WHATEVER YOUR ARE BE A GOOD ONE;

A nation that is afraid to let its people judge the truth and falsehood in an open market is a nation that is afraid of its people. John F. Kennedy

“Taifa letu – taifa lolote – ni zuri na mahali pazuri pa kuishi kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka (ki-elimu?) na wanajitambua, haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii na kubadili mawazo na matumaini ya taifa.” Julius Kambarage Nyerere


Wednesday, July 31, 2013

Ya ‘Papii Kocha’ na tweets za Nyalandu, Januari, Kikwete!



WAKATI taifa likiwa katika maombolezo ya vifo vya mashujaa wetu saba waliouawa huko Darfur, Sudan, wakitumikia kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kulinda amani nchini humo, Jeshi letu la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) lilifanya tukio linalostahili pongezi nyingi, japo huenda ni wananchi wachache tu wenye taarifa nalo.

Jumapili iliyopita jeshi hilo lilianza kutumia rasmi mtandao wa kijamii wa twitter likitumia ‘handle’ @jw_tz. Hatua hiyo ni ya kimaendeleo na inaonyesha kuwa jeshi letu limedhamiria kwenda na kukumbatia teknolojia ya kisasa ya mawasiliano.

Mtandao wa twitter na pengine mitandao ya jamii kwa ujumla, bado ni suala geni kwa Watanzania wengi. Na licha ya ugeni huo, ukweli kwamba umiliki na upatikanaji wa huduma ya kompyuta bado ni ‘anasa’ wanayomudu watu wachache unafanya matumizi ya twitter (na mitandao mingine ya kijamii) kutokuwa suala muhimu au maarufu kwa jamii yetu.

Hata hivyo, mitandao ya kijamii hivi sasa imekuwa sehemu muhimu ya mawasiliano; huku ikibadili kwa kiasi kikubwa upatikanaji na kupashana habari. Wakati kwa muda mrefu mawasiliano kati ya mtu na mtu yamekuwa yakitegemea aidha neno la mdomo (kwa maana ya watu kukutana au kwa njia ya barua) au magazeti na redio, na kwa kiasi fulani runinga, mitandao ya jamii na teknolojia ya mawasiliano kwa ujumla imetokea kuwa njia ya haraka ya mawasiliano katika jamii.

Ukitaka kupata mfano wa umuhimu wa teknolojia hiyo ya mawasiliano, ni jinsi ziara ya kihistoria ya Rais wa Marekani Barack Obama huko nyumbani Tanzania, hivi karibuni, ilivyoripotiwa in real time (kadri matukio yalivyokuwa yakitokea) badala ya kusubiri gazeti la kesho au ripoti za redioni au kwenye runinga.

Kadhalika, kwa kutumia mtandao wa twitter, wananchi wamekuwa wakiendesha kampeni mbalimbali, na ya hivi karibuni kabisa ni ile inayohamasisha kupinga kodi ya sim card ambapo inatumia hashtag #NoSIMcardTax.

Iwapo Serikali itasikiliza kilio cha wananchi na kusitisha au kufuta kodi hiyo, basi kampeni hiyo ya mtandaoni (hususan huko twitter) itastahili pongezi kubwa.

Pamoja na pongezi zangu kwa hatua hiyo ya JWTZ kujiunga na mtandao wa twitter, bado taasisi hiyo inakabiliwa na changamoto kubwa; hususan kutumia ipasavyo mtandao huo kama nafasi kwa jeshi hilo kuupasha umma habari stahili.

Kwa mfano, juzi Rais Jakaya Kikwete aliwaongoza Watanzania kutoa heshima zao za mwisho kwa miili ya wanajeshi wetu waliouawa Darfur, na katika mazingira mwafaka, tungetegemea akaunti ya twitter ya JWTZ ingetulea tukio hilo ‘live’ lakini haikuwa hivyo. Siwalaumu kwa vile pengine ni ugeni tu katika matumizi ya teknolojia hiyo.

