WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Monday, March 31, 2014

Yanga, Simba aibu yetu, aibu yao...

Mshambuliaji wa Simba, Amis Tambwe (kushoto) akiwania mpira na beki wa Azam, Aggrey Morris wakati wa mechi ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Azam ilishinda 2-1.
Dar es Salaam. Azam imezidi kunyemelea ubingwa wa Ligi Kuu msimu huu baada ya kuichapa Simba 2-1, huku mabingwa watetezi Yanga wakichapwa 2-1 na wachezaji 10 wa Mgambo Shooting kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
Mabao ya Hamisi Mcha na John Bocco yalitosha kuipa Azam pointi tatu muhimu na kuongoza ligi kwa pointi 53, huku beki Joseph Owino akifunga bao la kufutia machozi kwa Simba.
Nayo Mgambo wakicheza zaidi ya dakika 60 wakiwa pungufu waliwaduwaza Yanga kwa kuwachapa 2-1. Mgambo walikuwa pungufu baada ya beki wao Mohamed Netto kutolewa kwa kadi nyekundu katika dakika ya 30 na mwamuzi Alex Mahaji aliyehisi mchezaji huyo amevaa hirizi katika nguo yake ya ndani, lakini alipokaguliwa haikuonekana. Mabao ya Mgambo yalifungwa na Fully Maganga na Malima Busungu.
Wakati Yanga wakisuasusa na pointi 46, Mbeya City imejiimarisha katika nafasi ya tatu kwa kufikisha pointi 45, baada ya kuwafunga ndugu zao Prisons kwa bao 1-0.
Katika Uwanja wa Taifa; Mcha aliwainua mashabiki wa Azam dakika ya 16 akiunganisha krosi kutoka upande wa kushoto baada ya wachezaji wa Simba, Donald Musoti na Amis Tambwe kugongana walipokuwa wakijaribu kumzuia Tchetche na kutoa mwanya kwa mfungaji kupiga shuti lililomwacha kipa Mapunda asijue la kufanya.
Simba walisawazisha bao hilo dakika ya 45 baada ya mpira wa adhabu uliopigwa na William Lucian kutua kichwani kwa Joseph Owino na kuifungia Simba bao hivyo timu hizo kwenda mapumziko zikiwa 1-1 huku mashabiki wa Yanga waliojitokeza uwanjani wakiishangilia Simba kwa nguvu.
Kipindi cha pili, Azam walimtoa Mcha na kumwingiza Kelvin Friday dakika ya 52, mabadiliko yaliyokuwa na faida kubwa kwao kwani dakika mbili baadaye Bocco aliifungia bao la pili akiunganisha mpira uliopigwa na Tchetche na kugonga mwamba na kurudi uwanjani.
Mjini Tanga mshambuliaji Fully Maganga aliifungia Mgambo Shooting bao la kuongoza dakika ya kwanza kwa kichwa akiunganisha mpira uliokuwa umepigwa na kipa Juma Kaseja kwenda kwa Kelvin Yondani.
Hata hivyo, katika mechi hiyo, Mgambo walipata pigo baada ya Mohamed Netto kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 30 na mwamuzi Alex Mahaji aliyehisi mchezaji huyo amevaa hirizi katika nguo yake ya ndani, lakini haikuonekana.
Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub aliifungia timu yake bao la kusawazisha kwa mkwaju wa penalti dakika ya 51 baada ya beki wa Mgambo, Novart Lufunga kumchezea vibaya mshambuliaji wa Yanga kwenye eneo la hatari. Hii ni mara ya tatu kwa Yanga kushindwa kupata ushindi inapocheza dhidi ya timu pungufu, walitoka 0-0 na Mtibwa na sare 1-1 na Azam. Busungu aliipatia Mgambo bao la pili kwa mkwaju wa penalti dakika ya 66 baada ya Kelvin Yondani kumwangusha kwenye eneo la hatari.
Katika Uwanja wa Sokoine Mbeya mshambuliaji  Paul Nonga aliipatia Mbeya City bao la kuongoza dakika ya pili baada ya kuwazidi mbio mabeki wote wa Prisons na kufunga bao hilo lililoamsha shangwe.
Morogoro; Katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Manungu, wenyeji Mtibwa  Sugar walienda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 3-1, shukrani kwa mabao ya Jamal Mnyate dakika ya 14,  Mussa Hassan Mgosi (30), na Mohamed Mkopi (81), huku Behewa Behewa akiifungia Coastal Union dakika ya 16
Imeandaliwa na Sosthenes Nyoni (Dar), Yakubu Burhani (Tanga) Godfrey Kahango (Mbeya), Juma Mtanda (Morogoro).

source: Mjengwa blog 

Sitta ampa barua Mtikila aende kwa JK


Mwenyekiti wa Bunge la Katiba,Samuel Sitta.PICHA|MAKTABA 

Dodoma. Ombi la Mjumbe wa Bunge la Katiba, Mchungaji Christopher la kutaka Bunge hilo livunjwe, limekuwa zito kwa Mwenyekiti Samuel Sitta.
Kutokana na ugumu huo, Sitta amelazimika kumpatia barua Mtikila ili awasilishe hoja yake kwa Rais Jakaya Kikwete, ambaye kisheria ana mamlaka hayo ya kuvunja Bunge la Katiba, ambalo limekuwa likionekana kwenda mrama.
Mtikila, ambaye ni mwenyekiti wa Chama cha Kidemokrasia na mjumbe wa Bunge la Katiba aliwasilisha barua yenye hoja binafsi akitaka bunge hilo livunjwe na wajumbe warejee makwao kwa madai kuwa chombo hicho cha kutunga Katiba mpya hakijali maslahi ya umma na uongozi umekuwa haumtendei haki.
Majibu ya barua hiyo yalikuwa hivi: “Nimeagizwa na Mwenyekiti wa Bunge Maalumu nikujulishe kwamba Bunge Maalumu halina uwezo wala mamlaka ya kujitangaza kwamba ni haramu na hivyo livunjwe ; na kwamba hoja hiyo haistahili kuwa hoja ya Bunge Maalumu,” inasomeka barua hiyo iliyoandikwa na katibu wa Bunge hilo, Yahya Khamis Hamad.
Akizungumza na Mwananchi jana, Sitta alikiri kumpatia barua hiyo Mtikila ili aende kwa Rais Kikwete kwa sababu hoja yake kutaka kuvunjwa Bunge haiwezi kusikilizwa na chombo hicho kwa kuwa mwenye madaraka ya kuvunja Bunge ni Rais pekee.
“Ni kweli ametuletea hoja ya kuvunja Bunge. Ameandika mambo mengi, akitumia lugha ya uchochezi, kama kudai kwamba ‘Tanganyika imekuwa koloni la Zanzibar kwa muda mrefu’, lugha ya namna hii hatuwezi kuikubali,” alisema Sitta.
Sitta alisema siyo kila kitu ambacho mjumbe anasema, ni lazima kifuatwe katika mchakato huu wa kuandika Katiba Mpya.
“Mtu akija anasema anataka Bunge livunjwe amfuate aliyetuteua, siyo sisi wenyewe kujivunja,” alisema Sitta.
Alisema hoja ya Mtikila, ambaye alitishia kufungua kesi ya kuzuia Bunge la Katiba kufanya kazi, ya kutaka Bunge kuvunjwa imekwenda kinyume kabisa na taratibu za Bunge.
“Hoja hii imekwenda nyuzi 180 kwa sababu aliyetuteua alitaka sisi tutunge katiba kutokana na rasimu, ili sisi tupeleke kwa wananchi rasimu iliyopendekezwa,” alisema.
Mchungaji Mtikila alikiri kupokea barua kutoka Ofisi ya Bunge ikimweleza jambo moja; apeleke hoja yake kwa Rais Kikwete aliyeteua Bunge la Katiba.
Hata hivyo, alisema hakusudii kwenda kumuona Rais Kikwete baada ya kushauriwa kupitia barua ya Bunge kutokana na kutoa hoja ya kutaka kuvunjwa kwa bunge hilo.

