida kwa majirani sisi; Kenya na Tanzania, kuoneana wivu kwenye kupiga hatua kimaendeleo. Hakika ni wivu wa kimaendeleo tunaopaswa kuwa nao. Nikiri, safari hii, kama Mtanzania, nimejisikia kuwaonea wivu Wakenya kwa jinsi walivyoionyesha Afrika na Dunia kuwa nao wanaweza kuwa Taifa Kubwa; kisiasa na kiuchumi.
Mchakato ule wa mabadiliko ya Katiba yao na hata kufanya uchaguzi ule kwa amani na uwazi ni USHINDI mkubwa wa kimfumo. Ni ushindi wa Wakenya wote. Kwamba Wakenya wameujaribu mfumo mpya. Umeonyesha kuwa unafaa.
Kwa mfano, kufuatilia matokeo ya uchaguzi ule kutoka kwenye Tume yao Huru ilikuwa ni kama ‘ burudani’ ya kisiasa. Kila kitu kilikuwa kinawekwa wazi na kisayansi.
Si ajabu Wakenya waliweza kusubiri matokeo kwa juma moja bila kurushiana mawe. Na hata kama ingekuwa kusubiri kwa majuma mawili, naamini kuwa Wakenya wale wangesubiri bila kupigana, maana, wamekuwa na imani kubwa na Tume yao Huru ya Uchaguzi. Na hatukusia kule Kenya, habari ya watu ‘ kulinda kura’ wala kusimama hatua mia moja kutoka kituo cha kuhesabia kwa usiku mzima. Hiyo kazi iliachiwa Tume Huru ya Uchaguzi walioiamini.
Ndio, Wakenya wamejifunza kutokana na ujinga wa wanasiasa wao uliopelekea vurugu za baada ya Uchaguzi wa mwaka 2007. Wengi walikufa na wengine kupoteza makazi na mali zao. Wakaanza haraka mchakato wa kuifanyia marekebisho makubwa Katiba yao. Wakapata Katiba Mpya 2010. Wakenya wale wametumia gharama kubwa kwa kuitafuta amani yao. Kimsingi, tangu 2010, Wakenya wamekuwa ‘ wakiangushiwa mabomu ya ujumbe wa amani’- Ni kila kukicha.
Serikali yao imetumia fedha nyingi sana kufikisha ujumbe wa amani kwa Wakenya. Sasa wanavuna walichopanda; kuwa na chaguzi huru za amani na utulivu. Na walichokitafuta Wakenya kwa gharama kubwa, kwa maana ya amani, sisi Watanzania tulikuwa nayo, sasa tunaipoteza wenyewe ili baadae tuanze kugharamia kuitafuta. Ni ulimbukeni.
Kwa kupitia Katiba yao ya sasa Wakenya wameweza kupunguza kwa kiasi kikubwa tatizo la ukabila. Kwa namna gani?
Ona kwenye kugombea Urais; mgombea lazima afikishe asilimia 50+1 ( Asilimia 50 na kura moja) ili aweze kutangazwa mshindi. Mgombea pia lazima akubalike kwa asilimia 25 ya Counties zote ( Majimbo yote).
Sasa basi, kwa Kenya, Wakikuyu ni asilimia 23 ya Wakenya. Wajaluo asilimia 11.
Nyingine zilizobaki ni za makabila mengine madogo madogo. Hivyo, ili mgombea ushinde zaidi ya asilimia 50 una lazima ya kukubalika kwenye maeneo mengine nje ya wigo wa kabila lako. Kwamba kula za Wakikuyu pekee kwa Uhuru Kenyatta zisingetosha, vivyo hivyo kwa Odinga.
Utaratibu huo unaua ukabila na kujenga vema misingi ya Utaifa. Hata kama itachukua muda kufika mbali zaidi katika hilo lakini Wakenya wameanza kuondokana na ukabila kwenye siasa zao, kwa kupitia Katiba.
Kwa mantiki hiyo hiyo, Watanzania tungeweza kabisa kuondokana na siasa za udini kwa kuweka, kwenye Katiba yetu ijayo sharti la mgombea Urais kushinda kwa asilimia 50+1 ( Asilimia 50 jumlisha kura 1). Hilo lingewafanya wanasiasa wetu wenye kuwania Urais na vyama vyao pia ‘ Kutia akili’.