Licha ya ujio huo wa JWTZ huko twitter, mtandao huo wa kijamii unatumiwa pia na baadhi ya viongozi wetu wa serikali na wanasiasa, japo idadi yao ni ndogo. Rais Kikwete ni miongoni mwa viongozi hao; huku akiweka historia ya kuwa mmoja wa marais wachache wa Afrika wanaotumia mitandao ya kijamii.

Miongoni mwa mawaziri wachache wanaotumia mtandao wa twitter ni Mheshimiwa Lazaro Nyalandu (@LazaroNyalandu), Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii. Uwepo wake katika mtandao huo umenisaidia kumfahamu katika namna ambayo pengine Watanzania wengi hawaifahamu.

Nyalandu amekuwa mfano bora wa jinsi inavyostahili na inavyowezekana kuweka maslahi ya nchi mbele ya maslahi ya kiitikadi. Lilipotokea tukio la milipuko ya mabomu jijini Arusha, Waziri Nyalandu alishiriki kikamilifu kuufahamisha umma kuhusu hatua mbalimbali zilizokuwa zikifanyika kuwasaidia majeruhi.

Na japo Nyalandu ni Mbunge wa CCM, kamwe hajawahi ku-tweet mambo ya kiitikadi, na badala yake tweets zake zimekuwa zikihusu masuala ya Tanzania na Watanzania, badala ya masuala ya CCM.
Kingine kinachopendeza kuhusu Naibu Waziri huyo ni usikivu kwa hoja mbalimbali zinazowasilishwa kwake kupitia mtandao huo. Kama ilivyo kwa Naibu Waziri mwingine, Januari Makamba (@JMakamba), Nyalandu huwasiliana na wananchi waliopo twitter kwa heshima na unyenyekevu mkubwa, kiasi yaweza kuwa vigumu kudhani ni mtu mwenye dhamana kubwa serikalini.

Ni kwa sababu hiyo, kupitia mtandao wa twitter Jumapili iliyopita nilimtumia ombi Waziri Nyalandu kumsihi awasilishe kilio cha msanii Johnson Nguza (Papii Kocha) ambaye, pamoja na baba yake Nguza Viking na kaka zake wawili, wanatumikia kifungo kirefu jela kwa kosa la kubaka.

Mwishoni wa wiki, blog mbalimbali zilichapisha barua iliyoandikwa na msanii huyo (Papii Kocha) kwenda kwa Rais Kikwete akiomba msamaha kwa yeye na familia yake, na kumwomba Rais awatoe gerezani.

Nina sababu mbili za msingi za kuguswa na suala la ‘Babu Seya’ na wanae ambao wamekuwa gerezani kwa takriban miaka 10 sasa. Kwanza, japo kuna msemo maarufu kwenye kila jela kuwa ‘kila mfungwa hana hatia’ (yaani amefungwa kwa kuonewa), tangu Nguza na wanae walipokamatwa na hatimaye kufungwa nimebaki na hisia kuwa sheria ilipindishwa dhidi yao.

Mengi yameshasemwa huko mitaani kwamba kesi hiyo ilisababishwa na visasi binafsi dhidi ya msanii huyo na wanae. Ikumbukwe kuwa katika nchi zetu masikini kuna ‘haki za aina mbili,’ kwa wanyonge ambao wanaweza kwenda jela kwa kusingiziwa tu, na kwa vigogo ambao ni kama wana kinga ya kudumu ya kisheria.

Sababu ya pili ya kumwomba Waziri Nyalandu amfikishie Rais Kikwete ujumbe wa Papii Kocha ni ya kibinadamu zaidi. Tuweke kando hisia kuwa kifungo cha Nguza na wanae ni sheria kufuata mkondo au kupindishwa.