“Sitakwenda kumuona Kikwete, bali ninajua kwamba tukishindwa kuipata Tanganyika kwenye Bunge hili nitakwenda mahakama za kimataifa,” alisema Mtikila ambaye amekuwa akihubiri Utanganyika tangu nchi ilipoingia kwenye siasa za vyama vingi mwanzoni mwa miaka ya tisini.
Alisema kwa sasa anasubiri kumaliza majadiliano juu ya sura ya kwanza na ya sita ya rasimu ya katiba kuona mwelekeo na suala la muundo wa Muungano kuwa wa serikali tatu litakwamishwa, ataondoka Dodoma na kurejea Dar es Salaam kuandaa kesi.
Hoja kubwa katika mchakato wa kutunga Katiba mpya iko kwenye muundo wa Muungano baada ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba kuwasilisha rasimu inayoonyesha kuwa wengine wanataka muundo wa Muungano wa serikali tatu, jambo ambalo linaonekana kupingwa na wajumbe kutoka chama tawala cha CCM.
Bunge hilo linaundwa na wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, wawakilishi wa Baraza la wawakilishi wa Zanzibar na wawakilishi wa makundi mbalimbali wapatao 201 ambao walitangazwa na Rais Kikwete.
Lakini Mchungaji Mtikila anapingana na muundo wa Bunge la Katiba.
“Nitakwenda mahakamani kupinga sheria yote ya Mabadiliko ya Katiba kwani waliopaswa kushiriki Bunge la Katiba ni wajumbe waliochaguliwa na wananchi kwa ajili ya Bunge la Katiba, na siyo hawa wabunge na wengine wa kuteuliwa,” alisema.
Hoja ya Mtikila
Pamoja na mambo mengine katika hoja yake, Mtikila analalamika kuwa amezuiwa kuchangia katika Bunge hilo baada ya kuandikiwa barua na Ofisi ya Bunge.
Hata hivyo, katibu wa Bunge la Katiba, Yahya Khamis Hamad alisema: “Hili kwangu ni jipya na sidhani kuwa linawezekana.”
Mtikila alisisitiza kuwa alipewa barua hiyo Jumatano iliyopita ikiwa ni majibu ya barua yake aliyoiandika kwa ofisi hiyo wiki iliyopita.
“Nilianza kuhisi baada ya kuona ninanyimwa kuchangia; nikaandika barua kuomba maelezo kwa nini ninakosa nafasi ya kuchangia bungeni,” alisema na kuongeza:
“Lakini juzi nilipokea barua kutoka kwa katibu wa Bunge ikinikataza kuchangia tena bungeni kutokana na kauli zangu za kukosoa mchakato.”

Alisema kuwa alipomuuliza katibu sababu za uamuzi za kukatazwa kuchangia, alijibiwa kuwa ni maagizo kutoka kwa mwenyekiti wa Bunge la Katiba, Samuel Sitta.
“Hii imeniathiri sana mimi. Bunge hili limepotoka kwa kuwa wanachoangalia ni maslahi yao na si ya nchi,” alisema.
Alisema mchakato wote umekosewa kwa kuwaweka wabunge na wawakilishi kuwa sehemu ya Bunge badala ya wananchi kuchagua wajumbe wa Bunge.
“Hakuna nchi yoyote ambayo imefanya hivyo. Wanaharibu mabilioni ya fedha ambayo hayataleta Katiba yenye uhalali wowote,” alisema.
Alisema endapo Sitta atashindwa kutatua jambo hilo, anakusudia kuunganisha katika ushahidi wake kwenye kesi inayopinga mchakato wa Katiba.