Maana ingekuwa na tafsiri moja kuu; kuwa mgombea na chama chenye kuendekeza udini kisingekuwa na nafasi ya kutoa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wala nafasi ya kushika dola. Maana, hakuna dini hapa Tanzania yenye idadi ya waumini wanaovuka asilimia 50 ya jumla ya Watanzania.
Kwa maana, hiyo, muarobaini wa kumalizana na udini uko kwenye Katiba ijayo, kama tuna nia ya dhati ya kutoka hapa tulipo. Vinginevyo, udini huu tunaosema kuwa ni tatizo tutakuwa tunaulea wenyewe.
Hata tatizo la siasa za ukanda nalo litapotea, maana, hakutakuwa na mgombea au chama kitakachoweza kushinda na kutoa Urais kwa kuegemea kura za kikanda. Hakuna kanda itakayovuka peke yake asilimia 50 ya kura zote. Chama na mgombea kitahitaji kuungwa mkono na wapiga kura wa kanda hata zilizo nje ya anakotoka mgombea Urais.
Vinginevyo, kama alivyotamka Uhuru Kenyatta kwenye hotuba yake nzuri iliyojaa utaifa hivi majuzi, kuwa katika uchaguzi waliofanya, kila kura ilikuwa ina umuhimu. Hivyo, kila kabila lilikuwa na umuhimu. Na Uhuru Kenyatta akaweka wazi anachotaka Serikali yake kwa kushirikiana na Wakenya kufanya ili kuitoa Kenya hapo ilipo na kwenda mbele.
Kenyatat alimalizia na maneno matatu; Forward, Foward. Foward!- Kusonga mbele!
Ndio, Wakenya wameamua; KENYA KWANZA!
And really, The Kenyans are coming, Big Time!
Ni ukweli, Wakenya wanakuja. Kisiasa na kiuchumi. Sisi hatujajipanga na hatutaki kujipanga kwa dhati. CCM na wapinzani, na hata media yetu, kama kawaida, tumerudi kwenye kucheza ‘ Kiduku’ chetu. Hatuna cha kujifunza kutoka Kenya. Tumerudi kwenye mambo yetu ya hovyo hovyo; ni Siasa za Mwembe Yanga na Viwanja Vya Jangwani. Siasa za kupigana vijembe. Siasa za reja-reja- Retail politics.
CCM na wapinzani ni kama vile wapenzi wa soka. Wanaangalia kila siku soka la majuu. Wataongea sana kuhusu soka la majuu lilivyo bora.
Lakini, wakirudi kwenye soka lao, ni yale yale, hawana cha kujifunza na hawataki kujifunza. Ni madudu kwenye kuendesha vilabu na hata kufikia kununua mechi kwa kuhonga marefa, wachezaji na viongozi. Ukisema nini hiki?
Utajibiwa; “Wewe Bongo mpira pesa bwana!” “Mpira fitna!” Ni kama majibu ya wanasiasa, iwe wa CCM au vyama vya upinzani. Nao watakwambia; “Wewe, Bongo siasa pesa bwana!” “ Siasa mizengwe na fitna!”
Naam, nahofia, kuwa CCM na wapinzani hawana cha kujifunza kutoka Kenya!
Maggid Mjengwa,
Iringa,
0788 111 765
<a href=
Ndugu zangu,
Uchaguzi Mkuu wa Kenya umefuatiliwa kwa karibu sana na sisi Watanzania, ni pamoja na wanasiasa wa vyama vya siasa; Chama tawala, CCM na wapinzani.
Lakini, nahofia, kuwa hakuna ambacho vyama hivi vyetu vya siasa vitajifunza kutoka Kenya. Ndio, pamoja na mapungufu ya hapa na pale, lakini Wakenya, kupitia Uchaguzi wao wametuachia somo kubwa sana; kuwa hata Afrika tunaweza kuendesha siasa za kistaarabu ikiwemo chaguzi Huru.
Ni kawaida kwa majirani sisi; Kenya na Tanzania, kuoneana wivu kwenye kupiga hatua kimaendeleo. Hakika ni wivu wa kimaendeleo tunaopaswa kuwa nao. Nikiri, safari hii, kama Mtanzania, nimejisikia kuwaonea wivu Wakenya kwa jinsi walivyoionyesha Afrika na Dunia kuwa nao wanaweza kuwa Taifa Kubwa; kisiasa na kiuchumi.