Kama binadamu, na hasa katika Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan, unajiskiaje ukisoma barua ya kutoa majonzi kutoka kwa kijana mfungwa anayezeekea jela akiomba msamaha kuhusu hukumu ambayo tangu mwanzo wafungwa hao wamekuwa wakidai ni ya uonevu tu dhidi yao?

Ndio, huko jela ‘kila mfungwa hana hatia’ (yaani wafungwa wengi hudai wamefungwa kwa kuonewa hata kama walikamatwa red-handed wakifanya makosa).Lakini katika mazingira ya kawaida, ni wafungwa wangapi waliopo jela kwa takriban miaka 10 na wanaendelea kusisitiza kuwa walifungwa kwa uonevu na wanaomba hukumu dhidi yao ziangaliwe upya au wasamehewe?
Laiti ukisoma barua hiyo ya Papii Kocha (na amekuwa akiandika barua kama hiyo mara kadhaa) usipolengwa na machozi basi utakuwa na ‘moyo mgumu’ kweli.

Lakini hata tukiweka kando huruma ambayo baadhi yetu tunayo kwa Nguza na wanae, katika ubinadamu tu, msanii huyo na wanae wameshatumikia adhabu ndefu (bila kujali walitenda kosa au la), na adhabu waliyokwishapata inatosha kutoa fundisho kwao na kwa jamii kwa ujumla. Hivi sisi kama jamii tutaathirika vipi iwapo Nguza na wanawe wakisamehewa?

Kama nilivyotarajia, ‘mtu wa watu’ Naibu Waziri Nyalandu alinijibu juzi akisema kwa tweet (namnukuu) “copy that...” akimaanisha amesikia ombi langu na atalifanyia kazi.

Licha ya imani yangu kwa Nyalandu, nina imani pia kuwa Rais Kikwete atasikiliza ujumbe huo kutoka kwa mteuliwa wake. Vilevile ukweli kuwa huu ni Mwezi Mtukufu, na nina hakika Rais amefunga pia, roho ya huruma itamsukuma kusikiliza kilio cha mara kwa mara kutoka kwa Papii Kocha, kaka zake na baba yao.

Mwisho, ninaomba kila Mtanzania mwenye kuamini katika kuwasamehe waliotukosea (ikiwa ni pamoja na wanaotajwa kuwa wahanga wa makosa yaliyofanywa na ‘Babu Seya na wanawe) atajumuika nami kuwaombea msamaha wasanii hao.

Maandiko Matakatifu katika Surat Al I’mran 155 ya Kurani Tukufu na Marko 11:25 ya Biblia Takatifu ni baadhi za aya lukuki zinazotusisitiza kuhusu msamaha.

Mwenge juu ya Kilimanjaro, umulike hadi nje, ulete kitu gani?



Tunachokishuhudia hivi sasa ni hangaiko kuu lililotukumba kutokana na kushindwa kwetu kujiletea maendeleo tuliyojiahidi sisi wenyewe yapata miongo mitano iliyopita.

Nafsi zetu zinatusuta, na zinapotusuta tunakataa kukubali kwamba tunastahili kusutwa, na badala yake tunatafuta kila aina ya visingizio ili tuepuke uwajibikaji. Hebu turejee historia yetu kwa ufupi.

Tulipopata Uhuru tuliiahidi dunia, huku tukijiahidi sisi wenywe (hapa nazungumzia Watanganyika) kwamba tutafanya kazi kwa bidii na maarifa kuijenga nchi yetu na kuweza kuonyesha matunda mazuri zaidi kuliko yote waliyofanya Waingereza katika kipindi cha miaka arobaini waliyotutawala.
 Mwenge juu ya mlima Kilimanjaro
Mwaka 1958, muasisi wa Taifa la Tanganyika, Mwalimu Julius Nyerere alitamka, kwa niaba yetu, kwamba tungependa kuwasha mwenge na kuuweka juu ta Mlima Kilimanjaro, umulike nje ya mipaka yetu na ulete tumaini kila kusiko kuwa na tumaini, upendo kulikojaa chuki, na heshima kulikojaa dharau.