source: mwananchi

Warioba amshukia Prof Shivji


Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba akisisitiza jambo alipokuwa akizungumza na waandishi wa gazeti hili, nyumbani kwake jijini Dar es Salaam jana. Picha na Edwin Mjwahuzi
Dar es Salaam. Mjadala wa Mabadiliko ya Katiba jana ulihamia nje ya Bunge wakati Jaji Joseph Warioba alipomchambua mhadhiri maarufu nchini, Profesa Issa Shivji akimueleza kuwa si mkweli bali mpotoshaji wa Rasimu ya Katiba.
Jaji Warioba, ambaye ni mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, pia amemtuhumu Profesa Shivji kuwa ndiye mwanzilishi wa chokochoko za Zanzibar za kudai serikali tatu, jambo ambalo sasa analigeuka kutokana na kuona hali imekuwa mbaya.
Kauli ya Warioba imekuja baada ya Profesa Shivji kuichambua Rasimu ya Katiba jana asubuhi kwenye Kongamano la Vijana lililoandaliwa na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo lililokuwa na dhima ya Vijana Katika Kuimarisha na Kuendeleza Muungano Baada ya Miaka 50. Tamasha hilo lilifanyika kwenye hoteli ya Blue Pearl, Ubungo Plaza jijini Dar es salaam.
Akiwasilisha mada kwenye kongamano hilo, Profesa Shivji alisema katika kujadili Muungano, wananchi hawana budi kuzingatia mambo mawili ambayo ni nchi zinazozungumziwa kwenye Rasimu kuwa ni Zanzibar, Tanganyika au Tanzania, ambayo alisema haina mamlaka katika pande hizo mbili za Muungano.
Pia alisema suala la maadili kwa viongozi halina budi kuangalia kuwa linazungumzia maadili ya viongozi wa Zanzibar, Tanganyika au Tanzania na kwamba rasimu inazungumzia viongozi wa Tanzania ambao hawana mamlaka kwa Tanganyika na Zanzibar.
Katika majumuisho yake, Profesa Shivji, ambaye aliikosoa Rasimu kuwa haiwakilishi matakwa ya Watanzania kwa kuangalia sampuli zilizotumika, alisema kwamba wajumbe wa Tume ya Jaji Warioba walikuwa na nia njema.
Lakini Shivji akaenda mbali zaidi kwa kusema "the road to hell is paved in good intention," akimaanisha kuwa njia ya kuzimu imetengenezwa kwa nia njema.
Akijibu hoja hizo, Jaji Warioba alisema Profesa Shivji amegeuka maandishi yake yaliyokuwa yanachochea utaifa wa Zanzibar na sasa anaona Tanganyika ndiyo hatari kwa Muungano.
"Shivji ni msomi na mimi najua anaelewa matumizi ya takwimu," alisema Jaji Warioba, ambaye aliwahi kuwa Waziri Mkuu na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, wakati alipozungumza na gazeti hili nyumbani kwake jana jioni.
"Nasema hapa, Shivji akiwa msomi, amekuwa intellectually dishonest (si mkweli kiusomi). Anapotosha kwa makusudi."
Jaji warioba alisema Shivji ndiye amekuwa chanzo cha uchochezi wa kitaifa Zanzibar kupitia maandishi yake. Alisema waliokuwa wanadai serikali tatu kwa muda mrefu walikuwa wananchi wa Zanzibar.
"Shivji alikuwa anasema Tanganyika imejificha kwenye Muungano ili inufaike. Kwa hiyo anasema Tanganyika iwe wazi isijifiche," alisema Jaji Warioba. "Na Shivji amechochea hilo... wote wale waliokuwa wanamnukuu walikuwa wanatoa hayo kwenye maandishi yake na kwamba mpaka leo hii kuna watu wa Zanzibar wanaamini Muungano huu si halali kisheria kutokana na Shivji ambaye alisema Baraza la Mapinduzi halikuridhia articles (ibara) za Muungano."
Alipoulizwa jana usiku kuhusu tuhuma hizo za uchochezi na chanzo cha hisia za utaifa wa Uzanzibari na Utanganyika, Profesa Shivji alisema hawezi kujibu tuhuma hizo kwa kuwa hajamsikia Jaji Warioba akizungumzia hilo.
"Hey, amezungumza lini?" alihoji. "Siwezi kujibu kwa kuwa sijamsikiliza mwenyewe."
Lakini Jaji Warioba alisema watu walitumia msingi huo kudai utaifa wa Zanzibar na kusisitiza kuwa Shivji amesababisha hisia za utaifa na kwamba haya yanayoendelea sasa yanatokana uchochezi huo.
"Hata kabla ya sisi kuanza mchakato huu, Shivji alikwenda Zanzibar akazungumza na Baraza la Wawakilishi na akawaambia issue kwa Zanzibar ni self determination (kujitambua), Sasa leo anaona kama hatari ni Tanganyika, lakini yeye ndio amechochea nationalism (utaifa)," alisema Jaji Warioba.
Kuhusu takwimu, Jaji Warioba alisema mara ya kwanza Profesa Shivji alizungumzia takwimu za Zanzibar kuhusu muundo wa Muungano akisema kuwa waliozungumzia suala hilo walikuwa 47,000, huku watu 27,000 wakitoka Tanzania Bara na 19,000 kutoka Zanzibar.
"Safari hii ametaja zile za Tanzania Bara na kusema hiyo ni figure (namba) ndogo sana ukilinganisha na watu 300,000 waliotoa maoni," alisema Warioba.
Alisema Tume ilitumia takwimu zinatokana na watu waliozungumzia suala ambalo wameliwekea asilimia na si kwa ujumla na ndio maana anaona Profesa Shivji anataka kupotosha kwa makusudi.
Warioba alimuelezea Profesa Shivji kuwa sasa ameamua kueneza propaganda za serikali mbili kwa kuponda Rasimu ya Katiba ambayo inaonyesha kuwa muundo wa serikali tatu ndio unaoifaa Tanzani kwa sasa.
Aidha, Warioba alisema msimamo wa Profesa Shivji ni kwamba Zanzibar haikukosea kubadilisha Katiba mwaka 2010.
" Nimeshangazwa na Shivji kusema kwamba kitendo cha Zanzibar kubadili Katiba yao kuwa 'Zanzibar ni Nchi' halikuwa jambo la ajabu," alisema Warioba.
Alisema Shivji ni msomi ambaye anafahamu kitendo cha kubadilisha Katiba kilikuwa na madhara makubwa katika muundo wa Muungano.
"Nadhani mnakumbuka Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alipoulizwa Bungeni kama Zanzibar ni nchi au siyo nchi, alijibu kuwa Zanzibar siyo nchi, vurugu zake mnakumbuka," alisema.
Alisema lakini msomi kama Shivji haoni kama suala hilo la 'Zanzibar ni nchi' lina madhara makubwa katika mstakabali wa taifa letu.
Jaji Warioba alisema kama serikali tatu hazitakiwi, basi kinachotakiwa kufanywa ni kwa Zanzibar kubadili Katiba yake ili iseme kwamba Zanzibar ni sehemu ya Muungano, vinginevyo haiwezekani.
"Maana kama ni kusahihisha, ni lazima kwanza Katiba ya Zanzibar itumie maneno yale yale yaliyo kwenye Katiba ya Muungano. Yaani Zanzibar iwe sehemu ya nchi. Zanzibar wakubali hilo," alisema.
"Zanzibar wakubali Rais wa Muungano ana madaraka nchi nzima maana mabadiliko ya 2010 yamemuondolea Rais wa Jamhuri ya Muungano madaraka yake."
Akitoa mfano wa mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka, Jaji Warioba alisema amekuwa akidai takwimu hazionyeshi uhalisia wa maoni ya wananchi.
"Kwa mfano, Jimbo la Simanjiro linakuwa na watu 100,000 lakini waliojiandikisha kupiga kura ni watu 20,000 na waliopiga kura ni watu 15,000. Hii ina maana ushindi wake utakuwa katika watu waliopiga kura na siyo idadi ya watu wa Simanjiro," alisema Warioba.
Chanzo, mwananchi

DARAJA LA RUVU LAFUNGWA, MAMIA YA WATU WAVUSHWA KWA KULIPIA FEDHA

DARAJA LA RUVU LAFUNGWA, MKUU WA WILAYA YA BAGAMOYO AWAPIGA 'STOP' WAKAZI WA KIWANGWA KWENDA BAGAMOYO


Wakazi wa Kiwangwa, wakivushwa na vijana waliojitolea kujipatia ajira katika Daraja la Ruvu kwa kuwavusha wananchi kwa kuwabea ama kuwaongoza njia ili kuvuka eneo hilo la daraja lililojaa maji kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha nchini. Vijana hao wakiwavusha raia katika eneo hilo kwa ujila wa Sh. 2000 kwa kila aliyebebwa mgongoni asiyetaka kuvua viatu ama kugusa maji hayo, na Sh. 500 kwa kushikwa mkono kuongozwa njia kutoka mwanzo wa maji hayo hadi kuyavuka, na kuyaongoza magari kuvuka eneo hilo ni Sh. 3000 hadi 5000.
Kutokana na mvua kubwa iliyonyesha jana, Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Ahmed Kipozi, alifika eneo hilo na kujionea wananchi wakitaabika kuvuka ene hilo na huku magari ya abiria yaliyokuwa yakitokea Bagamoyo kwenda Kiwangwa, yakibeba abiria na kuishia eneo hilo na kubeba wengine walioshushwa upande wa pili na kugeuza kwa kila abiria kulipa Sh. 1000. Na kisha abiria hao wakipata usafiri mwingine wa kubebwa na Vijana waliopo eneo hilo kwa Sh. 2000 kwa aliyependa ama 500 kwa kuongozwa njia.

Vijana hao wakiliongoza moja ya gari lililokuwa likivuka eneo hilo ambapo dereva anafuata njia wanayopita vijana hao wa kulia na kushoto hadi kuvuka ili kuoepuka kupita eneo hatarishi na kutumbukia ama kusukumwa na maji hayo yaliyokuwa yakionekana kuwa na nguvu kubwa.

Mkuu wa Wilaya ya bagamoyo, Ahmed Kipozi, akizungumza na watendaji wake aliowaagiza kusimamia zoezi la kuwazuia wananchi kuvuka eneo hilo, ambapo watendaji hao walimueleza Mkuu huyo wa Wilaya kuwa wananchi wamekuwa wakaidi na kuamua kukataa kutii amri na kuvuka, jambo lililomfanya Mkuu wa wilaya kuamua kuagiza askari Polisi wenye silaha ili kulinda eneo hilo kuwazuia waanchi kuvuka ili kuepuka maafa.