Mchakato ule wa mabadiliko ya Katiba yao na hata kufanya uchaguzi ule kwa amani na uwazi ni USHINDI mkubwa wa kimfumo. Ni ushindi wa Wakenya wote. Kwamba Wakenya wameujaribu mfumo mpya. Umeonyesha kuwa unafaa.

Kwa mfano, kufuatilia matokeo ya uchaguzi ule kutoka kwenye Tume yao Huru ilikuwa ni kama ‘ burudani’ ya kisiasa. Kila kitu kilikuwa kinawekwa wazi na kisayansi.

Si ajabu Wakenya waliweza kusubiri matokeo kwa juma moja bila kurushiana mawe. Na hata kama ingekuwa kusubiri kwa majuma mawili, naamini kuwa Wakenya wale wangesubiri bila kupigana, maana, wamekuwa na imani kubwa na Tume yao Huru ya Uchaguzi. Na hatukusia kule Kenya, habari ya watu ‘ kulinda kura’ wala kusimama hatua mia moja kutoka kituo cha kuhesabia kwa usiku mzima. Hiyo kazi iliachiwa Tume Huru ya Uchaguzi walioiamini.


Ndio, Wakenya wamejifunza kutokana na ujinga wa wanasiasa wao uliopelekea vurugu za baada ya Uchaguzi wa mwaka 2007. Wengi walikufa na wengine kupoteza makazi na mali zao. Wakaanza haraka mchakato wa kuifanyia marekebisho makubwa Katiba yao. Wakapata Katiba Mpya 2010. Wakenya wale wametumia gharama kubwa kwa kuitafuta amani yao. Kimsingi, tangu 2010, Wakenya wamekuwa ‘ wakiangushiwa mabomu ya ujumbe wa amani’- Ni kila kukicha.


Serikali yao imetumia fedha nyingi sana kufikisha ujumbe wa amani kwa Wakenya. Sasa wanavuna walichopanda; kuwa na chaguzi huru za amani na utulivu. Na walichokitafuta Wakenya kwa gharama kubwa, kwa maana ya amani, sisi Watanzania tulikuwa nayo, sasa tunaipoteza wenyewe ili baadae tuanze kugharamia kuitafuta. Ni ulimbukeni.


Kwa kupitia Katiba yao ya sasa Wakenya wameweza kupunguza kwa kiasi kikubwa tatizo la ukabila. Kwa namna gani?

Ona kwenye kugombea Urais; mgombea lazima afikishe asilimia 50+1 ( Asilimia 50 na kura moja) ili aweze kutangazwa mshindi. Mgombea pia lazima akubalike kwa asilimia 25 ya Counties zote ( Majimbo yote).
Sasa basi, kwa Kenya, Wakikuyu ni asilimia 23 ya Wakenya. Wajaluo asilimia 11.

Nyingine zilizobaki ni za makabila mengine madogo madogo. Hivyo, ili mgombea ushinde zaidi ya asilimia 50 una lazima ya kukubalika kwenye maeneo mengine nje ya wigo wa kabila lako. Kwamba kura za Wakikuyu pekee kwa Uhuru Kenyatta zisingetosha, vivyo hivyo kwa Odinga.


Utaratibu huo unaua ukabila na kujenga vema misingi ya Utaifa. Hata kama itachukua muda kufika mbali zaidi katika hilo lakini Wakenya wameanza kuondokana na ukabila kwenye siasa zao, kwa kupitia Katiba.


Kwa mantiki hiyo hiyo, Watanzania tungeweza kabisa kuondokana na siasa za udini kwa kuweka, kwenye Katiba yetu ijayo sharti la mgombea Urais kushinda kwa asilimia 50+1 ( Asilimia 50 jumlisha kura 1). Hilo lingewafanya wanasiasa wetu wenye kuwania Urais na vyama vyao pia ‘ Kutia akili’.


Maana ingekuwa na tafsiri moja kuu; kuwa mgombea na chama chenye kuendekeza udini kisingekuwa na nafasi ya kutoa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wala nafasi ya kushika dola. Maana, hakuna dini hapa Tanzania yenye idadi ya waumini wanaovuka asilimia 50 ya jumla ya Watanzania.

Kwa maana, hiyo, muarobaini wa kumalizana na udini uko kwenye Katiba ijayo, kama tuna nia ya dhati ya kutoka hapa tulipo. Vinginevyo, udini huu tunaosema kuwa ni tatizo tutakuwa tunaulea wenyewe.


Hata tatizo la siasa za ukanda nalo litapotea, maana, hakutakuwa na mgombea au chama kitakachoweza kushinda na kutoa Urais kwa kuegemea kura za kikanda. Hakuna kanda itakayovuka peke yake asilimia 50 ya kura zote. Chama na mgombea kitahitaji kuungwa mkono na wapiga kura wa kanda hata zilizo nje ya anakotoka mgombea Urais.