Haya ni maneno yaliyofanana sana na yale ya Mtakatifu Francisco wa Asissi, ambaye aliyafunga maisha yake katika utumishi na huduma kwa masikini ingawaje alitokana na familia tajiri ya mjini Assisi na katika ujana wake alishiriki katika biashara na kukuza ukwasi wa baba yake.

Baada ya “kuona mwanga,” Francisco aliukana ukwasi wa familia yake na akajikita katika utumishi wa watu na viumbe hai wengine. Ni kwa heshima yake ulianzishwa utawala wa Wafransiska (Franciscans) ambao itikadi yao inakumbatia umasikini na unyenyekevu katika utumishi wa Mungu na watu wake.

Mwaka 1961, Mwalimu aliwaambia Waingereza (kupitia Richard Turnbull, gavana wa mwisho) kwamba angewaalika baada ya miaka kumi waje wajionee maendeleo ya Tanganyika waliyokuwa wameiacha masikini, hio,  hahehahe, baada ya utawala wao wa miaka arobaini.

Na kweli, miaka kumi baadaye, aliwaalika na wakaja kulikuta Taifa lililojiamini na lililokuwa linaonyesha kila dalili ya kupiga hatua za kusonga mbele. Desemba 1971 nilikuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu na nilikuwa mwongozaji (guide) wa wageni mashuhuri (VIP) wa kitaifa. Nilishuhudia binafsi ari na fahari iliyokuwepo wakati wa maadhimisho hayo, pamoja na hali tete ya usalama iliyosababishwa na kile kilichoelezwa kuwa njama za Wareno na vibaraka wao wa ndani.   

Wakati huo Tanganyika ilikwisha kuungana na Zanzibar kuunda taifa jipya la Tanzania, na hatima ya nchi yetu ilikuwa inaandikwa kwa ustadi mkubwa. Tulikuwa na viwanda vyetu vya nguo, vifaa vya kilimo na kadhalika, tulikuwa na asasi zetu za fedha na biashara, tulikuwa na uhuru wetu wa kuwaambia wakuu wa dunia wakome na wakakoma.

Tulijenga msingi, angalau mwanzo tu, na matumaini yalikuwa makubwa juu ya mustakabali wa nchi yetu. Tulikuwa ni nguzo kuu ya mapambano ya kulikomboa bara la Afrika, na vita ya ukombozi ilikuwa inarindima Msumbiji, Angola, Zimbabwe, Namibia na kwingineko.  Ilikuwa fahari kubwa kuwa Mtanzania.

Miaka hamsini baada ya Uhuru, tumekuwa wanyonge zaidi. Sababu kubwa ya unyonge huu ni kwamba hatujafanikiwa kufasiri ndoto za zama zile kwa kuwapa wananchi wetu, hasa masikini kabisa miongoni mwao, matumaini, angalau matumaini tu, ya maisha bora kwa wao wenyewe au kwa uzao wao. Badala yake, katika medani kadhaa, tumewapa sababu za kukata tamaa kabisa.

Naomba nieleweke vyema hapa. Hali ninayoieleza haikuanza leo hii wala jana, wala juzi. Tunaweza kuonyesha ni jinsi gani tulivyoanza kuteleza taratibu tangu awamu ya kwanza kabisa, chini ya uongozi wa muasisi tunaye muenzi. Hili nimeliandika mara nyingi mno, na sidhani kwamba yupo yeyote anayeweza kushuku dhamira yangu.
Tatizo ninaloliona ni kwamba hatutaki kuyajadili matatizo yetu, na badala yake tunaona faraja katika kuyafunikiza, kama vile tunaamini kwamba yasipoonyeshwa hadharani, yasipoonekana na kujadiliwa, yatatoweka.  Mawe!