''WA HUKU WA HUKU NA WA HUKO WA HUKO''
Baada ya hapo Mkuu huyo wa Wilaya aliwatoa tamko na kuwataka wakazi wa Kiwangwa kutokwenda Bagamoyo na waBagamoyo kutokwenda Kiwangwa, kwa kipindi chote cha mvua ili kuepuka maafa yanayoweza kutokea kwa kutumbukia na kusombwa na maji, ama daraja hilo la Jeshi kukatika kutokana na maji kuanza kupita juu ya daraja hilo jana.

Mkuu wa Wilaya, akizungumza na madereva wa magari waliokuwa wakisubiri kuvuka eneo hilo pamoja na vijana waliokuwa wakitoa huduma ya kuwavusha watu.

Vijana wakifanya kazi yao ya kuwavusha watu eneo hilo.

Baadhi ya magari yaliyokaidi amri yakivuka eneo hilo.

Vijana hao waliwavusha hadi wagonjwa katika eneo hilo kama anavyoonekana pichani akiwa amembeba mtu mzima anayeonekana kuwa ni mgonjwa.

Baadhi ya vijana walijiona kama wapo Beach, walikuwa wakipiga mbizi na kuogelea eneo hilo kwa furaha.


Magari yakiwa katika foleni kusubiri kuvuka eneo hilo.

Baadhi ya abiria walioshushwa upande wa pili wakiwania usafiri wa kuelekea Bagamoyo baada ya kufaulishwa na gari jingine la uapnde wa pili.

Hawa nao ni wa upande wa pili

Gari la Abbas Tarimba likivuka eneo hilo.

Vijana wakijipigia debe kwa dereva ili akibali kuvushwa, bila kujua kuwa ndani yake alikuwapo Mkuu wa Wilaya hiyo.

Katapila lililoletwa ili kuziba eneo hilo kuzuia magari kuvuka.


Haya ni baadhi ya madaraja ya barabara mpya inayojengwa yakiwa yamejaa maji.

Dereva wa pikipiki akipakia gunia la mkaa vizuri ili awapakie na abiria wake wawili baada ya kuvuka darajani hapo.

Haya ni baadhi ya maeneo hayo yaliyojaa maji, ambapo mmoja wa vijana hao anaonekana akipiga mbizi kwa furaha.


Pembeni (kulia) ni mtumbwi unaotumiwa na wakazi wa eneo hili kuvuka kuelekea upande wa pili.

Chanzo Sufiani Mafoto.com

Waumini Uganda wamshukuru Museveni


msv_34aaf.jpg
Rais wa Uganda, Yower Museven.
Raia wa Uganda kutoka dini mbali mbali hii leo wamekusanyika katika uwanja wa Kololo mjini Kampala kwa maombi maalum na kutoa shukurani kwa Rais Yoweri Museveni kwa kutia saini mswaada wa sheria unaozuia mapenzi ya jinsia moja.
Rais Museveni aliidhinisha sheria ya adhabu kali kwa Mashoga nchini Uganda mwezi Februari, kwa hatua hiyo viongozi wa dini mbalimbali wakristo na waislamu wamehimiza waumini wao kujitokeza kwa wingi katika ibaada hiyo maalum.
Hii ni mara ya kwanza viongozi wa dini mbali mbali nchini Uganda kujitokeza kwa pamoja na kuandaa Ibaada maalum ya kumshukuru Rais Museveni na kuliombea taifa kuepuka vitendo vya ushoga.
Rais Museveni aliidhinisha sheria hiyo ambayo raia wengi wa Uganda wameipigia debe sana.
Ibada hiyo maalum inafanyika uwanja wa uhuru wa Kololo mjini Kampala, baada ya karibu mwezi mmoja na nusu tangu rais Yoweri Museveni kuiidhinisha
Tangu Rais Museveni kuidhinisha sheria hiyo kumekuwa na shinikizo kubwa kutoka kwa mataifa ya Magharibi yakimtaka kubadili msimo wake, huku baadhi ya mataifa yakipunguza msaada kwa Uganda lakini raia wengi wa Uganda walimsifu Rais Museveni kwa hatua yake.
 
Chanzo, bbcswahili

DK.SHEIN AKUTANA NA MABALOZI WA ULAYA


IMG_9076
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Kiongozi wa Ujumbe wa Mabalozi wa Nchi za Jumuiya ya Ulaya nchini Filiberto CERIANI SEBREGONDI,walipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo asubuhi kwa mazungumzo ,[Picha na Ramadhan Othman Ikulu.]
IMG_9092
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na Ujumbe wa Mabalozi wa Nchi za Jumuiya ya Ulaya nchini ukiongozwa na Filiberto CERIANI SEBREGONDI,(wa pili kulia)walipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo asubuhi kwa mazungumzo.
IMG_9097
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akifuatana na Kiongozi wa Ujumbe wa Mabalozi wa Nchi za Jumuiya ya Ulaya nchini Filiberto CERIANI SEBREGONDI,baada ya mazungumzo yao Ikulu Mjini Zanzibar leo asubuhi kwa mazungumzo.
IMG_9102
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe wa Mabalozi wa Nchi za Jumuiya ya Ulaya nchini walipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo asubuhi baada ya mazungumzo yao.
 
 Chanzo, networkbloggers

Friday, March 28, 2014

Askofu wa Anglikana Dodoma afariki

Dodoma. Askofu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Dodoma, Godfrey Mdimi Mhogolo amefariki dunia akiwa kwenye matibabu nchini Afrika ya Kusini.

Katibu wa Dayosisi ya Dodoma, Luteni Mstaafu Daudi Kandila alithibitisha jana kutokea kwa kifo hicho na kusema kimeacha pengo kwa dayosisi na Kanisa la Anglikana kwa jumla.

Kandila alisema Askofu Mhogolo alifikwa na umauti katika Hospitali ya Mil Park iliyoko Afrika Kusini ambako alipelekwa Machi 19.

“Ni kweli Baba Askofu amefariki jana saa 6:00 mchana. Siwezi kuzungumzia suala hili zaidi kwani katibu mkuu wa jimbo ndiye atakayetoa taarifa kwa undani,” alisema Kandila.

Alisema mtumishi huyo alianza kuugua mapema mwezi Februari na ilipofika Machi Mosi, alipelekwa Hospitali ya African Medical ya Dar es Salaam ambako alitibiwa kwa siku 18 kabla ya kupelekwa Afrika Kusini.
Ugonjwa uliosababisha kifo chake Mhogolo haujajulikana kutokana na maelezo kuwa hadi watakapopata ripoti za madaktari juu ya nini kilikuwa kikimsumbua marehemu kabla ya uhai wake.

Mhogolo amekuwa Askofu wa Dayosisi ya Kati ya Tanganyika tangu mwaka 1999 kipindi kifupi baada ya kifo cha aliyekuwa Askofu wa Dayosisi hiyo, Marehemu Yohana Madinda. Katika uchaguzi uliomwingiza madarakani, alimshinda aliyekuwa Askofu Msaidizi wa wakati huo, Donald Mtetemela na kufanya aende kuwa Askofu wa Ruaha (Iringa).

Mhogolo pia aliwahi kuwa katibu wa dayosisi hiyo kabla ya kushika wadhifa huo na alifanya kazi ya kufundisha katika Chuo cha Theolojia cha Kongwa.
Katika uongozi wake, alifanikiwa kuigawa dayosisi yake ambapo Dayosisi za Mpwapwa na Kondoa zilianzishwa. Mpwapwa akawekwa Simon Chiwanga kuwa Askofu na Kondoa akapewa Askofu Yohana Mkavu.