Vinginevyo, kama alivyotamka Uhuru Kenyatta kwenye hotuba yake nzuri iliyojaa utaifa hivi majuzi, kuwa katika uchaguzi waliofanya, kila kura ilikuwa ina umuhimu. Hivyo, kila kabila lilikuwa na umuhimu. Na Uhuru Kenyatta akaweka wazi anachotaka Serikali yake kwa kushirikiana na Wakenya kufanya ili kuitoa Kenya hapo ilipo na kwenda mbele.


Kenyatat alimalizia na maneno matatu; Forward, Foward. Foward!- Kusonga mbele!

Ndio, Wakenya wameamua; KENYA KWANZA!
And really, The Kenyans are coming, Big Time!

Ni ukweli, Wakenya wanakuja. Kisiasa na kiuchumi. Sisi hatujajipanga na hatutaki kujipanga kwa dhati. CCM na wapinzani, na hata media yetu, kama kawaida, tumerudi kwenye kucheza ‘ Kiduku’ chetu. Hatuna cha kujifunza kutoka Kenya. Tumerudi kwenye mambo yetu ya hovyo hovyo; ni Siasa za Mwembe Yanga na Viwanja Vya Jangwani. Siasa za kupigana vijembe. Siasa za reja-reja- Retail politics.


CCM na wapinzani ni kama vile wapenzi wa soka. Wanaangalia kila siku soka la majuu. Wataongea sana kuhusu soka la majuu lilivyo bora.


Lakini, wakirudi kwenye soka lao, ni yale yale, hawana cha kujifunza na hawataki kujifunza. Ni madudu kwenye kuendesha vilabu na hata kufikia kununua mechi kwa kuhonga marefa, wachezaji na viongozi. Ukisema nini hiki?

Utajibiwa; “Wewe Bongo mpira pesa bwana!” “Mpira fitna!” Ni kama majibu ya wanasiasa, iwe wa CCM au vyama vya upinzani. Nao watakwambia; “Wewe, Bongo siasa pesa bwana!” “ Siasa mizengwe na fitna!”

Naam, nahofia, kuwa CCM na wapinzani hawana cha kujifunza kutoka Kenya!


Maggid Mjengwa,

source: mjengwablog

Rais Kikwete aongoza Sherehe za miaka 50 ya Muungano


joyce_075c0.jpg 

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Rais Joyce Banda wa Malawi katika sherehe za miaka 50 ya Muungano.Rais Banda kwa sasa ndiye mwenyekiti wa jumuiya ya uchumi kusini mwa Afrika SADC. 

(PICHA:FREDDY MARO)

source: mjengwa blog

Warioba: Matusi, uongo vinaniumiza

warioba2 d63d1

Na Hudugu Ng'amilo
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Joseph Warioba amesema baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba wametumia vibaya Bunge hilo kwa kumshambulia na kumsingizia mambo ya uongo kwa makusudi, akisema matusi yanayotolewa dhidi yake yanamuumiza.

Aidha, Warioba amesema ingawa haelewi kwa nini wanaomshambulia wameamua kutumia lugha za matusi dhidi yake binafsi, hatajutia kuchaguliwa kuiongoza tume hiyo kwa kuwa ilikusudia kuwaletea maendeleo wananchi wote kwa kuwapatia Katiba wanayoitaka.

Kauli hiyo ya Jaji Warioba imekuja wakati baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba na viongozi wa CCM wakiikosoa Rasimu ya Mabadiliko ya Katiba kwa maneno makali,huku wakimshutumu na kumkejeli yeye na baadhi ya wajumbe wa tume aliyoiongoza.

Akizungumza kwa mifano katika mahojiano na gazeti hili jana, Warioba alisema kuwa anawashashangaa wajumbe hao na viongozi wa CCM kwa kuacha kuijadili Rasimu ya Katiba, badala yake wanamkosoa yeye na kumsingizia maneno yasiyo ya kweli.

"Bulembo (Abdallah Bulembo mjumbe wa Bunge na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa CCM) amenitukana, amenitukana... amesema niliwahi kupokea rushwa huku akijua kabisa kuwa ni uongo. Yeye ni kiongozi wa Kamati Kuu ya CCM, anasema uongo akijua ni uongo. Kwanza mimi simjui wala sijawahi kumwona huyu mtu naambiwa tu anatoka Mara," alisema Jaji Warioba kwa sauti ya upole iliyoashiria kuumizwa.