Hayatoweki, na badala yake kila siku  yanakua na kuchukua sura mpya, mbaya zaidi na ya hatari zaidi. Kila unapotokea mlipuko watawala wetu wanadhani kwamba ni tatizo jipya, kwa hiyo wanaushughulikia mlipuko huo kwa nguvu zao zote (nguvu zao zote kwa maana halisi ya nguvu zisizo kiasi, nguvu za “kupiga,” si kwa umahiri wowote wa tafakuri na utafiti wa utatuzi wa suluhu).
Tofauti na tafakuri, kupiga ni rahisi kwa watawala, kwa sababu wakati tafakuri inawahitaji wao ndio watafakari, kupiga hakuwahitaji wao wafanye lolote zaidi ya kutoa amri, “Piga!” Wapigaji wapo wa kutosha.

Kwa bahati mbaya (nzuri kwa wengine), historia inatuonyesha (pale tunapotaka kuona) kwamba kila kipigo cha uonevu huzaa uadui usioisha, uhasama wa kudumu na ghadhabu za masafa marefu. Aidha historia inatufundisha (pale tunapokuwa tunafundishika) kwamba jamii haziburuzwi kwa maguvu ili zipate maendeleo; jamii hujenga utashi wa maendeleo taratibu, kila kizazi kikijenga juu ya msingi ulioachwa na kile kilichotangulia, kwa kudunduliza (incrementally).

Ule msemo wa zamani, kwamba mchungaji mmoja anaweza kuwaswaga ng’ombe mia kwenda mtoni, lakini wachungaji mia hawana uwezo wa kumlazimisha ng’ombe mmoja tu kunywa maji, unahusika hapa.

Naamini kwamba haya yote tunayajua, hata kama kwa sababu fulani, zilizofichika na zilizo wazi, hatutaki, au hatuwezi kuyaishi (kwa maana ya kuyatafsiri katika maisha yetu na kazi zetu).
Kwa mfano, tuchukue “ukorofi” wa baadhi ya wananchi wa Mtwara kuhusu gesi. Wanapigwa. Ikija kutokea “ukorofi” wa wananchi wa Kigoma kwa gesi hiyo hiyo, watapigwa. Wananchi wa Dodoma wakiandamana kuhusu madhara ya urani, watapigwa. Halafu wananchi wa Mbeya wakihoji juu ya makaa ya mawe, wapigwe, na kadhalika.

Ni dhahiri kwangu kwamba nchini humu, na katika maeneo mengi yaliyotofautiana kwa maumbile, wananchi wanazo sababu lukuki za kutoridhishwa na jinsi mambo yanavyoendeshwa na watawala. Ikiwa kila watakapoandamana, kulalama au kukataa kutii amri wanazoziona kama za kuwaumiza watapigwa, kipigo kitakuwa ni kila mahali nchini.

Tayari, katika maeneo kadhaa, kipigo kimekuwa ni jambo la kawaida. Tayari tumeona wazi wazi ambavyo watu wameumizwa kwa vipigo nje ya hukumu ya sheria. Bado tunasema watapigwa zaidi?

Ule mwenge tuliosema tutauweka juu ya Mlima Kilimanjaro (hadi leo tunaimba wimbo huu) ni wa kueneza vipigo kila ambako hakuna vipigo, vilio mahali pasipo na vilio na simanzi kwa wote wasio na simanzi?

Tume: Hakuna gharama kuendesha Serikali tatu



Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Humphrey Polepole akizungumza jambo.

Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya, imewabeza watu, hususan wanasiasa wanaosimama majukwaani kueleza Muundo wa Muungano wa Serikali tatu utaongeza gharama za kiuendeshaji kuwa ni uongo na sababu hizo hazina tija.

Mjumbe wa Tume hiyo, Humphrey Polepole alisema hayo jana wakati wa mkutano wa kuijadili Rasimu ya Mabadiliko ya Katiba Mpya mbele wa Wajumbe wa Baraza la Wilaya ya Nanyumbu Mkoani Mtwara.