Hadi mauti yanamkuta, alibakiza miezi kadhaa astaafu kwani ratiba ya kanisa inaonyesha Desemba mwaka huu ingekuwa na uchaguzi.

source: mwananchi

Loga: Azam tishio Simba kuliko Yanga

Kocha Mkuu wa timu ya Simba, Mcroatia,Zdravko Logarusic
Kocha Mkuu wa timu ya Simba, Mcroatia, Zdravko Logarusic, amesema mechi ya Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara dhidi ya Azam itakayofanyika Jumapili ni ngumu na inampa mawazo kwa kuwa anaihofia timu hiyo kuliko hata Yanga.
Logarusic alisema Azam iko katika kiwango cha juu na ushindi mfululizo wanaoupata unawaongezea hali ya kujiamini tofauti na kikosi chake ambacho kimekuwa kikipoteza mara kwa mara.

Kocha huyo alisema pia umuhimu wa pointi tatu za kuamua hatma ya ubingwa kwa wapinzani wao ndicho kinampa wasiwasi zaidi wakati wachezaji wake wanatafuta heshima.

"Ni ukweli usiofichika kwamba mechi hii ni ngumu, ninawahofia zaidi Azam kuliko Yanga," alisema Logarusic.

Alieleza kwamba amekiandaa kikosi chake kukabiliana na ushindani wa kila aina katika mchezo huo na anaamini wapinzani wao pia wamejipanga.

Aliongeza kuwa bado Simba inahitaji kushinda licha ya kutokuwa na matumaini ya kumaliza kwenye nafasi mbili za juu msimu huu unaomalizika Aprili 19.

Naye Kocha Msaidizi wa Azam, Kally Ongala, alisema kikosi chao kimejipanga kuendelea kufanya vizuri katika mechi za ligi zilizobakia ili waweze kutimiza malengo yao.

Ongala alisema wanaifahamu vyema timu ya Simba na wachezaji wake wanajua jinsi ya kuwakabili na hatimaye kupata ushindi katika mchezo wao wa Jumapili.

"Tumejipanga kufanya vizuri na kila siku tunaendelea kurekebisha makosa katika timu, lengo ni kuchukua ubingwa msimu huu," alisema kocha huyo msaidizi.

Simba itashuka dimbani Jumapili ikiwa na kumbukumbu ya kichapo cha  bao 1-0 dhidi ya Coastal Union wakati Azam wenyewe walipata ushindi wa mabao 2-0 ugenini kwenye Uwanja wa Mkwakwani kwa kuifunga JKT Mgambo.

Wekundu wa Msimbazi wana pointi 36 na Azam ndiyo vinara wa ligi wakiwa na pointi 50 wakifuatiwa na mabingwa watetezi wa ligi hiyo, Yanga wenye pointi 46 na mechi moja mkononi huku Mbeya City ikishika nafasi ya tatu kwa pointi zao 42.

Simba bado inaendelea na mazoezi yake kwenye Uwanja wa Kinesi ulioko Sinza, jijini Dar es Salaam na Azam ilirejea jana ikitokea Tanga.
 
CHANZO: NIPASHE

Mwenendo huu Bunge la Katiba haufai,unawagawa Watanzania

Katuni
Hali  iliyopo sasa kwenye vikao vinavyoendelea vya Bunge Maalum la Katiba inatia shaka. Inawaogopesha Watanzania wengi, hasa wale waliojawa na shauku ya kuona kuwa taifa linapata katiba bora kwa ajili ya kizazi cha sasa na kijacho.
Sisi ni sehemu ya Watanzania tulioingiwa na hofu kubwa juu ya kile kinachoendelea kwenye vikao vya bunge hili.

Kauli zinazotolewa ndani na nje ya Bunge hilo haziashirii mwisho mzuri. Hakika, misukosuko ndani ya Bunge hilo inaonekana kuwa mingi kiasi cha kutoa ishara mbaya juu ya ufanisi wa chombo hicho ambacho kimsingi, kina wajibu wa kupitisha rasimu ya katiba mpya kabla ya kutoa nafasi ya kupigiwa kura na wananchi.

NIPASHE tunaona kuwa hivi sasa, badala ya kutumia muda mwingi wa kuijadili na kuipitisha rasimu ya katiba, wajumbe wa Bunge hilo wamekuwa wakipigana vijembe na kubishana kwa mambo yanayozidi kuwagawa wenyewe na taifa.

Tofauti kubwa za kimtazamo baina ya wajumbe zinapata nafasi kubwa zaidi. Ni dhahiri kuwa, kama hatua zisipochukuliwa mapema katika kumaliza mabishano ya mara kwa mara, ni wazi kwamba hakutakuwa na mafanikio. Katiba bora haitapatikana na badala yake, taifa litazidi kugawanyika kutokana na misimamo ya vyama.

Kwa bahati mbaya sana, badala ya wajumbe wa Bunge la katiba kujielekeza katika masuala yatakayoleta katiba bora, wengi wao wamekuwa wakionyesha waziwazi kuwa wanapigania zaidi maslahi ya vyama vyao.

Kwa mfano, kila uchao, wajumbe wa Bunge hili wamekuwa wakipeana vijembe baina yao, vingi vikionekana kujawa na mitazamo ya kisiasa. Upo ushahidi wa kutosha vilevile kuwa wajumbe wengi wamekuwa wazuri katika kuibuliana tuhuma.

Wengi miongoni mwa wale wanaopata nafasi ya kuzungumza wamekuwa wakimwaga tuhuma. Kiti pia kinaonekana kuyumba.
Nacho kimeanza kutuhumu. Hiyo ilidhihirika juzi baada ya Mwenyekiti wa Bunge kutoa yake ya moyoni, akisema kuwa wanaoyumbisha mwenendo wa bunge hilo ni baadhi ya watu waliodhamiria kuona kuwa mchakato wa kupitisha rasimu ya katiba mpya unakwama.
Na sasa, hali ya kutuhumiana huko imefika mbali zaidi.Ni baada ya Waziri Mkuu kueleza yake, akisema kuwa kutokana na mwenendo unaoonekana sasa, anafikiria kumuomba Rais aliyeunda Bunge hilo kuliahirisha hadi wakati mwingine ili kutoa fursa kwa masuala mengine ya Kiserikali kuendelea. Waziri Mkuu alikuwa akizungumzia mkutano wa Bunge la Bajeti ambao unapaswa kuanza baada ya kumalizika kwa Bunge Maalum la Katiba.

Sisi tunaona kuwa chanzo cha mkanganyiko unaoendelea sasa kwenye Bunge la Katiba ni kimoja tu, nacho ni hali ya kutoaminiana. Wajumbe wamekuwa hawaaminiani. Matokeo yake wanaishia kutuhumiana hata kwa mambo ya wazi na yasiyohitaji kubishana.

Ushauri wetu kwa wajumbe wa Bunge la Katiba ni kuwa, wajitahidi kutanguliza utaifa na wala siyo vyama vyao. Wakumbuke kuwa Watanzania waliwapa fursa ya kwenda kwenye Bunge hilo kwa nia ya kuwaandalia katiba bora na siyo kuimarisha vyama vyao.

Wajumbe wa Bunge la Katiba wakumbuke vilevile kuwa Watanzania wanawaangalia, teknolojia ya matangazo ya moja kwa moja ya televisheni inawaonyesha wote mbele ya umma ambao bila shaka, kuna siku utawahukumu kwa kuonyesdha mapenzi zaidi kwa vyama vyao kuliko taifa. Ni vyema wakaacha kufanya mambo yasiyokubalika.