Aliongeza kwamba siyo mara ya kwanza kwa Bulembo kumshambulia kwa lugha za matusi, kwani aliwahi kufanya hivyo tena kwenye moja ya mikutano ya CCM mkoani Tanga.

"Alifanya hivyo Tanga, anachokifanya siyo kitu cha mzaha kwa sababu anafahamu kilichotokea," alisema.
Akizungumzia kauli aliyoitoa Waziri Hawa Ghasia wakati akichangia mjadala wa Rasimu ya Mabadiliko ya Katiba aliyemtaka Jaji Warioba kufunga mdomo kutokana na kazi yake ya kuwasilisha Rasimu kumalizika, Jaji Warioba alisema: "Wao wanataka waseme uongo, mtu mwingine asiseme kitu."

Warioba alieleza kuwa tangu lugha za matusi na kejeli zilipoanza kutolewa dhidi yake, baadhi ya watu walimshauri kwenda mahakamani kufungua kesi, lakini alikataa kwa kile alichodai kuliheshimu Bunge.
Alisema Bunge ndiyo lenye mamlaka ya kufuatilia na kudhibiti kauli zinazotolewa bungeni, kama wahusika hawafanyi hivyo hawezi kuchukua hatua yoyote.

"Kama kinga ya Bunge inatumika vibaya unafikiri mimi nitafanya nini? Sina nia ya kuchukua hatua, watu walipendekeza niende mahakamani, kuna wanasheria walisema hata nisipokwenda, wao watakwenda mahakamani nikawazuia," alisema Warioba ambaye pia ni Waziri Mkuu mstaafu.

Akisimulia kuhusu uchaguzi wa ubunge wa mwaka 1995 ambapo aligombea na kutuhumiwa kupokea rushwa na kufungiwa kwa miaka minne, Warioba alisema taarifa hizo siyo sahihi kwa kuwa aliyepokea rushwa ni aliyekuwa mgombea kwa tiketi ya NCCR Mageuzi (wakati huo), Stephen Wassira ambaye sasa yuko CCM na ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu."Uchaguzi ule ulikuwa umejaa sana rushwa, tukaenda mahakamani, Wassira akafungiwa asigombee," alisema.

Akizungumzia maadhimisho ya sherehe za miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Warioba alisema: "Mimi ni muumini wa muungano, kwa miaka 50 taifa limekaa kwa amani, mshikamano na umoja. Ni kweli tumekuwa na matatizo lakini yanaweza kutafutiwa ufumbuz
 
CHANZO MWANANCHI

MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR YAFANA


1
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete akiingia kwenye uwanja wa Uhuru kuwaongoza watanzania katika maadhinimisho ya miaka 50 ya uhuru wa Tanzania yanayofanyika kila mwaka Aprili 26 kusherehekea muungano wa Tanganyika na Zanzibar Aprili mwaka 1964 watanzania wengi wamejitokeza katika maadhimisho hayo wakiwemo viongozi mbalimbali na marais wa nchi mbalimbali za Afrika na wawakilishi wa nchi mbalimbali pia katika mataifa mbalimbali ya Ulaya,  
8
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Rais Yoweri Mseveni wa Uganda katikati nI King Mswati wa Swaziland na kushoto ni Rais Piere Nkurunzinza wa Burundi.
raaaaaaaa_b1d05.jpg
Kikosi cha Makomandoo kikionyesha ukakamavu na kuonyesha uwezo wake katika mapambano ya Karatee na  mbele ya Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Kikwete


0L7C0297 5e5bb
Na Hudugu Ng'amilo.
Sherehe za kuhadhimisha miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar iliyozaa nchi ya Tanzania zimefanyika leo mjini Dar es Salaam na kupambwa kwa maonyesho mbali mbali ya kijeshi pamoja na halaiki zilizoandaliwa na watoto.
Marais wanne wa nchi za Afrika Afrika Mashariki akiwemo Yoweri Museveni wa Uganda, Uhuru Kenyatta wa Kenya na Pierre Nkurunzinza wa Burundi ni miongoni mwa marais waliohudhuria sherehe hizo.
Wengine ni Rais Joyce Banda wa Malawi, Mfalme Mswati III wa Swaziland, mfalme Letsie III wa Lesoto Makamu wa Rais wa Nigeria Mohammed Sambo, Makamu wa Rais wa Zambia Guy Scott, Waziri Mkuu wa Rwanda Piere Habumurenyi, Waziri Mkuu wa Misri Ibrahim Mahlab na Rais Mstaafu wa Kenya Mwai Kibaki.
 