Alisema Muundo wa Serikali tatu hauna gharama zozote kwani chanzo cha mapato cha kuongoza Serikali ya Muungano kuwa tayari kimebainishwa.

Polepole alisema gharama za kuongoza Serikali hiyo zitatokana na Kodi ya Ushuru wa Bidhaa ambapo jumla yake zinazokusanywa si chini ya  Sh1 trilioni.

“Mpaka sasa Serikali ya Muungano inakusanya zaidi ya Sh3 trilioni hivyo kama itatumika  Sh1 trilioni na zitakazobaki zitaelekezwa katika shuguli zingine, fedha zitakuwepo,” alisema Polepole na kuongeza:

 “Nashangaa wanasiasa wanaosimama majukwaani kueleza wananchi kuwa kutakuwa na mzigo wa gharama, hii si kweli kwani Tume tumekwisha bainisha chanzo chake cha mapato na hao wanaozungumza hayo hawafuatilii mchakato kwa umakini.”

 Alisema uchambuzi walioufanya juu ya kodi inayokusanywa mwaka 2003/04 zilikusanywa jumla ya Sh500 bilioni na mwaka 2011/12 zilikusanywa Sh1 trilioni ambapo kila mwaka mapato hayo yanaongezeka.

 “Uzoefu unaonyesha kila mwaka mapato yanaongezeka hivyo uwepo wa Muungano wa Serikali tatu ni dhahiri hautaathiri kitu chochote na utasaidia kutatua kero zilizopo zinazojitokeza kila mwaka kila kukicha,” alisema Polepole

 Polepole aliwataka Wananchi kutokuwa na shaka na mapendekezo hayo ya Tume juu ya Muundo wa Muungano kuwa wa Serikali tatu kwani utapunguza malalamiko ya muda mrefu yaliyopo.

 “Hivi sasa kuna kero zaidi ya 47 na kwa Muungano huu uliopo hautamaliza na wala hauwezi kuyafanyia kazi lakini kutokana na mapendekezo ya Tume ya Serikali tatu ninahakika yatapungua na kila upande kutokuwa na  malalamiko,” alisema Polepole.

Polepole amesisitiza kwa kuwaomba wananchi kuendelea kutoa maoni katika hali ya kutoshinikizwa kwa namna yoyote.

“Kila mtu anapaswa kuwa huru kutoa maoni yake bila kuogopa chochote. Lengo la uwepo wa katiba mpya ni kujua hitaji hasa la wananchi ni nini na kwamba katika kutoa maoni wananchi wanapaswa kufanya hivyo bila woga,” alisisitiza Polepole.

Baadhi ya watu wengine walioshiriki kwenye tukio hilo waliomba Tume ya Katiba kuangalia namna ya kufanya ili hatimaye kweli Katiba itakayopatikana iwe ni kwa ajili ya wengi, si zaidi.

Walisema kwamba kuna watu wamekuwa maoni ambayo mengine yanaweza kuonekana kutokuwa na masilahi kwa baadhi ya vyama au viongozi, ni suala la msingi sana kufanya kila wanaloweza kuhakikisha kuwa maoni ya wengi yanazingatiwa ili hata watu wawe na wepesi katika kuzingatia yale ambayo yatakuwemo kwenye Katiba hiyo.