Tunawasihi wajumbe wa Bunge la Katiba kuwa, mara zote wajitahidi kufanya kazi yao kwa umakini mkubwa ili mwisho wa siku waipatie Tanzania katiba bora. Kinyume chake, itakuwa ni janga kubwa kwa taifa.

Haipendezi hata kidogo kuona mchakato wa katiba ukiharibika baada ya taifa kutumia muda mwingi kuandaa rasimu na pia kupoteza mabilioni ya fedha kugharimia mchakato huo.

Tunawakumbusha wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kuwa ni vyema kwa kila mmoja kuwa na lengo la kuona kuwa katiba mpya yenye kukidhi matakwa ya Watanzania inapatikana. Na hii ni fursa ya kihistoria inayopaswa kutumiwa vyema kwa manufaa ya taifa.

Shime, Bunge Maalum la Katiba lilete katiba bora. Siyo kuwagwa Watanzania.
 
CHANZO: NIPASHE

Kikwete: Tuwaache wabunge waamue serikali mbili au tatu


Rais Jakaya Kikwete
Rais Jakaya Kikwete amesema amemaliza  kazi ya kulihutubia Bunge Maalum la Katiba na sasa anawaachia wabunge wa bunge hilo kujadili na kuamua muundo wa Muungano unaofaa kama serikali mbili au tatu kwenye mapendekezo ya  Rasimu ya Katiba Mpya.
Rais Kikwete alielezea msimamo huo juzi wakati akizungumza na wazee  katika Ikulu ndogo ya Wilaya ya Muheza mkoani Tanga.

Rais Kikwete ambaye alikuwa katika ziara yake ya siku moja wilayani hapa, alitoa msimamo wake baada ya wazee hao kumweleza kwenye risala yao kuwa wao wanataka serikali mbili. Risala hiyo ilisomwa na   Mwenyekiti wa Wazee wa Wilaya ya Muheza, Hamisi Mzee.

Rais Kikwete alisema kwa sasa amewaachia wabunge kuamua muundo wa Muungano unaotakiwa na baadaye wananchi wataamua kama wanataka serikali tatu ama mbili wakati wa kupitisha Katiba.

Alisema kama watapendekeza serikali tatu ruksa kwani ndiyo mapendekezo yao, hivyo hayawezi kupingika kwa namna yoyote.

Hata hivyo, Rais Kikwetee alisisitiza kuwa lakini waelewe kuwa serikali tatu zina changamoto zake.
 
CHANZO: NIPASHE

Bunge machafuko

  Ni matumizi ya kura zote, wazi na siri
  Mwigulu achafua hali ya hewa
  Ezekiel Wenje awavuruga Mawaziri,Wajumbe

Mwenyekiti wa Kamati ya Kanuani na haki za Bunge Maalum la Katiba, Pandu ZAmeir Kificho (Kushoto), akiwasilisha mapendekezo ya kamati kuhusu butaratibu wa upigaji kura bungeni mjini Dodoma jana,kulia Mjumbe John Mnyika akichangia pia.(Picha na Khalfan Said)
Kitendawili cha kura ya wazi au ya siri limeemdelea kuliandama Bunge Maalum la Katiba kwa kuzua mvutano mkali jana jioni baada ya Kamati ya Kanuni na Haki za Bunge kuwasilisha azimio la kupendekeza utaratibu wa kura ya siri na ya wazi kutumika kupitisha vifungu vya Rasimu ya Katiba.
Jana jioni yalizuka malumbano baada ya Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Pandu Ameir Kificho, kuwasilisha mapendekezo ya azimio la utaratibu wa wajumbe kupiga kura kwa kutumia njia mbili za kura ya wazi na siri kwa kadri kila mjumbe atakavyoona inafaa.

Baada ya kamati hiyo kuwasilisha mapendekezo yake, baadhi ya wajumbe walitoa maoni wengine wakipendekeza kutumika kwa kura ya kielektroniki na wengine wakipinga vikali kwa madai kuwa itakuwa na uchakachuaji.

MAKONDA

Paul Makonda alipendekeza kutumika kwa kura ya kielektroniki ambayo itaokoa muda wa upigaji kura na kila mmoja kufanya kwa uhuru zaidi.

Alisema mvutano uko baina ya wajumbe waliowafuasi wa vyama vya siasa huku 201 wakiwa njiapanda.

PAMELA
Mjumbe Pamela Maasai alisema kura ya elektroniki ni rahisi kuchakachuliwa hivyo siyo vyema Bunge hilo kukubali utaratibu huo na badala yake kura ya siri ambayo itatoa uhuru kwa kila mjumbe kufanya kwa uhuru.

NASSARI
Joshua Nassari aliwataka wajumbe kuacha unafiki na kila mmoja auzungumze kama haifahamu kesho, Katiba iwe neema kwa makundi yote kwa miaka ijayo.

“Bunge moja, taifa moja, katiba moja, nchi moja halafu upigaji kura uwe tofauti, wenzetu wanatengeneza ndege zinaruka bila rubani unasema tumebuni kupiga kura kwa kila kundi kupiga watakavyo…wengi wa wabunge wa CCM wanataka serikali tatu, ila wanashindwa kusema, njia pekee ya kuwasaidia ni kura ya siri,” alisema.

Alisema uchaguzi wa viongozi mbalimbali kura ni ya siri, wajumbe wa Bunge hilo nao wameteuliwa na Rais ambaye alijifungia na kuwateua kwa siri,” alisema na kuongeza kuwa siyo ajabu kwa Bunge hilo kupiga kura ya siri.

OLUOCH
Ezekiel Oluoch alisema kura ya siri ndiyo itasaidia kuiwafanya watu kuwa huru kwa kuwa ndani ya katiba hiyo kuna masuala ya kidini yanayopaswa kuamuliwa kwa usiri.

Alisema kura ya siri inatumika kuamua mambo yenye imani na utata mkubwa kwa kuwa inamsaidia mtu kuwa huru katika kuamua.

LAIZER
Mjumbe Michael Laizer alisema Kamati hiyo imepeleka pendekezo la kutoa suluhisho la utaratibu wa upigaji kura na kama haukubaliki ni wakati wa Mwenyekiti kuwuandikia Rais avunje Bunge ili wajumbe watawanyike na kuondoka Dodoma.

MBOWE

Freeman Mbowe, alisema ni lazima wafike hatua wafanye uamuzi kuliko kuendelea kujadili huku akisema Machi 11, mwaka huu walipitisha kanuni bila kifungu cha 37 na 38 vinavyozungumzia utaratibu wa kura ya wazi na siri.

Alisema utaalamu wa kurushiana maneno na vijembe hausaidii lolote na kwamba ni dhahiri kuwa kwa mazingira ya jana hakuna utaalamu wa kufikia mwafaha kwenye ukumbi kwa kila mmoja kuzungumza kwa kadri utaalamu wake unavyomruhusu.

“Pamoja na utaalamu wetu wa kufanya maamuzi hatuwezi kuliamua suala hili, itakuwa ni aibu tutajikuta kwenye mazingira ya kulazimisha na kuvunja Bunge, hakuna atakayetakoka mshindi si aliyesababisha na ambaye hakusababishiwa,” alisema

Alishauri viongozi wenye busara kukutana na kuzungumza na kuja na uamuzi sahihi kwa kuwa jambo la Katiba ni jambo la maridhiano, hivyo ni lazima kuwe na makubaliano ya kusonga mbele.