Katika maadhimisho yao pia kulikuwa na maonyesho ya silaha mbali mbali za kivita zikiwemo ndege za kivita pamoja na za kiraia.
 
Hata hivyo kilichovutia  ni kikosi cha makomandoo wa jeshi la Tanzania ambao walionyesha umahiri wao kupambana na adui bila kutumia silaha na kuvunja vitu vigumu kwa kutumia kichwa  na mikono.
 
Onyesho jingine lililotia fora zaidi ni askari wa miamvuli ambao waliruka kutoka kwenye ndege umbali wa futi elfu arobaini  kutoka usawa wa bahari kwa kutumia miavuli na kutua katikati ya uwanja wa sherehe.
0L7C0250 888b4


source: mjengwa blog

UKAWA wamjibu Kikwete

ukawa5 eeb08
Na Hudugu Ng'amilo
SIKU moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kuwataka wajumbe wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) warudi bungeni akidai hawana sababu ya kwenda kushitaki kwa wananchi kwa sababu watawacheka na kuwasikitikia, umoja huo umemjibu wakisema wapo tayari kuchekwa.
Akihutubia vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) juzi, siku moja kabla ya sherehe za miaka 50 ya muungano, Rais Kikwete alisema kuwa huko nje wanakotaka kwenda UKAWA siko na siku yake sio sasa, hivyo akawaomba wasipoteze fursa hiyo muhimu ya kutoa mawazo yao bungeni ili yafanyiwe kazi.
Alisema wananchi hawahusiki wala hawana namna ya kuwasaidia kwani mengi ya hayo yanayowakasirisha ni matatizo waliyoyazusha wao.
Mwenyekiti wa UKAWA, Freeman Mbowe, aliliambia Tanzania Daima Jumapili kuwa
kama Kikwete anafikiri kwamba watarudi bungeni kwenye mijadala ya dharau, ubaguzi na matusi inayofanywa na wajumbe wa CCM, basi hajui chimbuko la tatizo.
"Kadiri anavyoendelea kuliacha Bunge liendelee na mijadala ya kibaguzi na matusi, taifa linazidi kupasuka na washauri wake hawamwelezi tatizo hilo," alisema.
Mbowe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), alisema kuwa Rais Kikwete asipokuwa makini atalitumbukiza taifa kwenye machafuko ingawa yeye anafanya utani kwa kuipasua nchi na kushangilia kauli za kibaguzi, kejeli na matusi zinazotolewa na baadhi ya wajumbe wa CCM.
"Rais na wasaidizi wake inaelekea hawajasikiliza hata kauli zinazotolewa na viongozi wa dini kuhusu rasimu ya Warioba, atuache twende kwa wananchi, wao ndio wataamua. Tumevumilia kwa kiwango fulani, lakini itafika mahali uvumilivu utaisha, kwani hatuwezi kuendelea kuzuiliwa kufanya mikutano na jeshi la polisi wakati mikutano ya CCM inafanyika kote nchini kutuchafua," alisema Mbowe. 
CHANZO: TANZANIA DAIMA/ mjengwa blog