Ni wazi kwamba ikiwa katiba itazingatiwa vizuri kwa maana ya kujali wanachosema wananchi, hakutakuwa na ugumu wa kuitekeleza.

source: mwananchi

Tuesday, July 23, 2013

HOTUBA YA MHE. JAKAYA MRISHO KIKWETE, WAKATI WA KUAGA WANAJESHI SABA WA KULINDA AMANI WALIOPOTEZA MAISHA DARFUR, SUDAN

 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza wakati wa zoezi hilo.Picha an Ofisi ya Makamu wa Rais
HOTUBA YA MHE. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, WAKATI WA KUAGA WANAJESHI SABA WA KULINDA AMANI WALIOPOTEZA MAISHA DARFUR, SUDAN 

TAREHE 22 JULAI 2013

Mhe. Mohammed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano;
Mhe. Balozi Seif Iddi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar;
Mhe Shamsi Vuai Nahodha, Waziri wa Ulinzi na Jeshi laKujenga Taifa;
Waheshimiwa Mawaziri; Jenerali Davis Mwamunyange, Mkuu wa Majeshi yaUlinzi;
Wakuu wa Majeshi ya Ulinzi Wastaafu;Chief of Staff na Chief of Staff Wastaafu;Majenerali;
Maafisa Wakuu;
Maafisa Wadogo; Askari, Wafanyakazi raia wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi laKujenga Taifa;
Waombolezaji wenzangu;
Familia za Wafiwa;
Mabibi na Mabwana.

Leo ni siku ngumu sana kutakiwa kuzungumza. Ugumuwenyewe unatokana na ule ukweli kwamba siyo siku ya furaha bali ya majonzi na huzuni kubwa kwangu, kwa taifaletu na familia za wanajeshi wetu saba marehemu ambaotumekusanyika hapa kuwaaga. Baada ya sherehe zakutunuku Kamisheni kwa Maofisa wapya katika Chuo chaMafunzo ya Kijeshi, Monduli Jumamosi tarehe 13 Julai, 2013 Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange aliniarifukutokea shambulio la kuvizia kwa baadhi ya wanajeshi wetuwalioko Darfur. Kwa kuwa wakati ule mapigano yalikuwayanaendelea, aliniambia kuwa atatoa taarifa zaidi baadae kadri taarifa zitakavyokuwa zinapatikana.

Baadae akanipa taarifa kuwa vijana wetu wamefarikina wengine wamejeruhiwa. Lazima nikiri kuwa taarifahiyo ilinihuzunisha, kunisikitisha na kunikasirisha. Kwa niniwatu wa Darfur wawaue wanajeshi wetu ambaowamekwenda kule kuwasaidia wapate utulivu, ili kunusurumaisha yao, kuwaondolea wasiwasi na kuwawezeshawafanye shughuli zenye tija kuendesha maisha yao. Mojakwa moja sikusita kuamini kuwa waliofanya hivyo ni watuwahalifu.

Tangu uhuru ni sera ya nchi yetu kutetea wanyongedhidi ya ukoloni, ubaguzi, uonevu, dhuluma na 
watu wotewalioko katika mazingira hatarishi Afrika na duniani. Njia za Kidiplomasia zilitumika na wakati mwingine JWTZlilishirikishwa. Ndio maana tumeshiriki kwenye vita vyaukombozi katika nchi kadhaa zilizopo Kusini mwa Afrika.Vilevile tumeshiriki katika shughuli za kulinda amani katikanchi mbalimbali zikiwemo Liberia, Sierra Leone na Eritrea.Hivi sasa Jeshi letu linaendelea na jukumu hilo nchiniLebanon, Cote d’Ivoire, Darfur (Sudan), Sudan Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Katika nchi zote hizo,askari wetu wanasifiwa sana kwa bidii ya kazi, uvumilivu,uhodari na nidhamu ya hali ya juu.

Wakati wote tulipoombwa na kukubali kupelekawanajeshi wetu kutekeleza majukumu hayo, uwezekano wawao kujeruhiwa au kufariki yanafikiriwa kutokea.Wanakwenda kwenye maeneo yenye mapigano hivyohatari hizo kutokea ni jambo linalowezekana. Tahadharizote husika huchukuliwa kuepusha hatari hizo. Ndiyomaana hupewa mafunzo ya kutosha na silaha za kutosha.Hata hivyo hutokea nyakati kukatokea yasiyotarajiwa kamayaliyotokea Darfur. Pia yaliwahi kutokea Liberia.