MWANGUNGA
Shamsha Mwangunga, alisema wanaotaka kura ya siri ni wanafiki, hawajiamini na wawajui walifanyalo na kwamba ni vyema likafanyika kwa uwazi.

“Tunashindwa kupiga hatua ya mbele kwa kuvutana, hivyo ni vyema kukubali ushauri wa kamati wa kila mmoja kupiga kura anayoona inafaa,” alisema.

RAZA
Mohamed Raza, alisema kura ya wazi ndiyo inayofaa na kwamba kuendelea kulumbana ni kutumia vibaya fedha za Watanzania.

MAKAIDI
Dk. Emmanuel Makaidi alisema kura ya siri itatoa nafasi kwa kila mjumbe kuonyeshana dhamira yake pasipo woga.

“Kura ya elektroniki haifai kuamua, tukubali kura ya siri kama ndiyo msingi wa maamuzi yetu,” alisema.

LEMA
Godbless Lema alisema kura ya siri itawaingiza baadhi ya wajumbe kwenye matatizo kwa kuwa kwa sasa kuna matamko mbalimbali yamesambaa kwenye mitanda ya jamii, vitisho vingi, ikiwamo Zanzibar inasema atakayerudi bila Zanzibar huru kichwa chake kitakuwa halali yao.

Alisema Waziri Mkuu ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya wabunge wa CCM akiamua kupiga kura ya siria haamini kama yupo anayeweza kwenda kinyume cha kiongozi wake ambaye amepinga kura ya wazi.

BULAYA
Esther Bulaya alisema msimamo wake ni kura ya siri, lakini amefurahia mapendekezo ya kamati ya kila mmoja kupiga kura kwa nutaratibu anaupenda, hivyo ni vyema wajumbe hao wakakubaliana na kamati.

MWIGULU
Mwigulu Nchemba ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha, alichafua hali ya hewa baada ya kuwatuhumu Freeman Mbowe na Ismail Jussa Ladhu kuwa wanataka kura ya siri kwa kuwa wanalengo la kuingiza ushoga.

Baada ya kauli ya Nchemba, Profesa Ibrahim Lipumba aliomba mwongozo wa Makamu Mwenyekiti, Samia Suluhu Hassan, akisema Bunge linaangaliwa na watu wa rika tofauti wakiwamo watoto na kwamba Nchemba ametumia lugha isiyo na staha.

Samia alimtaka Nchemba kufuta kauli yake na kuwaomba radhi Mbowe na Jussa, lakini aliendelea kutetea hoja yake akidai kuwa baadhi ya vyama (bila kuvitaja) vinafadhiliwa na nchi zinazokubali ushoga na kwamba ataondoa majina ya Mbowe na Jussa, lakini neno ushoga litabaki pale pale.

Kufuatia kauli za Nchemba, wajumbe waliendelea kupiga kelele na kutaka afute kauli na kuomba radhi, huku Samia akitumia dakika kadhaa kuwatuliza wajumbe na kumtaka Nchemba kufuta kauli na kuomba radhi.

Hata hivyo, baadaye Nchemba alifuta kauli hiyo na kuwaomba radhi Mbowe na Jussa.

MAPENDEKEZO YA KIFICHO

Akiwasilisha Azimio la kufanya marekebisho ya Kanuni za Bunge la Maalum jana, Kificho alisema kuwa marekebisho yanayofanywa ni kanuni za Bunge Maalumu kwenye kanuni ya 37 kwa kuongeza mwishoni mwa fasiri ya (3) maneno “ya siri kwa mjumbe anayetaka kupiga kura ya siri au kura ya wazi kwa mjumbe anayetaka kupiga kura ya wazi kwa kuzingatia utaratibu ulioanishwa katika kanuni ya 38.

WENJE AWASHA MOTO
Kauli ya Ezekiel Wenje kuwa baadhi ya mawaziri wamewahonga baadhi ya wabunge wa makundi ya wabunge 201 ilisababisha vurugu kubwa kwa mawaziri tajwa kutaka waombwe radhi, akiwamo, Profesa Jumanne Maghembe (Maji), Dk. Shukuru Kawambwa (Elimu na Mafunzo ya Ufundi).

Mbali na mawaziri hao pia wajumbe kutoka kundi hilo walitaka kuombwa radhi.

Awali Makamu Mwenyekiti aliyekuwa anaongoza kikao, Samia Suluhu Hassan,  alimtaka Wenje kuomba radhi, lakini alisema mawaziri hao wamethibitisha wenyewe kuwaalika watu hao na kuongeza orodha ya mawaziri kuwa ni pamoja na Gaudensia Kabaka (Kazi na Ajira) na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kwamba walihusika kuwakirimu wajumbe hao na kuwapa msimamo wa serikali mbili.

Wakati vurugu za kelele na kurushiana maneno zikielendelea, Mwenyekiti wa Bunge Maalum, Samuel Sitta, alirejea kwenye kiti chake na kumtaka Wenje amjibu kama kweli haoni kuwa kauli yake imewaudhi wajumbe wengine.

Wenje alisema kuwa inawezekana kuwa kuna watu wameudhika, lakini kwa kuwa alichosema ni ukweli na kwa kuwa anaomba radhi tu, lakini ukweli anausimamia.

Kwa kauli hiyo, Sitta alisema kwa kuwa Wenje amekataa kuomba radhi, basi suala hilo ameamua kulipeleka kwenye kamati ya Kanuni na Haki za Bunge la Bunge Maalum.

Baada ya uamuzi wa Sitta wajumbe walishangilia na Wenje alionekana alishangilia uamuzi huo.
 
CHANZO: NIPASHE

Saturday, March 22, 2014

Kikwete ‘avuruga’ mjadala


Rais Jakaya Kikwete akilihutubia Bunge Maalumu la Katiba, mjini Dodoma jana. Picha na Michael Jamson 