Wastaafu wamteka JK

wastaafu 13cf0
Na Hudugu Ng'amilo
RAIS Jakaya Kikwete amehujumiwa na viongozi wakuu wastaafu waliomlazimisha kuachana na msimamo wa muundo wa muungano wa serikali tatu na kukumbatia serikali mbili zilizopendekezwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Taarifa kutoka kwa baadhi ya vyanzo vya habari vilivyo karibu na rais, Ikulu na makao makuu ya CCM, zimelithibitishia  kwamba hadi Bunge Maalumu la Katiba linaanza, Rais Kikwete alikuwa na msimamo ule ule wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Baadhi ya viongozi wastaafu, wakiwamo marais na viongozi waandamizi wa CCM, walishinikiza rais aachane na serikali tatu, kwa vitisho kwamba zitaua muungano.
Baadhi ya wastaafu hao walimficha Rais Kikwete kwamba kwa kuwa yeye aliingia madarakani akiwa rais wa muungano wa serikali mbili, halikuwa jambo la busara kwake kujiingiza kwenye historia ya kuwa rais aliyevunja muungano.
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu, shinikizo hilo liliambatana na jingine la kumtaka asizindue Bunge kabla ya rasimu ya pili ya katiba mpya kuwasilishwa bungeni, ili apate fursa ya kudhoofisha hoja ya serikali tatu.
Mara baada ya Rais Kikwete kukubaliana na "washauri wake", serikali ililazimika kuingilia kati ili Mwenyekiti wa Bunge, Samuel Sitta atengue kanuni, Mwenyekiti wa Tume, Jaji Joseph Warioba awasilishe rasimu kabla ya rais kuzindua Bunge, jambo ambalo limesababisha mvurugano unaotishia kuvuruga kabisa mchakato wa katiba mpya.
Hata hivyo, hali hiyo inasemekana kumnyima amani Rais Kikwete ambaye ndiye aliyepokea na kusaini rasimu hiyo, kwa maana kwamba aliridhia.
Uamuzi huo umefanya rais aonekane kiongozi asiye na msimamo thabiti katika masuala muhimu.
Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanadai hatua hii imemfanya ashindwe kuacha urithi makini na muhimu katika utawala wake wa miaka 10, kama ambavyo alikuwa amedhamiria.
Wadadisi wanasema wastaafu walimzuia rais kutekeleza azima yake kwa sababu ya hofu tu, wakidhani kwamba katiba mpya yenye mfumo mpya inaweza kufumua mambo yaliyofichika na kuwaingiza matatani.
Wanadai kwamba muungano wenye mfumo mpya una kila dalili za kuiondoa CCM madarakani, na kuhatarisha maslahi ya watawala waliopo na waliopita.
Hoja hii, kwa mujibu wa vyanzo vyetu, ndiyo ilimkuna Rais Kikwete hata akabadili msimamo.
Kwa hali halisi ilivyo, na mchakato unavyoendelea, ahadi ya Rais Kikwete kuwapa Watanzania katiba mpya mwezi huu imeshindikana.
Alipohutubia taifa na kutangaza kuanzisha mchakato wa katiba mpya miaka mitatu iliyopita, alisema kwamba lengo lake lilikuwa kuzindua katiba mpya katika maadhimisho ya sherehe za miaka 50 ya muungano iliyofanyika jana.
Hadi Bunge Maalumu la Katiba linaahirishwa juzi, zilikuwa zimepita siku 68 kati ya 70 zilizotengwa kwa ajili ya Bunge hilo, huku kukiwapo mgawanyiko mkubwa wa wajumbe na kutishia uhai wa muungano, hasa baada ya wajumbe wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kususia Bunge baada ya kukerwa na hujuma na matusi kutoka kwa wajumbe wenzao wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Hadi sasa Bunge la Katiba limefanikiwa kujadili sura mbili za rasimu bila ya kuzipigia kura. CCM imekataa maoni ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba yanayopendekeza mfumo wa muungano wa serikali tatu, wakatetea mfumo wa serikali mbili.
Mapendekezo hayo ni kinyume kabisa cha yaliyomo kwenye rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyowasilishwa ili ijadiliwe na wajumbe hao na kisha kutunga katiba mpya.
UKAWA wanadai kuchoshwa na vitisho na matusi kutoka kwa wajumbe wa CCM na viongozi wa serikali, wakisema kuwa kwa hali ilivyo katiba bora ya wananchi haiwezi kupatikana kwa shinikizo la muundo wa serikali mbili.
Katika hili, Rais Kikwete analalamikiwa kuwa ndiye mvurugaji wa kwanza wa mchakato ambao aliuasisi na kuahidi kuwapatia wananchi katiba bora kabla ya kuondoka madarakani.
Wakati akilihutubia Bunge la Katiba na kulizindua rasmi Machi mwaka huu, Rais Kikwete aliibeza rasimu ya Tume ya Jaji Warioba, akisema takwimu zao kuhusu watu waliotoa maoni ya muundo wa muungano zinatiliwa shaka.
Alisema kuwa muundo wa serikali tatu unaopendekezwa hautekelezeki kwani rais wa dola hiyo hatakuwa na mamlaka kwa vile hana ardhi, rasilimali na hivyo hataweza kukopa.
Kwa mujibu wa Rais Kikwete, katika hali kama hiyo, jeshi linaweza kupindua serikali na hivyo ukawa mwanzo wa kuvunjika kwa muungano, huku akisisitiza kwamba wao kama CCM muundo ambao unaweza kutatua kero zilizopo ni ule wa sasa wa serikali mbili.
Kauli hiyo ya rais iliibua mjadala mkubwa, na hivyo kufifisha ndoto za kupatikana kwa katiba bora kwani ilionyesha wazi kwamba mapendekezo ya wananchi ya serikali tatu yaliyomo kwenye rasimu hayatazingatiwa.
Hali hiyo imeendelea kujitokeza kwenye Bunge Maalumu la Katiba baada ya wajumbe wote wa CCM kuendeleza msimamo wa rais wa serikali mbili na kumshambulia Jaji Warioba binafsi kwa matusi mazito wakidai ana ajenda ya kuvunja muungano kwa kupendekeza serikali tatu.
Hatua ya Rais Kikwete kubadilika na kuvuruga mchakato aliyouasisi na kuusimamia kwa mafanikio makubwa, imeelezwa kusababishwa na mambo makubwa mawili, likiwemo hilo la kuburuzwa na viongozi wastaafu.
Duru nyingine za kisiasa katika suala hilo la kukwama kwa mchakato wa katiba, zinahusisha na rasilimali ya gesi na mafuta zilizopatikana nchini, ambapo inadaiwa mataifa makubwa yanayotaka kuwekeza ndiyo yanaishinikiza serikali isibadili muundo wa muungano uliopo.
Vyanzo vyetu vya habari vinaeleza kwamba mataifa hayo tayari yameweka msimamo wa kuisaidia CCM kifedha ili kuhakikisha inapigana kufa au kupona kutobadili muundo wa muungano katika katiba mpya.
Inaelezwa kuwa muundo wa shirikisho la serikali tatu unaopendekezwa kwenye rasimu ya katiba mpya, unatoa fursa ya wazi kwa wananchi wa serikali washirika kusimamia rasilimali zao tofauti na ilivyo katika muundo wa sasa ambapo mambo mengi yamefanywa siri na serikali.
Hadi sasa majaliwa ya kupatikana kwa katiba mpya yametoweka baada ya UKAWA kujiondoa, na hivyo kulifanya Bunge la Katiba kushindwa kufanya maamuzi ya kupitisha ibara na sura za rasimu kutokana na theluthi mbili ya wajumbe kutoka Zanzibar kushindikana.
Chanzo Tanzania Daima./ mjengwa blog