Kufuatia tukio hilo, nilizungumza na Katibu Mkuu waUmoja wa Mataifa ambaye alinielezea masikitiko yakemakubwa kwa yaliyotokea na kutoa pole zake nyingi. Pia alinieleza kuwa alizungumza na Rais Bashir wa Sudanakitaka wahalifu hao wasakwe, wakamatwe na kuadhibiwaipasavyo. Aidha, nilifanya mazungumzo na Rais Omar AlBashir wa Sudan, ambaye naye alinielezea masikitiko yakena kutoa pole nyingi. Katika mazungumzo yangu naye nilimsisitizia umuhimu wa Serikali yake kufanya uchunguziwa kina wa shambulizi hilo na kuwawajibisha waliohusika. Rais Bashir alikubaliana nami na kuahidi kufanya kilalinalowezekana ili ukweli ufahamike na hatua stahikizichukuliwe.

Sisi kwa upande wetu, Jeshi la Wananchi wa Tanzanialimeunda Bodi ya Uchunguzi inayotarajiwa kuelekea Sudankwa ajili ya kufanya uchunguzi wa kina kubaini chanzo chashambulizi hilo.

Kwa huko Darfur, tangu shughuli za ulinzi wa amani waUNAMID zianze mwaka 2007 walinzi wa amani 41 kutokamataifa mbalimbali wameuawa na zaidi ya walinzi wa amani 55 wamejeruhiwa. Kwa kweli idadi hii ni kubwa mnoinayohitaji kutafakariwa vizuri na wadau wote. Penginewakati umefika wa kuutazama upya mfumo wa kulindaamani Darfur hasa kuhusu uwezo wa kujilinda na wanajeshiwanaolinda amani. Hapana budi uwezo wao uongezwe ili kupunguza vifo na majeruhi. Narudia kuahidi kuwa rai hiitutaifikisha kwa mamlaka husika katika Umoja wa Mataifana Umoja wa Afrika.

Napenda kuchukua nafasi hii kuishukuru serikali yaSudan, Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa kwaushirikiano mkubwa waliotupatia tangu kutokea kwa tukiola kushambuliwa kwa askari wetu. Pia nawashukuru nakutoa pongezi kwa Waziri Shamsi Vuai Nahodha, JeneraliDavis Mwamunyange na makamanda na askari wote wa JWTZ, kwa jinsi walivyoshughulikia msiba huu tanguilipopokelewa taarifa ya vifo vya mashujaa wetu hawampaka sasa. Mmewapa heshima kubwa wanaoistahili.Asanteni sana.

Kwa namna ya pekee, narudia kutoa pole nyingi kwafamilia za wafiwa. Nawashukuru kwa dhati kwa moyo waowa uvumilivu na subira. Naomba mfahamu kuwa, mimi naWatanzania wote tupo pamoja nanyi katika kuombolezavifo vya mashujaa wetu. Msiba huu ni wa taifa letu lote nawatu wote wenye kupenda amani duniani.

Daima tutawakumbuka mashujaa wetu na tutaendeleakuenzi na kujivunia kazi zao na mchango wao mkubwa kwanchi yetu na dunia kwa ujumla. Nawaomba sote tuendelee kumuomba Mwenyezi Mungu aziweke roho za mashujaawetu mahala pema peponi. Amen.

Kwa Jeshi na wanajeshi wetu wote, napenda kumaliziakwa kuwaasa kuwa yaliyotokea Darfur yasiwakatishe tamaakatika kutimiza wajibu wetu Darfur na kwingineko. Yaliyopita si ndwele, tugange yajayo.

Yaliyotokeayanatukumbusha kuchukua tahadhari zaidi na kuongezauwezo wa kujihami wa wanajeshi wetu kila wanapotumwakutekeleza jukumu lao.

Asanteni
 
source: Haki Ngowi