Rais Jakaya Kikwete jana alibadili upepo wa mchakato mzima wa Katiba baada ya kutoa maoni yake binafsi, akitaka muundo wa Serikali mbili badala ya tatu zilizopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Akizungumza katika ufunguzi wa Bunge Maalumu la Katiba mjini Dodoma, Rais Kikwete alipangua hoja moja baada ya nyingine zilizotolewa na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Joseph Warioba wakati akiwasilisha Rasimu ya Katiba bungeni Machi 18, mwaka huu.
Katika hotuba yake hiyo ya saa 2:49 iliyokuwa na maneno ya ‘kuuma na kupuliza’ kuhusu yaliyomo katika Rasimu ya Katiba, Rais Kikwete alisema  suala la muundo wa Muungano ndiyo ajenda mama katika Rasimu ya Katiba na kwamba iwapo wajumbe watatoa uamuzi usio sahihi, nchi inaweza kujaa migogoro ambayo haikuwapo.
Huku akishangiliwa na wajumbe wa Bunge hilo, Kikwete alisema kuwa wanaotaka Serikali tatu waangalie changamoto zake na kuzitafutia majibu, kwa maelezo kuwa muundo huo unaweza kuvunjika kirahisi.
Alisema ingawa Jaji Warioba aliwatoa hofu wananchi kuwa Serikali tatu hazitakuwa na gharama kubwa, ukweli ni kwamba muundo huo una gharama na utekelezaji wake ni mgumu na kusisitiza kuwa CCM inaweza kuzimaliza kero za Muungano bila kuhitaji uwapo wa Serikali ya tatu.
Huku akichambua kile kilichoelezwa na Jaji Warioba sambamba na kuwapiga vijembe wenyeviti wa vyama vya upinzani akiwamo Christopher Mtikila (DP) na Freeman Mbowe (Chadema), Rais Kikwete alisema Tume ya Mabadiliko ya Katiba imetoa sababu mbili kubwa  za kupendekeza muundo wa Serikali tatu;
“Sababu ya kwanza ni kwamba muundo huo ndiyo matakwa ya Watanzania wengi Bara na Zanzibar.  Sababu ya pili muundo huo unatoa majibu ya uhakika na endelevu kwa changamoto za muundo wa sasa wa Serikali mbili zinazolalamikiwa na pande zote mbili.”
Aliongeza, “Wapo wanaokubaliana na tume na kwamba muundo wa Serikali tatu ni matakwa ya wengi na hauepukiki na kwa msemo wa Kiswahili wengi wape. Lakini wapo wanaopingana na takwimu za tume kwamba hazionyeshi ukweli huo. Mimi nasema maneno yanayosemwa na watu siyo yangu.” Huku akishangiliwa na wajumbe wa Bunge hilo alisema, “Watu wanasema Watanzania waliotoa  maoni kwa tume ni 351,664, kati yao 47,820 sawa na asilimia 13.6 ndiyo waliokerwa na muundo wa Muungano. Watu 303,844 sawa na asilimia 86.4 hawakuwa na tatizo na muundo wa Muungano na wala hawakuuzungumzia wakati wa kutoa maoni.”
Alisema hivi sasa watu wanahoji iweje asilimia 13.6 ndiyo wageuke Watanzania walio wengi ambao wametoa maoni ya kutaka Serikali tatu.
“Watu wanahoji mbona taarifa ya tume inayohusu takwimu (ukurasa 66,67), inaonyesha kati ya watu 47,820 waliotoa maoni kuhusu muungano watu 17,280 ndiyo waliotaka Serikali tatu ambao ni sawa na asilimia 37.2 na waliotaka muundo wa Serikali mbili ni asilimia 29.8, Serikali ya mkataba asilimia 25.3 na Serikali moja asilimia 7.7” alisema. Alisema taarifa ya tume inaonyesha kuwa watu 772,211 waliotoa maoni ni asilimia 10.4 ndiyo yaliyozungumzia muundo wa Muungano na asilimia 88.6 hawakuzungumzia Muungano, bali mambo mengine.
“Watu wanahoji kama Muungano ni jambo linalowakera sana Watanzania ingethibitika kwenye wingi wa wale waliotoa hoja. Usahihi wa hoja hii ni upi, nawaachie nyie (wajumbe) mjadili” alisema huku akishangiliwa kwa nguvu.
Akizungumzia sababu ya pili ya tume kwamba muundo wa Serikali tatu unajibu changamoto za muundo wa Serikali mbili, huku akifafanua kero zinazotolewa na kila upande wa Muungano alisema; “Nyinyi ndiyo waamuzi, sikilizeni vizuri hoja hizi mtafakari na kuamua. Tume yenyewe imekiri kuwa muundo wa Serikali wa Serikali tatu una changamoto zake ikiwa ni pamoja na gharama kubwa za uendeshaji wa shughuli za umma.”

Alisema wajumbe wa Bunge hilo wanatakiwa kutafuta majibu mwafaka kuhusu changamoto za muundo wa Serikali tatu kwa sababu maelezo ya tume kuhusu muundo huo hayana majibu.
Aliongeza, “Kupanga ni kuchagua. Wanaounga mkono Serikali mbili wanasema mlolongo wa changamoto ulioanishwa na tume kuhusu Serikali tatu hautapunguza matatizo bali utayaongeza kuliko ilivyo sasa na wanasema changamoto hizo zinatatulika bila kuwepo Serikali ya tatu.”
Alisema kama mfumo wa Serikali tatu ukipita ni lazima Serikali ya tatu ijengewe msingi imara kwa sababu haitakuwa na chanzo cha uhakika cha mapato yake yatakayoiwezesha kusimama yenyewe na haitakuwa na chombo cha kukusanya mapato zaidi ya kutegemea kukusanyiwa mapato na nchi washirika.
“Kama tunataka Serikali ya tatu lazima tuitengenezee misingi ya uhakika. Hivi nani atakudhamini kwa virungu, pingu, magari ya kuwasha, majeshi au bunduki. Serikali hii ya tatu haidhaminiki wala kukopesheka,” alisema huku akitolea mfano jinsi mataifa kama Urusi yalivyoanguka baada ya kujitenga.
Huku akifafanua jinsi kero za muungano zilivyotatuliwa na kamati na tume mbalimbali mpaka kubaki kero sita, Rais Kikwete alisema Serikali ya Muungano na ile ya Zanzibar zimeamua kutumia mchakato wa Katiba  kuyamaliza yale yanayohitaji kuingizwa kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Alisema wakati Tanganyika na Zanzibar zinaungana kulikuwa na mambo 11 ya muungano, baadaye kuongezeka hadi mambo 22 na kusisitiza kuwa mambo mengi yaliibuka baada ya kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka 1977.
Alisema jambo ambalo  Serikali hizo mbili walikubaliana kuliondoa katika mambo ya Muungano ni suala la gesi asilia na mafuta.
Ammwagia sifa Warioba
Alisema Jaji Warioba wa wajumbe wenzake wa Tume ya Katiba wameandika Rasimu ya Katiba vizuri na kwa weledi wa hali ya juu, na kwamba wametoa maoni ambayo kwa kiasi kikubwa yanahuisha na kuboresha Katiba tuliyonayo sasa.
“Katiba inayopendekezwa imejumuisha dhana na mambo kadhaa mapya yanayokwenda vyema na wakati tuliokuwa nao na kuweka misingi mizuri kwa huko mbele tuendako,” alisema.
Alisema Rasimu ya Katiba ni kitabu kikubwa kilichosheheni mambo mengi kina kurasa 106, sura 17, hivyo wajumbe wa Bunge la Katiba wanapaswa kusoma kila kitu na kuelewa na kuamua kwa utashi wao.
“Uamuzi wako siyo uamuzi wa kuambiwa na mwenzako, unaulizwa na wenzako kwenye hilo tusemeje unasema na mimi nimeambiwa, ebo! Umeambiwa, umefundishwa na mimi nasema akili za kuambiwa…” alisema Rais Kikwete.

Mambo mengine
Pia Rais Kikwete aligusia suala la mbunge kupoteza ubunge iwapo atashindwa kufanya kazi kwa miezi sita mfululizo, kutokana na maradhi au kizuizi ndani ya gereza.

Alisema anaungana na wote wanasema jambo hilo liangaliwe vizuri na kwamba anashauri kama akiwa kizuizi amepatikana na makosa apelekwe mahakamani.

“Kwa mazoea ya duania ukomo unawekwa kwa wakuu wa nchi, hawaweki ukomo kwa wabunge, Tanzania wanataka kuwa wa kwanza,” alisema Kikwete.

Kuhusu suala la ugonjwa alisema mbunge anaweza kupata ajali akiwatumikia wananchi wake, hivyo siyo sahihi kumwekea mgonjwa muda maalumu wa kuugua kwake.
Huku akicheka, Rais Kikwete alisema kitendo hicho kitawafanya wabunge kuanza kutembea na dripu katika majimbo yao kabla hawajapona vizuri.

source: Mwananchi