Tsvangirai asimamishwa uongozi MDC



Chama cha upinzani nchini Zimbabwe cha Movement for Democratic Change MDC kimesema kimemsimamisha kiongozi wake Morgan Tsvangirai kwa kukiuka kanuni za kidemokrasia.

Taarifa hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa MDC Tendai Biti kufuatia mkutano wa chama hicho uliofanyika katika mji Mkuu Harare.

Tangu mwaka 2009 hadi 2013 Bwana Tsvangirai alitumikia taifa la Zimbabwe katika nafasi ya Waziri Mkuu katika serikali ya umoja wa kitaifa iliyoundwa kwa pamoja na Rais wa sasa Robert Mugabe.
Serikali ya Umoja wa Kitaifa ilifikia kikomo mwezi julai mwaka 2013 baada ya Rais Mugabe kushinda kwa wingi wa kura katika uchaguzi wa rais na Tsvangirai kususia uchaguzi kwa madai ya udanganyifu. (J M)
Kushindwa kwake kulipunguza nguvu yake kama kiongozi ambaye alikuwa mshindani mkuu wa Rais Mugabe.

Waangalizi wanasema ndani ya MDC kumekuwa na mgogoro wa kiuongozi kwa miezi kadhaa.

Viongozi wengine wa ngazi za juu wameripotiwa kusimamishwa katika mkutano huo uliofanyika siku ya jumamosi na wanachama wengine wa chama hicho watachukua nafasi zao.

source: mjengwa

Papa wawili watangazwa watakatifu


Papa Francis, kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani
Umati mkubwa wa watu wamekusanyika mjini Vatican kushuhudia tukio la kihistoria ambapo viongozi wawili wa zamani wa Kanisa Katoliki, Papa John Paul II na Papa John XXIII wametangazwa watakatifu.

Ibada iliyoendeshwa kwa pamoja kati ya Papa Francis na mtangulizi wake Papa Benedict XVI imeangaliwa na karibu mahujaji milioni moja na wengine mamilioni ya watu kupitia matangazo ya televisheni na redio.

Karibu ujumbe wa wageni 100 wamehudhuria sherehe hiyo, wakiwemo kutoka koo za kifalme na wakuu wa nchi na serikali.

Hii ni mara ya kwanza kwa papa wawili kutangazwa kwa wakati mmoja kuwa watakatifu.

Waandishi wa habari wanasema hatua hii inachukuliwa kama njia ya kuziunganisha kambi mbili za wapenda mageuzi na wasiotaka mabadiliko ya sheria katika Kanisa Katoliki.(P.T)

source: mjengwa blog